Mtoto Anatoka Wapi?

Mhache

JF-Expert Member
Jun 20, 2008
345
24
Swali kuhusu mtoto anatoka wapi huwa linaulizwa na watoto walio wengi. Wanamwuliza baba au mama kwamba mtoto anatoka wapi? Mtoto anayeuliza ni wa miaka mitatu au minne. Naomba mchango kuhusu jibu sahii la kumpa mtoto?
 
Swali kuhusu mtoto anatoka wapi huwa linaulizwa na watoto walio wengi. Wanamwuliza baba au mama kwamba mtoto anatoka wapi? Mtoto anayeuliza ni wa miaka mitatu au minne. Naomba mchango kuhusu jibu sahii la kumpa mtoto?

...anatoka kwa mungu, anamzawadia mama amtakaye.
 
Oooh best way is kumake a story like - mama na baba, wanalala wanaota halafu katika ndoto Mungu anamwekea mama katika tumbo lake ka yai kadogo, halafu kwa miezi tisa, yai linakuwa na baada ya miezi tisa linakuwa mtoto mchanga, wanaenda hospitali daktari anamsaidia mama kumtoa mtoto tumboni, kwa sababu Mungu atamwelekeza daktari...
 
Watoto ni watu wanaotokana na watu...Watu hutokana na MUNGU...Mtu kama mfano wa Mungu hutoka kwa Mungu na Mungu huwapa watu watoto ambao nao pia ni watu mara baada ya majukumu ya ulezi ya watu hao kwa watoto...Watoto ambao mara baada ya kuwa watu...Nao huwa na majukumu ya kuwa na watoto ambao majukumu yao ni kuwafanya wawe watu through malezi bora...The cycle goes on and on....I AND I ni MUHIMU kwa NEXT GENERATION.

NB:Hiyo defintion ya Lady Mzuri nimeikubali at least kwa sasa..Haya tunasubiri na wengine maana issue hii wengine tuliambiwa wanatoka kwa Mungu...Na mara wanatolewa ama kununuliwa hospitali.
 
i do hope some other people will contribute...haya maswali ni real life kabisa, wazazi tusaidiane kujiandaa na majibu yanayoeleweka...na hii mitandao watoto hawachelewi kuingia na kuona live how babies are born..ukaja kuulizwa with details macho yanakutoka!!
 
i do hope some other people will contribute...haya maswali ni real life kabisa, wazazi tusaidiane kujiandaa na majibu yanayoeleweka...na hii mitandao watoto hawachelewi kuingia na kuona live how babies are born..ukaja kuulizwa with details macho yanakutoka!!

Nakubaliana na maelezo yako...Kwasababu sisi tunapenda sana UNAFIKI...NDIO SIFA YETU KUBWA...Sasa kwa wale wakristo...Watoto wanaelezwa wazi kabisa kuwa ni malaika alimtembelea mariam na akamwambia something about kwa uwezo wa Mungu atabeba Mimba..Na imewekwa wazi kabisa kuwa tumbo lake limebarikiwa...Sasa ukimwambia mtoto eti watoto wanatolewa kisimani wakati wa kwenda kuchota maji watakuelewa vipi?
Na ukiwaambiwa kuwa simply..Wametoka kwa Mungu...Watakuuliza tena...Je ni malaika Gabrieli amekuja tena kufanya kazi yake?
Hapo sidhani kama ni possible kwani kila mtu ni Kristo?
Kwa upande wa wenzetu waislam na watu wengine pia lazima na utamaduni wao kama ilivyo kwa jamii nyingine...Je Utamaduni wetu mwafrika unasemaje kuhusu hili suala la watoto wanatoka wapi?
 
My 6yr old daughter has been relentless for the past 2weeks asking this question.We have got to the part anauliza mtoto anaingiaje tumboni kwa mama?Jasho linanatoka mama yake anamwambia mi na kazi kamuulize babako
 
Hee mi nakumbuka wakati nina umri kama huo mama yangu aliniambia pale muhimbili kuna sehemu kuna pool, sasa yeye kama mama alienda pale akakuta katoto kazuri akakapenda akamchukia ambaye ni mimi....... basi nilikuwa nikisikia hivyo nafurahi kweli.... nilikuja jua ukweli nilipokuwa................ ila naona def ya Mchongoma ipo poa kwa mtoto wa miaka kama hiyo
 
Mtoto mwenye uwezo wa kuuliza swali hili anaweza kuambiwa ukweli. Stop insulting children's intelligence by making up some concoctions.The truth is simpler and need no further lies to protect.

Unamwambia tu maumbile ya binadamu yamekuwa kwamba mtu mke na mtu mume wakikutana kuna wakati yai linanawiri tumboni kwa mama na baadaye linakuwa mtoto, akiulizia sana kuhusu "kukutana" huku unampa according to his/ her age kama mdogo sana unamwambia mengine utafundishwa wakati ukifika.

Siku hizi with TV and all watoto wanajua kuliko tunavyofikiri.
 
Swali kuhusu mtoto anatoka wapi huwa linaulizwa na watoto walio wengi. Wanamwuliza baba au mama kwamba mtoto anatoka wapi? Mtoto anayeuliza ni wa miaka mitatu au minne. Naomba mchango kuhusu jibu sahii la kumpa mtoto?

Unaenda kumnunua baharini.
 
My 6yr old daughter has been relentless for the past 2weeks asking this question.We have got to the part anauliza mtoto anaingiaje tumboni kwa mama?Jasho linanatoka mama yake anamwambia mi na kazi kamuulize babako

Jamani kwa utamaduni wetu wa Kitanzania/Kiafrika mtoto mwenye umri huo hastahili kuambiwa process yote ya jinsi mtoto anavyopatikana. Wazazi lazima muwe creative katika kutafuta majibu ya kuwaridhisha watoto wenu. Wakati muwafaka ukifika wa wao kujua jinsi mtoto anavyoingia tumboni basi watafahamu tu.
Mtoto: Baba Mtoto anaingiaje tumboni?
Baba:Mama yako alimeza mtoto wakati wewe umelala
Mtoto: Hawezi kumtafuna?
Baba: Hawezi kumtafuna inabidi ammeze bila kumtafuna
Mtoto: Halafu mtoto atatokaje tumboni?
Baba: Mama ataenda hospitali na madaktari watamsaidia kumtoa mtoto mdomoni au tumboni.
Mtoto: Mama hataumia?
Baba: Anaweza kuumia kidogo.

Miaka ya nyuma watoto wa umri mdogo wala walikuwa hawaambiwi kwamba family inategemea kupata mtoto mwingine. Walikuwa wanamuona mtoto akishazaliwa, lakini siku hizi tumeiga mambo ya kizungu basi hata watoto wadogo wanaambiwa tangu mama ana mimba changa!!!
 
Jamani kwa utamaduni wetu wa Kitanzania/Kiafrika mtoto mwenye umri huo hastahili kuambiwa process yote ya jinsi mtoto anavyopatikana.
Baba:Mama yako alimeza mtoto wakati wewe umelalaMtoto: Mama hataumia?
Baba: Anaweza kuumia kidogo.


Hapo tunajidanganya wenyewe! Leo tunalalamika na mafisadi kuwa wametoka wapi na wanasiasa kuwa ni waongo tunasahau kuwa malezi kam haya ya kuwambia watoto uongo ndiyo yanazaa jamii ya watu tulionao leo,

mwambie mtoto Ukweli, unajua ukimwambia mtoto kwa mfano ukipata maswali yote leo shuleni nitakununulia kigari tulichokiona dukania au kama cha Juma basi akipata nunua, usiseme kitu ambachon huwezi, km ukimwaga hicho chakula nitakuua. Akimwaga utamuua kweli? usipomuua atajua kumbe unaweza kusema jambo usifanye, hakuna shida anakuwa hivyo hivyo. Tusiwaambie watoto wetu malaya Mkubwa eweee kwa kosa la kubamiza mlango tu! Watanzania Bwana.

Hakuna cha mila ya Kitanzania wala ya kizungu chukueni yaliyomazuri ya kweli tufanye bila kisingizio cha mila. Watoto wanastahili ukweli kwa lugha inayoweza kueleweka kwao.
 
Hapo tunajidanganya wenyewe! Leo tunalalamika na mafisadi kuwa wametoka wapi na wanasiasa kuwa ni waongo tunasahau kuwa malezi kam haya ya kuwambia watoto uongo ndiyo yanazaa jamii ya watu tulionao leo,

mwambie mtoto Ukweli, unajua ukimwambia mtoto kwa mfano ukipata maswali yote leo shuleni nitakununulia kigari tulichokiona dukania au kama cha Juma basi akipata nunua, usiseme kitu ambachon huwezi, km ukimwaga hicho chakula nitakuua. Akimwaga utamuua kweli? usipomuua atajua kumbe unaweza kusema jambo usifanye, hakuna shida anakuwa hivyo hivyo. Tusiwaambie watoto wetu malaya Mkubwa eweee kwa kosa la kubamiza mlango tu! Watanzania Bwana.

Hakuna cha mila ya Kitanzania wala ya kizungu chukueni yaliyomazuri ya kweli tufanye bila kisingizio cha mila. Watoto wanastahili ukweli kwa lugha inayoweza kueleweka kwao.
... Marvelous Mbogela, ni muda mfupi tu uliopita nimepita mahali nakuta mama anamshambulia mtoto wake wa kama miaka 6-7 hivi kwa matusi ikabidi niulize ni mtoto wake au wa jirani wenyeji wakasema wake mwenye....Mtoto anaambiwa " we mbwa ukichelewa kurudi nitakupasua kichwa chako muone kwanza miguu kama umefufuka leo".....Nina imani mtoto wa aina hii ukimuongezea na tabi aya uongo kama huo kuwa mtoto ananunuliwa au anamezwa yumkini atakuwa na akili hiyo kuwa uongo ni sehemu ya maisha yetu....Nadhani ni afadhali kuwajibu kwa polite language angalau kuwa mama anapewa mtoto na mungu....inatosha sana kwani ukweli unabaki pale pale hata ukiweka darasa na kumueleza the whole process still na kudra za mwenyezi mungu zinaingia katika kupatika mtoto!!!
 
Matusi kuwatukana sawa, lakini "matusi" ya kuwafundisha baiolojia mwiko!
 
Back
Top Bottom