Mtikila: Shujaa wa Demokrasia, Mwanamapinduzi halisi na Shujaa wangu...

Provisional, Meaning and Constructivism rely heavily on imposed ideologies, those are the basis that forms a human reason-ability or the commonsense. The're based on past experience and socialization process that is to say a human nature is never a myth scientifically to a large extent, explore the human thinking and you would understand his/her socialization process.


That is the beauty of knowledge it makes you aware of those procedure and how they are acquired before becoming your ideas.

Knowledge allows you to make rationale decisions, since politics is a study of managing social creature it is a matter of aspiring politicians utilizing what they understand about human ideas and how to make them work for the better whole. Therefore a politicians has to think in terms of benefiting his society whilst including every ideology.

That explains your understanding on what it takes to a build a society.

Mods delete this post please


Usiku mwema.[/QUOTE]
 
I beg differ with you. Ukitaka utawala wa haki na sheria ni lazima ujifunze au uwe na utaratibu wa kufuata vyombo vya sheria. Mtikila anatumia katiba japo haipendi. Na anakwenda mahakama japo kuwa mahakama zetu ni za kubabaisha.

Viongozi wengi wa upinzani wameisoma katiba baada ya uchaguzi wa 2010. Na mahakama hawataki kuitumia. Je utamaduni wa kutumia katiba, sheria na mahakama watejenga lini? Wakiwa watawala?

Nakubaliana na wewe, and mahandamano na mikutano also falls under utawala wa sheria na katiba. Lakini swala siyo kujifunza utawala washeria au kufuata sheria, mi nadhani la muhimu ni which strategy is the best to win your case. Hauwezi kushinda mahakamani kila siku ilikumconvince mtu kijijini kwa ccm is a ****. Hotuba, mikutano au vipeperushi is one of the best to address critical issues, na ndo maan tunashule and university and we do not do home schooling. Swala la mahakama could be a political strategy but is very weak. Mahakama to me should be used only if the level of intelligence in politics is within our reach. But, i dare to say, chadema is perhaps far and beyond the interpretation of our laws kwenye mahakama. Its good for Mtikila coz he lks to make contraverse, may be he is genetically predispose to do that. Otherwise, si amini kama kushinda mahakamani ni nnjia bora ya kujenga chama au kueneza sera za chama.
 
Huyu Mtikila hata UHURu wetu aliupinga akisema wazungu walikuwa watu bora sana ndio walotuletea ustaarabu (dini) na kadhalika leo waondolewe kwa kuitwa mabeberu!. Alipingana na dhana nzima ya Uhuru wa mwafrika leo mnamwona ndiye hero wenu? ama kweli sasa naanza kuelewa wapi hasa tunapogongana..
 
Nakubaliana na wewe, and mahandamano na mikutano also falls under utawala wa sheria na katiba. Lakini swala siyo kujifunza utawala washeria au kufuata sheria, mi nadhani la muhimu ni which strategy is the best to win your case. Hauwezi kushinda mahakamani kila siku ilikumconvince mtu kijijini kwa ccm is a ****. Hotuba, mikutano au vipeperushi is one of the best to address critical issues, na ndo maan tunashule and university and we do not do home schooling. Swala la mahakama could be a political strategy but is very weak. Mahakama to me should be used only if the level of intelligence in politics is within our reach. But, i dare to say, chadema is perhaps far and beyond the interpretation of our laws kwenye mahakama. Its good for Mtikila coz he lks to make contraverse, may be he is genetically predispose to do that. Otherwise, si amini kama kushinda mahakamani ni nnjia bora ya kujenga chama au kueneza sera za chama.

I am a teacher by profession and I can tell you that we do have home schooling. It has been shown that students whose parents care about education perform better than their peers. For, environments play a big part in child or student development.

1995 kulikuwa na suala na mgombea huru. Na nchi za wahisani zilishinikiza serikali kuangalia uwezekano wa kubadilisha katiba hili kuruhusu mgombea huru.

Ghafla bin vuu, NCCR, CHADEMA (wakati huo ikiwa bado CCM B) na CUF wakakubali kuingia kwenye uchaguzi bila marekebisho ya katiba. Na matokeo yake ni hasara kubwa kwa taifa.
 
Huyu Mtikila hata UHURu wetu aliupinga akisema wazungu walikuwa watu bora sana ndio walotuletea ustaarabu (dini) na kadhalika leo waondolewe kwa kuitwa mabeberu!. Alipingana na dhana nzima ya Uhuru wa mwafrika leo mnamwona ndiye hero wenu? ama kweli sasa naanza kuelewa wapi hasa tunapogongana..

Bila ya wazungu hiyo nchi inayoitwa Tanganyika isingekuwepo. Kila mtanzania anataka kuishi maisha ya kizungu. Sasa anamekosea vipi Mtikila? Au kwa sababu alisema Nyerere mtusi?
 
Kwa hiyo hata wewe unapingana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar sio? Kiini macho ni swala jingine kabisa na kupinga muungano wa Tanganyika na Zanzibarakifikia kushtaki na kudai usd millioni 160.. Lazima ujue tofauti.. na kuhusu mahubiri sijui wewe unaelewa vipi au unakisia vipi?..

Mkuu Mkandara,
Tuliache suala la mtikila na madai yake ya mamilioni, naomba uelewe kwamba msingi wa hoja yangu ni madai ya Tanganyika hata kama mtikila hata husishwa; Lakini kabla sijaenda mbali, naombe nisema kwamba: Nitakuwa mwehu kama itaeleweka kwamba Mchambuzi anapinga muungano; Naomba iende on records kwamba sipingi muungano bal mfumo wake, na ninapendelea tuwe na serikali tatu kwani hivyo ndivyo tutaweza kuimarisha muungano huu ambao hakika tunauhitaji sana, na kama tunautakia mema, ni lazima tuache siasa na viini macho na tuangalie realities, vinginevyo tutauvunja bila kutegemea;

I strongly believe in panafricanism above all, na ni Nyerere ndiye ambae alimpinga Kwame Nkrumah juu ya THE MEANS TOWARDS A UNITED STATES OF AFRICA; lakini cha ajabu, ni yeye alikuja kukosea kuhusu the MEANS kwa Tanzania; with all due respect to Mwalimu, hapa alikosea na nisingependa kuwa mwoga au mnafiki kuweka msimamo huo;

On the one hand, Nyerere alihimiza umuhimu wa kuanza na regional blocks kama vile EAC, ECOWAS lakini muhimu zaidi kwana kulikomboa bara zima kwanza, kabla ya fikra za Nkrumah za UMOJA WA AFRIKA; On the contrary, Nkrumah yeye alitaka Afrika iungane right away; in the short run, Nyerere alionekana dhaifu kihoja na Nkrumah akageuka kuwa a REAL PANAFRICANIST, lakini baada ya miaka mingi, sasa historia imempa alama ya "A+" Mwalimu Nyerere juu ya means towards a UNITED STATES OF AFRICA, huku Nkrumah akipata tu credit ya kuanzisha wazo hilo but marks anazopata kwenye suala la MEANS ni ndogo sana ingawa sio "F";

With all due respect to muungano and Nyerere's vision, kwa kweli he rushed suala hili sana, may be because it transpired in the womb of Cold War ambapo marekani walikuwa wanaogpa sana Zanzibar pengine isigeuke kuwa another Cuba, especially baada ya vurugu za Chege kule East Congo; Mbaya zaidi ni kwamba muungano pamoja na kuwa ni wazo zuri, ulijengwa kwa mfumo wa kuiga iga hiki na kile kwani hauku reflect realities on the ground bara na visiwani licha ya kwamba zanzibar na ukanda wa pwani wa tanganyika ulikuwa na historia na muingiliano wa muda mrefu, na hata kuwa himaya moja ya Sultani katika kipindi fulani; Vinginevyo muundo wake uliiba a few elements za United Kingdom, na hili Nyerere alilizungumza wazi na lipo kwenye vitabu vingi vya historia; kwa mtazamo wangu, hili likawa kosa la kwanza, na kosa hili lilikuja kuwa dhahiri zaidi pale assumption za Mwalimu kwamba pengine Tanzania ingeendelea kuwa nchi ya chama kimoja for the next unforeseable future ilipogota, kwani katika suala la muungano, suala la vyama vya siasa halikutajwa - halikuwepo na bado halipo kwenye hati ya muungano, lilikuja ingia baadae kwenye katiba ya muda mwaka 1965 kwa mara ya kwanza;

Kwa kifupi, mwalimu hakuweka provision of WHAT IF baadae another political party wins visiwani, na chama kingine wins bara katika uchaguzi mkuu; katika hali ya kuchanganyikiwa, mfumo wa vyama vingi ulipo ingia, mwalimu akampa Jaji Bomani jukumu la kutafuta suluhisho juu ya hili, na ndipo Jaji akapendekeza mfumo wa mgombea mwenza unaotumika Marekani; kwahiyo, mfumo wetu wa muungano upo based on muundo wa Unitary Government wa Uingereza na Federation government ya Marekani, kuwaunganisha wananchi walio mbali kabisa from these two contexts; Kama wahenga wetu walivyonena, mshika mawili, moja humponyoka, .... Surely, this was not going to work, na ndio maana leo tupo kwenye mgogoro huu mkubwa kwa kujitakia;

Mkuu Mkandara, inastaajabisha wewe kutoona madhaifu kama haya, ambayo ni muhimu tuyarekebishe ili tuweze kujenga muungano ulio imara; nitafafanua mengi zaidi katika makala yangu ya kumuunga mkono Tundu Lissu juu ya msimamo wake kuhusu muungano wetu;
 
Mkuu Mkandara,
Tuliache suala la mtikila na madai yake ya mamilioni, naomba uelewe kwamba msingi wa hoja yangu ni madai ya Tanganyika hata kama mtikila hata husishwa; Lakini kabla sijaenda mbali, naombe nisema kwamba: Nitakuwa mwehu kama itaeleweka kwamba Mchambuzi anapinga muungano; Naomba iende on records kwamba sipingi muungano bal mfumo wake, na ninapendelea tuwe na serikali tatu kwani hivyo ndivyo tutaweza kuimarisha muungano huu ambao hakika tunauhitaji sana, na kama tunautakia mema, ni lazima tuache siasa na viini macho na tuangalie realities, vinginevyo tutauvunja bila kutegemea;

I strongly believe in panafricanism above all, na ni Nyerere ndiye ambae alimpinga Kwame Nkrumah juu ya THE MEANS TOWARDS A UNITED STATES OF AFRICA; lakini cha ajabu, ni yeye alikuja kukosea kuhusu the MEANS kwa Tanzania; with all due respect to Mwalimu, hapa alikosea na nisingependa kuwa mwoga au mnafiki kuweka msimamo huo;

On the one hand, Nyerere alihimiza umuhimu wa kuanza na regional blocks kama vile EAC, ECOWAS lakini muhimu zaidi kwana kulikomboa bara zima kwanza, kabla ya fikra za Nkrumah za UMOJA WA AFRIKA; On the contrary, Nkrumah yeye alitaka Afrika iungane right away; in the short run, Nyerere alionekana dhaifu kihoja na Nkrumah akageuka kuwa a REAL PANAFRICANIST, lakini baada ya miaka mingi, sasa historia imempa alama ya "A+" Mwalimu Nyerere juu ya means towards a UNITED STATES OF AFRICA, huku Nkrumah akipata tu credit ya kuanzisha wazo hilo but marks anazopata kwenye suala la MEANS ni ndogo sana ingawa sio "F";

With all due respect to muungano and Nyerere's vision, kwa kweli he rushed suala hili sana, may be because it transpired in the womb of Cold War ambapo marekani walikuwa wanaogpa sana Zanzibar pengine isigeuke kuwa another Cuba, especially baada ya vurugu za Chege kule East Congo; Mbaya zaidi ni kwamba muungano pamoja na kuwa ni wazo zuri, ulijengwa kwa mfumo wa kuiga iga hiki na kile kwani hauku reflect realities on the ground bara na visiwani licha ya kwamba zanzibar na ukanda wa pwani wa tanganyika ulikuwa na historia na muingiliano wa muda mrefu, na hata kuwa himaya moja ya Sultani katika kipindi fulani; Vinginevyo muundo wake uliiba a few elements za United Kingdom, na hili Nyerere alilizungumza wazi na lipo kwenye vitabu vingi vya historia; kwa mtazamo wangu, hili likawa kosa la kwanza, na kosa hili lilikuja kuwa dhahiri zaidi pale assumption za Mwalimu kwamba pengine Tanzania ingeendelea kuwa nchi ya chama kimoja for the next unforeseable future ilipogota, kwani katika suala la muungano, suala la vyama vya siasa halikutajwa - halikuwepo na bado halipo kwenye hati ya muungano, lilikuja ingia baadae kwenye katiba ya muda mwaka 1965 kwa mara ya kwanza;

Kwa kifupi, mwalimu hakuweka provision of WHAT IF baadae another political party wins visiwani, na chama kingine wins bara katika uchaguzi mkuu; katika hali ya kuchanganyikiwa, mfumo wa vyama vingi ulipo ingia, mwalimu akampa Jaji Bomani jukumu la kutafuta suluhisho juu ya hili, na ndipo Jaji akapendekeza mfumo wa mgombea mwenza unaotumika Marekani; kwahiyo, mfumo wetu wa muungano upo based on muundo wa Unitary Government wa Uingereza na Federation government ya Marekani, kuwaunganisha wananchi walio mbali kabisa from these two contexts; Kama wahenga wetu walivyonena, mshika mawili, moja humponyoka, .... Surely, this was not going to work, na ndio maana leo tupo kwenye mgogoro huu mkubwa kwa kujitakia;

Mkuu Mkandara, inastaajabisha wewe kutoona madhaifu kama haya, ambayo ni muhimu tuyarekebishe ili tuweze kujenga muungano ulio imara; nitafafanua mengi zaidi katika makala yangu ya kumuunga mkono Tundu Lissu juu ya msimamo wake kuhusu muungano wetu;
Katika hilo mkuu wangu tupo wengi sana tu tunahoji Muungano lakini kwa mwenye kufahamu ataelewa wazi kwamba ndio njia pekee ilituwezesha kuwa pamoja kwa miaka karibu 50. Nina hakika serikali tatu ingekufa hata kabla ya miaka 10, serikali moja isingechukua miaka 10 kwa sababu sisi MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO na tutaendela kuwa watumwa wa fikra za kugawana umaskini. PanAfricanism isingewezekana ikiwa hili dogo la nchi mbili tu limetushinda wala sio sisi tu Tanzania bali nchi kibao zimetengana baada ya miaka 10 na zinaendelea utengana kila siku. Sasa tunagombania mipaka tena ya maji ambako watu hawaishi isipokuwa kuna nmafuta, halafu wanasema kwa nini hatukuweka mipaka yetu wakati wa Uhuru. Hapo PanAfrica utaitazama wapi na viongozi wa leo kina mama banda wanaotumia ushahidi wa mwaka 1800..

Kama Tanganyika ingekuwepo nina hakika Wazanzibara wangepewa taabu sana kuishi Bara na pengine ubaguzi ungeendelea hadi ktk makabila. Kuna kila sababu Nyerere alitumia kuondokana na ubaguzi iwe kufuta kabisa matumizi ya lugha zetu za asili na kukiweka kiswahili.. Mtu unaweza kusema kwa nini nazuiwa kuongea Kikerewe ama kufundishia Kikerewe ikiwa watoto wote wa Ukerewe wanazungumza Kikerewe fluently kuliko Kiswahili. Kwa nini alitaifisha mashule na kadhalka wakati makanisa walikuwa na asimilia 90 nya shule zote nchini.. Haya yote ukiyatazam kwa jicho la Ubinafsi utaweza kabisa kuitafuta sababu na hakika mengi ya haya huwezi kuweka kura za maoni maana mnawanyima wananchi UHURU pale wanapoendekeza Ukabila, Udini au Utanganyika..

Pamoja na yote, kwa nafasi ulokuwa nayo wewe na uwezo wako ktk kufikiri bila shaka wewe na Mtikila ni mbingu na Ardhi. Hafai kabisa kutolewa mfano mzuri isipokuwa ni mtu wa kumwogopa na mt yeyote mwenye kuelewa undani wa mtu huyu mnafiki anayeishi ktk ngozi ya Kondoo na kujifanya Mchungaji baada ya kushindwa maisha ati kaijiwa na Roho mtakatifu kumwongoza njia inabidi tuwe makini sana na matapeli kama hawa..
Utanisamehe sina maana mbaya kwako ila nilipigwa na mshangao sikuamini nilipokusema..lakini ndivyo ukweli mwingine hautakiwi kufichwa na ktk kupitia haya sasa tumeweza kuelewana.
 
Mchambuzi
Unasoma makala za Mzee Mwanakijiji hukusu Muungano?
Unasoma michango ya Nguruvi3 na JokaKuu kuhusu Muungano?

Hawa watu wanawafundisha wazanzibari kujitoa kwenye Muungano lakini hawashajihishi au kutoa elimu kwa wadanganyika kudai Tanganyika.

Katika JF hawa ni watu wa fikrapevu lakini linapokuja suala la kudai Tanganyika na serikali ya Tanganyika huwa wanakuwa kama kuku aliyemwagiwa maji. Huwa napata mashaka wakati mwengine kama Chai Chapati Maharage wamewaweka mfukoni au ni kuhofia utaifa wa Tanganyika dhidi ya utanzania?
Mbona utaifa mbili unawezekana? (dual nationality), mfano british lakini pia ni english, scotish au welsh.

Bado hata Lissu ameishia kauli ya kusema upo umuhimu wa kuirudisha Tanganyika, vitendo bado (awasilishe mswada bungeni unaodai kuirudisha serikali ya Nchi ya Tanganyika ili kumaliza hiki kiini macho.
Liko wapi kundi jipya la G55 au G110?

Hiki ni kipindi cha kutoa maoni kuhusu katiba mpya, hakuna anaetoa elimu kwa wananchi kudai serikali ya Tanganyika bali wapo akina MMjj na Nguruvi3 wanaotushajihisha tudai serikali moja.

Siasa za Tz zinaweza kumtia mtu maradhi ya moyo.

Nguruvi3, Mzee Mwanakijiji karibuni katika hili kundi la kudai serikali ya Tanganyika na saa ya ukombozi ni sasa!

Mkuu Nonda,

Ninavyowaelewa Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3 na Joka Kuu ni kwamba wao kwa kiasi kikubwa ni Nkrumanists ambao, just like him, they tend to believe zaidi juu ya A UNITARY AFRICA OR UNITED AFRICA, hence this belief shapes their ideas kuhusu mfumo wa muungano wetu; This is one of the two schools of thoughts on Panafricanism; the other school of thought ni ile ya incremental integration ambayo i would call it Nyerereist, ambayo inaamini katika kuanza liberation of Africa, then regional blocks kama SADC, EAC, ECOWAS etc, not a rapid integration kama ile aliyohimiza Nkrumah; ni katika hili ndipo Nyerere na Nkrumah walianza kujenga tofauti baina yao kuhusu vision zao juu ya Afrika; Lakini for some reasons, ghafla Nyerere decided to apply kwa kiasi kikubwa sana the Nkrumanism approach kwenye suala la muungano wa Tanganyika na Zanzibar contrary to his earlier subscription;

All that being said and done, the original Nkrumanists and Nyerereists juu ya suala la muungano wa Afrika wote wapo sahihi, tatizo linakuja kwenye implementation; Kwahiyo kama nipo sahihi kuhusu Mzee mwanakijiji, Nguruvi3 na Joka Kuu kama ulivyowajadili, mtazamo wao ni sahihi kabisa, ni kwamba tu wajiandae na MGONGANO WA MAWAZO;
 
I beg differ with you. Ukitaka utawala wa haki na sheria ni lazima ujifunze au uwe na utaratibu wa kufuata vyombo vya sheria. Mtikila anatumia katiba japo haipendi. Na anakwenda mahakama japo kuwa mahakama zetu ni za kubabaisha.

Viongozi wengi wa upinzani wameisoma katiba baada ya uchaguzi wa 2010. Na mahakama hawataki kuitumia. Je utamaduni wa kutumia katiba, sheria na mahakama watejenga lini? Wakiwa watawala?

Naweza kusema pasi ya shaka kuwa udhaifu mkubwa kabisa wa CHADEMA kama chama ni kushindwa kwake kutumia mahakama kuchallenge the status quo. Hili linanishangaza sana na sijalielewa hadi leo hii. Hata kama wao hawataki kufungua kesi basi wajibambikize kwenye kesi za Mtikila ili angala waonekane kuwa in "principle" wanakubaliana na hoja zake. Lakini wapi. Ikumbukwe ushindi wa Mtikila ni upepo ambao CDM wanaweza kutumia kusukumizia ngalawa zao. Lakini kwanin pamoja na umaarufu wote hawajafungua kesi yoyote ya kikatiba ambayo wakaisimamia hata kushinda? siyo hivyo tu, kwanini na wenyewe wasifanye trial cases za kuchallenge vitu fulani fulani.

Kwa mfano, CDM inaumizwa sana kwa kukosa wapiga kura - mashabiki ambao wamegeuzwa kuwa wapiga kura - kwa sababu ya kuchelewa kujiandikisha au kutoandikishwa kutokana na mfumo wa sasa ulivyo. Kwanini basi wanaendelea kwenda kwenye uchaguzi wakti ili washinde inawapasa watumie nguvu zaidi kuliko kawaida. Kama gari limekwema zipo njia nyingi za kulikwamua; kusukuma, kuweka magogo, kuchimba udongo au ikibidi kusubiri gari jingine lije kuvuta huku watu wanasukuma. Mahakama ni kama gari hilo.

Wanasiasa wa CDM wanaweza kujikuta wanakumbukwa kwa umati wa watu waliokuwa wanakusanya, kwa hotuba motomoto za kusisimua na jinsi walivyoweza kuichachafya CCM Bungeni na kwenye vyombo vya habari. Lakini Mtikila ataukumbukwa kama mwanasiasa aliyebadilisha welekeo wa siasa za Tanzania bila umati wala jukwaa la Bunge. It is true.
 
Kwangu binafsi Mtikila will never be a hero. Bado nashangilia kile kichapo alichokipata Tarime.
 
Kweli mkuu, Mtikila ni shujaa wa demokrasia ya Tanganyika aliyepuuzwa lakini mpiganaji wa ukweli. Only time will tell!
 
Huyu Mtikila hata UHURu wetu aliupinga akisema wazungu walikuwa watu bora sana ndio walotuletea ustaarabu (dini) na kadhalika leo waondolewe kwa kuitwa mabeberu!. Alipingana na dhana nzima ya Uhuru wa mwafrika leo mnamwona ndiye hero wenu? ama kweli sasa naanza kuelewa wapi hasa tunapogongana..

Mzee hapa usiende mbali sana; Mtikila ni shujaa wa demokrasia kama nilivyoonesha hapo juu tu kidogo. Kwamba, ni Mtanzania pekee aliyekataa sheria ambazo zilikuwa zinambagua na akaenda mbele na kuzipa changamoto kwa kutumia mfumo ule ule. Nguvu zake za hoja zimeshinda mara nyingi kuanzia mwaka 1993. Ameweza kufanya kwa kweli kile ambacho kimetushinda wengi wetu. Kumshika ng'ombe mapembe na kumuweka zizini. Historia ya siasa za Tanzania haiwezi kabisa kuandikwa bila kumtaja Mtikila na mchango wake katika kukuza haki za kiraia.

Ni shujaa wangu kwa namna ya pekee kwa sababu ni mtu mmoja ambaye ni mbishi na asiyeheshimu watawala na ving'ora vyao. Tena yeye hakuanzia na kina Kikwete tu kaanza na kina Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete. Hana huruma kabisa na wala hana heshima mbele zao. Hakuna mwanasiasa mwingine aliyethubutu hivyo. Of course, siwezi kusema ndiye mwanasiasa ninayemhusudu zaidi katika Tanzania la hasha na wala hafikii kwa mbali wale ninaowahusudu kama wanasiasa. Yeye kwenye eneo moja he has done better and greater than any other politicians. Na huwa wanasema "give the devil his due" au tunavyosema "mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni" (japo sielewi kwanini wamnyonge kama anayo haki).

Mtikila alivyoumbuliwa na Rostam was classic lakini yenyewe haiondoi ukweli wa anachosimamia. Nimesoma wengi wamemfutilia mbali ati kwa vile alimuomba Rostam fedha kama deni na Rostam akampa. Kinachonishangaza sana na nimewasoma wengi hapa wakirudia hilo la Rostam kumpa fedha Mtikila na limeniacha na maswali. Watu wameamini kabisa bila kuhoji wala kujiuliza kama Rostam alisema kweli na kama alisema ukweli wote wa suala la fedha zile. Na wengi wanakumbuka kabisa alichosema Rostam lakini wachache (sijaona hadi hivi sasa hata mmoja) anayekumbuka majibu ya Rostam juu ya madai ya kupewa fedha Rostam. Lakini cha kushangaza zaidi ni kuwa watu wanasahau kuwa Rostam ndiye aliyejiuzulu (kama wengine tulivyoitisha) kwa kuwa kashfa za ufisadi zilikuw zimemzidia! Sasa huyu Rostam kwa wengine amegeuka mara moja mtu wa kumtolea mfano?

Lakini jambo jingine la kushangaza ni kuwa wapo watu hapa wanataka tuamini kuwa ukiwa na njaa usiombe chakula- hata kwa adui yako! Kwamba kwa vile mtu fulani ni adui yako wa kisiasa basi kama yuko katika uwezo wa kukusaidia usikubali msaada wake? Ya kweli haya? Lakini huyo huyo adui siku ya msiba wako atakuja na kutoa pola na watu watapokea? Hatujafika mahali pa uadui wa aina hiyo (japo labda wapo wanaomini kuwa iwe hivyo). Kwamba kwa vile Mtikila anampinga Rostam (na alifanya hivyo hata baada ya kupokea hizo fedha) basi Mtikila hapaswi kupokea msaada kutoka kwa Rostam? Really? Ni nani kati yetu ambaye watoto wakiwa wakiwa wagonjwa au yeye mwenyewe ambaye akiletewa msaada na adui yake hatopokea hasa kama ni msaada ambao kweli unaweza kumsaidia? Leo hii mimi binafsi kuna watu ambao tunatofauti kubwa sana za kisiasa (na labda wanniweka kama adui yao) sasa kweli unafikiria nikimkuta kaanguka au kaumia basi nitamwambia "ukome" ati kwa sababu ya tofauti za kisiasa? Well, siwezi kusema kuhusu wao lakini siwezi kushangaa kuwa wapo watu ambao wanaweza kusema kuwa adui yangu wa kisiasa kapatwa na baya basi akome na akomege!! Lakini watu wenye dhamiri hawawezi kufanya hivyo? Kuna mtu ameuliza Mtikila alienda kuomba fedha za nini kwa Rostam? Wengi wameshasema hapa kuwa Mtikila anaishi maisha ya dhiki kulinganisha na wengi tu sasa tunajuaje wakati huo kweli maji yalikuwa shingoni? Wanasema "angekufa kiume tu ndio aombe msaada kwa Rostam"?

Kuna uadui ambao kweli mtu hata kumpa maji unaweza usimpe lakini huu wa kisiasa sidhani. Ni kweli kinadharia ningeweza kusema Mtikila asingemwomba Rostam msaada na Rostam asingempa Mtikila msaada. Lakini sisi ni nani wa kusema kuwa asingeombwa na yule asingeomba? Wapo watu katika historia ambao katika ugumu wa shida waliomba msaada wa maadui zao nao wakasaidiwa na kuopolewa. Wakati wa vita ya pili ya dunia kuna mifano mingi ya matendo ya kibinadamu kati ya maadui wengi tu. Wapo waliojitoa mhanga kusaidia maadui zao bila kubadilisha uadui uliopo. Ndio ubinadamu wetu.

Sorry nimeenda kuzama kidogo kwenye hili maana limenikumbusha kisa cha rafiki yangu mmoja ambaye aliporudi nyumbani miezi kadhaa nyuma alijikuta ananyimwa usafiri wa gari pale alipojaribu kuitetea CCM. Watu wanakumbuka ya CUF na CCM kule Pemba kabla ya "maridhiano" ambapo watu hata kuzikana walikuwa hawazikani kisa "huyu CCM" na hyule ni "CUF". Tusiache siasa zetu zifikie huko.
 
Vyovyote vile alivyo. Mtikila ni shujaa. Kikwazo kikubwa alichonacho ni yeye kuwa mbele miaka kumi ya akili za watanzania wengi.
 
Hakuna mwanasiasa yeyote nchini tangu uhuru ambaye amepigania haki za kiraia na kushinda kama Christopher Mtikila. NInaamini historia itakuja kumkumbuka kama shujaa wa demokrasia kwani pamoja na yote ambayo amepitishwa ameendelea kusimama kudai haki za raia wa Tanzania kwa namna ambayo mahakama zimekuwa upande wake mara ZOTE!

Leo hii napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa mtetezi huyu wa haki za raia. Ni mwanasiasa pekee ambaye amefanikiwa kulazimisha serikali kufanya isiyotaka kufanya na hata ilipokataa kufanya ametuwezesha kuona kuwa serikali haitaki kwa sababu tu haipendi si kwamba hoja ziko upande wake. HE IS MY HERO!

Ukweli ni kuwa amewapita kwa mbali sana wale wanasiasa wetu ambao labda majina yao ni maarufu sana na ambao wanaonekana ni maarufu; siyo tu Mtikila anazungumza anachozungumza bali anafanya pia anachozungumza. Of course, haiondoi ukweli mwingine wa mapungufu yake au siasa zake lakini ukweli ni kuwa kila alipojaribiwa na watawala amewashinda. Rekodi yake ya ushindi kwa miaka ishirini na ushee sasa inasimama kama ushahidi wa ushujaa wake.

Inasikitisha haijatokea wanasiasa wengine wa upinzani hata mara moja kuwa sehemu ya kesi zake au kuonekana wanajiingiza kama friends of the court (amicus curiae) kuonesha wanaunga mkono hoja zake.

When it comes to the 'walking' Mtikila does the walk!

mtetezi wa haki za raia then polisi wamwangalie tu? ni kweli analeta changamoto, lakini isiyo na madhara kwa utawala/serikali, kama ingekuwa na effect- basi ungeona jinsi ambavyo angeshughulikiwa kiukweli. mara nyingi anashindana na kutoa challenge kwa mahakama, lakini kwa ajili yake binafsi, hebu ajaribu kutetea jambo kwa ajili ya mtu mwingine tuone kama atabaki hivyo. ajaribu kutetea mauaji ya mwangosi au utekaji na uteswaji wa ulimboka, achachamae sana -tuone huo ushindi atakaoupata. nina maana aingilie kati mambo au issue zinazohusu/kugusa jamii moja kwa moja
 
aliponifurahisha ni pale alipomwambia yule karagosi, 'huwezi nikamata mimi. We mtu wa cheo kidogo sana...'
 
Mkuu Mchambuzi naisubiri siku ukiishusha tafadhali nijulishe unajua JF ina mada nyingi sana wakati mwingine unaweza kupitwa na mambo ya maana.

Sawa sawa mkuu, nimekuwa naandaa mjadala wa namna hiyo, hasa nikilenga kufafanua kwanini Lissu yupo sahihi anaposema muungano wetu ni kiini macho; nitakuwa tayari na mada hiyo kabla ya mwisho wa mwezi;
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom