Mtoto haramu katika familia

Kuna rafiki yangu wakat tupo sekondari Mzee mmoja jiran yao alimfata akamwambia ww ni mtoto wangu nilimpa mimba mama yako jamaa alimind kichz
 
Mbuutananga ila kuna kapasenti kaukweli hasa wale wazee wa zamani walilea sana watoto wa mtaa wapili unakuta mama mweupee baba mweupeee watoto wa mwanzo mwanzo huko weupeee anatokea mtumbili au mmoja mweusi tiii hapa sasa ndio kichwa kinapata moto.
Heshima kwa kila mmoja

Inafahamika wazi mama ndiye anayejua baba halisi wa mtoto..

Kutokana na uhalisia huo, watu wengi wamekuwa na maswali yasiyo na majibu ya moja kwa moja..mfano

1. Unaweza ukakuta familia ina watoto 5, wamesoma na wana kazi nzuri tu..ila Kuna mmoja haendani kabisaa na wenzake...yeye ana tabia za kipekee..hamtii mzee wake wala mama yake, wala ndugu zake....yaani ni pasua kichwa..

Hapa nina maanisha unaweza ukakuta watoto 4 ni wapole, wasikivu na wanasikilizana ila huyo mmoja ni pasua kichwa....hawa 4 wanabaki na maswali, Je inakuwa ndugu yetu hafanani na sisi kitabia..?

2.Mnaweza mkawa kwenye kikao cha famili, huyu ndugu mmoja hawaachi mfikie muafaka mzuri lazima atawavuruga tu....si kosa lake...mama anajua siri.

3.Baba anaweza akawa anaumwa, kalazwa hospitali ndugu wote mpo bega kwa bega kumuuguza baba, huyu ndugu mmoja yeye hana time....tena wakati mwingine msishangae kusikia akiwaambia mzee kashazeeka...inatakiwa arest in peace atuachie mali...mnajiuliza huyu kalogwa, hampati majibu...

4.Huyu ndugu mmoja pamoja na ukorofi na tabia zake mbaya , unakuta mama anampenda sana na anamtetea sana haswa kwenye swala la kupewa mali...mnajiuliza mbona sisi tunajitoa hivi lakini mama hatukingii kifua namna hii..?

%%%%%% Majibu ya haya maswali 4 ni marahisi...Mara nyingi mtoto wa namna hiyo huwa ni mtoto haramu katika familia...yaani si damu moja na ndugu zake..

Kuna Mila na desturi za makabila fulani fulani hapa nchi mwanamke anafundwa vilivyo.

Wanawake hao huwa wanafundishwa kuwa akiingia kwenye ndoa, asizae watoto wote na mume mmoja.. mtoto mmoja au wawili anafundishwa azae na baba mwingine.

Lengo na mafundisho haya lilikuwa ni kama ifuatavyo.

1. endapo ukoo wa mume wa ndoa una laana fulani, asili ya wizi, magonjwa ya kurithi kama kifafa, kuna uwezekano mkubwa watoto wa baba huyo wakarithi matataizo hayo.

Hivyo mama hutafuta mwanaune mwingine kwa siri kubwa, anazaa naye ili kupata mtoto mmoja wa kukomboa wenzake endapo matatizo niliyoyaeleza yatatokea..

Jambo hili hufanyika kwa siri kubwa na wamama wafundaji wanajua wazi kuwa mtoto wa 3 kuzaliwa si wafulani..

Wanawake huwa hawana desturi ya kutunza siri, lakini kwa hili, hata umchome na mshale wa moto jichoni, hatasema siri hii....yupo radhi afe.

Lakini yale maswali 4 ya mwanzo yanaweza yakaja kinyume, watoto wakazaliwa 5 , watoto 4 wakawa na tabia mbaya zisizovumilika, wizi, ugomvi, ulevi, umalaya, hawataki kazi wao ni kumtesa mzee awape pesa za kula bata, ila huyu mtoto mmoja akawa smart, mpole, msikivu, mchapakazi, yaani baba ndiyo akawa anamtegemea hata kumrithisha biashara zake...maskini kumbe si damu yake..

Lakini ukweli ni kwamba hapa tunasema mama aliona ameolewa na zuzu, mume ambaye dish lineyumba, hivyo akatafuta mwanaune wa kweli, akazaa naye kwa siri ,....baba ukalea ukijua ni mwanao...kumbe ni damu ya ukoo mwingine..

Mama atajitahidi sana kumsihi mzee amwandikie mtoto huyu mali nyingi zaidi...coz mama anajua siri.

Mtoto wa namna hii ndiyo hawa tunawaita watoto haramu katika familia, ...anaweza akawa mbaya au akawa mzuri.....il hatafanana na wenzake hata kidogo...

Mwisho....usijeukashangaa kwenu kuna ndugu mmoja anawatesa balaa, rangi hata hamfanani...baba ameshamchoka ila mama uenu haachi kuwasihi, msimchukie ndugu yenu.....Kachukua tabia za mjomba wake wa Sumbawanga....hakuna cha Sumbawanga..baba ni wa mtaa wa pili hapo....trust me.

NB...wanaume tuamke hawa wanawake wanatuzidi kete






View attachment 1181121
 
Mbuutananga ila kuna kapasenti kaukweli hasa wale wazee wa zamani walilea sana watoto wa mtaa wapili unakuta mama mweupee baba mweupeee watoto wa mwanzo mwanzo huko weupeee anatokea mtumbili au mmoja mweusi tiii hapa sasa ndio kichwa kinapata moto.
Yaani hiki ulichokiongea nakiona hapa jirani.....me si msemaji wa hiyo familia nakaa kimya..
 
Aiseeh,
Ila maandiko yanatutia moyo kuwa "SISI SOTE NI NDUGU" kwakua wote tumetoka kwenye DNA ya babu na bibi yetu Adam na Hawa.
Wahenga pia hawako nyuma kwa faraja kupitia misemo yao "Kitanda hakizai haramu" na pia "mtoto wa mwenzio ni wako".
 
Anaweza akawa amezaliwa na nyinyi pamoja kwa baba na mama mmoja na bado akawa na tabia za ajabu ajabu tu
 
Anaweza akawa amezaliwa na nyinyi pamoja kwa baba na mama mmoja na bado akawa na tabia za ajabu ajabu tu
Anaweza akawa na tabia za ajabu ajabu lakini kuna tabia common mtafanana...anaweza akawa mlevi, mvuta bangi na bado akawa na roho ya utu kama mlivyo ninyi..

Mtoto haramu lazima tu awe tofauti na ninyi...yaani lazima awe kinyume kila kitu
 
Aiseeh,
Ila maandiko yanatutia moyo kuwa "SISI SOTE NI NDUGU" kwakua wote tumetoka kwenye DNA ya babu na bibi yetu Adam na Hawa.
Wahenga pia hawako nyuma kwa faraja kupitia misemo yao "Kitanda hakizai haramu" na pia "mtoto wa mwenzio ni wako".
Ndo maana nakupenda mzee mwenzangu!
 
Kwenye kila familia hawakosekanagi vichaa
Umeandika kama fulani hivii
 
Aiseeh,
Ila maandiko yanatutia moyo kuwa "SISI SOTE NI NDUGU" kwakua wote tumetoka kwenye DNA ya babu na bibi yetu Adam na Hawa.
Wahenga pia hawako nyuma kwa faraja kupitia misemo yao "Kitanda hakizai haramu" na pia "mtoto wa mwenzio ni wako".

Umenichekesha sana
 
Mimi ni wa mwisho kuzaliwa kwa baba,ila kwa mama ni wa kwanza. Baba yangu na mama yangu mkubwa walicheza tofauti kidogo ya hiyo picha. Mama yangu mkubwa yaani mke wa baba. Alimtafutia mzee binti ili amuoea. Zamani wivu ulikuwa sio sawa na sasa. Mzee akamuoa mama yangu mzazi,akiwa binti mdogo kwa umri alikuwa sawa na mtoto wa 4 wa pale home,katika familia yenye watoto 8. Nikazaliwa mimi kwa mke mdogo,na wa mwisho na wa 9,katika uzao wa hapo home. Baadae mama mkubwa kumbe alichotaka ni kupata mtoto wa sample nyingine mbali na wale wa kwake nane. Baada ya kuzaliwa mimi,bi mkubwa akaanza kumtibua tibua mama. Ikabidi mother arudi kwao ksbb ya visa vya mkubwa. Hapo mimi nina mwaka mmoja na nusu. Wakanikatalia nisiondoke na mother,wakati mother anaondoka. Bahati mbaya mzee alifariki mimi nikiwa na miaka miwili. Kwa hiyo nimelelewa na mama mkubwa. Lakini amenielea kama mtoto wake. Nimelelewa hapo,nimekulia hapo. Nimesoma nikiwa hapo. Nimehadithia haya kwa sababu nataka tujue sisi ni wa kupita tu duniani. Mtendee mema yoyote bila kujali ni nani kwako. MUNGU alivyo wa ajabu. MUNGU anakutunzia WEMA wako na kukulipa kwa muda usiodhania. Basi ndugu zangu yaani kaka zangu na dada zangu hawakufanikiwa sana kimaisha. Kati yao ni mmoja tu aliekuwa amefanikiwa,kakaetu mkubwa,yeye alikuwa ni afisa fulani huko Zambia,lakini hakuwa msaada kabisa kwa familia. Unajua mtu akilowea zambia,mpaka kufa kwake alizikwa huko huko,hakutaka kurudi nyumbani,lakini kule alikuwa ni mtu mwenye uwezo. Mimi wa mwisho ndie niliekuja kuinua familia,japo bahati mbaya ndugu zangu wengi wamefariki,nimebaki mimi na,dadaangu wa 6 kuzaliwa. Lakini nimewajengea home. Na hakiwezi kufanyika jambo nyumbani bila mimi. Na hivi naandika haya niko kijijini nimemtembelea mamaangu mkubwa,alinipigia simu anaumwa. Ni mtu mzima,ana miaka 98 mpaka sasa. Busara zake,hekima zake,ndizo zimenijenga mimi. Nakiri wazi nampenda zaidi ya mama yangu. Bahati mbaya umri unataka kumchukua mamaangu mpenzi. Kwa hiyo mtoto wa vinasaba tofauti anaweza akawa msaada. Mpaka hivi sasa mimi ndio nguzo ktk familia yangu na msaada mkubwa kwa mamaangu alienilea kama mwanae. MUNGU ANAKURUDISHIA FADHIRA KWA WAKATI USIOUJUA. MUNGU NI MWEMA WAKATI WOTE
 
Mimi ni wa mwisho kuzaliwa kwa baba,ila kwa mama ni wa kwanza. Baba yangu na mama yangu mkubwa walicheza tofauti kidogo ya hiyo picha. Mama yangu mkubwa yaani mke wa baba. Alimtafutia mzee binti ili amuoea. Zamani wivu ulikuwa sio sawa na sasa. Mzee akamuoa mama yangu mzazi,akiwa binti mdogo kwa umri alikuwa sawa na mtoto wa 4 wa pale home,katika familia yenye watoto 8. Nikazaliwa mimi kwa mke mdogo,na wa mwisho na wa 9,katika uzao wa hapo home. Baadae mama mkubwa kumbe alichotaka ni kupata mtoto wa sample nyingine mbali na wale wa kwake nane. Baada ya kuzaliwa mimi,bi mkubwa akaanza kumtibua tibua mama. Ikabidi mother arudi kwao ksbb ya visa vya mkubwa. Hapo mimi nina mwaka mmoja na nusu. Wakanikatalia nisiondoke na mother,wakati mother anaondoka. Bahati mbaya mzee alifariki mimi nikiwa na miaka miwili. Kwa hiyo nimelelewa na mama mkubwa. Lakini amenielea kama mtoto wake. Nimelelewa hapo,nimekulia hapo. Nimesoma nikiwa hapo. Nimehadithia haya kwa sababu nataka tujue sisi ni wa kupita tu duniani. Mtendee mema yoyote bila kujali ni nani kwako. MUNGU alivyo wa ajabu. MUNGU anakutunzia WEMA wako na kukulipa kwa muda usiodhania. Basi ndugu zangu yaani kaka zangu na dada zangu hawakufanikiwa sana kimaisha. Kati yao ni mmoja tu aliekuwa amefanikiwa,kakaetu mkubwa,yeye alikuwa ni afisa fulani huko Zambia,lakini hakuwa msaada kabisa kwa familia. Unajua mtu akilowea zambia,mpaka kufa kwake alizikwa huko huko,hakutaka kurudi nyumbani,lakini kule alikuwa ni mtu mwenye uwezo. Mimi wa mwisho ndie niliekuja kuinua familia,japo bahati mbaya ndugu zangu wengi wamefariki,nimebaki mimi na,dadaangu wa 6 kuzaliwa. Lakini nimewajengea home. Na hakiwezi kufanyika jambo nyumbani bila mimi. Na hivi naandika haya niko kijijini nimemtembelea mamaangu mkubwa,alinipigia simu anaumwa. Ni mtu mzima,ana miaka 98 mpaka sasa. Busara zake,hekima zake,ndizo zimenijenga mimi. Nakiri wazi nampenda zaidi ya mama yangu. Bahati mbaya umri unataka kumchukua mamaangu mpenzi. Kwa hiyo mtoto wa vinasaba tofauti anaweza akawa msaada. Mpaka hivi sasa mimi ndio nguzo ktk familia yangu na msaada mkubwa kwa mamaangu alienilea kama mwanae. MUNGU ANAKURUDISHIA FADHIRA KWA WAKATI USIOUJUA. MUNGU NI MWEMA WAKATI WOTE
una stori nzuri ya kusisimua...
Lakini nilichojaribu kuzungumza hapa ni pale unakuta mume ana mke moja...mke kwa namnaanayojua yeye au alivyofundishwa kwao, anachepuka..anabeba mimba, then hiyo tarehe aliyobebeshwa mimba anamtegeshea mume wa ndoa...kwa hiyo mume wa ndoa analea akijua ni damu yake...kume mama ana siri nzito..
 
Inawezekana lakini kwa mwanamke ambaye ni malaya ....unakuta zike tarehe za hatari amesex na wanaume kibao tofauti tofauti....tena pengine akiwa amelewa...hapo ni ngumu kubaini baba wa mtoto....ndiyo pale boya analengeshewa anashikishiwa
Siyo mara zote mama huwa anajua baba wa mtoto ni nani. Fact.
 
Back
Top Bottom