Mtikila akamatwa na polisi kwa kumkashifu Rais

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Polisi wa upelelezi (CID) kutoka makao makuu ya CID Dar es Salaam walimkamata Mchungaji Christopher Mtikila, jana saa 11 jioni (1700hrs) saa za Afrika Mashariki na kufanya naye mahojiano hadi saa 3.30 usiku (2100hrs) walipomuachia kabla ya kumkamata tena leo baada ya kumfanyia upekuzi nyumbani kwake Ilala flats, Block F 4 namba A 8, pale pale karibu na TBL, na sasa wamemshikilia Central Police station, hadi Jumatatu atakapopelekwa mahakamani.

Miongoni mwa matamshi aliyoyatoa ni pamoja na kumuita Rais Gaidi na mhuni. Katika mahojiano yote, Mtikila amekiri kusema maneno hayo na hakukataa hata neno moja na mengine makali zaidi na aliyahalalisha kwa kurejea maandiko mbalimbali
 
Hapo patamu, naona watu wameshachoka kabisa na mambo yanayoendelea nchini ndiyo maana amediriki kuyakubali matamshi yake bila kukana.Huyu ni mwanaharakati mwenye uchungu na nchi yake.
 
Kwa sasa Mtikila yuko Makao Makuu ya Polisi, akiendelea na mahojiano na maofisa waandamizi wa polisi
 
I respect Mtikila. Ana uchungu na nchi yake. Je ni kwa nini tusiwe na 100000000 mtilkilas? Tatizo viongozi wamejiwekea ukuta wa sheria kuwalinda! wafanye machafu na bado sheria iwalinde! Therefore tuwaache wafanye wafanyavyo. Hata Burma wachungaji waliamua kuingia barabarani. Ngoja mahakma ifanye kosa imtie hatiani Mtikila watakuwa wanasaign downfall of Peace ya ukondoo!!! kondoo atagaeuka mbuzi!!
 
Pole bwana Mtikila, hayo ndio mapambano ambayo wengi tungetaka yatokee. Mapambano ya kubadilisha katiba ili hata akija nani madarakani, asiwezi ku abuse katiba yetu.

Kweli kumwambia rais mhuni kunaweza kukufanya ulale polisi?

Polisi badala ya kutumia resources chache tulizo nazo kupambana na majambazi, mafisadi, na wavunja sheria wengine, wao wanamwandama mtu kama Mtikila ambaye msimamo wake unajulikana miaka na miaka.
 
Huyu Mtikila ataleta balaa na machafuko ktk nchi walivyofanya kumsweka ndani ni sawa kabisa. Juzi juzi hapa kawatukana waislam leo Rais tunakwenda wapi jamani huu uhuru gani usio na mipaka?
 
Mtikila sasa amekwishakuwekwa ndani Central, muda mchache uliopita.

Namheshimu sana Mtikila kwa kuwa mwenye msiamo na upeo mkubwa. Kuna mlolongo mkubwa wa mambo ambayo awali tuliomuona kama mwendawazimu, lakini sasa tunajivunia na kuyajadili na mengine tunayatamani. Baadhi yamepata hata baraka za mahakama.

Lakini katika suala la kutukana nadhani hapo amevuka mipaka
 
Mtikila anajulikana kama ni mzee wa biashara ya kesi.
Sijui katika hili la kushambulia watu analenga nini.
 
Mtikila anajulikana kama ni mzee wa biashara ya kesi.
Sijui katika hili la kushambulia watu analenga nini.

Nungunungu, sina hakika unaposema "mzee wa biashara ya kesi" lakini kuna taarifa kwamba Mtikila huwa analipwa kwa kazi ya kuchafua watu na kuna tuhuma kwamba alikua akitumiwa na wana mtandao, sasa je kwa hili la JK anatumiwa na wanamtandao gani? ama ndio ile mbinu za kumzunguka JK ili aahirishe kuwachukulia hatua mafisadi? Ndio maana sasa angalia JK amewekwa kundi moja na kina, Dr Slaa, Mengi, Mbowe, Zitto, Hosea na hata Butiku ndio wanaovurumishiwa kashfa.., Je, ni bahati mbaya ama ni baada ya tuhuma za ufisadi kushika kasi? INAWEZEKANA MTIKILA ALIONA WANAMLETEA MABOMU NI WAZALENDO KUMBE WAKATI ULE WALIKUA WANATAFTA MADARAKA NA SASA KWA KUWA WALIKUA KARIBU WATAENDELEA KUMTUMIA MAANA ALISHAONJA "PEREMENDE" KUTOKA KWAO
 
uzuri ni kusikiliza yatakayo jiri kwenye hiyo kesi.

hii imekaa uzuri
 
Huyu Mtikila ataleta balaa na machafuko ktk nchi walivyofanya kumsweka ndani ni sawa kabisa. Juzi juzi hapa kawatukana waislam leo Rais tunakwenda wapi jamani huu uhuru gani usio na mipaka?


Masatu nadhani huo ni wasiwasi wako tu. Moja, Mtikila hajaanza leo kuzungumza hayo mambo!!! Kama kuna kiongozi ambaye aliwahi kutukanwa na Mtikila, si mwingine bali ni the late Jullius Kambarage. Mbili, kama ni machafuko, yangelikwishatokea siku nyingi tu. Hebu niambie mchango wa mtikila katika mauwaji ya pemba, mauwaji ya mwembechai, mauwaji ya bulyanghulu, mauwaji yanayofanywa na viongozi wetu kwenye zahanati na hospitali kwa kufuja mali ya umma nk.

Tatu, ukitembelea nchi za magharibi, akina mtikila wapo wengi sana. Mara ngapi george bush ametukwana??? mara ngapi tonny blair ametukwana alipokuwa waziri mkuu??? wale wanaomtukana bush na blair wameleta machafuko gani katika nchi hizo za magharibi???
 
I respect Mtikila. Ana uchungu na nchi yake. Je ni kwa nini tusiwe na 100000000 mtilkilas? Tatizo viongozi wamejiwekea ukuta wa sheria kuwalinda! wafanye machafu na bado sheria iwalinde! Therefore tuwaache wafanye wafanyavyo. Hata Burma wachungaji waliamua kuingia barabarani. Ngoja mahakma ifanye kosa imtie hatiani Mtikila watakuwa wanasaign downfall of Peace ya ukondoo!!! kondoo atagaeuka mbuzi!!

...Mkuu Maarifa, heshima yako! unajua kwanini haiwezekani?

"some people are born to be heroes, some are born to wave them at parades"
 
Hivi kuna sheria ya kumfunga mtu kwa sababu katukana?...
Ningependa kujua hili hata ktk nchi za magharibi kwani sijawahi kusikia mtu akifungwa kwa sababu kamtukana rais wa nchi. Ila nilichowahi kusikia ni mtu kuifukuzwa kazi na kuwekewa kauzibe asipate ajira tena ktk fani alokuwa nayo. Mara nyingi huombwa aombe msamaha laa sivyo fitna inajengwa na hata kama kuna mashtaka huwa ktk mahakama ndigo za kijamii.
 
Hii issue ya kutukana viongozi ni ya kawaida kwa democratic countries. Ndio maana utakuta watu kama wadachi wametenga sehemu maalum (garden) ya raia kwenda kutolea dukudumu na hazira zao ikiwemo kuwatukana viongozi
 
Kwa hili naona tusubiri hiyo charge itakuwaje? Lakini hapa kutakuwa na kazi maana wote wanajifanya wajuaji wa sheria. Je, kama Mtikila akishinda ni fidia kiasi gani Polisi watamlipa kwa usumbufu na kumuweka ndani bila kosa lolote?
 
Hapo watatumia sheria ya uchochezi si ya kutukana. let's wait and see hiyo jumatatu
 
Hakuna cha kesi wala nini, ndiyo gharama ya demokrasia.. Nyerere aliwaitwa wapumbavu mbele ya hadhara na hakuna aliyesema lolote .. aliyesema "stupid is as stupid does" ina ukweli kwani "muhuni yuko kama anavyofanya"..
 
Back
Top Bottom