Mtikila, wenzake kufungua kesi dhidi ya mafisadi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Waungwana kama kuna yeyote mwenye more info kuhusu kamati hii au kama akipata hizo info siku za usoni azimwage hapa ukumbini.

Alutta Continua


Date::7/8/2008
Mtikila, wenzake kufungua kesi dhidi ya mafisadi
Na Kizitto Noya na James Magai
Mwananchi

KAMATI ya Kupambana na Uporaji wa Nchi (PILCOM) imesema hairidhishwi na kitendo cha baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi, kutumia makanisa kujisafisha.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo na kiongozi wa Kanisa la Full Salvation, Christopher Mtikila, alidai jana katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam kwamba, ni ukiukwaji wa haki na misingi ya sheria za nchi, kwa wezi wa kuku na vibaka kufungwa gerezani na mafisadi wa fedha za umma kuachwa huru.

Alidai kuwa kamati hiyo inakusudia kufungua kesi mahakamani dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

''Moja ya kazi za kamati hii ni kuwafikisha mbele ya sheria watu wote walioshiriki katika wizi wa matrilioni ya fedha za nchi yetu katika Benki Kuu na kurejesha mapesa yote waliyoyaiba pamoja na riba na gharama kutoka kila walikoyaweka nje na ndani ya nchi,'' alisema Mchungaji Mtikila.

Alisema katika maandalizi ya kufungua kesi hiyo, jana kamati ilimwandikia barua Jaji Mkuu na Jaji Kiongozi kuwataka waharakishe hukumu ya kesi ya Katiba namba 86/2006, iliyofunguliwa na kamati hiyo kuitaka iruhusu watu binafsi kuendesha kesi za jinai.

Alisema hivi sasa kamati hiyo inangoja hukumu ya kesi hiyo, ili iweze kufungua kesi dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi.

Alidai kuwa wamemwandikia Gavana wa BoT na Spika wa Bunge waipatie taarifa muhimu za wizi huo, ili sheria ichukue mkondo wake.

''Tunawahakikishia wananchi kwamba, kama inavyosema Katiba ya Jamhuri ya Muungano, hakuna mwizi aliye juu ya sheria, awe rais mstaafu au aliye madarakani, waziri, kigogo wa CCM au gabacholi jeupe au jeusi, mradi ameshiriki katika wizi wa mali za umma lazima atafikishwa mahakamani,'' alisema Mtikila

Kwa mujibu wa Mtikila, Kamati hiyoambayo inawahusisha viongozi wa makisa kadhaa, inashughulikia wizi wa Sh216 kutoka Mfuko wa Import Support, mabilioni ya EPA, DCP na OGL, ufisadi katika mkataba wa Richmond na Dowans, Meremeta na Tangold, IPTL, Songas, Aggreko, Netgroup Solutions, TICTS, Radar, TTCL, Benki ya Taifa ya Biashara,Tanzanite, migodi ya dhahabu na uporaji wa majumba ya serikali na vigogo wa CCM.

Kamati pia ilimtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kushiriki kikamilifu katika vita hiyo ya ufisadi na kuhakikisha kuwa wahusika wote umma wanazirejesha na kufikishwa mahakamani.

Akizungumza katika mkutano huo, Askofu Gordon Kiaro wa kanisa la Pentecostal Fellowship (INT) alisema suala la kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wa ufisadi sio la kidini wala dhehebu na kwamba, linapaswa kuungwa mkono na Watanzania wote.
 
Nami Nataka Kujiunga Na Kamati Hiyo......!
Big Up ......!
Big Up....!
 
Haiwezekani Wenye Makosa Madogo Wawe Wamejaa Lupango Hali Magabacholi Wanatanua Nje...!
 
Jana mchungaji mtikila kwenye taarifa ya habari ITV aliongea sana kuwa mafisadi wasitumie nyumba za mungu kama sehemu ya kusafisha maovu yao,alisema ibilisi hawezi kuingia chumbani kwa bwana mungu na kujifanya eti yeye ni msafi.kwa kweli aliongea maneno makali sana ya kumshutumu rostam kuwa ni dharau mbele za mungu kuja kusimama kwenye mimbari ya kanisa na kuongea uchafu wake.
Lakini Askofu mkuu jana hakupatikana kuongelea hilo jambo...,
 
watanzania Wasitegemee Lolote La Maana Baada Ya Hii Kesi. Hii Ndio Silaha Kubwa Ya Mwisho Waliyobakiwanayo Mafisadi.

Si Jambo Geni Kwa Mchungaji Mtikilo Kufungua Kesi Dhidi Ya Aidha Serikali Yenyewe Au Waandamizi Wakuu Wa Hiyo Serikali Kisha huifuta Kwa Kisingizio Cha Kukosa Ushahidi. Hata Hii Mwisho Wake Ni Kufutwa.

Ninalazimika Kuamini Kwamba Mtikilo Na wenzake wameandaliwa Ili Kupotosha Na Kuua Swala Zima La Epa. Watanzania Tusisahau Kwamba Hawa Mafisadi Ndio Watoaji Wakubwa Wa Sadaka Na Zaka Huko Makanisani Na Misikitini Hivyo Tusitegemee Viongozi Wa Kidini Kuwageuka wawezeshaji Wao. Kwani Bado Wanayahitaji Hayo Mabilioni Ya Pesa Yasaidie Kujenga Makanisa Na Misikiti Zaidi. Angalieni Jinsi Akina rostoam Aziza wanavyohaha Kupeleka Vijisenti Vyao Makanisani. Kwani Wanafahamu Fika Viongozi Wa Kidini Si Lolote Wala Chochote Bali Nao Ni Mafisadi Wenzao Wanaoendeleza Ufisadi Kwa Waumini Wao Kwa Kuwakamua Kila Kidogo Walichonacho Kwa Njia Ya sadaka Na Michango Mingi Ya Ajabu!

Tukumbuke, Siasa Za Tanzania Zimejikita makanisani Na Misikitini Tangu Enzi Za Mwalimu. Ndo Maana Serikali Iliwaundia Viongozi Hawa Wa Kidini Vyombo Kama Vile bakwata Na Mengineyo ili Kuwaweka Karibu Zaidi Na Serikali Pamoja Na Wanasiasa Kwa Ujumla.

Hii Ndiyo Sababu Ya Kwanini Mafisadi hawajatengwa Na Makanisa Au Misikiti yao. Sanasana Wnadai Ati Wanaendelea Kuwakumbatia Kwa Kisingizio Cha Kwamba Wanawaombea Ili Waache Zambi Ya Ufisadi! Ajabu!

*Mafisadi hawa Ni Wafadhili Wakubwa Wa Misikiti Na Makanisa. Ndio Wanaowawezesha Viongozi Wa Dini Wamiliki Majumba Na Magari Ya Anasa. Tusitegemee Lolote*. tumekwisha!
 
Jana mchungaji mtikila kwenye taarifa ya habari ITV aliongea sana kuwa mafisadi wasitumie nyumba za mungu kama sehemu ya kusafisha maovu yao,alisema ibilisi hawezi kuingia chumbani kwa bwana mungu na kujifanya eti yeye ni msafi.kwa kweli aliongea maneno makali sana ya kumshutumu rostam kuwa ni dharau mbele za mungu kuja kusimama kwenye mimbari ya kanisa na kuongea uchafu wake.
Lakini Askofu mkuu jana hakupatikana kuongelea hilo jambo...,

Ninavyofahamu mimi, Rostam alialikwa na kanisa kama mgeni rasmi katika hafla fulani, iliyohusisha pia kuchangia kwaya. Sidhani kama mualiko huo ulitokana na uwezo wake wa kushawishi wadau watoe, bali uwezo wa yeye mwenyewe kutoa miongoni mwa 'vijisenti' vyake. Yasemekana alitoa 7m. Wa kulaumiwa hapa ni kanisa ambao walitoa mwaliko huo huku wakijua kwamba watanzania wako katika juhudi za kuhakikisha watuhumiwa wa Ufisadi akiwemo RA wanachukuliwa hatua za kisheria. Hata hivyo, aibu hii kwa kanisa ni funzo kwa taasisi nyingine zinazonyemelewa na mafisadi kwa lengo la kujisafisha (Dini, majimbo, magazeti, vyama vya siasa n.k). Ni funzo pia kwa mafisadi kwamba katika vita inayoendelea dhidi yao, hawana pa kujificha!
 
Ninavyofahamu mimi, Rostam alialikwa na kanisa kama mgeni rasmi katika hafla fulani, iliyohusisha pia kuchangia kwaya. Sidhani kama mualiko huo ulitokana na uwezo wake wa kushawishi wadau watoe, bali uwezo wa yeye mwenyewe kutoa miongoni mwa 'vijisenti' vyake. Yasemekana alitoa 7m. Wa kulaumiwa hapa ni kanisa ambao walitoa mwaliko huo huku wakijua kwamba watanzania wako katika juhudi za kuhakikisha watuhumiwa wa Ufisadi akiwemo RA wanachukuliwa hatua za kisheria. Hata hivyo, aibu hii kwa kanisa ni funzo kwa taasisi nyingine zinazonyemelewa na mafisadi kwa lengo la kujisafisha (Dini, majimbo, magazeti, vyama vya siasa n.k). Ni funzo pia kwa mafisadi kwamba katika vita inayoendelea dhidi yao, hawana pa kujificha!
kanisa la KKKt Kinondoni kwa nini lilimualika Rostam? si walijua anazo feza za wizi na wao feza za wizi kwao halikuwa tatizo bali tatizo kwao ilikuwa ni vipesa hivyo vya wizi tu.
Naona ndugu zangu wa makanisa wanachojali ni pesa tu hata kama wataambiwa zimetokana na wizi wao watapokea tu. Nawasikitikia sana.
 
Kila kesi anayofungua huyu huanza kwa kishindo then huishia hewani

Yeye na viongozi wenzake wa din hawanalolote bali wanataka kuwayumbisha watanzania. Hawa viongozi wa dini wanachotafuta ni uhalali wao wa kuweza kuliongelea hili makanisani mwao kwa lengo la kuua mjadala ili watimize azima yao ya kuisadia serikali yao ya kifisadi. Hii ndiyo kazi yao siku zote, yaani kusaidiana na serikali kunyonya watanzania. Wanakusanya peasa makanisani kwao kwa lengo hilo hilo la kunyonya wananchi kwa kwenya mbele.

MUNGU WASAMEHE HAWA VIONGOZI WA MAKANISAAE NA MISIKITIKO YA TZ KWANI HAWAJUI MALITENDALO.
 
Alisema katika maandalizi ya kufungua kesi hiyo, jana kamati ilimwandikia barua Jaji Mkuu na Jaji Kiongozi kuwataka waharakishe hukumu ya kesi ya Katiba namba 86/2006, iliyofunguliwa na kamati hiyo kuitaka iruhusu watu binafsi kuendesha kesi za jinai.


...katika vitu muhimu vya kupigania katika katiba mpya hii ni muhimu sana na itawapa weapon wananchi kupambana na system mbovu iliyopo na hii ndio imefanya nchi kama states serikali ifanye kazi yake maana wanajua wasipofanya individuals wanaweza kuleta lawsuit katika mahakama kwa chochote as long as judge anaona kuna kesi ya kusikiliza
 
watanzania Wasitegemee Lolote La Maana Baada Ya Hii Kesi. Hii Ndio Silaha Kubwa Ya Mwisho Waliyobakiwanayo Mafisadi.

Si Jambo Geni Kwa Mchungaji Mtikilo Kufungua Kesi Dhidi Ya Aidha Serikali Yenyewe Au Waandamizi Wakuu Wa Hiyo Serikali Kisha huifuta Kwa Kisingizio Cha Kukosa Ushahidi. Hata Hii Mwisho Wake Ni Kufutwa.

Ninalazimika Kuamini Kwamba Mtikilo Na wenzake wameandaliwa Ili Kupotosha Na Kuua Swala Zima La Epa. Watanzania Tusisahau Kwamba Hawa Mafisadi Ndio Watoaji Wakubwa Wa Sadaka Na Zaka Huko Makanisani Na Misikitini Hivyo Tusitegemee Viongozi Wa Kidini Kuwageuka wawezeshaji Wao. Kwani Bado Wanayahitaji Hayo Mabilioni Ya Pesa Yasaidie Kujenga Makanisa Na Misikiti Zaidi. Angalieni Jinsi Akina rostoam Aziza wanavyohaha Kupeleka Vijisenti Vyao Makanisani. Kwani Wanafahamu Fika Viongozi Wa Kidini Si Lolote Wala Chochote Bali Nao Ni Mafisadi Wenzao Wanaoendeleza Ufisadi Kwa Waumini Wao Kwa Kuwakamua Kila Kidogo Walichonacho Kwa Njia Ya sadaka Na Michango Mingi Ya Ajabu!

Tukumbuke, Siasa Za Tanzania Zimejikita makanisani Na Misikitini Tangu Enzi Za Mwalimu. Ndo Maana Serikali Iliwaundia Viongozi Hawa Wa Kidini Vyombo Kama Vile bakwata Na Mengineyo ili Kuwaweka Karibu Zaidi Na Serikali Pamoja Na Wanasiasa Kwa Ujumla.

Hii Ndiyo Sababu Ya Kwanini Mafisadi hawajatengwa Na Makanisa Au Misikiti yao. Sanasana Wnadai Ati Wanaendelea Kuwakumbatia Kwa Kisingizio Cha Kwamba Wanawaombea Ili Waache Zambi Ya Ufisadi! Ajabu!

*Mafisadi hawa Ni Wafadhili Wakubwa Wa Misikiti Na Makanisa. Ndio Wanaowawezesha Viongozi Wa Dini Wamiliki Majumba Na Magari Ya Anasa. Tusitegemee Lolote*. tumekwisha!



Hakika nimeamini kuwa watanganyika ni wadanganyika. Yaani kweli wamedanganyika na wakaamini kwamba Mtikila "anaubavu" wa kupambana na "mafisadi" kwa kufungua kesi mahakamani?! Yaani mtikila huyuhuyu ambaye anadaiwa tuvijisenti alitotukopa toka kwa mafisadi?! Hivi ni kweli inawezekana mtu mwenye akili timamu akaamua kuvua nguo zake zote, hata ile ya ndani, kisha akaamua kutembea barabarani akiwa uchi wa munyama??!!! Hivi kweli inawezekana mtikila akawashitaki wawezeshaji wake??!! Kweli??!!
 
...Mtikila credibility ni sifuri na kikatiba hana uwezo huo yaani kaamua kuchezea watu akili tuu na hii ndio kula yake mjini,huyu jamaa ni hatari kuliko hao mafisadi wenyewe..... saa ya ukombozi my azz!
 
Back
Top Bottom