Mtikila akamatwa na polisi kwa kumkashifu Rais

Inabidi utulie upitie tena maandishi ya wachangiaji wenye maoni tofauti hapa. Hakuna anayemtete au kumkandamizi Mtikila hapa. Hapo kinachogomba ni uhalali na haki ya mtu kutoa hisia zake pamoja na kupinga mtu kuhukumiwa nje ya mahakama kama baadhi yenu mnavyofanya hapa. Nyie mnatia Mtikila hatiani kama nani? Tunapinga vilevile hii tabia ya kumsweka ndani badala kumfikisha mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake. Ni hilo, kwamba alitukkana matusi na kama amevunja sheria, ni mahakama ndiyo yenye uwezo wa kuamua, sisi hapa hatuwezi!

Mwisho ni swala zima la uvumilivu. Tunachosema ni kwamba huwezi kukuza demokrasia bila uvumilivu. Sasa demokrasia inahitaji uvumilivu pamoja na wananchi kama Mtikila. Bila uvumilivu hakuna demokrasia. Sasa wewe ukiambiwa ni gaidi na wakati unajua sio gaidi, tatizo liko wapi? Au mtu akikwambia wewe ni mwanamke wakati wewe inajulikana kuwa ni mwanamume ndio kusema utageuka kuwa mwanamke? Ingekuwa ni hivyo akina Bush na Blair wangeshafunga watu wangapi katika utawala wao? Leo hii mchana nilikuwa naangalia katuni inayomwigiza Gordon Brown, ni ya ajabu na ya kudhalilisha mno, tena kwenye BBC. Lakini Gordon anaendelea na uPM wake bila kutetereka wala kunyooshea watu vidole achalia mbali kusweka watu ndani. Sasa sisi mtu kusema wewe ni gaidi imekuwa nongwa? Ndio kusema urais wako unapungua thamani? Nani mwenye wajibu hapo, Mtikila kuthibitisha kauli yake au huyu aliyeambiwa ni gaidi kuthibitisha kwamba yeye sio gaidi? It take two to tangle!
Hakuna anayemuhukumu Mtikila Bali kwa upande wangu na wengine wanaomuona Rev. Mtikila amevunja sheria ni kutokana na sheria za nchi tulizonazo ni kwamba amekiuka, tena hasa ukizingatia kwamba yeye ni mmoja wa watu ambao amekuwa msitari mbele kutafuta Haki kupitia sheria na katiba ya nchi. Kutoa kauli za Uchochezi ni kosa Tanzania na kutumia lugha ya Matusi Ni Kosa, Sasa kama haya ameyafanya ,kisheria amekosa.Sasa mimi si Mhukumu kwasababu hiyo si kazi yangu Lakini kama yaliyoripotiwa hapa ni kweli ameyafanya anaangukia kwenye kundi la uvunjaji wa sheria kwa kutenda kosa na huo ndiyo ukweli. Kwa kuyadiscuss haya hakunifanyi niwe nimemuhukumu bali nimeelezea sheria inasema nini juu ya hilo.swala la kupatikana na hatia au laah hilo tunawaachia wenye wajibu wao.
 
....the whole thing about this is just bullshit,hawana kesi hao ni kujipendekeza tuu,waende wakamshtaki na yule aliyewaita wenzake mapaka tuone tutafika wapi,mpaka kichefuchefu!
 
Whatever the case, suala la kumtukana Rais si strategy nzuri. Mtikila angetumia mkakati mwingine kwani athari za kumtukana Rais ni mbaya sana kwa heshima na stability ya nchi
 
....the whole thing about this is just bullshit,hawana kesi hao ni kujipendekeza tuu,waende wakamshtaki na yule aliyewaita wenzake mapaka tuone tutafika wapi,mpaka kichefuchefu!
Hivi Huyu Rev. Mtikila alipofungwa Mwaka jela ilikuwa kwa kosa gani vile?Tukumbushane Wakuu.................Kama Hapa Hapana Kosa!
 
Whatever the case, suala la kumtukana Rais si strategy nzuri. Mtikila angetumia mkakati mwingine kwani athari za kumtukana Rais ni mbaya sana kwa heshima na stability ya nchi

..strategy nzuri ni kuwaita wapinzani mapaka!
 
Hakuna anayemuhukumu Mtikila Bali kwa upande wangu na wengine wanaomuona Rev. Mtikila amevunja sheria ni kutokana na sheria za nchi tulizonazo ni kwamba amekiuka, tena hasa ukizingatia kwamba yeye ni mmoja wa watu ambao amekuwa msitari mbele kutafuta Haki kupitia sheria na katiba ya nchi. Kutoa kauli za Uchochezi ni kosa Tanzania na kutumia lugha ya Matusi Ni Kosa, Sasa kama haya ameyafanya ,kisheria amekosa.Sasa mimi si Mhukumu kwasababu hiyo si kazi yangu Lakini kama yaliyoripotiwa hapa ni kweli ameyafanya anaangukia kwenye kundi la uvunjaji wa sheria kwa kutenda kosa na huo ndiyo ukweli. Kwa kuyadiscuss haya hakunifanyi niwe nimemuhukumu bali nimeelezea sheria inasema nini juu ya hilo.swala la kupatikana na hatia au laah hilo tunawaachia wenye wajibu wao.


sheria za nchi ziko sawa ila watakaokaa kuitafsiri ndio kazi kwao. ni kesi ngapi serikali na waandamizi wake wamekuwa wanalalamika eti wametuknwa bila kushinda. kila kifungu kiko wazi, na kinahitaji kutafsiriwa mbele ya mahakama.

sasa tukikutana na mahakimu au majaji wenye roho za kama Mwalusanya au lugakingira, basi hamna kesi, ila hii kesi ikikaliwa na majaji watakaotuambia eti' serkali tayari imeisha tumia ela nyingi sana kwenye hii kesi kwa hiyo tukimwachia huru Mtikila, atadai ela nyingi na hivyo kutitia serikali hasara' hapo kuna kesi.

unajua sheria imewagawa hawa waamuzi katika ngazi mbili, bold spirit wale wenye mtazamo mpana katika mambo ya jamii, wenye kutoa maamzi kulingana na jamii endelevu na sio sheria kandamizi, ni wale niliowataja kama mwalusanya na Lugakingira kwa tanzania. ila kwa sasa hivi hatunao tanzania waamuzi wa aina hii. kama wapo basi ni wachache.

pia tunao wale waamuzi uchwala, timurous souls ambao ni waoga wa kutafsiri sheria kwa upana. ambao kwao hukumu inatolewa akilini mwao hata kabla ya kesi kusikilizwa. na bahati mbaya hawa ndio wengi sana tanzania. hawa huwa hawana trouble ya kuangalia kamusi inasemaje, au waandishi wanaongeleaje hili swala, au watu wengi wangepokeaje hili swala hata kama sheria hipo. wao tu kazi yao ni kuipendezesha serikali. hata hukumu na matukio ya nje ya nchi hawaangalii.

ila kwa uelewa wangu hata kama waamuzi hawa ndio wengi mtikila ataachiwwa huru. wataona aibu
 
....the whole thing about this is just bullshit,hawana kesi hao ni kujipendekeza tuu,waende wakamshtaki na yule aliyewaita wenzake mapaka tuone tutafika wapi,mpaka kichefuchefu!
Kesi za maana hawana muda wa kuzifatilia, bali zile za kujikombakomba ili waonekane wanawapenda sana viongozi na hawako tayari kuona lolote baya linasemwa juu yao.
Tusubiri sasa hata wachora katuni mtasikia wanahatarisha AMANI NA UTULIVU kwa kuwachora wenye nchi.
 
Wakati huo huo Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania kwa Vyama vyenye Uwakilishi Bungeni (TCD), Bw. John Cheyo amemtaka Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, kuelekeza mpambano ya rushwa katika vyama vyote na chaguzi zote zijazo ili kukata mizizi ya tatizo hilo.

"Kwa kweli hotoba yako ya jana ni nzuri sana, mapambano hayo ya rushwa yaende mpaka chaguzi za udiwani na ule Mkuu. CCM ikikubali rushwa iwamalize basi vyama vya upinzani vitachakazwa kabisa," alisema.

Bw. Cheyo alisema siasa si kutukanana bali ni hoja na kwamba hoja hizo zisielekezwe kwa mtu bali kwa chama na sera.

Bw. Cheyo ambaye alitumia muda mrefu kupongeza hotuba ya Kikwete, alisema siasa za kutukanana ni hatari na lazima zipigwe marufuku ili nchi iendelee kuwa na amani na utulivu na kwamba ni jambo jema kwa vyama vyote kuwekeza katika amani .

Alisema kwa kuwa TCD ndio eneo pekee ambapo vyama vinaweza kukaa pamoja na kujadili mapungufu mbalimbali, ni vizuri Serikali kusaidia zaidi badala ya kazi hiyo kuachiwa wafadhili pekee.

Alisema kwa kuwa Rais Kikwete amekubali kufanya marekebisho aliyoyaita ya kutosha na yanayoeleweka ni bora mikataba ya madini ikawa wazi kwa kila mwananchi na kuondoa usiri usiokuwa na lazima.

Alisema Rais Kikwete kuwawekea hadharani wana CCM kuhusu rushwa ni dalili njema ya kutaka kukiimarisha chama hicho na kwamba anafurahishwa na hilo.

Hotuba hiyo ya Bw. Cheyo iliyotafsiriwa kuwa ni ukomavu wa kisiasa na wana CCM wengi ilijibiwa papo hapo na Mwenyekiti wa CCM Rais Kikwete na kusema "hiyo ni changamoto kwa CCM kuwa TCD inasaidiwa zaidi na wafadhili na sio sisi, tumekusikia
Bwana Cheyo."
 
JMushi1,
Sawa usipokubaliana na mawazo yangu lakini hilo la machinga na kuwanyanyasa wananchi sijui umelitoa wapi?..rudia kusoma taarifa nzima utaona kuwa inahusu DINI tu hakuna swala la viongozi na wananchi mahala popote zaidi ya kuwataja viongozi na Uislaam...
Kama nilivyosema hapo awali, kila tusi lina chanzo chake, leo hii siwezi kusimama hapa na kutukana mtu bila kuwepo hoja tuliyofarakana na ni hiyo hoja ndiyo sababu haswa. Pili, unaweza kuniita msenge na nisichukulie maanani tusi hilo ikiwa hoja (accusation) ilotangulia haikuwa na kashfa inayolingana na usenge huo.

Kitila Mkumbo,
Mjomba hakuna mtu anayemhukumu Mtikila hapa ni mawazo yetu kama ndio hivyo basi hata wewe unaposema anaonewa ni hukumu vile vile. Hukumu sio lazima iwe na matokeo ya kwenda jela ama Guilty laa hata Not guilty ni hukumu vile vile kwa hiyo tuzungumze kama hoja na tupe hasa sababu ya wewe kufikia kusema freedom hii ya speach!
Ndugu yangu freedoom of speach inakuja na ukweli ndani yake.. Utanisamehe nitatoa kimfano kidogo hapa!.. kumradhi natanguliza.
Kitila, siwezi kukuita wewe mwanaamke malaya na kisha kutoa taarifa za uke wako na umalaya wako ambao ni UONGO mtupu, kisha basi ukweli ni kwamba wewe ni mwanamme rijali mwenye mke na watoto. Hiyo freedom yangu nitakuwa nimesha ipunga na nimetangaza vita. Sasa uamuzi wako wa kuvumiliana, utategemea na wewe kuwa mtu wa aina gani na wala sio demokrasia hata kidogo unapokubali umalaya huo ama kukaa kimya, haihusiani hata kidogo na wala sidhani kama kukuita kwangu malaya kunaweza kuharibu nyumba yako.
Huko Marekani na hata Uingereza kuna watu wangapi wameswekwa jela wakisubiri mahakama zao, tena vijana hasa weusi ndio kibao na wengi wao hawana hata hatia...
Mwaka juzi waislaam hapa walifungua chuo chao haikuchukua hata week Polisi walikivamia na kupekuwaliwa wasipate kitu lakini bado walihakikisha kinafungwa baada ya kumwambia mwenye nyumba kuwa vyuo kama hivyo huzaa Magaidi. Hii freedom gani jamani ikiwa wao hao hao waislaam hawaruhusiwi kuzungumza ama kunyoosha kidole.
A lie can never be freedom of speach! hata siku moja na kama bado yupo Jela atie akili maanake mwenyewe kasema amejiunga na Siasa ili kueneza neno la Mungu!..That says a lot more than what he want us to believe!
 
sheria za nchi ziko sawa ila watakaokaa kuitafsiri ndio kazi kwao. ni kesi ngapi serikali na waandamizi wake wamekuwa wanalalamika eti wametuknwa bila kushinda. kila kifungu kiko wazi, na kinahitaji kutafsiriwa mbele ya mahakama.

sasa tukikutana na mahakimu au majaji wenye roho za kama Mwalusanya au lugakingira, basi hamna kesi, ila hii kesi ikikaliwa na majaji watakaotuambia eti' serkali tayari imeisha tumia ela nyingi sana kwenye hii kesi kwa hiyo tukimwachia huru Mtikila, atadai ela nyingi na hivyo kutitia serikali hasara' hapo kuna kesi.

unajua sheria imewagawa hawa waamuzi katika ngazi mbili, bold spirit wale wenye mtazamo mpana katika mambo ya jamii, wenye kutoa maamzi kulingana na jamii endelevu na sio sheria kandamizi, ni wale niliowataja kama mwalusanya na Lugakingira kwa tanzania. ila kwa sasa hivi hatunao tanzania waamuzi wa aina hii. kama wapo basi ni wachache.

pia tunao wale waamuzi uchwala, timurous souls ambao ni waoga wa kutafsiri sheria kwa upana. ambao kwao hukumu inatolewa akilini mwao hata kabla ya kesi kusikilizwa. na bahati mbaya hawa ndio wengi sana tanzania. hawa huwa hawana trouble ya kuangalia kamusi inasemaje, au waandishi wanaongeleaje hili swala, au watu wengi wangepokeaje hili swala hata kama sheria hipo. wao tu kazi yao ni kuipendezesha serikali. hata hukumu na matukio ya nje ya nchi hawaangalii.

ila kwa uelewa wangu hata kama waamuzi hawa ndio wengi mtikila ataachiwwa huru. wataona aibu

Ndiyo Maana nikaandika sijamuhukumu bali kazi ya hukumu ni ya wenye wajibu nayo, nayo ni Mahakama kupitia majaji wake.Ila sheria ndiyo hivyo inavyosema..................Na hapo Hakuna Ubishi na hata MARA YA KWANZA ULE MWAKA ALIOPATIKANA NA HATIA NA KULAMBWA MWAKA JELA KOSA LILIKUWA NI HILOHILO LA UCHOCHEZI!
 
Sasa Mtikila jana ametoa ufafanuzi wa hoja alizozitoa. Ametoa hoja nzito sana in a very simple language. Wala hakusema hayo maneno ambayo yamekuwa yakitembea hapa. Ameeleza vizuri sana kwa nini anapinga mahakama ya kazi. Kimsingi anasema anachopinga sio mahakama ya kadhi, bali mahakama ya kadhi kuingizwa katika katiba. I wish ningekuwepo wakati wa mkutano wake huu. Soma maelezo yake kutoka gazeti la TZ Daima.
_____________________________________________________________

JK atakiwa kuomba radhi
MZOZO MAHAKAMA YA KADHI



na Agnes Mlundachuma (TZ Daima, 10 Novemba 2007)



SUALA la uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi nchini linazidi kupanuka, na kwa mara ya kwanza tangu mjadala huo uanze, jina la Rais Jakaya Kikwete limeanza kuingizwa katika mzozo huo.
Rais Kikwete ametajwa katika sakata hilo pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema, wakidaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika mgogoro huo, ambao sasa unazidi kuchukua sura tofauti.

Kwa upande wake, Rais Kikwete ametajwa akitakiwa kuwaomba radhi Watanzania, kwa kile kinachodaiwa kuwa, dhamira yake ya kutaka kuigeuza Tanzania kikatiba kuwa nchi ya Kiislamu na hivyo kuirejesha katika mzozo wa miaka ya mwanzo ya 1990 uliohusisha juhudi za baadhi ya viongozi kuiingiza katika kundi la nchi wanachama wa Jumuiya ya Kiislamu Duniani (OIC).

Aidha, IGP Mwema amepewa siku 21 kumuomba radhi Mchungaji Christopher Mtikila, kutokana na kitendo chake cha kuwatuma askari wamkamate (Mtikila), kumhoji na hatimaye kumfungulia mashtaka ya uchochezi wakati hana kosa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Mchungaji Mtikila, ambaye ndiye aliyeibua mjadala unaoendelea kuhusu uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, alitaka tamko la Rais Kikwete la kuomba radhi liambatane na hatua kali za kisheria dhidi ya watumishi wote wa umma, waliohusika kwa namna yoyote katika kitendo hicho cha kuingiza Uislamu katika ilani yake ya uchaguzi, serikali na Bunge.

Aliongeza kuwa sambamba na hilo, Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambacho alidai ni kikundi cha maslahi ya kibinafsi cha watu fulani, nacho kifutwe kama inavyoagiza katiba.

Mtikila alisema, Baraza la Maaskofu Katoliki nchini (TEC), Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) na Halmashauri ya Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (PCT), walikutana na walitaka kutoa tamko la kupinga mapinduzi hayo ili kulinda katiba ya nchi, lakini serikali iliwahadaa wasifanye hivyo bali wangojee tume yao ilifanyie kazi suala hilo.

Hata hivyo, Mtikila alisema, inashangaza kuwa tofauti na ahadi iliyotolewa na serikali kwa taasisi hizo nyeti za kidini nchini, harakati zilianzishwa ili muswada kuhusu Mahakama ya Kadhi upelekwe bungeni bila Wakristo kujua, mpaka Mungu alipowafunulia na kuwawezesha kuwahisha ulinzi wao wa katiba mahakamani.

Alisema yeye hapingi kuanzishwa kwa mahakama hiyo, bali anachopinga ni kuingizwa katika katiba ya nchi ambayo kimsingi inapingana na suala hilo.

“Tunachopinga vikali sisi ni kuingizwa kwa dini ya Kislamu au Mahakama ya Kadhi katika katiba ya nchi yetu,” alisema na kuongeza kuwa hata kama kutakuwa na harakati za kutaka kardinali, askofu au paroko wa Kanisa Katoliki kuingizwa katika katiba ya nchi, atapinga kama atakavyopinga kuingizwa mtandao wowote wa kidini katika katiba.

Aliwataka Waislamu wasidanganywe kwa kuwa Mahakama ya Kadhi ni mradi wa watu wachache, na kuongeza kuwa, kuna nchi kadhaa za Kiislamu zimekataa mahakama hiyo kwa sababu sharia zake ni kinyume cha haki za binadamu.

Alisema hoja ya kuwa mahakama hiyo itashughulikia mirathi, hija na ndoa tu, ni ulaghai ili iingizwe katika katiba, baadaye makadhi waue watu wasiokubali dini ya Kiislamu na kuangamiza Wakristo na Wayahudi na kuchinja Waislamu watakaoiacha dini yao.

Alisema hivi sasa nchi haina Mahakama ya Kadhi, lakini Waislamu wanaoa, wanaolewa, wanapata mirathi na kesi zao za mirathi zinashughulikiwa na pia wanakwenda hija na kuhoji mahakama hiyo italeta mabadiliko gani katika masuala hayo yanayodaiwa kuwa itayashughulikia.

Aidha, Mtikila alisema kitendo cha baadhi ya Waislamu kupinga ziara ya Papa ni kutofahamu kwamba mbali ya Vatican kuwa makao makuu ya Kanisa Katoliki duniani, pia ni nchi huru ingawa ipo ndani ya nchi ya Italia.

Alifafanua kuwa Vatican ni sawa na Swaziland na Lesotho ambazo zimezingirwa na nchi ya Afrika Kusini.

Alisema Papa atatembelea Tanzania kiserikali sawa na kiongozi mwingine wa nchi na kwa kuwa kuongoza kanisa ni huduma ya kiroho, hawezi kuiweka roho pembeni anapokuwa katika ziara ya kiserikali.

Akifafanua kauli zake za awali kuhusu kupinga kwake utaratibu unaotaka kutumiwa kuanzisha Mahakama ya Kadhi, Mtikila alikanusha kutamka kuwa Uislamu ni ugaidi na kusisitiza kuwa Mahakama ya Kadhi ndiyo chombo cha ugaidi ndiyo maana hata baadhi ya nchi za Kiislamu zinaikataa.

“Uislamu wa Watanzania usio na ukatili wa Mahakama ya Kadhi hauwezi kuitwa ugaidi kamwe,” alisisitiza.

Kwa upande mwingine, alisema mbinu ya kamati inayotetea mali za Waislamu iliyotangaza azma yake ya kumkata kichwa, ni hasira tu, kwa kuona pesa walizokuwa wanataka kupewa hazitakuwepo na suala hilo halitazungumziwa bungeni wala serikalini kwa kuwa lipo mahakamani.

Aliongeza kuwa, yeye hawakatalii Waislamu kuabudu, lakini si kuliiingiza suala hilo la kidini ndani ya katiba.

Kauli hiyo ya Mtikila inakuja wakati taifa likipita katika kipindi kigumu cha msigano wa hoja zinazokinzana kuhusu uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi jambo lililogusa hisia za makundi mbalimbali ya Wakristo na Uislamu kiasi cha kutishia amani.

Baadhi ya kauli za waumini wa dini hizo mbili, ndizo ambazo kwa upande fulani zilisababisha taasisi za dola kuamua kuingilia kati na kuchukua hatua za kisheria.
 
Kitila heshima yako mkuu . Maneno ya Mtikila huwa daima ni moto na lazima uwe na akili timamu kumwelewa kama hujatimia utakimbilia kumlaumu na kumlaani.Amesema mambo ya msingi sana na haya kwa kweli ni mgogoro mkubwa na major set back kwa Mahakama yenyewe.The guy is not lunatic kama amabyo watu walitaka tuamini .Wacha tuone moto sasa mahakamani .
 
Siku zote mi najua Mtikila sio Mwendawazimu, ila kwa vile huzungumza maneno ambayo Watanzania wengi hawangesubutu kuyasema tena hadharani, ndipo anapopewa huo uwendawazimu na CCM.Mtikila hana maneno ya kuzungukazunguka.Mkate ni mkate hataki lugha za Ohh ni unga wa ngano ulioumliwa na kisha kuokwa.Hii 9inaleta tafsiri nyingi.Yeye anataka watu waelewe kile anachozungumza.
 
Huyu Mtikila ataleta balaa na machafuko ktk nchi walivyofanya kumsweka ndani ni sawa kabisa. Juzi juzi hapa kawatukana waislam leo Rais tunakwenda wapi jamani huu uhuru gani usio na mipaka?

Akili zilizochini ya masaburi utazijua tu! kwenye sensa anaonyesha kuwapinga waislam nyuma ya sensa anawashambulia viongozi wa kikiristo! huu kama si ushetwani ni nini! ikulu kuna jini jamani tujiadhali
 
Polisi wa upelelezi (CID) kutoka makao makuu ya CID Dar es Salaam walimkamata Mchungaji Christopher Mtikila, jana saa 11 jioni (1700hrs) saa za Afrika Mashariki na kufanya naye mahojiano hadi saa 3.30 usiku (2100hrs) walipomuachia kabla ya kumkamata tena leo baada ya kumfanyia upekuzi nyumbani kwake Ilala flats, Block F 4 namba A 8, pale pale karibu na TBL, na sasa wamemshikilia Central Police station, hadi Jumatatu atakapopelekwa mahakamani.

Miongoni mwa matamshi aliyoyatoa ni pamoja na kumuita Rais Gaidi na mhuni. Katika mahojiano yote, Mtikila amekiri kusema maneno hayo na hakukataa hata neno moja na mengine makali zaidi na aliyahalalisha kwa kurejea maandiko mbalimbali
Mwache aende akahamasisha m4c mahabusu na magerezani. Ninajua akishtakiwa atashinda huyu mpiganaji Lakini CC MABWEPANDE wana mbinu lukuki. Mnakumbuka miaka ya 1999 kifo cha JK Nyerere Mtikila alitokezea na kutuhumu kwa mzee kifimbo aliondoka kwa "ngoma' hivyo hakuhitaji heshima!! Alipobanwa aliwashinda!! ndipo walipomtegea tena katika shitaka la uchochezi akalamba "mvua" moja. Hivyo hata hili litaenda hivyo hivyo!!
 
hawamuwezi mch. Mtikila. hii si mara ya kwanza. Alishasema serikali ilimuua Kolimba na aliachiwa. Alishamtukana Rais Mwinyi na mengineo mengi. hili mbona dogo tu!
 
Back
Top Bottom