PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,723
Nimeshuhudia kituko leo ofisini.
Ofisi yangu ina Makao Makuu huko Dar, na huko ndo aliko Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni. Bosi wangu mimi ni Meneja wa Idara hapa Mkoani.
Leo hapa ofisini amepita mtoto wa huyo Mkurugenzi, binti mdogo wa miaka 20, ambapo alikuwa tu ana mambo yake binafsi maeneo haya!
Ajabu, bosi wangu, pamoja na difference ya umri ya miaka almost 35 na hako kabinti, ameacha kazi zake, amempokea mabegi na kuanza kumuulizia shida yake hapo kwa nia amsaidie yeye personally!
Tumejaribu kumsaidia huyu mkuu ili arudi kwenye kazi zake, wapi bana...ni kwamba amechanganyikiwa jumla,anapanda na kushuka kwenye ngazi kwa kukimbia. Leo ndo nimemwona mkuu wangu huyu kwa mara ya kwanza anakimbia, bila kujali umri wake!
Sijui ndo nini, mi sielewi. Au ndo ile wanaita nidhamu ya woga, sasa ina'apply hadi kwa mtoto wa bosi?
Angekuwa Kihiyo ningesema labda analinda ajira yake, lakini ni msomi mzuri!
Embu wanajamvi nisaidieni, hii ni behavior gani mahala pa kazi?
Ofisi yangu ina Makao Makuu huko Dar, na huko ndo aliko Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni. Bosi wangu mimi ni Meneja wa Idara hapa Mkoani.
Leo hapa ofisini amepita mtoto wa huyo Mkurugenzi, binti mdogo wa miaka 20, ambapo alikuwa tu ana mambo yake binafsi maeneo haya!
Ajabu, bosi wangu, pamoja na difference ya umri ya miaka almost 35 na hako kabinti, ameacha kazi zake, amempokea mabegi na kuanza kumuulizia shida yake hapo kwa nia amsaidie yeye personally!
Tumejaribu kumsaidia huyu mkuu ili arudi kwenye kazi zake, wapi bana...ni kwamba amechanganyikiwa jumla,anapanda na kushuka kwenye ngazi kwa kukimbia. Leo ndo nimemwona mkuu wangu huyu kwa mara ya kwanza anakimbia, bila kujali umri wake!
Sijui ndo nini, mi sielewi. Au ndo ile wanaita nidhamu ya woga, sasa ina'apply hadi kwa mtoto wa bosi?
Angekuwa Kihiyo ningesema labda analinda ajira yake, lakini ni msomi mzuri!
Embu wanajamvi nisaidieni, hii ni behavior gani mahala pa kazi?