kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 266
Mwana mdogo wa kiume wa kiongozi wa Libya Muammar Gadafi jana alijiunga na wananchi wanaoandama kuupinga utawala wa baba yake huko magharibi mwa nchi hiyo. Ripoti zinaarifu kuwa Saif al Arab mwana mdogo wa kiume wa Gaddafi ambaye alitumwa na baba yake kushirikiana na vikosi vya usalama kuyakandamiza maandamano ya wananchi wanaopigania demokrasia huko Libya jana alijiunga kwenye maandamano huku akidokeza kuwa baba yake huenda akajiuwa au kukimbilia Amerika ya Latini. Hadi kufikia sasa Walibya wasiopungua elfu moja wameuwa na vikosi vya Gadafi. Aidha jumla ya askari jeshi 130 wameuawa huko Libya kwa kukataa kwao kuwafyatulia risasi waaandamanaji.
Huku hayo yakiripotiwa balozi wa Libya nchini Jordan amejiuzulu wadhifa wake huo katika kupinga ukandamizaji na utumiaji nguvu unaofanywa na vikosi vya Gaddafi dhidi ya wafanya maandamano nchini humo. Mohammad Hassan Barghathi ametangaza kujiuzulu wadhifa wa ubalozikutokana na matukio yanayojiri sasa huko Libya.
Mtoto mdogo wa kiume wa Gadafi ajiunga na maandamano ya wananchi
Huku hayo yakiripotiwa balozi wa Libya nchini Jordan amejiuzulu wadhifa wake huo katika kupinga ukandamizaji na utumiaji nguvu unaofanywa na vikosi vya Gaddafi dhidi ya wafanya maandamano nchini humo. Mohammad Hassan Barghathi ametangaza kujiuzulu wadhifa wa ubalozikutokana na matukio yanayojiri sasa huko Libya.
Mtoto mdogo wa kiume wa Gadafi ajiunga na maandamano ya wananchi