Mtikila kuwaburuza mawaziri wa JK mahakamani

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779
MWENYEKITI wa chama kidemokrasia (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, anaandaa utaratibu wa kuwafungulia mashtaka Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Philip Marmo kwa kuidharau Katiba.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Mchungaji Mtikila alisema kitendo cha viongozi hao wawili kwa nyakati tofauti kueleza kuwa suala la mgombea binafsi haliwezekani na linahitaji lipelekwe kwa wananchi kwa ajili ya kura za maoni ni kuvunja Katiba.
“Utaratibu wa kuwasimamisha kizimbani Marmo na Membe kwa kuvunja Katiba na sheria kwa kuthubutu kuifanyia jeuri na dharau mahakama ya nchi uko palepale,” Mtikila alisema.
Mwenyekiti huyo wa DP alisema kwa sasa wanasheria wake wanashughulikia kesi nyingine zipatazo tisa za Kikatiba lakini suala hilo litashughulikiwa hadi haki hiyo kwa Watanzania ipatikane.
Alisema hoja ambazo zimekwishatolewa na mawaziri hao pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Rajab Kiravu, ni porojo na haziwezi kuathiri utendaji wa mahakama.
Aliukosoa utetezi wa Waziri Marmo kwamba muda hautoshi kwa kuandaa mazingira ya mgombea binafsi kwa vile suala hilo linahitaji umma kushirikishwa na kusema hiyo ni haki ya Kikatiba, haihitaji umma kuulizwa iwapo wanaitaka.
Mtikila alisema amri ya mahakama kuruhusu mgombea binafsi ilitolewa Mei 5, 2006 na kuwatuhumu watendaji wa serikali akiwemo mwanasheria mkuu kufanya njama za kutotekeleza amri hiyo kwa miaka minne sasa.
“Pili, hakuna mabadiliko kufanywa katika Katiba wala mahakama haiamuru hivyo kwa sababu Katiba ndiyo inayotoa haki hii kwa kila raia hasa Ibara ya 21 (2)...mahakama tu ndiyo inayotoa haki nchini ya kutafsiri sheria pamoja na Katiba ...siyo Marmo, Membe wala Rais Jakaya Kikwete,” alisema.
Akinukuu maneno ya Waziri Membe aliyoyatoa kwa mabalozi baada ya kukutana nao katika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Mchungaji Mtilila alisema hatua ya kuwataka mabalozi wavute subira juu ya suala la mgombea binafsi ni kuliuza taifa.
Katika hilo, mwanasiasa huyo anayeongoza kwa kufungua kesi nyingi dhidi ya serikali, alisema waziri huyo ameuza uhuru wa taifa kwa kitendo chake cha kuwanyima Watanzania haki yao huku akijadiliana na wanadiplomasia hao.
“Membe amethibitisha tabia inayowachukiza wananchi kwamba wanaotawala nchi yetu hawana ridhaa ya wenye nchi, bali wanajisalimisha kwa mataifa makubwa,” alisema.
Alisisitiza kwamba suala la kugombea uongozi ndani ya nchi ni nyeti na ni la utaifa ambalo kulitafutia uhalali kwa mataifa mengine ni kuuza uhuru wa nchi, kosa alilolifananisha sawa na uhaini.
Aliushutumu uongozi wa Rais Kikwete kwa kutaka kuhujumu haki hiyo na kutabiri kutokea machafuko yatakayoifanya Tanzania kutengwa na jumuiya za kimataifa.
Alisema mbinu ya kuzima suala la mgombea binafsi inayofanywa na watendaji wa Rais Kikwete inatokana na hofu ya kumpata mgombea atakayechuana naye katika kinyang’anyiro cha urais Oktoba.
“Rais Kikwete hata akifaulu kuzima ushindani ndani ya chama chake, ataibuka mgombea binafsi na wanachama wote watamfuata na kuiacha CCM inamfia mikononi,” alisema. Aliongeza kwamba baada ya usajili wa Chama cha Jamii (CCJ), hatma ya CCM ilianza kuwa mashakani kutokana na ukweli kwamba
 
Hold on,tafadhali naomba rekebisha kichwa cha habari kwanza.

Mkuu,kichwa cha habari kinapotosha.

Ungeweza kuweka Mtikila kuwaburuza mawaziri wa JK mahakamani

au

Mtikila awageukia mawaziri wa JK

au

Mtikila kuwashtaki mawaziri wawili wa JK.
 
Kaka MBARONI ninavyoelewa mimi ni kukamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi lakini kushtakiwa sio kutiwa mbaroni.
Labda ungerekebisha kichwa cha habari.
By the way thanks a lot.
 
You know, the recent statement by the Chief Justice on the Independent Candidates has really rattled the JK regime out of its hole. Walifikiri kuchelewesha rufaa hadi 2010 (tangu 2006) ingewasaidia lakini it has cought them with pants down! Wanatapatapa. Anachosema Mtikila ni kitu cha maana kwa vile Mahakama inasema kugombea madaraka ni haki ya msingi kabisa kama ilivyokula, kulala na kwenda msalani. Huwezi kusema tuwaulize wananachi kama tule au la. Vile vile huwezi kuwauliza watu kama wanataka kugombea madaraka kupitia vyama vya siasa au la. That is the point and the regime is scared stiff!
 
ni kweli byasel ila kwa serikali yetu unafikiri watakubali br
tutaishia kununua magazeti kama sijakosea
 
Kimsingi Mtikila ana point kwa sababu mahakama ikishatoa maamuzi ya namna hii ilikuwa kazi ya wizara husika kutengeneza draft bill ya mabadiliko ya sheria zote husika ikiwemo katiba ambayo ni sheria mama na kuzipitisha kwa vyombo husika kuzipitia kabla ya kupeleka final draft bungeni. Sasa serikali imekalia swala hili tangu 2006 hadi leo ili waanze kuja kubabaisha watu mwaka huu wa uchaguzi. Is this a good governance or mere politics? A justice delayed is not a justice at all, we needto see the justice be done. Lawyers, kindly assist Mchungaji on this matter so that the justice can be done as soon as it deem fit. Naona Serikali inaleta madharau kwa muhimili mwingine wa dola.
 
Ama kweli hapa mchungaji amekua mwiba! Napenda mambo kama haya, yanazidi kudhihirisha kuwa ufisadi unaleweshaaa!! na umelaaniwa na Mnyazi Mungu!
 
Serekali inatakiwa kuheshimu uamuzi wa mahakama sasa inapotokea mawaziri ambao ni washauri wakuu wa Rais wanapotosha umma kwa maksudi au kwa faida za kisiasa nchi inaweza kutumbukia kwenye migogoro isiyo na sababu.
 
Mtikila ukimaliza hiyo - buruza na nyingine ya kudai Tume Huru ya Uchaguzi - Bara. hii iliyopo ni ya CCM.
 
Back
Top Bottom