Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 612
Polisi wa upelelezi (CID) kutoka makao makuu ya CID Dar es Salaam walimkamata Mchungaji Christopher Mtikila, jana saa 11 jioni (1700hrs) saa za Afrika Mashariki na kufanya naye mahojiano hadi saa 3.30 usiku (2100hrs) walipomuachia kabla ya kumkamata tena leo baada ya kumfanyia upekuzi nyumbani kwake Ilala flats, Block F 4 namba A 8, pale pale karibu na TBL, na sasa wamemshikilia Central Police station, hadi Jumatatu atakapopelekwa mahakamani.
Miongoni mwa matamshi aliyoyatoa ni pamoja na kumuita Rais Gaidi na mhuni. Katika mahojiano yote, Mtikila amekiri kusema maneno hayo na hakukataa hata neno moja na mengine makali zaidi na aliyahalalisha kwa kurejea maandiko mbalimbali
Miongoni mwa matamshi aliyoyatoa ni pamoja na kumuita Rais Gaidi na mhuni. Katika mahojiano yote, Mtikila amekiri kusema maneno hayo na hakukataa hata neno moja na mengine makali zaidi na aliyahalalisha kwa kurejea maandiko mbalimbali