Mtoto ana haki ya kujua asili yake. Wamama msiwafiche Watoto Baba zao

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,882
MTOTO ANAHAKI YA KUIJUA ASILI YAKE.

Anaandika Robert Heriel.

Hakuna sababu yoyote inayozuia na kumnyima Haki mtoto kuijua Asili yake.

Mtoto lazima amjue Baba yake mzazi,
Mtoto lazima ajulishwe mama yake Mzazi.
Hiyo ni Haki ya Mtoto.

Mtu ili ajitambue lazima atambue asili yake. Mtu ambaye haijui asili yake kamwe hawezi kujitambua, atajitambuaje Kama hajui alipotoka, kumaanisha hajui alipo na Kule anapoenda.

Wazazi hasa wa kike waliofunzwa wakafunzika, wenye maadili na wenye ukike kiasili kamwe hawawezi kumficha mtoto Baba yake hata Kama wangefarakana vipi na Baba Mtoto.

Inawezekana kabisa Mama anaweza kuogopa kumwambia mtoto Bab yake halisi Kwa sababu kadha WA kadhaa, mathalani;
1. Kubakwa
2. Kujamiiana na Ndugu wa karibu, au Baba mzazi au Baba Mkwe.
3. Kufanya umalaya na wanaume wengi Kwa mara moja.
4. Mwanamke kufanyiwa mambo mabaya na Baba Mtoto, hivyo kujenga chuki. Miongoni mwa sababu zingine.

Kimsingi sababu hizo hapo juu na zingine hazimzuii Mama kumuambia Mwanaye Asili yake, asili ya kuzaliwa kwake, mama lazima amwambie mtoto asili yake ikiwa anampenda Kwa dhati yote.

Ingawaje lazima mzazi/Mama aangalie umri sahihi wa kumwambia mtoto wake ili isije ikamuathiri kiakili, kiroho na kihisia.

Mtoto akishakuwa mkubwa mwenye umri wa kutaka kuoa, kuanzisha familia ndio umri sahihi wa kumwambia mtoto Baba yake halisi, ili kuiweka historia yake Sawa pindi aanzishapo ukoo wake.

Umri huo ni umri mkubwa kabisa, mtoto mwenye miaka 25 kuendelea anajielewa, anajua mambo mazuri na mabaya ya Dunia, hivyo kumuambia mtoto asili yake ni ipi hata Kama inaumiza itamsaidia zaidi kuliko kumficha ambapo sio tuu itamuumiza yeye Bali utaumiza mpaka watoto wake(wajukuu zako) na kizazi chake chote.

Mtoto ndio ataamua aendelee na majina yako(upande wa mama) au afuatane na ukoo wa Baba.

Hakuna ubaya mtoto kujua asili yake ni matokeo ya kubakwa Mama yake(zingatia umri wa mtoto hasa akiwa mtu mzima) hakuna ubaya wowote mtoto kujua yaliyotokea.

Ni kweli yanaumiza lakini tuufiche ukweli?
Ukweli haufichwi,
Ukweli ukifichwa unatabia ya kuumiza na kudhalilisha huko mbeleni, ukweli unatabia ya kuumbua watu.

Pesa inanguvu zake lakini kamwe pesa haishindi asili.
Kumsomesha mtoto hakukufanyi mtoto awe wako

Narudia, hakuna sababu yoyote ya kumzuia Mama kumnyima mtoto wake kujua asili yake.
Hapo ni ishu ya Umri tuu WA Mtoto, akishakuwa mtu mzima mtoto aambiwe ukweli hata Kama unaumiza kiasi gani. Huo ndio utuuzima wenyewe
 
Haiwahusu.

Na ni Haki ya Baba kujua mtoto ni wake au kapigwa msumari
Haiwahusu vipi

Sidhani ni sawa kubambikiwa mali sio yako na mtoto kujua ukweli alipotoka

Sema ikitokea nikajua mimba si yangu mama mtu anafosi hata aende serikali za mitaa au polisi kama sio yangu sio yangu tu

Kitanda hakizai haramu ni kauli ya kifala
 
Ni Mwanamke ambaye Mwanaume alivyojua amempa Mimba, akaikataa mimba, hakudiriki kamwe kuilea, na hata kumkataa mwanamke.

Mtoto akazaliwa ,Mama aka endelea kumfata Baba mtoto, amtunze, ampe matunzo mtoto... baba MTU aliendelea kumfukuza na hatimaye Akaoa mwanamke mwingine.

Mama kapambana, kalea, kasomesha, Baba MTU Hataki kujua HABARI za mtoto, na Mara zote anamkataa nakumkana !!

Mama kukomaa,kasomesha, mtoto katusua.

EWE MAMA, WALA USIHANGAIKE KUMJUZA HUYO MTOTO, BABA ZAO WAKO WAPI !!

ACHA KABISA ,.IKIKUPENDEZA TOKA MALEZI, MFUNZO MTOTO KUA ALIKATALIWA, BABA YAKE ALISHAKUFA.
 
Ni Mwanamke ambaye Mwanaume alivyojua amempa Mimba, akaikataa mimba, hakudiriki kamwe kuilea, na hata kumkataa mwanamke.


Mtoto akazaliwa ,Mama aka endelea kumfata Baba mtoto, amtunze, ampe matunzo mtoto... baba MTU aliendelea kumfukuza na hatimaye Akaoa mwanamke mwingine.


Mama kapambana, kalea, kasomesha, Baba MTU Hataki kujua HABARI za mtoto, na Mara zote anamkataa nakumkana !!



Mama kukomaa,kasomesha, mtoto katusua.



EWE MAMA, WALA USIHANGAIKE KUMJUZA HUYO MTOTO, BABA ZAO WAKO WAPI !!

ACHA KABISA ,.IKIKUPENDEZA TOKA MALEZI, MFUNZO MTOTO KUA ALIKATALIWA, BABA YAKE ALISHAKUFA.

Hapo anamkomoa mtoto sio BABA.

Hivyo unataka kusema Baba akimlea Mtoto na Mama asipochangia chochote, Baba amfiche mtoto Mama yake aliyemzaa??

Mafarakano ya wazazi yasiathiri Mtoto,
Na mtoto asiingilie ugomvi wa wazazi hiyo ndio kanuni.
 
kuna lijamaa linatumia ubini wa mama kwa kulishwa maneno mabaya na mama yake.
yeye na mzee wake walikuwa wanaishi mkoa mmoja na hana time nae kbs!
hv ss naandika hapa mzee wake kashafariki.
 
Lkn s vyema kupandkiza chuki kuwa amchukie babayee, ugomv wa mama na baba usmshrkishe mtoto.

Mueleze anayopaswa kuyafahamu tu, "baba yako n mzee Lema, ww n mchaga wa machame, na hii ndyo picha ya baba yako kwa sasa anakaa rombo mashati kisale. Ameoa na anafamilia pale" yatosha s kumuambia ooh alikukataa ukiwa kijus, alinitesa sana hapaana ndyo mana tunaleta kizaz cheny kisas na chuki ndani yake chimbuko la yoote huanzia hapa.

Wamama n watu wny vsas sana, na wanajua kupandkiza chuki s vyema" ooh! Nilibakwa na mzee Mush nikapata mimba yako, niliteseka sanaa" hiyo haimuhusu muambie ww baba yako n mzee Mushi anyekaa pale mtaa wapili huyo ndye baba yako halisi. Inatosha
 
Ni Mwanamke ambaye Mwanaume alivyojua amempa Mimba, akaikataa mimba, hakudiriki kamwe kuilea, na hata kumkataa mwanamke.

Mtoto akazaliwa ,Mama aka endelea kumfata Baba mtoto, amtunze, ampe matunzo mtoto... baba MTU aliendelea kumfukuza na hatimaye Akaoa mwanamke mwingine.

Mama kapambana, kalea, kasomesha, Baba MTU Hataki kujua HABARI za mtoto, na Mara zote anamkataa nakumkana !!

Mama kukomaa,kasomesha, mtoto katusua.

EWE MAMA, WALA USIHANGAIKE KUMJUZA HUYO MTOTO, BABA ZAO WAKO WAPI !!

ACHA KABISA ,.IKIKUPENDEZA TOKA MALEZI, MFUNZO MTOTO KUA ALIKATALIWA, BABA YAKE ALISHAKUFA.
Point.
 
Ni haki ya mtoto kujua asili yake lakini pia ni muhimu haki ya mama ya kukataa kusema asili ya mtoto iheshimiwe. Umeyataja mazingira magumu mfano mtoto ajue baba yake ndo babu yake! Acha aise
 
Lkn s vyema kupandkiza chuki kuwa amchukie babayee, ugomv wa mama na baba usmshrkishe mtoto.

Mueleze anayopaswa kuyafahamu tu, "baba yako n mzee Lema, ww n mchaga wa machame, na hii ndyo picha ya baba yako kwa sasa anakaa rombo mashati kisale. Ameoa na anafamilia pale" yatosha s kumuambia ooh alikukataa ukiwa kijus, alinitesa sana hapaana ndyo mana tunaleta kizaz cheny kisas na chuki ndani yake chimbuko la yoote huanzia hapa.

Wamama n watu wny vsas sana, na wanajua kupandkiza chuki s vyema" ooh! Nilibakwa na mzee Mush nikapata mimba yako, niliteseka sanaa" hiyo haimuhusu muambie ww baba yako n mzee Mushi anyekaa pale mtaa wapili huyo ndye baba yako halisi. Inatosha
 
Back
Top Bottom