MAHAKAMA KUU ya Tanzania Kanda ya Tabora imemuhukumu adhabu ya kunyongwa hadi kufa Juma Mayala (23) kwa kosa la kumuua baba yake mzazi
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Jaji Simon Lukelewa huku upande wa Mashitaka uliongozwa na Wakili wa Serikali, Magreth Ndaweka
Jaji Lukelewa alisema kuwa, alitoa adhabu hiyo kwa kuwa mshitakiwa alipatikana na hatia ya kuumua baba yeke mzazi na nkuridhishwa na ushahidi wa hali ya juu kuhusiana nna hilo
Ilidaiwa Mei 5, 2004 mshitakiwa alimuua baba yake Mayala Ngamba kwa kumkata kwa shoka mara tatu kichwani hali iliyopelekea kifo chake papo hapo.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa,mara baada ya kufanya mauaji hayo mshitakiwa aliufukia mwili huo katika choo kisichotumika na kisha kufunika kwa mawe juu ambapo mwili huo uligundulika baada ya siku tatu.
Awali imedaiwa kuwa mshitakiwa alifanya mauaji hayo kutokana na kuchukizwa na hali ya kunyimwa chakula na mzazi wake huyo mara kadhaa hali iliyofanya ajichukulie maamuzi mikononi kinyume na sheria
Mayala mkazi wa kijiji cha Maskati, Wilaya ya Shinyanga
Source: Nifahamishe
Mytake:
Kama kosa alilifanya mwaka 2004, mtuhumiwa alikuwa na miaka 15, je hii kesi ilisikilizwa mahakama ya watoto?
Hawa watu wa Haki za watoto kesi hii waliisikia? au huwa wanasikia tu kesi za watoto ambao ni Ma-star?
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Jaji Simon Lukelewa huku upande wa Mashitaka uliongozwa na Wakili wa Serikali, Magreth Ndaweka
Jaji Lukelewa alisema kuwa, alitoa adhabu hiyo kwa kuwa mshitakiwa alipatikana na hatia ya kuumua baba yeke mzazi na nkuridhishwa na ushahidi wa hali ya juu kuhusiana nna hilo
Ilidaiwa Mei 5, 2004 mshitakiwa alimuua baba yake Mayala Ngamba kwa kumkata kwa shoka mara tatu kichwani hali iliyopelekea kifo chake papo hapo.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa,mara baada ya kufanya mauaji hayo mshitakiwa aliufukia mwili huo katika choo kisichotumika na kisha kufunika kwa mawe juu ambapo mwili huo uligundulika baada ya siku tatu.
Awali imedaiwa kuwa mshitakiwa alifanya mauaji hayo kutokana na kuchukizwa na hali ya kunyimwa chakula na mzazi wake huyo mara kadhaa hali iliyofanya ajichukulie maamuzi mikononi kinyume na sheria
Mayala mkazi wa kijiji cha Maskati, Wilaya ya Shinyanga
Source: Nifahamishe
Mytake:
Kama kosa alilifanya mwaka 2004, mtuhumiwa alikuwa na miaka 15, je hii kesi ilisikilizwa mahakama ya watoto?
Hawa watu wa Haki za watoto kesi hii waliisikia? au huwa wanasikia tu kesi za watoto ambao ni Ma-star?