Mtikila ndani kwa uchochezi!!!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
48,851
18,948
Mtikila kortini kwa uchochezi

2008-08-05 10:35:17
Na Hellen Mwango

Mchungaji Christopher Mtikila, jana alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, akikabiliwa na mashtaka ya kutoa lugha ya uchochezi na kudai kuwa Rais Jakaya Kikwete ni gaidi.

Mtikila alisomewa mashtaka yake jana mbele ya Hakimu Mkazi Focus Mkeha wa mahakama hiyo.
Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Charles Kenyella, alidai kuwa, Oktoba 21, mwaka jana, eneo la Ilala katika kota za Shirika la Nyumba (NHC) zilizopo karibu na Kiwanda cha Bia (TBL), jijini Dar es Salaam, mshtakiwa alitoa lugha za uchochezi.

Ilidaiwa kuwa, maneno hayo yalikuwa ya kuikashifu serikali na kwamba yalisababisha upotevu wa amani kwa wananchi.

Kenyella, alinukuu maneno ya Mtikilila akidai kuwa, ``Papa alikuwa na mgeni ambaye ni gaidi ninaomba niseme haya kwa sababu ninasema mimi, Rais Kikwete ni gaidi wa kwanza kutaka kupeleka bungeni,`` alinukuu kupitia hati ya mashtaka.

Katika shtaka la pili, Mtikila anadaiwa kuwa, siku na eneo la tukio la kwanza alitoa lugha ya uchochezi na kudai kuwa, ``ahadi zote za Jakaya Kikwete siku zote zinaongozwa na imani yake ya dini, tena kutekeleza malengo yake ya kusilimisha nchi, ``hatuwezi kuvumilia mtu anayekuwa muhuni aongoze nchi``.

Mtikila alikana mashtaka yote ambapo upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika na kwamba uliomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Hata hivyo, Hakimu Mkeha aliahirisha shauri hilo hadi Agosti 22, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
 
Mambo hayo yamewakuta MaCUF wa Zanzibar mpaka wameyazoea na nyie msilegeze mwendo ,mwisho mtazoea si mlimsikia Dr Karume akiwambia waZanzibar kuwa shida ya umeme wataizoea eti na yeye hapati usingizi kwa kelele za majenereta.Yaani Tanzania ni vituko vitupu .
 
Huyu Mchungaji huku akitoka salama sijui,maana hapa naona kuwa tangu alipotamka haya maneno leo ndio wanamaliza uchunguzi ama sijui tuuite ni upelelezi wa kauli husika ?

Ama baada ya kukorofishana na RA kuhusiana na mchango wa kanisa basi ikaonelewa kuwa isiwe shida aende gerezani tuu....
 
Mtikila anataka kuvuka mpaka, kuna struggle na vita dhidi ya mafisadi halafu kuna kupayuka kuliko destructive, sasa Mtikila pamoja na point zote anazokupa Kikwete umbane unataka kujipa kazi ya ku prove ugaidi wa Kikwete? In Tanzania where Kikwete's is effectively the state a la King Louis?

Hapo anaweza kupigwa misheria kandamizi ya sedition na kupigwa ma clause ya usalama wa taifa mpaka akome mwenyewe.

Lazima kupanga mashambulizi kwa kina, sio kupayuka tu mradi mdomo haulipiwi kodi kwa maneno.
 
Hii kesi si ndogo hii...Maana tuhuma za Mtikila ni NZITO.
Sasa na yeye akiombwa atowe ushihidi ndio itakuwa kazi.
Na kama HANA USHAHIDI KUWA JK NI GAIDI...BASI ANAWEZA OZEA JELA.
Hii ina maana hata mimi nikirudi Bongo nitafunguliwa mashtaka...Ila mimi ushahidi wangu wa Umafia...Issue ambayo ilipelekewa mimi kufungiwa hapa itatokana na ukweli kuwa mpango mzima wa UFISADI ambao una kila sifa ya umafia...Mpango huo mchafu wa kuliangamiza Taifa usiposimamiwa na kushughulikiwa na viongozi wetu wakuu wa nchi ikiwa ni pamoja kuhakikisha uwajibikaji...Kama lisipofanyiwa kazi na mkuu wa nchi ni nani mwingine anayestahili kupewa cheo hicho cha umafia?
Kama vile wakuu wengine wa nchi wanapoulizwa maswali kuhusu matatizo ya wananchi na wanapokataa kuyajibu ama kuyafanyia kazi...Matokeao yake ni MACHAFUKO.
Na kama kweli anataka aitwe muungwana...BASI AZIFANYIE VITENDO KASHFA HIZO NA SI VINGINEVYO.
 
eti "Mtikila ndani kwa uchochezi!!!" Mkuu kushtakiwa mahakamani kuna maana tofauti na 'ndani' labda kiswahili cha kijelajela kinakupiga chenga.
 
Ujinga mtupu pesa za walipa kodi zinapotea kwa jambo la kipumbavu kama hili. Waswahili walisema maneno matupu hayavunji mfupa. Wameshindwa kuwashitaki waliokula pesa za EPA, Richimondulian, etc. Sasa wanakomalia upumbavu kama huu. Hata walioua waliachiwa, itakuwa hili.

Kama yeye sio gaidi kwa nini wanamshitaki? Absolutely stupid.
 
Huyu Jamaa mahakamani ameshaona kama ni sebuleni kwake....amekua sugu wakwenda mahakamani na yeye mwenyewe anapenda sababu anajua atashinda na jina litakua....aisingekua anapenda asingeweza kua anabwabwaja bwabwaja tu maneno kama bata nakuropoka ovyo.....mi naona huyu bwana ameona atoke kwa stahili iyo...sasa ni bora wamfunge ki ukweli .....kwanza kashatukera na ufisadi wake wakujificha.....anapiga keleleee kumbe ni mshkaji wake na rostam....hana maana tena huyu..
 
Huyo mshikaji hawamuwezi na ninavyosema hao polisi wa upelelezi watakosa ushahidi wa kumpeleka gerezani huyo jamaa. Huyo tabia yake iko hivyohivyo tokea sekondari aliwahi kutoa tuhuma dhidi ya headmaster wake kuwa shuleni kwao wanapewa chakula sawasawa na wanyama huku yeye kalihifadhi bakuli lake la chakula muda wa siku kadhaa jamaa walivyokuja kukagua shuleni jamaa akalitoa kwenye loka ikawa noma juu ya soo. Huyo jamaa hawamuwezi . Kantalamba wanamtambua huyo hawamuwezi....
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom