Mtoto wa kiafrika-abuse, mila au mazoea?

Kana-Ka-Nsungu

JF-Expert Member
Oct 4, 2007
2,257
353
Naukumbuka msiba wa babu,wakati wa kula ulipowadia,
Sinia la ugali mkubwa, bakuli la mboga pembeni
Wanaume kumi wamelizungunguka,mtoto mimi peke yangu,
Bakuli la maji ya kunawa lawadia.Ile nataka nawa tu,"Mtoto wa nani huyu asiye na adabu? subiri wakubwa wanawe" aling'aka mmoja wa wazee.Hadi bakuli lanifikia,maji yalishakua meusiiii!! Kama hiyo haitoshi,nataka kuokota nyama zee jingine lanidaka mkono-"subiri wakubwa waokote kwanza", mtumee-hadi zamu yangu inawadia,mifupa mitupu!

Vichapo, vichapo, vichapo, si nyumbani si shuleni.
Wazazi wananichapa eti kwa kuwa nacheza mpira,wangenisupport enzi zile saa hizi si ningekua Madrid?
Hawataki nicheze, wanataka nisome,nioshe vyombo, nifue na kudeki, jumamosi na jumapili twende shamba tukalime-si ndio child labour hii wazungu wanaita?

Walimu nao -nikikosa namba asubuhi- viboko.Mbona hawaniulizi sababu, jana usiku nimekaa hadi saa 6, wazazi hawajasema kitu!Nikiwa mchafu kwenye ukaguzi-viboko, ntakuaje msafi wakati dingi hela ya soap hakuacha?.7 X 7 nikijibu 40- viboko, kwani ndo vitanipa majibu?labda nilikua dyslexic? halafu wakati wa brake saa 4 wenzangu wacheza ,mwalimu nanihii bila haya, aniomba nimuuzie mandazi na vitumbua vyake!

Jirani naye yumo, kampira kangu ka matambara na vipande vya godoro, nimekasuka kwa kamba ya manila na kukavisha sox-kanadunda kwelikweli,masaa karibu mawili metumia. Shuti la kwanza tu, boom-kametua bustanini kwake, mamaaa-bila huruma kakatia moto!Siku ingine basi hata siri asinifanyie, viboko vya bure kanisababishia -ndio nini kumuambia mama kuwa nimekula kwake wakati nilimuambia kuwa nimekatazwa na asiseme?

Serekali nayo haikuwa nyuma. Nanusurika kugongwa na gari kwa kucheza mpira barabarani, eneo langu lililotengwa kwa kuchezea wameliuza kwa mwarabu. Naumwa malaria, hospitali dawa hakuna, thanks to mkwinini lakini shubiri yake unaijua? Tofali ndio dawati langu, chini ya mwembe darasa langu- baba si aliniambia kodi analipa na hii ndo kazi yake?

Maskini mimi mtoto wa kiafrika, nina mengi ya kulalama, natamani ningezaliwa ng'ambo ambapo kero zote hizi waziita Child Abuse.

Kana-Ka-Nsungu
 
Machozi yamenitoka maana hakuna hata moja halikunigusa wakati huo nikiwa Primary. Nakumbuka nilikataa kwenda secondary ya Day kwa sababu ya kuepuka kuendelea hizo kero thanks God nilienda shule ya Boarding
 
Machozi yamenitoka maana hakuna hata moja halikunigusa wakati huo nikiwa Primary. Nakumbuka nilikataa kwenda secondary ya Day kwa sababu ya kuepuka kuendelea hizo kero thanks God nilienda shule ya Boarding

Thanks God nilifaulu darasa la saba nikaenda sekondari, na enzi hizo kufaulu ilikua mbinde kichizi, kuna miaka shule ilikua haifaulishi hata mtoto mmoja! Hata mimi nipoenda sekondari kidogo kero zikapungua lakini napo jembe, kufagia na kudeki,kuchanja kuni na viboko ilikua kama kawa!
 
Machozi yamenitoka maana hakuna hata moja halikunigusa wakati huo nikiwa Primary. Nakumbuka nilikataa kwenda secondary ya Day kwa sababu ya kuepuka kuendelea hizo kero thanks God nilienda shule ya Boarding

I should have said "pole" kwako Bowbow, nilikamiss hako kajipart mwanzoni- Pole sana, najua haya ni mengi ambayo wengi tuliotokea familia za chini yanatugusa.
 
hahahaahahah mzee haiwezekani kwanini unasimulia maisha yangu?
Haiwezekani mkuu hii umenikopi tuu maisha yangu. Basi nakumbuka nilimwekea mtoto wa mwalimu kioo chini ya miguu yake nakuambia kama ni kuchapwa hiyo ndio ilikuwa funga kazi kwanza nilipiga magoti kwenye changarawe hati nikatoka damu.Maskini kasichana kenyewe kalikuwa hakajui kumbe nilikuwa nakapenda.Si unajua ukiwa na GF mtoto wa mwalimu ni ujiko? maana ndie msichana pekee anayevaa viatu tena vya chacha. Zilikuja kanda mbili za SKYWAY basi ukiwa unacheza mpira inabidi uzivae mikonono ili wajanja wasiibe. Duh kweli Mtoto waafrica!
 
hahahaahahah mzee haiwezekani kwanini unasimulia maisha yangu?
Haiwezekani mkuu hii umenikopi tuu maisha yangu. Basi nakumbuka nilimwekea mtoto wa mwalimu kioo chini ya miguu yake nakuambia kama ni kuchapwa hiyo ndio ilikuwa funga kazi kwanza nilipiga magoti kwenye changarawe hati nikatoka damu.Maskini kasichana kenyewe kalikuwa hakajui kumbe nilikuwa nakapenda.Si unajua ukiwa na GF mtoto wa mwalimu ni ujiko? maana ndie msichana pekee anayevaa viatu tena vya chacha. Zilikuja kanda mbili za SKYWAY basi ukiwa unacheza mpira inabidi uzivae mikonono ili wajanja wasiibe. Duh kweli Mtoto waafrica!
Duu MWK kumbe hizo za kioo nawe ulikua nazo? Mimi nilikua nikishawawekea kioo bila wao kujua badae tukiwa tumekaa kwenye dawati,najidai "Unajua mi ni mwana mazingaombwe? (Eyeso Magic Show),Nikuambie leo umevaa chupi ya rangi gani?" Basi nikiwatajia wanashangaa kichizi!Kandambili za katambuga nikua naziweka mkononi wakati tunakimbia kuwahi namba!
 
Now that im in 'majuu' ndio nagundua kwamba I survived a great deal of abuse from my parents, my childhood was absolutely sh.t!My parents never put me into bed, no story book was ever read to me before I slept, I had to make my own playing toys, I got zero support from them on my hobbies, my opinion was never sought or listened to when there was any issue envolving me.
 
Now that im in 'majuu' ndio nagundua kwamba I survived a great deal of abuse from my parents, my childhood was absolutely sh.t!My parents never put me into bed, no story book was ever read to me before I slept, I had to make my own playing toys, I got zero support from them on my hobbies, my opinion was never sought or listened to when there was any issue envolving me.
Same to me, sometime i get angry why the did it to me like that, . Just imagine, if you had to live with African foster mother. Okey all in all "Kama Ulikuwa Unakojoa Kitandani", every body will know, neighbours, your classmtes, when you woke up, Your breakfast is sticks, then you have to carry around 10kg of mattress outside plus abusive languages, shit,beotch. Most of time when i remember those days tears start to come from my eyes
 
KKN
fimbo/mboko za walimu zilikuwa hatari. mimi nilibahatika kuachwa kuchapwa nilipokuwa STD V, kwani ilitokea nilichapwa hadi kupoteza fahamu kwa ajili ya 'kupiga kelele darasani'.

Lakini hadi leo mtoto wa kitanzania ambaye yuko kijijini bado anateseka, anasumbuka? inawezekana akaja kuvumbua kitu katika mazingira hayo??

Mtoto wa TANZANIA,
....ni work force katika familia,
....ni asset ya baadae kwa wazazi.

Anakuwa abused na hakuna wa kumtetea, wanomtendea hayo wao hawajui kama wanafanya makosa, kwani na wao wamerithi kutoka kwa babu zao.

Vijijini
Bado wanafanyishwa kazi mashambani kabla ya kwenda shule.
Bado wanatembea muda mrefu kufata elimu.
Bado hawapatiwi kifungua kinywa wakati wanakwenda shule.
Bado wakirudi nyumbani wanafanya kazi za ziada ikiwepo ufata maji umbali mrefu, n.k
Hawapati muda wa kucheza na kujifunza.
Watoto wakike wanaolewa wakiwa bado awdogo.

IGNORANCE!!! is a serious problem.
 
Naukumbuka msiba wa babu,wakati wa kula ulipowadia,
Sinia la ugali mkubwa, bakuli la mboga pembeni
Wanaume kumi wamelizungunguka,mtoto mimi peke yangu,
Bakuli la maji ya kunawa lawadia.Ile nataka nawa tu,"Mtoto wa nani huyu asiye na adabu? subiri wakubwa wanawe" aling'aka mmoja wa wazee.Hadi bakuli lanifikia,maji yalishakua meusiiii!! Kama hiyo haitoshi,nataka kuokota nyama zee jingine lanidaka mkono-"subiri wakubwa waokote kwanza", mtumee-hadi zamu yangu inawadia,mifupa mitupu!

Vichapo, vichapo, vichapo, si nyumbani si shuleni.
Wazazi wananichapa eti kwa kuwa nacheza mpira,wangenisupport enzi zile saa hizi si ningekua Madrid?
Hawataki nicheze, wanataka nisome,nioshe vyombo, nifue na kudeki, jumamosi na jumapili twende shamba tukalime-si ndio child labour hii wazungu wanaita?

Walimu nao -nikikosa namba asubuhi- viboko.Mbona hawaniulizi sababu, jana usiku nimekaa hadi saa 6, wazazi hawajasema kitu!Nikiwa mchafu kwenye ukaguzi-viboko, ntakuaje msafi wakati dingi hela ya soap hakuacha?.7 X 7 nikijibu 40- viboko, kwani ndo vitanipa majibu?labda nilikua dyslexic? halafu wakati wa brake saa 4 wenzangu wacheza ,mwalimu nanihii bila haya, aniomba nimuuzie mandazi na vitumbua vyake!

Jirani naye yumo, kampira kangu ka matambara na vipande vya godoro, nimekasuka kwa kamba ya manila na kukavisha sox-kanadunda kwelikweli,masaa karibu mawili metumia. Shuti la kwanza tu, boom-kametua bustanini kwake, mamaaa-bila huruma kakatia moto!Siku ingine basi hata siri asinifanyie, viboko vya bure kanisababishia -ndio nini kumuambia mama kuwa nimekula kwake wakati nilimuambia kuwa nimekatazwa na asiseme?

Serekali nayo haikuwa nyuma. Nanusurika kugongwa na gari kwa kucheza mpira barabarani, eneo langu lililotengwa kwa kuchezea wameliuza kwa mwarabu. Naumwa malaria, hospitali dawa hakuna, thanks to mkwinini lakini shubiri yake unaijua? Tofali ndio dawati langu, chini ya mwembe darasa langu- baba si aliniambia kodi analipa na hii ndo kazi yake?

Maskini mimi mtoto wa kiafrika, nina mengi ya kulalama, natamani ningezaliwa ng'ambo ambapo kero zote hizi waziita Child Abuse.

Kana-Ka-Nsungu

Kana ka Nsungu
Kwa kuongezea ni kwamba wakati unajaribu kuopoa kipande cha nyama, Mzee mmoja anakushikilia mkono na kukunyang'anya kile kipande na anafyonza mchuzi wote katika kipande kile kisha kukupatia nyama ikiwa kavu kabisa. Tatizo si hilo ila huyu Mzee ukimuangalia meno yake hajawahi kupiga mswaki tangu uhuru may be halafu akafyonza mchzi katika kipande cha nyama uliyotaka ule, hapo usalama wako upo??? TB, infection mbali mbali za bacteria wa meno kwa 100% utegemee. Nikikumbuka machozi yanajitokea yenyewe, it was dark era!!! Anyway tusahau ila imenigusa sana. Asante Kana
 
Same to me, sometime i get angry why the did it to me like that, . Just imagine, if you had to live with African foster mother. Okey all in all "Kama Ulikuwa Unakojoa Kitandani", every body will know, neighbours, your classmtes, when you woke up, Your breakfast is sticks, then you have to carry around 10kg of mattress outside plus abusive languages, shit,beotch. Most of time when i remember those days tears start to come from my eyes

Umenikumbusha 'kindumbwendumbwe chalia', yaani mtoto anavishwa matambara na kufungwa makopo na kuzungungushwa mitaani huku watoto wenzie wakimzomea ili asikojoe kitandani tena,ina maana madingi zetu walikua hawajui kuwa huu ni ugonjwa?
 
Kana ka Nsungu
Kwa kuongezea ni kwamba wakati unajaribu kuopoa kipande cha nyama, Mzee mmoja anakushikilia mkono na kukunyang'anya kile kipande na anafyonza mchuzi wote katika kipande kile kisha kukupatia nyama ikiwa kavu kabisa. Tatizo si hilo ila huyu Mzee ukimuangalia meno yake hajawahi kupiga mswaki tangu uhuru may be halafu akafyonza mchzi katika kipande cha nyama uliyotaka ule, hapo usalama wako upo??? TB, infection mbali mbali za bacteria wa meno kwa 100% utegemee. Nikikumbuka machozi yanajitokea yenyewe, it was dark era!!! Anyway tusahau ila imenigusa sana. Asante Kana

Yaaakhhhh!! lol!
 
KKN
fimbo/mboko za walimu zilikuwa hatari. mimi nilibahatika kuachwa kuchapwa nilipokuwa STD V, kwani ilitokea nilichapwa hadi kupoteza fahamu kwa ajili ya 'kupiga kelele darasani'.

Lakini hadi leo mtoto wa kitanzania ambaye yuko kijijini bado anateseka, anasumbuka? inawezekana akaja kuvumbua kitu katika mazingira hayo??

Mtoto wa TANZANIA,
....ni work force katika familia,
....ni asset ya baadae kwa wazazi.

Anakuwa abused na hakuna wa kumtetea, wanomtendea hayo wao hawajui kama wanafanya makosa, kwani na wao wamerithi kutoka kwa babu zao.

Vijijini
Bado wanafanyishwa kazi mashambani kabla ya kwenda shule.
Bado wanatembea muda mrefu kufata elimu.
Bado hawapatiwi kifungua kinywa wakati wanakwenda shule.
Bado wakirudi nyumbani wanafanya kazi za ziada ikiwepo ufata maji umbali mrefu, n.k
Hawapati muda wa kucheza na kujifunza.
Watoto wakike wanaolewa wakiwa bado awdogo.

IGNORANCE!!! is a serious problem.

Sasa Kasana unadhani nini kifanyike ili tuwaokoe wadogo zetu, haswa wale waliopo vijijini ambao hadi leo hii wanaendelea kuteswa na hizi mila na mazoea ya kishenzi?
 
After long time abroad i come across with one short minded person, claiming that, Europeans, Asian etc don't know how to manner their kids, i asked him why?, then his response was
"They don't bit punish them heavenly when they do something wrong, their very week,they don't do home activities like farming etc"
My response to him was, punish doesn't help it creates more cruel human, it is abuse, but he refuted 100 time, then i realized how far we are from human rights and children rights
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom