Mtikisiko wa uchumi wapamba moto, hali mbaya kwa wafanyabishara wengi wafunga maduka

MP CHACHANDU

JF-Expert Member
Dec 4, 2016
875
615


Haya yamebainishwa na waziri Wa fedha ndugu Mpango katika mazungumzo yake ya ripoti ya hali halisi ya uchumi Wa Tanzania.

"Madai ya biashara nyingi kufungwa: Kwa upande wa madai ya biashara nyingi kufungwa katika siku za karibuni, tumefuatilia na kwa kiasi fulani kuna ukweli. Imebainika kwamba kasi ya wafanyabiashara kufunga biashara zao imeongezeka kati ya mwezi Agosti na Oktoba 2016. Mfano Ilala 1,076, Kinondoni 443, Temeke 222 na Arusha 131. Aina ya biashara nyingi zilizofungwa ni katika sekta ya ujenzi na biashara ya jumla na rejareja, na chache katika huduma za usafiri.

Hata hivyo, sababu hasa zilizopelekea biashara hizo kufungwa hazijabainika kutokana na ugumu wa kupata taarifa kutoka kwa wenye biashara zilizofungwa.

Sababu za mtu kufunga biashara yake zinaweza kuwa nyingi, ikiwemo, kushindwa kuingiza bidhaa nchini bila kulipa kodi stahiki, kushindwa kulipa au kulipwa madeni, kubadilisha aina ya biashara, kushindwa kusimamia biashara, gharama kubwa za uendeshaji, wabia katika biashara kutoelewana au kutapeliana, kuibuka kwa washindani wa kibiashara wenye nguvu au huduma bora zaidi n.k."

9.jpg
 
Funga bakuli lako... Si ukalime wewe.
Nalima waje tulime biashara nilifunga enzi za kikwete kariakoo kwahiyo sioni tofauti yoyote ya utawala zaidi kilimo changu kinanifurahisha kwa maendeleo kuliko wakati nafanya kariakoo kila siku nilikuwa nagombana na tra mikopo ya mabank na kodi ya pango. Sasa hivi naamua mazao niyauzie shamba au niyapeleke sokoni mwenyewe. Kiufupi waachane na ghost economy ya huko waje huku shamba tulime.
 
Kipindi Hiki kitumike vizuri Watu wa mipango miji waitumie vizuri kurekebisha kasoro zilizojitokeza Huko nyuma
 
Wafanyabiashara hewa waache wakawe wakulima.
Mkuu,mie nalima mboga za majani,we unalima nini ili tuunganishe nguvu?
Wakati baadhi wakitamani Magufuli aje aongezewe muda wa kutawala…… binafsi natamani katiba ibadilishwe iruhusu kikwete agombee tena huku tukijipanga nani wa kumpa nchi!
Ndoto za Alinacha!
Mbona Maduka mengi bado yanaendelea kufanya kazi? Kwani zamani watu hawakuwa wakifunga Maduka, hawakuwa wakifunga na kurudisha fremu? Kufunga kumeanza leo?
Wakiona Mawili yanafungwa wanajua ni Tanzania nzima...
Nalima waje tulime biashara nilifunga enzi za kikwete kariakoo kwahiyo sioni tofauti yoyote ya utawala zaidi kilimo changu kinanifurahisha kwa maendeleo kuliko wakati nafanya kariakoo kila siku nilikuwa nagombana na tra mikopo ya mabank na kodi ya pango. Sasa hivi naamua mazao niyauzie shamba au niyapeleke sokoni mwenyewe. Kiufupi waachane na ghost economy ya huko waje huku shamba tulime.
Nitakuja tuongeze nguvu!
Hali sio mzuri kwa wafanyabiashara...!mauzo yapo chini sana..pesa imekuwa dhahabu.
Sema imekuwa dhahabu kwako!
 
Hali sio mzuri kwa wafanyabiashara...!mauzo yapo chini sana..pesa imekuwa dhahabu.
Mauzo yako chini kwa sab nidhamu ya matumizi ya pesa imerudi lazima wafanyabiashara wabuni biashara za kumvutia mteja sio kuigana. Kwa mfano maduka ya nguo yamejaa kila kona, mabaa na maguest kila baada ya nyumba kumi, kila mtu ananunua bodaboda. Biashara za kuuza matoy ya kuchezea watoto haina nafasi tena. Pesa ipo sana bali watu ndio wana nidhamu ya matumizi yake. Nchi zilizoendelea duniani ndivyo zilivyo kama bongo ya leo pesa ngumu inapatikana kwa kufanya kazi tu ndio maana unasikia ndugu zetu huko ulaya wanafanya kazi zaidi ya mbili ili wapate pesa ya kutosha. Maduka yote makubwa ya nguo vyombo vya nyumbani magari na furniture yanakopesha wananchi kisha wanawakata kwenye mishahara yao kila mwezi vinginevyo hakuna mtu atakwenda na milioni kadhaa kufanya shopping ya viatu kama wapiga deal wa bongo. Wafanyabiashara badilikeni njoni na product mpya tutakuja.
 
Biashara zinafungwa,bandarini mizigo imepungua alafu TRA kila mwezi wanavuka lengo!!
Wanaofunga biashara ni wale ambao hata serikali haikuwa inawajua hivyo hawana impact yoyote kwenye mapato ya serikali bandarini mizigo imepungua wapiga deal wamekimbia na wengine wamebadilisha biashara lkn mizigo michache iliyobaki inalipa kodi stahiki ndio maana mapato yameongezeka kwa mizigo michache.
 
Back
Top Bottom