Mtikila atafuta fedha kumfungulia kesi Pinda...................

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,380
911,169
Mtikila atafuta fedha kumfungulia kesi Pinda
Saturday, 04 December 2010 22:36

Mwandishi Wetu
MWENYEKITI wa Chama cha DP, Mchungaji Cristopher Mtikila amesema anatafuta Sh 10 milioni za kumfungulia kesi ya kupinga ushindi wa ubunge Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na wabunge wengine waliopita bila ya kupingwa katika uchaguzi mkuu uliopita.

Kutokana na uamuzi huo wa Mtikila baadhi ya mawaziri na wabunge kadhaa wano watapandishwa kizimbani kuomba mahakama ibatilishe ushindi wao.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana, Mtikila alisema kuwa ameshindwa kutimia azima yake hiyo kutokana na ukosefu wa fedha za kufungulia hiyo kesi.

Alisema hivi sasa anahamasisha watu wamchangie fedha hizo ili aweze kufungua kesi hiyo ya kikatiba nchini.

Lengo la Mtikila ni kufungua kesi kwa kile kinachoeleza ni kushinda kwa njia zisizo sahihi kulingana na vipengele vya katiba ya nchi, hivyo kuitaka mahakama itamke kuwa ushindi wao ni batili.

Mbali na waziri mkuu, mawaziri watakaokumbana na hali hiyo pamoja na majimbo yao katika mabano ni Profesa Anna Tibaijuka (Mbunge wa Muleba Kusini) ambaye ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Waziri wa Maji Profesa Mark Mwandosya (Rungwe Magharibi) na William Ngeleja (Sengerema) Waziri wa Nishati na Madini.

Wengine ni Philip Mulugo (Singwe), Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, na William Lukuvi (Ismani), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge).

Wamo pia Celina Kombani (Ulanga Mashariki), Waziri wa Katiba na Sheria; Gregory Teu (Mpwapwa) ambaye ni Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, pamoja na Ezekiel Maige ambaye ni Waziri wa Maliasili na Utalii.

Wengine ni Spika wa Bunge Anne Makinda (Njombe Kusini), na naibu wake, Job Ndugai ambaye ni mbunge wa Kongwa, nao wanapingwa na DP.

Wabunge wengine waliopita bila ya kupingwa ni Christopher Ole Sendeka (Simanjiro), January Makamba (Bumbuli); Nimrod Mkono (Musoma (Vijijini); na Deo Filikunjombe (Ludewa).
 
Nadhani hata mahakama ikitengua ubunge wao,basi tunabidi tuiombe mahakama iwaachie uwaziri wao,ili tuwe na mawaziri wasio wabunge kama kilio cha wengi kilivyo. Nashukuru!
 
Huyu naye sijui yukoje?????????, mbona anaanika utupu wake!!!!!!!!!!! Watamhonga halafu itakuwa kama Tarime!!!!!!!!!! Tarime alikula pesa za sisiemu halafu akambaulia ngeo ikawa ndiyo mwisho!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mtikila atafuta fedha kumfungulia kesi Pinda
Saturday, 04 December 2010 22:36

Mwandishi Wetu
MWENYEKITI wa Chama cha DP, Mchungaji Cristopher Mtikila amesema anatafuta Sh 10 milioni za kumfungulia kesi ya kupinga ushindi wa ubunge Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na wabunge wengine waliopita bila ya kupingwa katika uchaguzi mkuu uliopita.

Kutokana na uamuzi huo wa Mtikila baadhi ya mawaziri na wabunge kadhaa wano watapandishwa kizimbani kuomba mahakama ibatilishe ushindi wao.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana, Mtikila alisema kuwa ameshindwa kutimia azima yake hiyo kutokana na ukosefu wa fedha za kufungulia hiyo kesi.

Alisema hivi sasa anahamasisha watu wamchangie fedha hizo ili aweze kufungua kesi hiyo ya kikatiba nchini.

Lengo la Mtikila ni kufungua kesi kwa kile kinachoeleza ni kushinda kwa njia zisizo sahihi kulingana na vipengele vya katiba ya nchi, hivyo kuitaka mahakama itamke kuwa ushindi wao ni batili.

hivi huyu mtikila aliishia wapi katika kumfikisha pinda mahakamani? au kakosa hela......................???????
 
Kama ana vigezo vyote ushahidi wa kutosha buruza mahakamani.kwan kupita bila kupingwa kunakua na namna flan flan babuuu.hata mitume walipingwa sasa waliopita bila kupingwa wote ni zaidi ya mitume?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom