EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Mtoto wa aliyekuwa mgombea wa ubunge jimbo la Ulanga marehemu Celine Kombani ameshinda kura ya maoni ndani ya chama chake CCM hivyo kumrithi mama yake kugombea ubunge kupitia chama chake CCM.
===============================
Chanzo: Mtembezi
===============================
MOROGORO
HATIMAYE mtoto wa marehemu Selina Kombani ndiye ameibuka mshindi katika kura za maoni za kuwania nafasi ya ubunge katika Jimbo la Ulanga Mashariki kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM.
ambaye ni mtoto wa Kombani wa kwanza aliibuka katika uchaguzi wa kura za Maoni wa CCM uliofanyika jana katika jimbo hilo , nafasi ambayo iligombewa na watu 8.
Akitangaza matokea hayo msiamamizi wa uchaguzi huo, Hamza Mfaume amesema Gooluck aliibuka kidedea kwa kupata kura 731, akifutiwa na Azizi Jawadi aliyepata kura 134, Thabit Dokodoko kura 52, Agustino Matefu kura 41, Wencheslous Ikumla kura 39, Pontian Kipao kura 11, Herrieth Mwakifulefule 9 na Daud Kitolelo 8.
Mfaume amesema katika uchaguzi huo jumla ya kura zilikuwa 1029 , ambapo kura zilizoharibika zilikuwa 4 ambapo kura halali zilikuwa 1025.
Goodluck amewashukuru wananchi wa jimbo hilo kwa kumpa kura nyingi, na kuwaahidi atatekeleza yote ambayo ameahidi na hata yale aliyoahidi marehemu mama yake enzi za uhai wake.
Amesema akipata ridhaa ya kuongoza jimbo hilo atahakikisha anaboresha huduma za Afya, barabara ,mawasiliano simu, elimu na makazi hususani nyumba za walimu.
'' Wananchi wa Ulanga wamenipa ridhaa hii kwa sababu muda kampeni zote za kura za maoni wakati mama akigombea nilikuwa nafanya mimi, nawajua watu kwa sura na majina, na wao wananijua hata utendaji wangu wa kazi''
Amesema atahakikisha analitendea haki jimbo hilo kwa kufanya kazi kwa kasi kubwa zaidi kwa kuzingatia yeye ni kijana na anamudu kasi hiyo.
Marehemu Celina Kombani,alifariki mnamo Tarehe 24/09,nchini India ambapo alikuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa Saratani ya Kongosho,alikuwa mgombea Ubunge katika Jimbo la Ulanga Mashariki.
Kombani aliongoza jimbo la Ulanga kwa vipindi viwili mfululizo tangu mwaka 2005 hadi 2015, sambamba na hilo aliwahi kuwa mwenyekiti wa umoja wa wanawake Tanzania UWT wilaya ya Morogoro mjini kabla ya kushika wadhifa wa ubunge.
Chanzo: Mtembezi