Mtikila akamatwa na polisi kwa kumkashifu Rais

Mwanakijiji,
Mzee wangu umezungumza mengi sana kuhusu Lowassa na hakuna mtu alochoka kusoma malalamiko yako. Sii peke yako hapa JF kila siku tunarusha madongo na kukemeana tunapotaka kutoka ktk msitari.. huo ndio uhuru wa maoni, hata siku moja tusije fikiria uhuru wa maoni una include matusi toka kwa kiongozi mwingine wa chama.
Jamani Mitkila sio Machinga, huyu ni Mchungaji tena mgombea urais lakini lugha anayotumia hakika imetoka nje ya uhuru huo.
Pili, Upande mwingine wa shilingi hiyo hiyo, JK pia amekuwa mtu wa kuvutwa sana bila kujaribu kufanya utafiti wa swala hili kupitia wanasheria wetu kwanza. Tatizo lolote linalohusu Waislaam linaweza tatuliwa kama vile tunavyoweza kutatua matatizo ya wanawake kwa kumleta mtaalam wa mabo yao kama shahidi wa upande wowote ule uwe wamashtaka ma mshtakiwa. Wendawazimu huitwa Psychiatrist na pengine hata maswala ya alama na DNA wapo wataalam wake. Kinachotakiwa ni kuongezwa kipengele kimoja tu kinachohusu swala husika kama kweli lipo maanake nashindwa kabisa kufikiria kitu ambacho kinahitaji korti ya kadhi hasa Tanzania.
Nimezaliwa ktk Uislaam lakini wazee wetu walikuwa na wake kibao wengine wametumia mila zetu kuoa na sio Uislaam ( wakiwa na wake zaidi ya wanne), wamezaa nje ya ndoa, wazinifu na wanapiga maji (pombe) kama hakuna kesho.
Hesabu ya waislaam wanao yafanya haya ni kubwa sana na nadiriki kusema labda asilimia 70 hawafuati sheria za dini hii ktk maisha yao ya kila siku pamoja na kwamba wengi huenda misikitini kusali.
Hivyo basi mimi mwenyewe pamoja na kuwa muislaam siwezi kukubali kuhukumiwa ktk korti hizi hata siku moja kwani mengi yaliyojengwa ktk sheria hizi yanahusu Uislaam kwa ujumla na pia mazingira tofauti kabisa. Kuna vitendo ambavyo Shia wanavipa uhalali wakati havikubaliki ktk Sunni na vise verse, mfano ndoa za safar tutatoa hukumu kwa kufuata sheria ipi.
Jibu la yote haya ni kwamba mahakama hizi hazitufai hata kidogo ila tunaweza kumtumia Mtaalam wa sheria hizi kama atahitajika...Na sidhani kama kuna nafasi hiyo.

WELL SAID ! SINA LA ZIADA HAPA !
 
...cant believe baadhi yenu humu mnaona hii ni kitu ya kutumia pesa za walalahoi kufungua kesi,hakuna kesi hapo ni kutafuta misifa tuu ....tangu lini mtu kuitwa muhuni ni kosa la jinai na hawa mafisadi ni wahuni kweli maana wametuibia sana
 
koba,
hata kama hawa jamaa ni MAFISADI WAKUBWA DUNIA NZIMA, but that does not mean they dont have to be respected ! wee huoni ughaibuni babu hata kama umekamatwa na cocaine, bangi, lakini still watakutreat kama bosi wao (which in fact you are), sasa tusichanganye hii kesi na kusema kwamba accused (mafisadi) ndio hawawezi kupewa haki yao ! (katika haki ninaposema, simaanishi kutukanwa, bali maneno ya kukashifu na yasiyo na uthibitisho)

Maneno aliyotoa Mchungaji Mtikila kwa kweli hayakupaswa kusemwa na mtu kama yeye, nilitegemea watasema baadhi ya members hapa JF na vivuli vyao lakini sio yeye !

Lazima akae akijua kwamba, yeye kama Public Figure (halafu mbaya zaidi kwa sistem zetu hizi yupo kwenye opozishen) basi yupo kwenye risk kubwa kuandamwa time yoyote ! Nilidhani pale aliposema aliwekea unga kwenye begi lake atakuwa amejifunza mengi*ikiwemo kuwa makini* lakini naona sijui alidhani ndio getaway yake ya kupata buzz tena kwenye siasa, lakini naona sasa kalikanyaga !
 
Uuaji ni kitendo na kina maana ya kutoa uhai.Muuaji ni mtu anaye au aliyetoa uhai.Ditopile ni muuaji au hatupaswi kumwita hivyo eti tu kwa vile alikuwa na hadhi ya ukuu wa mkoa?Kiongozi mlevi ni mlevi tu hata kama watu hatasema hadharani,hivyohivyo kwa kiongozi malaya na mwizi.Watu watakuwa wanaogopa kusema fulani ni malaya au mwizi simkwa kuwa wanamuheshimu ila kwa kuwa wanamuogopa. Hatujajua ni vigezo gani vilivyopelekea Mtikila kumwita Gaidi ni bora tukasubiri.Naamini Mtikila ana akili timamu ila tu wakati mwingine naye kama binadamu huchemka.Tatizo lingine tulinalo watanzania hatujazoea kuwaita viongozi wetu kwa kwa kutumia sifa wanazojipa kutokana na vitendo vyao.Sifa hizo ni kama UMALAYA,WIZI,UONGO nk. Ukiwa mwongo lazima uitwe mwongo hata kama wewe ni mh.kiasi gani.
Kwa upande mwingine sikubaliani na kitendo cha kumwita mtu kwa sifa ya kitendo ambacho hakufanya.Mfano Sikubaliani na kumwita dreva wa Ditopile Muuaji kwa kuwa si yeye aliyeua.
 
...kada acha hizo wewe,juzi Bush kaitwa mgonjwa wa akili na Kucinich hata kope ya FBI haikutikisika sasa leo kuitwa muhuni tuu eti kesi....hivi kuitwa muhuni au gaidi kunahatarisha vipi usalama wa taifa au kufanya uchochezi...mambo mengine yanaonyesha jinsi wanavyofanya kazi kwa kujipendekeza tuu na uelewa mdogo wa mambo
 
Koba,
Na wamekuwa wakitumia hako kamsemo ka kuhatarisha usalama na amani ya nchi ili kupata support ya Watanzania.Kwa Dr Slaa napo walisema hivyo hivyo.Wanafanya hivyo kwa kuwa wanaamini watanzania wako tayari kukumbatia umasikini na madhambi ya viongozi ili kulinda neno "AMANI"
 
koba,
hata kama hawa jamaa ni MAFISADI WAKUBWA DUNIA NZIMA, but that does not mean they dont have to be respected ! wee huoni ughaibuni babu hata kama umekamatwa na cocaine, bangi, lakini still watakutreat kama bosi wao (which in fact you are), sasa tusichanganye hii kesi na kusema kwamba accused (mafisadi) ndio hawawezi kupewa haki yao ! (katika haki ninaposema, simaanishi kutukanwa, bali maneno ya kukashifu na yasiyo na uthibitisho)

Maneno aliyotoa Mchungaji Mtikila kwa kweli hayakupaswa kusemwa na mtu kama yeye, nilitegemea watasema baadhi ya members hapa JF na vivuli vyao lakini sio yeye !

Lazima akae akijua kwamba, yeye kama Public Figure (halafu mbaya zaidi kwa sistem zetu hizi yupo kwenye opozishen) basi yupo kwenye risk kubwa kuandamwa time yoyote ! Nilidhani pale aliposema aliwekea unga kwenye begi lake atakuwa amejifunza mengi*ikiwemo kuwa makini* lakini naona sijui alidhani ndio getaway yake ya kupata buzz tena kwenye siasa, lakini naona sasa kalikanyaga !

Why on earth should i respect mafisadi na wanyonyaji? kama heshima walishajishushia zamani wao wenyewe, kilichobaki ni kuwapa shavu zaidi kwenye kuishusha zaidi.Theydont deserve respect at all.
 
Mwanakijiji,
Mzee wangu umezungumza mengi sana kuhusu Lowassa na hakuna mtu alochoka kusoma malalamiko yako. Sii peke yako hapa JF kila siku tunarusha madongo na kukemeana tunapotaka kutoka ktk msitari.. huo ndio uhuru wa maoni, hata siku moja tusije fikiria uhuru wa maoni una include matusi toka kwa kiongozi mwingine wa chama.

Mzee Mkandara, kwenye suala la maoni ninaamini kuwa watu wana uhuru mkubwa ikiwemo kuita watu majina ya kejeli na hata ya dhihaka. Katiba inapolinda watu kuwa au kutoa uhuru wa maoni haisemi maoni hayo ni ya namna gani.

Linapokuja suala la matusi nchi nyingi duniani zinazosheria ambazo zinatakaza obsenities, na hapa mara nyingi mahakama zinahangaika kusema what is obsene.

katika Lugha ya Kiswahili vivyo hivyo tunayo sheria inayokataza matusi hadharani lakin haiorodheshi matusi ni nini. Kumuita Rais Mjinga inawezekana kuwa ni tusi na kwa wengine inawezekana kuwa si tusi. Ujinga ni sifa ya kuashiria uwezo wa mtu kujua jambo fulani. Mtu mjinga hajui, na ujinga hutoka. Kumuita mtu ******** yaweza kuwa tusi na laweza kuwa sifa ya kuelezea kuwa mtu huyo hawezi kujua hata akijulishwa vipi. Lakini, mtu anapotoa matusi ya nguoni ambayo lengo lake ni kumdhalilisha mtu kwa matusi ya "mama" au ya viungo vya mwili, ni rahisi zaidi kuona wapi mtu anapotoka.

Uzuri ni kuwa katika Lugha ya Kiswahili matusi yako very clear hayana ile ambiguity ya maana. Kama mtu si hanithi, halafu mtu mwingine akamuita ni hanithi, hilo ni tusi. Lakini kama mtu ni hanithi halafu akaitwa hanithi, haliwezi kuwa tusi.

Now, kwa upande wa Mtikila naamini charges zinazoweza kustick and as a matter of fact should stick ni charges za uchochezi hasa kama aliyosema ndivyo alivyosema. Kumuita Rais Mhuni he can get away with that. Ila anaposema.

Rais Gaidi - amevuka mstari wa matusi na kufika mstari wa madai ambayo atatakiwa ayaoneshe ukweli wake. Tanzania tunayo ile sheria ya Dhidi ya Ugaidi, je Kikwete anastahili kuitwa Gaidi. Hakuna nchi ambayo iko tayari kuongozwa na Gaidi, hivyo lengo la Mtikila kusema Rais ni Gaidi ni kuwafanya wananchi waichukie serikali na indirectly watake kuiondoa kwani kama kweli tunaye Rais Gaidi ni jukumu la wananchi kumuondoa Rais huyo hata kwa nguvu! Ndio maana charges hizo ni more serious (and should be serious) kuliko za kumuita Rais Mjinga.

Na anaposema kuwa lengo la Waislamu ni "kuwachinja wakatoliki" ni madai mazito hayo kwani ni sawa na kile ambacho Marekani kinatenganisha uhuru wa maoni na maoni ya hatari. Wenyewe Marekani wanasema ni sawa na "kupiga kelele 'Moto, moto' kwenye ukumbi wa sinema uliojaa watu". Yeye anataka Wakatoliki wafanye nini kujihami, wakikaribishwa na Waislamu wasiende na wakiona waislamu wanatambe mtaani na upanga kwenda msituni wajifungie ndani!

Ni kwa sababu hiyo utaona kuwa simtetei Mtikila hata kidogo kwani ninaelewa vizuri sana maana ya uhuru wa maoni na mipaka iliyopo. Ndio maana utaona kuwa katika makala zangu zote ninawaelezea viongozi wa nchi kwa jinsi walivyojieleza wao wenyewe au kutokana na mambo waliyoyafanya. Sijawahi kumuita kiongozi yeyote jina lolote ambalo si la cheo chake au hata la utani (kwa mfano, ingawa wengi hapa wanapenda kumuita JK "Muungwana" miye siwezi, ninamuita Rais Kikwete). Siku akifanya mambo ya woga nitamuita mwoga, akifanya mambo ya kijinga nitamuita mjinga, hata Lowassa mara nyingi nasema ni "kiongozi mahiri, hodari, shujaa aliyetamba Bungeni" ambalo ni kweli!


Jibu la yote haya ni kwamba mahakama hizi hazitufai hata kidogo ila tunaweza kumtumia Mtaalam wa sheria hizi kama atahitajika...Na sidhani kama kuna nafasi hiyo.

Mkandara katika sehemu ya pili ya Makala yangu ninaelezea ni jinsi gani tunaweza kuanzisha mahakama ya Kadhi Tanzania Bara pasipo kuwa na hofu. Kama India wameruhusu kuwa nazo (japo hazitambuliki kisheria) na kama Waisraeli wameruhusu (na zinatambulika kisheria) nadhani Tanzania tunaweza kuwa nazo pia. Cha kushangaza Uturuki (nchi yenye waislamu wengi) haina mahakama za kadhi! Upande mwingine Indonesia taifa lenye Waislamu wengi zaidi duniani halina mahakama ya kadhi kama tunavyoifikiria sisi. So in essence there is a wide range of models of how we can establish Qadi courts without contravening the Constitution or other laws. Tatizo inawezekana tutahitaji wataalamu toka nje kutufikiria jinsi tunaweza kufanya hivi kwanini sisi wenyewe hatuwezi kufikiri vya kutosha na ni waoga kulifikiria jambo hili na kulipatia utatizo wa Kitanzania.
 
Mwanakijiji,
ninavyoelewa mimi, kunapokuwa na masuala ya ndoa au mirathi, wahusika wana haki ya kuamua shauri lao lihukumiwe kwa kufuata sheria za ndoa na mirathi ya Kiislamu. sasa kwanini Waislamu hawaridhiki na utaratibu uliopo sasa hivi?

niliwahi kusikia tetesi kwamba serikali ilikuwa na mpango wa kurekebisha sheria ya mirathi na malezi Tanzania. Sheria hiyo ingetoa zaidi haki kuwalinda watoto wanaozaliwa nje ya ndoa. Nimeambiwa suala hilo ndilo linalowakwaza Waislamu na kuamua kushinikiza waanzishiwe mahakama ya Kadhi.

Suala ninalojiuliza mimi ni hukumu za Mahakama ya Kadhi zitakuwa enforced na chombo kipi? Kutoa hukumu ni suala moja, na kuhakikisha hukumu inatekelezwa ni suala lingine.

Hivi hakuna uwezekano wa Waislamu kuwa na utaratibu wao ktk Jumuiya zao wa kuamua masuala yao ya ndoa na mirathi nje ya KATIBA YA JAMHURI?
 
mahakama iliyo huru haifanyi kazi kwa kuangalia tu nani kasema

na mtikila atawabwaga chini kama waendesha mashtaka watendelea na charge hii bila kuirekebisha.

upande wa mashtaka utapaswa kuiridhisha mahakama maana ya tusi kwa kuangalia definition ya watu tofauti, na ndipo itabidi koti ikubali kama maneno aliyoyasema yanaangukia kwenye hiyo definition.

mtikila naye atahitajika kuelezea vilevile maana ya tusi na kupinga kuwa maneno yake aliyoyatoa sio tusi bali ni ukweli mtupu.

By the way, sheri inatambua tusi kuwa ni maneno ya uongo ambayo hayana ukweli wowote kwa niaba ya kumchafulia mtu sifa.

kama mtikila atadhibitisha kuwa maana ya gaidi tafsiri yake inainvolve mtu ambaye sio msikivu au mtu ambaye hasikii hakubaliani na yale yasemwayo na watu wengine, basi koti itakubaliana kuwa yuko sahii.

mfano, GAIDI linatokana na kitenzi KUGHAIRI, au kutofanya yale ambayo ulipaswa kufanya. na kama rais kuna jambo kaisha ghairi kufanya na anapaswa kulifanya basi rais ni ghaidi kwa definition ya Mtikila ya neno ghaidi.

Malaya, pia itategemea tafsiri yake ni ipi. kama kwenda nje ya ndoa inaamount kuwa ni umalaya, na mtikila navyo vielelezo, basi sio tusi bali ni ukweli mtupu.

yapo mengi ambayo mtikila anweza kutumia kupangua hoja zote mpaka waendesha mashtaka kubaki wanahaha. hata mimi hii keshi ninaiweza, kama mahakama zetu zitakuwa huru.
 
...kada acha hizo wewe,juzi Bush kaitwa mgonjwa wa akili na Kucinich hata kope ya FBI haikutikisika sasa leo kuitwa muhuni tuu eti kesi....hivi kuitwa muhuni au gaidi kunahatarisha vipi usalama wa taifa au kufanya uchochezi...mambo mengine yanaonyesha jinsi wanavyofanya kazi kwa kujipendekeza tuu na uelewa mdogo wa mambo
KOBA LINA POINTI HILO!WAPE MAMBO MKUU!
 
Mwanakijiji,

Binafsi napotazama swala la Mtikila nadhani kitu kikubwa sio kumwita rais Gaidi kilichochukua uzito wa mashtaka haya ila ni pale unapoweka sababu ama ambition ya huyu rais kuyafanya yaliyompa sifa hiyo ya Ugaidi. Mshikaji hii ni tuhuma nzito sana na kwa kila ushahidi nadhani Mtikila ndiye anayeonyesha wazi kuwa ana mission ya kidini zaidi ktk kujiingiza kwake kisiasa, and he confessed on that!...
Kwa mfano, naweza kumwita JK Kichaa, msanii na kadhalika lakini yote yasiwe na uzito wa matusi kwa sababu hilo jina limetokana na Ahadi zake hewa!, kuacha watu wakihujumu uchumi wetu n.k. Hivyo basi ahadi hewa sio tusi hata kidogo.
na tukirudi ktk swala la Mafisadi hili sio tusi pia kwa sababu kinachofanyika ni Uharibifu wa uchumi wetu.
Nitaendelea kukupa mifano mingine let's say tutumie maneno ya Masatu na fisadi kuwa ni utongozaji. Well mtu anaweza kutongoza na asiwe fisadi ikiwa ana nia nzuri ktk ndoa. Malaya pia kama hakuharibu ndoa ama mahuniano - friendship fulani hawezi kuitwa fisadi.
Kwa hiyo watu kama Karamagi, kitendo cha kuweka mikataba sio kinachowafanya wao kuwa mafisadi ila ni results (uharibifu) wa kinoma, roho mbaya, ubinafsi wao unaotokana na mikataba hiyo.
sasa tukirudi kwa Mtikila ni pale anaposema kuwa dhamira ya rais ni Waislaam kuichukua nchi na kuwachinga wakristu.. dhamira hii ndiyo inayompa jina la Gaidi akiwa na maana Terrorist ambayo imekuwa alama ama nembo ya Uislaam.
Ni ajabu watu wanshindwa kuelewa kwa nini Bush kaitwa alivyoitwa FBI wasiseme kitu bila kuzingatia kilichotangulia.
Tukirudi tena ktk hii korti ya kadhi mimi nawashangaa sana nyie mnapopiga makelele kuhusiana na korti hii. Binafsi naipinga lakini kama kweli waislaam wanaililia sana wapeni wembe wajikate wenyewe. Kwanza wazinifu - hukumu yake ijnajulikana. mwizi hukatwa mkono waacheni wakatwe mikono yao maanake vibaka ni watoto wao wenyewe. Wauza unga hukumu yake wanaijua...
Mwisho wa yote watalia kurudi huku kwenye diversity!... kulilia korti ya kadhi ni kutafuta njia za kujitenga hali hawawezi kuondokana na maisha tuliyokwisha yajenga toka babu zao.
 
WaTZ tulipigwa msasa sana na siasa za kijamaa, hivyo itatuchukua muda sana kuafikiana na mawazo ya kidemokrasia. Mtikila kama kiongozi wa kisiasa kasema mawazo yake na si matusi mpaka atapofahamisha ana maana gani, na JK kama ni gaidi ama mhuni KWELI lakini hajamdhuru mtu tokana na sifa zake hizo basi hamna tatizo na Mtikila apuzwe. Lakini kama Mtikila atatufahamisha VIZURI na tukakubaliana na mawazo yake basi JK ni kweli hafai. Kama ukizuia kusema watu watakacho ni udikteta. Mimi naamini JK MSANII, na ni kama tusi lakini ni ukweli.
 
Na huyu Mtikila hajui kama alikuwa anasakwa na hapa ndipo alipobanika hatoki,na huenda akaozea jela pia itakuwa ni fundisho kwa wengine wenye kuiletea serikali matatizo.Hapa hakuna cha Raisi ila kuna CCM na CCM ina wenyewe ambao walikuwa hawalali kwa kelele zake sasa ataijua CCM.
 
Na huyu Mtikila hajui kama alikuwa anasakwa na hapa ndipo alipobanika hatoki,na huenda akaozea jela pia itakuwa ni fundisho kwa wengine wenye kuiletea serikali matatizo.Hapa hakuna cha Raisi ila kuna CCM na CCM ina wenyewe ambao walikuwa hawalali kwa kelele zake sasa ataijua CCM.

..We should put these kinda people on the list to nuke after mafisadi
 
Mwanakijiji,

Binafsi napotazama swala la Mtikila nadhani kitu kikubwa sio kumwita rais Gaidi kilichochukua uzito wa mashtaka haya ila ni pale unapoweka sababu ama ambition ya huyu rais kuyafanya yaliyompa sifa hiyo ya Ugaidi. Mshikaji hii ni tuhuma nzito sana na kwa kila ushahidi nadhani Mtikila ndiye anayeonyesha wazi kuwa ana mission ya kidini zaidi ktk kujiingiza kwake kisiasa, and he confessed on that!...
Kwa mfano, naweza kumwita JK Kichaa, msanii na kadhalika lakini yote yasiwe na uzito wa matusi kwa sababu hilo jina limetokana na Ahadi zake hewa!, kuacha watu wakihujumu uchumi wetu n.k. Hivyo basi ahadi hewa sio tusi hata kidogo.
na tukirudi ktk swala la Mafisadi hili sio tusi pia kwa sababu kinachofanyika ni Uharibifu wa uchumi wetu.
Nitaendelea kukupa mifano mingine let's say tutumie maneno ya Masatu na fisadi kuwa ni utongozaji. Well mtu anaweza kutongoza na asiwe fisadi ikiwa ana nia nzuri ktk ndoa. Malaya pia kama hakuharibu ndoa ama mahuniano - friendship fulani hawezi kuitwa fisadi.
Kwa hiyo watu kama Karamagi, kitendo cha kuweka mikataba sio kinachowafanya wao kuwa mafisadi ila ni results (uharibifu) wa kinoma, roho mbaya, ubinafsi wao unaotokana na mikataba hiyo.
sasa tukirudi kwa Mtikila ni pale anaposema kuwa dhamira ya rais ni Waislaam kuichukua nchi na kuwachinga wakristu.. dhamira hii ndiyo inayompa jina la Gaidi akiwa na maana Terrorist ambayo imekuwa alama ama nembo ya Uislaam.
Ni ajabu watu wanshindwa kuelewa kwa nini Bush kaitwa alivyoitwa FBI wasiseme kitu bila kuzingatia kilichotangulia.
Tukirudi tena ktk hii korti ya kadhi mimi nawashangaa sana nyie mnapopiga makelele kuhusiana na korti hii. Binafsi naipinga lakini kama kweli waislaam wanaililia sana wapeni wembe wajikate wenyewe. Kwanza wazinifu - hukumu yake ijnajulikana. mwizi hukatwa mkono waacheni wakatwe mikono yao maanake vibaka ni watoto wao wenyewe. Wauza unga hukumu yake wanaijua...
Mwisho wa yote watalia kurudi huku kwenye diversity!... kulilia korti ya kadhi ni kutafuta njia za kujitenga hali hawawezi kuondokana na maisha tuliyokwisha yajenga toka babu zao.[/quot

MKANDARA
SIKUBALIANI HATA KIDOGO NA MTIKILA KAMA ALIMWITA MH RAIS GAIDI KWASABABU NI MUISLAM!MIMI NILIFIKIRI NI KWASABABU YA VITENDO VYA SERIKALI DHIDHI YA WANANCHI KWA MFANO UNYANYASAJI WA WAMACHINGA NK.WANANCHI WANAPOTENDEWA MAMBO MABAYA HUO NDIO UGAIDI!SIO TU ETI KWASABABU NI MSLAMU!ANA WAZIMU AMA ANA KICHAA!?
 
Huyo JK na CCM yake wote ni wasanii, GAIDI & WAHUNI tu, bila hivyo nchi ingeshaendelea. Kutukanwa ni haki yao ingawa Mtikila hajatukana ila kasema ukweli. Kama kiongozi wa upinzani na raia mwenye uchungu wa dhati na nchi yake msimamo wa Mtikila na maneno yake ni sawa kabisa, atawasifiaje mafisadi? Hamna njia rahisi kuondoa ama kuwaanika mafisadi, ni mashujaa wachache km kina Mtikila watatuongoza ktk vita ya kweli. Kama atafungwa CCM watakua wameonyesha makucha yao ya wazi ya ufisadi, kwa nini wamuweke selo?
Kuiondoa CCM ambayo imejengwa ktk mioyo ya waTZ kama mithili ya kidini lakini haijaleta au kua na mtegemeo ya kuleta maendeleo SI LELEMAMA kwa waTZ. Walishinda uraisi kwa kura 80%, na baadhi yetu hata hatuamini huo ukweli. Mtikila anajua hilo.
 
Mzee Mkandara, kwenye suala la maoni ninaamini kuwa watu wana uhuru mkubwa ikiwemo kuita watu majina ya kejeli na hata ya dhihaka. Katiba inapolinda watu kuwa au kutoa uhuru wa maoni haisemi maoni hayo ni ya namna gani.

Linapokuja suala la matusi nchi nyingi duniani zinazosheria ambazo zinatakaza obsenities, na hapa mara nyingi mahakama zinahangaika kusema what is obsene.

katika Lugha ya Kiswahili vivyo hivyo tunayo sheria inayokataza matusi hadharani lakin haiorodheshi matusi ni nini. Kumuita Rais Mjinga inawezekana kuwa ni tusi na kwa wengine inawezekana kuwa si tusi. Ujinga ni sifa ya kuashiria uwezo wa mtu kujua jambo fulani. Mtu mjinga hajui, na ujinga hutoka. Kumuita mtu ******** yaweza kuwa tusi na laweza kuwa sifa ya kuelezea kuwa mtu huyo hawezi kujua hata akijulishwa vipi. Lakini, mtu anapotoa matusi ya nguoni ambayo lengo lake ni kumdhalilisha mtu kwa matusi ya "mama" au ya viungo vya mwili, ni rahisi zaidi kuona wapi mtu anapotoka.

Uzuri ni kuwa katika Lugha ya Kiswahili matusi yako very clear hayana ile ambiguity ya maana. Kama mtu si hanithi, halafu mtu mwingine akamuita ni hanithi, hilo ni tusi. Lakini kama mtu ni hanithi halafu akaitwa hanithi, haliwezi kuwa tusi.

Now, kwa upande wa Mtikila naamini charges zinazoweza kustick and as a matter of fact should stick ni charges za uchochezi hasa kama aliyosema ndivyo alivyosema. Kumuita Rais Mhuni he can get away with that. Ila anaposema.

Rais Gaidi - amevuka mstari wa matusi na kufika mstari wa madai ambayo atatakiwa ayaoneshe ukweli wake. Tanzania tunayo ile sheria ya Dhidi ya Ugaidi, je Kikwete anastahili kuitwa Gaidi. Hakuna nchi ambayo iko tayari kuongozwa na Gaidi, hivyo lengo la Mtikila kusema Rais ni Gaidi ni kuwafanya wananchi waichukie serikali na indirectly watake kuiondoa kwani kama kweli tunaye Rais Gaidi ni jukumu la wananchi kumuondoa Rais huyo hata kwa nguvu! Ndio maana charges hizo ni more serious (and should be serious) kuliko za kumuita Rais Mjinga.

Na anaposema kuwa lengo la Waislamu ni "kuwachinja wakatoliki" ni madai mazito hayo kwani ni sawa na kile ambacho Marekani kinatenganisha uhuru wa maoni na maoni ya hatari. Wenyewe Marekani wanasema ni sawa na "kupiga kelele 'Moto, moto' kwenye ukumbi wa sinema uliojaa watu". Yeye anataka Wakatoliki wafanye nini kujihami, wakikaribishwa na Waislamu wasiende na wakiona waislamu wanatambe mtaani na upanga kwenda msituni wajifungie ndani!

Ni kwa sababu hiyo utaona kuwa simtetei Mtikila hata kidogo kwani ninaelewa vizuri sana maana ya uhuru wa maoni na mipaka iliyopo. Ndio maana utaona kuwa katika makala zangu zote ninawaelezea viongozi wa nchi kwa jinsi walivyojieleza wao wenyewe au kutokana na mambo waliyoyafanya. Sijawahi kumuita kiongozi yeyote jina lolote ambalo si la cheo chake au hata la utani (kwa mfano, ingawa wengi hapa wanapenda kumuita JK "Muungwana" miye siwezi, ninamuita Rais Kikwete). Siku akifanya mambo ya woga nitamuita mwoga, akifanya mambo ya kijinga nitamuita mjinga, hata Lowassa mara nyingi nasema ni "kiongozi mahiri, hodari, shujaa aliyetamba Bungeni" ambalo ni kweli!




Mkandara katika sehemu ya pili ya Makala yangu ninaelezea ni jinsi gani tunaweza kuanzisha mahakama ya Kadhi Tanzania Bara pasipo kuwa na hofu. Kama India wameruhusu kuwa nazo (japo hazitambuliki kisheria) na kama Waisraeli wameruhusu (na zinatambulika kisheria) nadhani Tanzania tunaweza kuwa nazo pia. Cha kushangaza Uturuki (nchi yenye waislamu wengi) haina mahakama za kadhi! Upande mwingine Indonesia taifa lenye Waislamu wengi zaidi duniani halina mahakama ya kadhi kama tunavyoifikiria sisi. So in essence there is a wide range of models of how we can establish Qadi courts without contravening the Constitution or other laws. Tatizo inawezekana tutahitaji wataalamu toka nje kutufikiria jinsi tunaweza kufanya hivi kwanini sisi wenyewe hatuwezi kufikiri vya kutosha na ni waoga kulifikiria jambo hili na kulipatia utatizo wa Kitanzania.

MH MWANAKIJI NI MUHIMU TUKUMBUKE KUWE NENO "UGAIDI"LILIKUWEPO KABLA HATA HILI VUGUVUGU LA UKRISTO NA UISLAM HALIJAPAMBA MOTO!KUMBUKA KUWA KAMA KUNA MWANANCHI ANAYELALA NJAA ANAUWEZO WA KUMUITA RAIS GAIDI KWASABABU HAJUI KESHO ATAKULA NINI!UNAPOFANYA MAMBO AMBAYO MWENZAKO ANAFIKIRI NI YENYE NIA MBAYA DHIDI YAKE ANAUWEZO WA KUKUITA GAIDI.KAMA POLISI WAKIWANYANYASA WAMACHINGA HUO NI UGAIDI WA POLISI DHIDI YA WAMACHINGA!MTIKILA ATAKUWA HATIANI KAMA ATAKIRI KWAMBA ALIMWITA RAIS GAIDI KWA SABABU NI MUISLAM!ILA KAMA ANAJUA ANACHOFANYA THEN ANAWEZA AKATOA SABABU YOYOTE ILE INAYOONYESHA UNYANYASIKAJI WA WANANCHI,CHAMA,MTU FLANI AMA KIKUNDI FLANI KAMA REASON YA KUMUITA RAIS GAIDI!
 
Back
Top Bottom