Katika kudhirisha kuwa sasa CCM imechokwa leo juzi mtoto wa balozi wa CCM kata ya Mjimwema Njombe aliamua kuchoma bendera ya CCM kwa imani kuwa chama hicho ndicho kimesababisha mgomo wa walimu na yeye kukosa fursa ya kupata masomo wakati huu wa mgomo wa walimu.Mtoto huyo ni darasa la saba na anayetarajia kufanya mtihani wa kumaliza shule mwaka huu.Baada ya kufanya tendo hilo mama yake mzazi ambaye alikuwa balozi mpya wa CCM aliamua kujisalimisha kwenye mkutano wa CHADEMA na kuchukua kadi ya CHADEMA mbele ya mwenyekiti wa vijana Taifa aliyefanya ziara hapa Njombe.Tukio hili limeleta hamasa kubwa kwa wananchi wa Njombe kwa uamsho mpya toka kwa watu ambao zamani wasingewezA kufanya hivyo.