Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,316
Je, kuna umuhimu wa wazazi kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo? Unawapelekaga watoto wako?
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa JamiiForums.
Ndugu zangu watanzania;
Siku za hivi karibuni nimekuwa nikishuhudia matukio mengi sana zaidi ya mara 4 katika misiba niliyopata kuhudhuria ambapo watoto waliozaliwa mijini (1980's - 1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kusababisha mpasuko wa mahusiano ndani ya ukoo.
Kwa hapa Tanzania, makabila yetu yamegawanyika katika makundi makuu mawili. Kuna makabila ambayo kuzika mtu kwao sio jambo la maana sana kiasi kwamba hata ukifia Magomeni wao kukuzika makaburi ya Kinondoni ni kawaida tu.
Kundi la pili ni yale makabila ambayo ni mwiko kabisa kuzika mwili wa ndugu yao nje ya kijiji. Yaaani kama mtu alifia Dar, basi ni lazima asafirishwe mpaka mkoa wa Mara, tena akazikwe katika makaburi ya ukoo.
Hata kama mtu amekufa tuseme huko Ulaya, basi ni lazima aletwe kutoka huko New York mpaka Rorya hukoooo Shirati au Utegi. Juzi hapa nilienda katika msiba mmoja hapa jirani na nilipopanga wa watu wa kabila moja la huko Mkoa wa Kigoma.
Katika msiba huu ndio ninakutana na hiki kisanga cha watoto 3, ambao financially wapo njema sana na mmoja wao ni Country Manager wa kampuni moja ya wazungu huku Dar tena ni mtoto wa kiume.
Sasa wakuu ninaomba kujua chanzo kikuu ni nini? Je, ni wazazi wenyewe kutopenda kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo ya mwaka ili wajuane na mazingira pamoja na ndugu zao wa huko au shida ipo wapi hapa wakuu?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa JamiiForums.
Ndugu zangu watanzania;
Siku za hivi karibuni nimekuwa nikishuhudia matukio mengi sana zaidi ya mara 4 katika misiba niliyopata kuhudhuria ambapo watoto waliozaliwa mijini (1980's - 1990's) wanavyokataa kusafirisha miili ya wazazi wao kwenda kuzikwa kijijini na kusababisha mpasuko wa mahusiano ndani ya ukoo.
Kwa hapa Tanzania, makabila yetu yamegawanyika katika makundi makuu mawili. Kuna makabila ambayo kuzika mtu kwao sio jambo la maana sana kiasi kwamba hata ukifia Magomeni wao kukuzika makaburi ya Kinondoni ni kawaida tu.
Kundi la pili ni yale makabila ambayo ni mwiko kabisa kuzika mwili wa ndugu yao nje ya kijiji. Yaaani kama mtu alifia Dar, basi ni lazima asafirishwe mpaka mkoa wa Mara, tena akazikwe katika makaburi ya ukoo.
Hata kama mtu amekufa tuseme huko Ulaya, basi ni lazima aletwe kutoka huko New York mpaka Rorya hukoooo Shirati au Utegi. Juzi hapa nilienda katika msiba mmoja hapa jirani na nilipopanga wa watu wa kabila moja la huko Mkoa wa Kigoma.
Katika msiba huu ndio ninakutana na hiki kisanga cha watoto 3, ambao financially wapo njema sana na mmoja wao ni Country Manager wa kampuni moja ya wazungu huku Dar tena ni mtoto wa kiume.
Sasa wakuu ninaomba kujua chanzo kikuu ni nini? Je, ni wazazi wenyewe kutopenda kuwapeleka watoto kijijini wakati wa kipindi cha likizo ya mwaka ili wajuane na mazingira pamoja na ndugu zao wa huko au shida ipo wapi hapa wakuu?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.