Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,462
- 21,334
Mtoto wa kigogo ahusishwa tukio la ubakaji hoteli ya KNCU
Daniel Mjema,Moshi
MTOTO wa mfanyabiashara mashuhuri wa mjini Moshi (jina tunalo), ametiwa mbaroni na polisi kwa tuhuma za kuhusika katika tukio la kumlawiti mwanamme mmoja katika hoteli ya KNCU mjini Moshi baada ya kufumaniwa na mke wa mtu.
Mwanaume huyo alilawitiwa na wanaume watano katika chumba namba 53 cha hoteli hiyo baada ya kuwekewa mtego na mume wa mwanamke huyo ambaye pamoja na mkewe nao wameshitakiwa mahakamani.
Mtoto wa mfanyabiashara huyo ambaye ni muuzaji maarufu wa bia na pombe kali za jumla alikamatwa juzi saa 9:00 alasiri na anatarajiwa kuunganishwa na watuhumiwa wengine watano katika kesi hiyo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ngâhoboko jana alithibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo na kueleza kuwa kesho Jumatatu anatarajiwa kufikishwa mahakamani.
"Tulimkamata jana(juzi) saa 9:00 alasiri na tumemwachia kwa dhamana wakati tukikamilisha taratibu za kumuunganisha na washtakiwa wenzake kesho Jumatatu"alisisitiza Kamanda Ng'hoboko.
Watuhumiwa ambao tayari wamefikishwa mahakamani ni pamoja na Kelvine Mushi (32) na mkewe Vaileth Swai (30),na Kassim Mohamed(28), Albeth August (25) na Leon Kimambo(34) wote wakazi wa Mailisita wilayani Hai.
Katika shtaka la kwanza, upande wa mashtaka ukiongozwa na wakili wa serikali,Hellen Moshi ulidai mahakamani kuwa washtakiwa hao watano walikula njama na kufanikisha kulawitiwa kwa mwanaumme huyo.
Katika shtaka la pili, washtakiwa wanne ukimwondoa Vaileth, wanatuhumiwa kuwa Desemba 16,2009 saa 12:00 jioni, walitenda kosa la kumlawiti mwanaume huyo.
Washtakiwa hao walikanusha mashtaka hayo na waliachiwa kwa dhamana ya wadhamini wawili kila mmoja ambao walitakiwa kusaini hati ya dhamana ya Sh2 milioni au kuwasilisha hati za mali isiyohamishika.
Habari zaidi zinadai kuwa kufumaniwa kwa mwanamume huyo kulitokana na mume wa mwanamke huyo kukamata simu ya mkewe na kuishikilia kwa siku na kuwasiliana na mwanamume huyo huku akijifanya ni mwanamke huyo.
Mwanamume aliyetendewa unyama huo alipoteza fahamu katika purukushani za kupambana na watuhumiwa hao wasimkate uume wake na alipozinduka ndipo aliposhangaa amezungungwa na polisi na wafanyakazi wa hoteli hiyo
Daniel Mjema,Moshi
MTOTO wa mfanyabiashara mashuhuri wa mjini Moshi (jina tunalo), ametiwa mbaroni na polisi kwa tuhuma za kuhusika katika tukio la kumlawiti mwanamme mmoja katika hoteli ya KNCU mjini Moshi baada ya kufumaniwa na mke wa mtu.
Mwanaume huyo alilawitiwa na wanaume watano katika chumba namba 53 cha hoteli hiyo baada ya kuwekewa mtego na mume wa mwanamke huyo ambaye pamoja na mkewe nao wameshitakiwa mahakamani.
Mtoto wa mfanyabiashara huyo ambaye ni muuzaji maarufu wa bia na pombe kali za jumla alikamatwa juzi saa 9:00 alasiri na anatarajiwa kuunganishwa na watuhumiwa wengine watano katika kesi hiyo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ngâhoboko jana alithibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo na kueleza kuwa kesho Jumatatu anatarajiwa kufikishwa mahakamani.
"Tulimkamata jana(juzi) saa 9:00 alasiri na tumemwachia kwa dhamana wakati tukikamilisha taratibu za kumuunganisha na washtakiwa wenzake kesho Jumatatu"alisisitiza Kamanda Ng'hoboko.
Watuhumiwa ambao tayari wamefikishwa mahakamani ni pamoja na Kelvine Mushi (32) na mkewe Vaileth Swai (30),na Kassim Mohamed(28), Albeth August (25) na Leon Kimambo(34) wote wakazi wa Mailisita wilayani Hai.
Katika shtaka la kwanza, upande wa mashtaka ukiongozwa na wakili wa serikali,Hellen Moshi ulidai mahakamani kuwa washtakiwa hao watano walikula njama na kufanikisha kulawitiwa kwa mwanaumme huyo.
Katika shtaka la pili, washtakiwa wanne ukimwondoa Vaileth, wanatuhumiwa kuwa Desemba 16,2009 saa 12:00 jioni, walitenda kosa la kumlawiti mwanaume huyo.
Washtakiwa hao walikanusha mashtaka hayo na waliachiwa kwa dhamana ya wadhamini wawili kila mmoja ambao walitakiwa kusaini hati ya dhamana ya Sh2 milioni au kuwasilisha hati za mali isiyohamishika.
Habari zaidi zinadai kuwa kufumaniwa kwa mwanamume huyo kulitokana na mume wa mwanamke huyo kukamata simu ya mkewe na kuishikilia kwa siku na kuwasiliana na mwanamume huyo huku akijifanya ni mwanamke huyo.
Mwanamume aliyetendewa unyama huo alipoteza fahamu katika purukushani za kupambana na watuhumiwa hao wasimkate uume wake na alipozinduka ndipo aliposhangaa amezungungwa na polisi na wafanyakazi wa hoteli hiyo