Kwitughutila
Member
- Oct 30, 2011
- 52
- 11
Safi sana Mtendaji, hii mijitu huwa inaudhi sana na moshi wao!
Yeye kaenda kuona mgonjwa au kuvuta sigara? Kama anafanya hivyo tena hospital huyo baba hata hako katoto hata kaonea huruma atakuwa anavuta tu katoto kanavuta moshi, unajua moshi unaotolewa ndiyo mbaya kwa wale wanaopokea nje!Mamlaka ya kutoa hukumu na adhabu huyo mtendaji anayapata wapi?... Tusiishi Kama ng'ombe huku taratibu na kanuni zipo.
Kuchapana bakora na kupiga watu huu Ni ukoloni wa kidikteta..
Kazi za watu hizo mambo ya kufikirika hayoKipindi ananipiga hao mabodigadi watakuwa wamenishikilia? Kitendo cha sekunde tu, mtu ameshadhurika. Ushawahi kujitoa mhanga? Dunia hii si kila mtu unaweza kumfanyia kila unachofikiria halafu akakuangalia haijalishi una cheo gani.
Weka akilini hilo.
Mpaka ukaanza kuona nyota nyota,Nimeishia hapo akanipiga Kofi la kwanza kabla sijakaa sawa akanipiga Kofi la pili...
Jamaa alitaka akae sawa ndo apigwe Kofi la pili..🤣🤣Mpaka ukaanza kuona nyota nyota,
WanavozabanaSasa mkuu unataka picha ya nini? Sigara? Mvuta sigara au mtendaji?
sasa akawahiwa la piliJamaa alitaka akae sawa ndo apigwe Kofi la pili..
Kwanini unanifanyia hivi lkn..?Wanavozabana
Na wewe nikuzabue?Kwanini unanifanyia hivi lkn..?
Ha haa! Huwezi nakuambia huwezi..😜Na wewe nikuzabue?
Ongeza sauti uoneHa haa! Huwezi nakuambia huwezi..😜
Wanazingua sana hawa gari moshiSafi.
Wavuta sigara ni watu wasio na akili kabisa, wako kama bata, bata akijisikia kunya hata kwenye sufuria ya ugali anakunya. Mvuta sigara akishikwa kiu popote tu anavuta.
Wanasayansi wanasema wavuta sigara ni binadamu wenye kiwango kidogo sana cha akili.
Smoking lowers IQ, thinking ability
The poorer mental function seen among alcoholics, many of whom also regularly smoke cigarettes, may be partially due to the long-term effects of nicotine, new research suggests.www.abc.net.au
Kwenye packet pameandikwaNi kweli kabisa Wavutaji sigara ni watu wasio na akili kabisa maana hata kwenye packet ya sigara kuna maandishi yanasomeka Cigarette smoking is dangerous to your healthy Lakini bado wanavuta hata akili ya kusoma kilichoandikwa hawana!!
🏃🏃Ongeza sauti uone
Mamlaka ya kutoa hukumu na adhabu huyo
mamlaka ya kuvuta sigara katika eneo la kutolea huduma za afya aliyatoa wapi??mtendaji anayapata wapi?... Tusiishi Kama ng'ombe huku taratibu na kanuni zipo.
Kuchapana bakora na kupiga watu huu Ni ukoloni wa kidikteta..
Hizi ndio habari za magazeti yaliyobaki.Mkazi wa kijiji cha Mbwemkuru mkoani Lindi, Athumani Ndumba amelalamika kitendo cha mtendaji wa kijiji hicho, Azidu Mwenda kumpiga makofi hadharani kwa madai ya kuvuta sigara katika kituo cha afya Kitomanga.
Tukio hilo limetokea Januari 31, 2021 katika kituo hicho na kushuhudiwa na waliokuwa wamekwenda kuwajulia hali wagonjwa.
Ndumba ambaye mke wake amelazwa katika kituo hicho amesema alitoka nje kwa ajili ya kuvuta sigara na ndipo alipokumbana na mtendaji huyo.
Amesema wakati akiendelea kuburudika na sigara ndipo alipovamiwa na mtendaji huyo na kupigwa vibao viwili na hakujibu lolote wala kuzusha ugomvi kwa madai kuwa alikwenda kwa ajili ya kumjulia hali mkewe ambaye ni mjamzito.
“Nilipomaliza kuvuta sigara alitokea mtendaji na kutaka kujua aliyekuwa anavuta na nilipojibu alinishambulia kwa kunipiga makofi. Alinipiga la kwanza kabla sijakaa sawa akanipiga la pili. Waliokuwa karibu walimtaka aache kunipiga ndio akaacha,” amesema Ndumba huku Sharifa Rashid aliyeshuhudia tukio hilo akisema kitendo kilichofanywa na mtendaji huyo sio cha kiungwana.
Kwa upande wake Mwenda alikiri kufanya hivyo kwa madai kuwa alipomuuliza Ndumba alikana kuvuta sigara.
"Nilipofika kituo cha afya nikasikia harufu ya sigara na nikamuona Athumani anazimia sigara yake chini nilipomuita akaleta ubishi ndio tukaanza kuvutana" amesema Mwenda.
Mganga mfawidhi wa kituo hicho, Gidion Edward amesema hajapata taarifa zozote za malalamiko kutoka kwa Ndumba kauli iliyotolewa pia na mkurugenzi wa manispaa ya Lindi, Jomari Satura.
“Tukio hilo silijui lakini kama limetokea mtu aliyeshambuliwa anatakiwa akaripoti polisi ili hatua za kisheria zichukue mkondo wake,” amesema Satura.
Chanzo: Mwananchi