Mtoto aliyemuuliza maswali Lowassa matatani

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Yale makuu mliyo hisia kuhusu huyu mtoto yamewadia:

MTOTO aliyemuhoji swali Waziri Mkuu Edward Lowassa, Aron Wambura Shera anadaiwa kuandamwa na maofisa usalama wa taifa wakimhoji kila mara kuhusiana na swali alilouliza.

Habari kutoka kwa ndugu wa karibu wa kijana huyo, ambaye ni mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Pius Msekwa kidato cha kwanza, zimedai kuwa maofisa hao siku hiyo ya mkutano walimfuata mwalimu wake na kumtaka amweleze historia ya kijana huyo.


Akiwa wilayani Ukerewe katika ziara, mwanafunzi huyo alimuuliza swali Waziri Mkuu kuwa viongozi wamekuwa wakiwaambia kuwa mshika mawili moja humponyoka na kuwa vijana ni taifa la kesho, wasome ili kulitumikia taifa vipi wao wamekuwa wakirundikiana vyeo zaidi ya kimoja na kutoa mfano uteuzi wa mkuu wa mkoa wa Mwanza Dk Alex James Msekela kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa ilhali ni mbunge.

Swali hili halikujibiwa na Waziri Mkuu baada ya kujibu maswali mengine na kumaliza hotuba yake bila ya kujibu hatua ambayo iliwafanya wananchi katika mkutano huo kumkumbusha kujibu na yeye kuwaeleza kuwa atarudi siku nyingine.


"Tangu siku hiyo katika mkutano alifuatwa na watu
wakijitambulisha kuwa wao ni maofisa toka usalama wa taifa na kumtaka awaeleze juu ya swali hilo iwapo kafundishwa na mtu hatua ambayo ilimshangaza kijana na kushindwa kuwajibu," alieleza kwa simu mmoja wa ndugu na jamaa wa kijana huyo ambaye aliomba asitajwe jina gazetini.

Alisema kuwa kutokana na kijana kushindwa kuwajibu vyema walikwenda kuuliza kwa wanafunzi wengine ili kujua anasoma kidato cha ngapi na kuomba majina ya walimu wa kidato cha kwanza kwa lengo na nia ambayo haijajulikana hatua ambayo imewatia woga.

Alisema ndugu huyo kuwa kutokana na hatua hiyo wanahofu huenda haki na uhuru wa kujieleza kwa kijana huyo huenda ikamtumbukia nyogo hata akapoteza masomo au walimu wake wakapoteza kazi.


Chanzo: Mwananchi


SteveD.
 
Masikini kijana wa watu ... hivi kweli Usalama wa Taifa hawana kazi! Sioni kama issue hiyo ni serious kiasi cha kupoteza muda wao kufuatilia swala hilo. Kitakachofuata itakuwa ni kuwatia woga walimu wa Civics na may be kuwauliza ni kwanini wanafundisha mambo hayo. Tukae tusubiri tutasikia kuna mabadiliko ya mtaala wa somo la Civics na Uraia. Kinachoshangaza hao hao viongozi wa serikali kila siku wanahubiri wananchi wafundishwe uraia, siku wakikumbana na maswali hayo wanaanza kutuhumu kwamba wanafunzi wametumwa na wapinzani. Na si ajabu walimu wa Civics wa shule hiyo wanaweza kutuhumiwa kwamba ni wapinzani.

Hapa naona South Africa ya miaka ya ubaguzi inanukia ... somo la history lilikuwa na mtaala tofauti na lilikuwa haliongelei kabisa mambo ya siasa.
 
Masikini kijana wa watu ... hivi kweli Usalama wa Taifa hawana kazi! Sioni kama issue hiyo ni serious kiasi cha kupoteza muda wao kufuatilia swala hilo. Kitakachofuata itakuwa ni kuwatia woga walimu wa Civics na may be kuwauliza ni kwanini wanafundisha mambo hayo. Tukae tusubiri tutasikia kuna mabadiliko ya mtaala wa somo la Civics na Uraia. Kinachoshangaza hao hao viongozi wa serikali kila siku wanahubiri wananchi wafundishwe uraia, siku wakikumbana na maswali hayo wanaanza kutuhumu kwamba wanafunzi wametumwa na wapinzani. Na si ajabu walimu wa Civics wa shule hiyo wanaweza kutuhumiwa kwamba ni wapinzani.

Hapa naona South Africa ya miaka ya ubaguzi inanukia ... somo la history lilikuwa na mtaala tofauti na lilikuwa haliongelei kabisa mambo ya siasa.

Hapa umenena, hawa jamaa naona hawana kazi za kufanya!! Hivi kumfatilia huyo mtoto hata kama kafundishwa kuuliza wao itawasaidia nini, jamaa kashindwa kumjibu, nani amfatilie jibu lake? Waache kutumia vyeo vyao kuwakandamiza na kuwatisha watu wa chini. Nilisema kwenye post moja kuwa kijana alikuwa sahihi kutaka kujua anaambiwa asome awe kiongozi wa baadae, je atakuwaje kiongozi wa baadae wakati wao wamejilimbikizia madaraka, utawala ukaona umegongwa Pentagon kwani swali lilikuwa na ukweli ndani yake akavunga kujibu, hii ndio Ari mpya, Nguvu mpya na Kasi mpya (ANGUKA).
 
Na Frederick Katulanda, Mwanza

MTOTO aliyemuhoji swali Waziri Mkuu Edward Lowassa, Aron Wambura Shera anadaiwa kuandamwa na maofisa usalama wa taifa wakimhoji kila mara kuhusiana na swali alilouliza.

Habari kutoka kwa ndugu wa karibu wa kijana huyo, ambaye ni mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Pius Msekwa kidato cha kwanza, zimedai kuwa maofisa hao siku hiyo ya mkutano walimfuata mwalimu wake na kumtaka amweleze historia ya kijana huyo.


Akiwa wilayani Ukerewe katika ziara, mwanafunzi huyo alimuuliza swali Waziri Mkuu kuwa viongozi wamekuwa wakiwaambia kuwa mshika mawili moja humponyoka na kuwa vijana ni taifa la kesho, wasome ili kulitumikia taifa vipi wao wamekuwa wakirundikiana vyeo zaidi ya kimoja na kutoa mfano uteuzi wa mkuu wa mkoa wa Mwanza Dk Alex James Msekela kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa ilhali ni mbunge.

Swali hili halikujibiwa na Waziri Mkuu baada ya kujibu maswali mengine na kumaliza hotuba yake bila ya kujibu hatua ambayo iliwafanya wananchi katika mkutano huo kumkumbusha kujibu na yeye kuwaeleza kuwa atarudi siku nyingine.


"Tangu siku hiyo katika mkutano alifuatwa na watu
wakijitambulisha kuwa wao ni maofisa toka usalama wa taifa na kumtaka awaeleze juu ya swali hilo iwapo kafundishwa na mtu hatua ambayo ilimshangaza kijana na kushindwa kuwajibu," alieleza kwa simu mmoja wa ndugu na jamaa wa kijana huyo ambaye aliomba asitajwe jina gazetini.

Alisema kuwa kutokana na kijana kushindwa kuwajibu vyema walikwenda kuuliza kwa wanafunzi wengine ili kujua anasoma kidato cha ngapi na kuomba majina ya walimu wa kidato cha kwanza kwa lengo na nia ambayo haijajulikana hatua ambayo imewatia woga.

Alisema ndugu huyo kuwa kutokana na hatua hiyo wanahofu huenda haki na uhuru wa kujieleza kwa kijana huyo huenda ikamtumbukia nyogo hata akapoteza masomo au walimu wake wakapoteza kazi.
 
WAZIRI MKUU- naomba Haraka sana Ujibu hili swali?
Hutubia Taifa Mjibu swali mtoto!!
Jua Kwamba bila kufanya hivyo uta-na Unanikera sana!!!
 
Huyu mkuu wao (OR) mwenyewe yuko hapa, hivi kweli unaruhusu vijana wako kumnyanyasa huyo mtoto?

OR una heshima kubwa kwa tunaokufahamu, badili hao Usalama wa Taifa waache kunyanyasa wananchi.

Mnatakiwa kulinda mali zetu zisiibiwe na sio kuanza kunyanyasa wananchi wasio na hatia.

Mkiendelea hivyo na wewe tutakuingiza kwenye jina la mafisadi.
 
Gigo ... kwi kwi kwi kwi kwi
EL hana jibu la swali na ndiyo maana kaamua kutumia usalama wa taifa ku-create fear ili siku nyingine asiulizwe maswali magumu japo yana majibu.
 
Kweli serikali yetu imejaa mambumbumbu,punda kasoro kubeba mizigo,yaani huyo mtoto wanamufuata wa nini?
 
Hivi hao ndugu za huyo mtoto kwanini wasiwasiliane na akina Tundu Lissu ili wawashitaki hao usalama wa Taifa. It is definately illegal kwa chombo hiki cha serikali kunyanyasa mtu ati kwa sababu ameuliza swali, hata kwa katiba yetu uchwara na inayochechemea nadhani uhuru wa mtu kuuliza swali "gumu" unalindwa. They should take these MOFOs to court.
 
Kwa ufupi baadhi ya viongozi wa Tz are very ignorant, sijui kama hata walienda shule kwa kweli, au huko shuleni walikazwa na walimu wao, ili tu wamalize hizo degree. Yaani mtoto anakuuliza swali wewe unamsakama kwa nini? Mjibu, wewe si mwanaume wewe! kwa nini jamani hawa viongozi wanafikiria watz wote ni wapambe wao, wajinga wasiojua kinachoendelea?
Hawa viongozi kama Lowassa ndio wanaoharibu nchi hawa, huyu sijui ana undugu na Kibaki, maanake wanaonekana kuwa na tabia moja za kibabe, walilelewa na mama mmoja nini?
 
Kuna mtu Wa kujibu mule? Mbona yapi massali mengi tu hawajayajibu? Kagoda na meremeta ni zanani? Wakina nani walirudisha fedha walizoiba EPA?
 
Mnatuaminisha huyu dikteta dhid ya mawazo tofauti naye kuwa edit chaguo bora? Kumbe si tu kwamba ni ufisadi of the first class Bali pia ni dikteta wa kutosha.
 
Huyu ndo tunataka kumfanya awe Rais? Halafu tumempa rungu kwa kukaza sheria za kupata habari na kuhoji mambo?
 
Back
Top Bottom