Mtoto wa kigogo akamatwa na dawa za kulevya huko China - Dr Slaa

Status
Not open for further replies.
Hivi huyo Riz1 mpumbavu kiasi gani ayabebe madawa ya kulevya yeye mwenyewe na asitumie watu wengine?
 
Si ndiyo wewe unagunaguna ya kwamba siyo kweli fuatilia nyendo zote ya fisadi wenu Jk kama siyo kweli urudi na Jibu kamili!


QUOTE=Elungata;4914156]Kama kuna mtu mwenye kumbukumbu kuanzia tarehe 1 july hadi 5 july atuwekee hapa tuone jk alikua wapi tarehe hizo.kumbukumbu kutoka magazetini au threads za tarehe hizo.maana kila rais akiondoka huwekwa uzi hapa.[/QUOTE]
 
Hii hbr ya uwongo hata hizo namba za gari za CDR sio za Julai..wkt huo zilikua hazijafika na zilikua around CB..
 
Saint Ivuga bora umeirudisha thread hii kwani kule ilikokuwa wameshani-block kuchangia sijajua ni mdudu?

Kwa tarehe zilizotajwa ni vigumu kuamini kama kuna ukweli au ni kumchafua JK kama walipodai kuna Container 40ft lina kura zilizopigwa za Urais
Simsemei Ridhiwani kwa tarehe hizo kuwa hakuhusika inawezekana alitumia Jet kufika Hong Kong na Baba yake kumfuata na asubuhi akawa DSM

Kulikuwepo Msiba wa Kada mmoja aliyekuwa Diwani wa Viti maalum awamu iliyopita wa Kawe na Kamanda wa UVCCM Kibaha, Msiba huo ulikuwa huko Mbezi Louis, kwa muda wa siku 3, Ibada ya Mazishi ilifanyika huko KKKT Tangi bovu na Mazishi yalifanyika Makaburi ya Kinondoni Ridhiwani alikuwepo kuanzia siku ya kwanza hadi hizo tarehe za mazishi ambazo wanadai alikuwa Hongkong waliokuwepo wengine ni km Nape Mnauye Mwenyekiti wa CHADEMA na viongozi mbalimbali huyo Ridhiwani alionekana.

Story yenyewe ina utata katika yafuatayo BOFYA HAPO Jason Bourne DU HII PICHA KALI HATA JAMES BOND, asingeweza kutoa picha hii
Mnamo tarehe 2/7/2012 majira ya saa nne (4:13) za usiku hapa Tanzania, rais Jakaya Kikwete alipokea simu kutoka kwa mtanzania mmoja aitwae Philip Malmo ambae ni balozi wa Tanzania nchini China, Taarifa muhimu baada ya salamu ilikuwa ni Ridhiwani amekamatwa uwanja wa ndege wa Hong Kong na madawa ya KULEVYA,

Rais alikata simu huku hali yake usoni ikibadilika gafla, ilichukua kama dakika 20 hivi rais akiwa kimya hata kutikisa macho tu hatikisi, baadae akainua simu na kumpigia rais Hu Jintao wa China, Waliongea kwa mda mrefu yapata dakika 40 hivi, na walikonekana kama hawakubaliana kitu fulani katika mazungumzo yao. Baadae simu ikakatwa,
Akampigia simu Malmo nakumwambia suala hili walifanye kwa siri kubwa asijue mtu yeyote, naaweke maandalizi yawe tayari yeye anajiandaa kuja kulimaliza, kasha akampigia tena simu Hu Jintao na walitumia dakika 16 tu akainuka nakusema, vijana, mwambie SD53 aandae ndege haraka kwa safari ya China,

Gari ya kirai namba T 435 CDR aina ya Landcruiser nyeusi iliingia nakuwabeba watu watatu akiwemo rais Jakaya kuelekea airport, kama dakika 13 ikafika airport, tayari ndege ilishaandaliwa na palikuwa na maafisa watatu, wote tuliingia katika ndege ile isipokuwa yule dereva wa gari ambae aligeza mjini, hiyo ilikwa sasa ni saa 7:43 za usiku.
Majira ya saa 11 alfajiri kwa saa za china, Ridhiwani aliletwa akiwa katika gari dogo, nakupokelewa na jk huku wakikumbatiana wote WAKILIA.
Majira ya saa 12 za asubuhi tukaondoka kurudi Tz.

T 435 CDR kwa wakati huo wa June 2012 No. bado zilikuwa CCX ilikuwa bado kufikia CDA
watu watatu, maafisa watatu, wote tuliingia inaelekea huyu JB (mm nitamwita James Bond) toka simu ya Philip Marmo mpaka wanapanda Jet Fighter na kwenda Hong Kong (+8 GMT) DSM IPO (+3 GMT) Umbali huo sio mchezo eti masaa 3 (wengine wanadai ni masaa ya kwenda Ruvuma au Dodoma) Hata ukifuata masaa ya jua kwenda Hong Kong ni Negative lazima utakuta jua linapambazuka lakini saa 11 alfajiri Ridhiwani aliletwa na gari ndogo na wakarejea TZ hata hakujapambazuka. Kumbuka ni tarehe 02/07/2012 saa 8 kasoro robo na asubuhi 03/07/2012 yupo DSM
 
Si ndiyo wewe unagunaguna ya kwamba siyo kweli fuatilia nyendo zote ya fisadi wenu Jk kama siyo kweli urudi na Jibu kamili!


QUOTE=Elungata;4914156]Kama kuna mtu mwenye kumbukumbu kuanzia tarehe 1 july hadi 5 july atuwekee hapa tuone jk alikua wapi tarehe hizo.kumbukumbu kutoka magazetini au threads za tarehe hizo.maana kila rais akiondoka huwekwa uzi hapa.
[/QUOTE]

at least mimi nimeitilia shaka story hiyo kuliko wewe unaeamini kila kitu.unaonyesha jinsi usivyo na reasoning capacity.unapokea tu bila kudigest
 


Hii habari ni ya kweli kabisa na na mtuhumiwa ni Riz-One. Ilishawahi kutoka huko nyuma humu JF lakini Mods aliiondoa mara moja. Mimi niliwahi kusave text yake tu kwani nilibahatika kuiona thread muda mfupi tu baada ya kuwekwa na mtoa thread mmoja ambaye sikubahatika kusave jina lake. Thread niliisave tarehe 6 Sept 2012 saa 7.28 pm.

Thread yenyewe inasomeka hivi:



Ridhiwani na madawa ya kulevya china...


Hii nimeikuta kwenye mtandao mmoja hivi..

Rais Jk auza nchi kumuokoa mwanae Ridhiwani asinyongwe China

Huwezi kuamini lakini ni UKWELI

Taarifa za upelelezi makosa ya jinai nchini China zinasema tarehe 01/7/2012, vijana wawili wenye asili ya kiafrika walikamatwa katika uwanja wa ndege wa Hong Kong usiku, wakiwa na madawa ya kulevya yenye thamani ya shilingi za Tanzania Bilioni nne, mkuu wa kitengo chakuzuia mihadarati cha uwanja wa Hong Kong Yiu-Kwong anawataja kuwa ni Ridhiwani Jakaya Kikwete na Abdalah Aman Mohamed

Mnamo tarehe 2/7/2012 majira ya saa nne (4:13) za usiku hapa Tanzania, rais Jakaya Kikwete alipokea simu kutoka kwa mtanzania mmoja aitwae Philip Malmo ambae ni balozi wa Tanzania nchini China, Taarifa muhimu baada ya salamu ilikuwa ni Ridhiwani amekamatwa uwanja wa ndege wa Hong Kong na madawa ya KULEVYA,

Kwa haraka, rais akamuuliza vipi suala hili limeshafika hapo ubalozini? Akajibiwa hapana ni mimi na kaimu wangu tu ndie tumepata taarifa hii mda huu, bado hatujaliifanya lakiofisi, tunasubiri ushauri wako mheshimiwa.
Rais alikata simu huku hali yake usoni ikibadilika gafla, ilichukua kama dakika 20 hivi rais akiwa kimya hata kutikisa macho tu hatikisi, baadae akainua simu na kumpigia rais Hu Jintao wa China, Waliongea kwa mda mrefu yapata dakika 40 hivi, na walikonekana kama hawakubaliana kitu fulani katika mazungumzo yao. Baadae simu ikakatwa,

Akampigia simu Malmo nakumwambia suala hili walifanye kwa siri kubwa asijue mtu yeyote, naaweke maandalizi yawe tayari yeye anajiandaa kuja kulimaliza, kasha akampigia tena simu Hu Jintao na walitumia dakika 16 tu akainuka nakusema, vijana, mwambie SD53 aandae ndege haraka kwa safari ya China,

Gari ya kirai namba T 435 CDR aina ya Landcruiser nyeusi iliingia nakuwabeba watu watatu akiwemo rais Jakaya kuelekea airport, kama dakika 13 ikafika airport, tayari ndege ilishaandaliwa na palikuwa na maafisa watatu, wote tuliingia katika ndege ile isipokuwa yule dereva wa gari ambae aligeza mjini, hiyo ilikwa sasa ni saa 7:43 za usiku.

Tarehe 3, majira ya saa nane za usiku kwa china, tulifika China, hakukuwa na aina ya mapokezi yoyote ya kiserikali, na baada ya kushuka tulimkuta Malmo na msaidizi wake wakitusubiri, Malmo alikuwa tayari ameshaandaa hoteli lakini kulingana na tukio lilivyo tulikubaliana tusilale na tukammwambia mheshimiwa rais amwambie Hu Jintao kuwa ameshafika. Rais alitekeleza hilo na baada ya dakika 15 maafisa watatu wa china walifika nakujitambulisha kuwa wenyeji wetu, wakatuchukua hadi alipo Hu Jintao katika moja ya ikulu ya Hong Kong,

Kikao chao kilichukua masaa manne, na jambo kuu walilokuwa wanakubaliana ni mashariti ya kumuachia, Hu Jintao alihitaji jambo moja tu, kwamba nini serikali ya china itapata kwakumwachia huru Ridhiwani? Kilichomvutia Hu Jintao naakamua muachia Ridhwani ni ahadi ya makubaliano ya Rais Kikwete kuwa ataipa China fursa ya uwekezaji wakudumu kusini mwa Tanzania ambako kumegunduliwa mafuta, gesi, na makaa ya mawe.


Kwakuwa sera ya china kwa sasa ni “Now we are going to Africa”, ilisaidia sana kukubali ombi hilo la jk na kuahidi kuanza utekelezaji kuanzia mwaka 2013

Majira ya saa 11 alfajiri kwa saa za china, Ridhiwani aliletwa akiwa katika gari dogo, nakupokelewa na jk huku wakikumbatiana wote WAKILIA. Jk na Jintao wote kwapamoja wakamuonya sana nakumwambia ameliaibisha taifa la Tanzania, lakini kwakujitetea akasema sio yeye, ila inawezekana yule kijana waliyesafiri wote kutoka Ethiopia ndie mwenye mzigo huo.

Majira ya saa 12 za asubuhi tukaondoka kurudi Tz.
Someni kwa makini hizo sehemu nilizo bold na RED ndio uongo wenyewe wote uko hapo, Jason bourne ni mtu wa kufikirika tu nashangaa kama kuna watu wenye akili timamu wanashindwa kutofautisha hadithi za Willy Gamba na Inside Story.
 
Last edited by a moderator:
si ndiyo wewe unagunaguna ya kwamba siyo kweli fuatilia nyendo zote ya fisadi wenu jk kama siyo kweli urudi na jibu kamili!


quote=elungata;4914156]kama kuna mtu mwenye kumbukumbu kuanzia tarehe 1 july hadi 5 july atuwekee hapa tuone jk alikua wapi tarehe hizo.kumbukumbu kutoka magazetini au threads za tarehe hizo.maana kila rais akiondoka huwekwa uzi hapa.
[/quote]


tarehe hizo fuatilia
  • kulipigwa mabomu pale mwenge na j.kikwete alikuwa na safari ya bagamoyo wenye kiwanja jirani na big bon walifunga barabara ffu walimpitisha salama
  • dr ulimboka alipelekwa afika kusini kwa matibabu
  • ridhiwani alikuwa makaburi ya kinondoni na vijana wa uvccm

 
Kama simu ilipokelewa saa nne usiku wa tarehe 1 july ,tayari china ilikua ni asubuhi ya july3.ukiweka na safari ya kufika china zaidi ya masaa nane.
Process zote pamoja na kurudi dar hio tayari inakua tarehe 4 july
 
Hivi huyo Riz1 mpumbavu kiasi gani ayabebe madawa ya kulevya yeye mwenyewe na asitumie watu wengine?
halafu eti anayapeleka China..kweli Riz 1 ana akili za aina hii? kwa shia gani aliyokuwa nayo hadi a take risk kubwa hivi...? LMAO!!!!!!!!
 
Huyu mtoto ni nani: kwa tetetsi zilizopo Usalama wa Taifa ni Kijana wa Kikwete anayeitwa Miraji Kikwete, ilibidi Jamaa (Rais) aondoke kimya kimya kwenda China kunusuru maisha ya kijana wake.

Next : Dr. Slaa anasema baada ya makubaliano ya kumtoa huyu kijana je Serikali ya China itafaidika vipi na kumwachia huyu kijana,maana sheria zao ni kwamba lazima angeuwawa tu.

Tanzania Daima (27/10/2012)
 
miraji?? daa mbona bado kijana mdogo tu...sie aliepiga kibaha secondary akasepa st patrick arusha\?
 
Wale watoto hawana ujinga huo mnavyowafikiria,kwa vile wako money minded basi kila biashara watafanya,huyo Slaa naye kama hana la kusema akae kimya tu,lile la Uswiss limewa shinda wanataka kutu brain wash huku.Wewe Slaa hebu tutajieni hayo majina basi,tuanze na Drama nyingine!man ake TZ is full of Drama!
 
Huyu mtoto ni nani: kwa tetetsi zilizopo Usalama wa Taifa ni Kijana wa Kikwete anayeitwa Miraji Kikwete, ilibidi Jamaa (Rais) aondoke kimya kimya kwenda China kunusuru maisha ya kijana wake.

Next : Dr. Slaa anasema baada ya makubaliano ya kumtoa huyu kijana je Serikali ya China itafaidika vipi na kumwachia huyu kijana,maana sheria zao ni kwamba lazima angeuwawa tu.

Tanzania Daima (27/10/2012)

Acha uongo, weka link. Siyo wote tunaweza kusoma hardcopy
 
Baada ya kuona whereabout ya riz imekua accounted for tarehe hizo.wanamgeuzia ubao miraji.
Kweli siasa ni mchezo mchafu.
 
miraji huyu huyu au?.

MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete, Miraj Jakaya Kikwete, amekitetea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akipinga chama hicho kuhusishwa na vurugu mbalimbali zinazotokea nchini, zikiwemo zile za Wamachinga, zilizotokea jijini Mbeya hivi karibuni.


Mtoto huyo wa Rais alionyesha kukerwa na watu wenye mtazamo wa kukisingizia chama hicho kikuu cha upinzani kwa kukihusisha na vurugu, wakati hali halisi inaonyesha wazi kuwa wananchi wenyewe hawaridhishwi na hali ya mambo ilivyo na hivyo kuamua kuwa mstari wa mbele kupigania haki zao.


Miraj aliweka wazi msimamo wake huo kupitia mtandao wake wa facebook akichangia mjadala mzito uliohoji kwa nini CHADEMA inasingiziwa vurugu Mbeya?


Mtoto huyo wa Rais, aliweka wazi ujumbe wake huo baada ya mchangiaji mmoja, kuchangia kwa jazba akitabiri machafuko kutokea kabla ya 2015.


Mchangiaji huyo alisema yeye si mtabiri, lakini kwa hali ilivyo nchini, tunaelekea kwenye vita na haina hata mpito wa chaguzi mbili mbele kwa maana ya 2015 na 2020.


Mchangiaji mwingine, Gallus Mpepo, ambaye ndiye aliyekuwa akijadiliana na Miraj, alianza kwa kumrushia lawama Mkuu wa Mkoa mpya wa Mbeya, Abbas Kandoro, kwamba kila mkoa anaokwenda, amekuwa ukikumbwa na vurugu za Wamachinga.


Mpepo alisema anashangaa kuona baadhi ya wachangiaji wa mjadala huo, wanahusisha vurugu za Mbeya na maandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), licha ya kwamba chanzo chake kiko wazi kwamba wafanyabiashara hao walikuwa wakipinga kuondolewa kwenye maeneo yao ya biashara bila kupewa maeneo mbadala.


Alisema hii inatokana na hali ya kutaka kuficha makosa yaliyofanywa na uongozi wa mkoa huo chini ya Kandoro, kutoongoza kwa busara katika kutatua kero za wananchi.


Katika ujumbe huo, Mpepo alieleza kufurahishwa na ujumbe wa mtoto wa Rais Kikwete na kwamba ameupenda ufafanuzi wake kuhusu mjadala huo.


Akichangia mjadala huo, Miraj ambaye ni nadra kujihusisha na masuala ya siasa, alihoji nani anayedai haki Mbeya kati ya CHADEMA na wananchi hadi kusababisha vurugu hizo.


Mtoto huyo wa Rais Kikwete alisema ni makosa kuihusisha CHADEMA na vurugu hizo kwani CHADEMA si nchi.


“CHADEMA si nchi ni chama na si kwamba wanachama wa CHADEMA ndio pekee wenye shida na matatizo, ni Watanzania wote,” alisema mtoto huyo wa Rais.


Miraj alienda mbali kwa kusema ni fikra potofu kufanya kama vile kuna Tanzania na CHADEMA.


“Maana serikali ndiyo Tanzania na CHADEMA ni chama ndani ya Tanzania, ni chama cha Watanzania kwa ajili ya Watanzania, kama kilivyo Chama cha Mapinduzi (CCM), NCCR-Mageuzi na kadhalika.


“Tofauti ni harakati na sera... tupendane Watanzania, tutafika mbali kwa umoja na mshikamano wetu na wala si kwa kejeli na matusi…, wenye haki tuwasimamie wote na penye haki tusimame sote,” alisema Miraj


CHANZO: Tanzania Daima
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom