Mtizamo: Kikosi cha 'Lala Salama' Baraza la Mawaziri kinakuja lini na sura zipi?

DSN

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
2,837
1,674
Natamani kuona baraza jipya la mawaziri japo lala salama tuone juhudi za mwisho kuinusuru Nchi na heka heka zijazo ambazo, kwa wale wasiopenda kuona maswali yasiyo na majibu yakiwa hayana majibu mapaka dakika za uchaguzi ni kufuga bomu lislo na mteguzi.Majibu hayo yakijibiwa sasa inatoa unafuhu kwa wanamagamba kuingia kwenye uchaguzi wakiwa na sura ambayo zile kero kuu za wananchi walau zinapata muonekano na aueni kuwa sasa zimepata majibu.

Lakini kuendelea kubuy time kuwa zinatafutiwa majibu huku zikionekana kupewa likizo ni kufuga ugonjwa na uvundo.Ili kuepuka hayo na kujiandaa na mapokepo mapya ni vema tukaona baraza jipya la mawaziri lenye sura na picha ya ukombozi halisi wa kupewa uhakika wa kimchakato makini na kisayansi.Kwa kuwa kwa sasa Wanagamba watambue dhama hizi ni zile za kushindana kwa hoja na utafiti wa kisayansi dhidi ya wapinzani wao Chadema.Na sas sio zama za ubabe kwani nao Chadema wameanza kukubalika huko ambako Wanamagamba walikuwa wanajivuni kuwa ni ngome yao ya mwisho ya kucheze turufu zao.

Tunataka kuona michezo ya sayansi ambayo mwamuzi ni Mwananchi wa Taifa hili,mbinu za ubabe hazina nafasi kwa sasa.Kwa ushauri wangu kwa wanamagamba ni kuwa wajipange kwa safu mpya za mawaziri.Kwa kuwa uteuzi wao wa sasa utaleta nafasi nzuri ya kujudge wateule waliopata nafasi hizo kukubalika kwa jamii ili kutayarisha safu ya Chama cha Mapinduzi na si Safu za Makundi ya Watu.

Tatizo la Wanamagamba sijui wanatatizo gani?Wanachadema Wanazungumzia Mkakati wa Kichama wanamagamba watajitazama kimakundi matokeo yake inakuwa shagalabhala.Mikakati ya kisayansi na mbinu zake katika siasa za Watanzania ambazo nazo sasa imekuwa ni dalili na mwanzo mpya wa siasa zenye mwelekeo wa kuwafanya kuchagua kiongozi kwa matendo na ushawishi wa hoja zake na sio kwa kuwa ni Mwanamagamba wa siku nyingi au yeye ni kigogo kwenye mfumo wa kibongo.

Ili Wanamagamba waweze kujipanga vyema ni vyema wakafumua baraza la mawaziri ili kuanza kutengeneza safu ya kichama kimkakati,Manake wakitegemea kufanya dakika za tia tia maji itakuwa imekula kwao.Kwa kuwa watako simama sasa watakuwa ndio picha na safu ya muoonekano wa ujio wa timu mpya yenye mkakati wa kichama zaidi.

Kwa sasa Chadema bila upinzani wa kisayansi na mkakati wa kwao na pia wananamagamba vile vile hakika changamoto nzima za maendeleo yetu ziatabaki ni vichekesho.

Wanamagamba watuonyeshe hiyo timu mpya biashara asubuhi jioni mahesabu.chelewa chelewa watakuta mwana sio wao.

Nawasilisha.
 
kama pinda ateendelea kuwa PM na ngereja na malima wakaendelea kuwa mawaziri katika hilo baraza jipya basi itakuwa ni ujinga kubadilisha baraza la mawaziri bora waendelee na hili lililoshindwa kazi mpaka tutakapopata ukombozi wetu 2015!
 
Hivi ccm itajivuaje gamba ikasahau kichwa cha nyoka ambacho ni JK mwenyewe?.........let us be serious and move on from these shenanigans' circuses..................
 
jk hana utashi wa kuunda baraza makini la wamaziri
yawezekana ni uwezo wake mdogo au uswahiba una msumbua, tatizo kubwa alilonalo ni makundi
na yeye ni mwaasi hivyo anaogopa kuwapa wachapa kazi vyeo wasije pata sifa kuliko watu wake kina membe n.k
hata huyu shemeji yake IGP amtoe na JAIRO anaweza kuondolewa kama alivyopewa hicho cheo ana contract ya kushika hicho cheo
milele,
lakini unapokuja kwa raisi muoga ni ngumu nchi kusonga mbele kwa kufanya maamuzi mazito na majumu kama haya
 
Jk hana uwezo wa kuunda kwakuwa hakuna wa kumtoa. Nafasi zote ameweka maswahiba zake. Labda awabadilishe ktk wizara. Unahisi ana uwezo wa kumuondoa Ngeleja?, amejaza ndg, jamaa na Marafiki.
 
Siioni hiyo hamu ya kuwa na cabinet mpya kwani Mk wer e hawezi kuwaondoa hawa waliopo ni kama amefunga nao ndoa ya kikatoliki (Marafiki, ndugu na washkaji) Yetu macho. WM Pindua! hakuna jipya hapo
 
Siioni hiyo hamu ya kuwa na cabinet mpya kwani Mk wer e hawezi kuwaondoa hawa waliopo ni kama amefunga nao ndoa ya kikatoliki (Marafiki, ndugu na washkaji) Yetu macho. WM Pindua! hakuna jipya hapo
<br />
<br />
true!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom