Mtemi Mirambo VS Mtemi Mkwawa

Bajeti ya kunguru

JF-Expert Member
Sep 21, 2014
1,371
1,041
Habari zenu wakuu.

Kumekuwa na upotoshaji mkubwa wa historia hasa linapokuja suala la uwezo wa Mwafrika kutokupewa sifa zinazotakiwa kama ilivyo kwa hayati J.K. Nyerere na Nelson Mandela. Afrika inaaminishwa Mandela ni zaidi ya Nyerere hiki ni kituko.

Kuna hili pia la Chief Mirambo na chief Mkwawa eti sifa kubwa anapewa Mkwawa ili tumuone ndio shujaa wetu na pia alipambana akashindwa na wazungu. Nadhani wanataka kutujengea mazingira ya kuwasujudia na kuwaogopa. Itawezekanaje uniamnishe shujaa wangu wa kuigwa ni yule aliyepigwa wakati kuna waliopiga?

Baada ya kuifatilia historia ya mtemi Mirambo a.k.a. Napoleon wa Afrika kama alivyojulikana na wazungu nimegundua kuna upotoshaji mkubwa wa historia.

Chief Mkwawa japo naye si haba ila kwa chief Mirambo hatii mguu hata kucha.

Nguvu za jeshi la Mirambo kwa Afrika mashariki alikuwa hana wakumlingasha. Ndiye aliyetawala eneo kubwa kuliko machief wengine. Tabora mpaka Kigoma eneo lake lilipakana na ziwa Tanganyika japo aliona haitoshi akaingia mpaka Burundi akapiga himaya ya Urundi akasambaratisha.

Wakati Mkwawa anasilaha za jadi kabla hajaletewa bunduki moja na Mwarabu, Mirambo alikuwa anatengeneza bunduki yeye mwenyewe na alimiliki jeshi lilikowa na active personnel zaidi ya 10000.

Hapakuwa na cha mzungu wala mwarabu aliyeleta fyoko kwenye himaya yake aliua kama anau panzi tu ikabidi wafate masharti yake kila wanapopita kwenda Zambia na Kongo walimlipa kodi kwa kuikanyaga ardhi yake huna kodi mzigo wote unabaki na kuwa mali yake.
Wafipa walijichanganya hawakumjua vizuri kichwa chake kikoje. Huyu jamaa alikuwa hana masihara kabisaa!

Wazungu baada ya kubanwa sana waliomba nguvu ya jeshi kutoka kwa sultan wa Zanzibar wakimwambia kwamba Napoleon wa Afrika anataka kuiharibu biashara yako kwakuwa ndiye alikuwa mnunuzi mkubwa wa pembe za ndovu na watumwa kutoka Zaire na Zambia.

Sultan akatuma askari 3000 kuja kuongeza nguvu kwa wazungu wakishirikiana na jeshi la snitch wa Mirambo alikuwa anaitwa Chief Mkasiwa. Jamaa walinyoosha mikono sultan akaona anamaliza watu wake akaamuru jeshi lake lililosalia lirudi Zanzibar haraka walikuwa wamebaki 1500 ndio waliokuwa wamesalimika na jeshi la awali la Mtemi Mirambo lililokuwa likiitwa Luga Luga (walugaluga).

Mtemi Mirambo alikuwa na majeshi matatu ambayo aliyapanga kwa ubora kutoka la kwanza hadi la tatu. Jeshi kali kabisa lenye mafunzo na uwezo wa juu kabisa liliitwa Abaoko kama sijakosea herufi.

Sasa Mkwawa aliuza mali zake kwa Mwarabu pembe za ndovu na kuletewa nguo Mirambo hakuuza mali zake bali alichukua za wazungu walizokuwa wamekusanya sehemu mbalimbali.

Mirambo alichukua watumwa kutoka mikononi mwa wazungu na waarabu na kuwasajili kwenye jeshi lake. Yaani unapomtaja Mirambo jua unataja habari kubwa.

Sasa historia za namna hii zinafichwa na kuoneshwa historia dhaifu ya kumtukuza mzungu kuwa ni bora.

Mtemi Mirambo alifariki kwa ugonjwa wa rovu miaka ya 1880.

Nimeweka hapa kwa kifupi sana. Kwa mwenye interest anaweza kufatilia ahakikishe mwenyewe.

MAGUFULI4LIFE.
 
Umekuza sana story za Mtemi Mirambo.

Jamaa alikuwa mtemi wa kawaida sana, ila alikuwa anajimwambafai kama Magufuli.

Hivi unajua Mirambo ndio mtemi maarufu aliyekuwa akipenda hongo?

Hivi unajua Mtemi Mirambo alikuwa mfanyabiashara maarufu wa watumwa kwa huku bara?

Hivi unajua Mtemi Mirambo alikuwa mtemi aliyekuwa na mikataba mingi zaidi ya kibiashara za kilaghai ambayo alifanya na waarabu, wajerumani.

Kuhusu Mtemi Mkwawa hiyo ni level nyingine kabisa. Misimamo yake isiyoyumba, nidhamu ya askari wake na mbinu za medani za kivita alizokuwa nazo, mpaka leo hii wajerumani wanampigia saluti.

Kama hujui tu, Mkwawa aliwachinja mpaka wamisionari wa kizungu waliofika kwenye himaya yake ambao kiasili walikuwa hawaguswi maana enzi zile walionekana kama wajumbe wa amani (malaika!).
 
Umekuza sana story za Mtemi Mirambo.
Jamaa alikuwa mtemi wa kawaida sana, ila alikuwa anajimwambafai kama Magufuli.

Hivi unajua Mirambo ndio mtemi maarufu aliyekuwa akipenda hongo?

Hivi unajua Mtemi Mirambo alikuwa mfanyabiashara maarufu wa watumwa kwa huku bara?

Hivi unajua Mtemi Mirambo alikuwa mtemi aliyekuwa na mikataba mingi zaidi ya kibiashara za kilaghai ambayo alifanya na waarabu, wajerumani.


Kuhusu Mtemi Mkwawa hiyo ni level nyingine kabisa. Misimamo yake isiyoyumba, nidhamu ya askari wake na mbinu za medani za kivita alizokuwa nazo, mpaka leo hii wajerumani wanampigia saluti.

Kama hujui tu, Mkwawa aliwachinja mpaka wamisionari wa kizungu waliofika kwenye himaya yake ambao kiasili walikuwa hawaguswi maana enzi zile walionekana kama wajumbe wa amani (malaika!).
Naona mjukuu wa waarabu umekuja baada ya kusikia kuwa ndugu zako wafanya kazi wa sultan walinyooshwa n'a Mirambo
 
Naona mjukuu wa waarabu umekuja baada ya kusikia kuwa ndugu zako wafanya kazi wa sultan walinyooshwa n'a Mirambo
Kama hajui tu, waunguja wengi wa leo hapa Zanzibar, babu na bibi zao walikuwa wanyamwezi, waliuzwa na mtemi Mirambo. Asili ya sisi wazanzibar wengi ni unyamwezini (waunguja) na Uarabuni (wapemba).

Kiufupi tu, mtemi Mirambo na Sultan wa Zanzibar walikuwa wanafanya biashara moja, biashara ya utumwa. Muuzaji alikuwa Mtemi Mirambo na Mnunuzi alikuwa Sultan.
 
"Wakati Mkwawa anasilaha za jadi kabla hajaletewa bunduki moja na Mwarabu, Mirambo alikuwa anatengeneza bunduki yeye mwenyewe na alimiliki jeshi lilikowa na active personnel zaidi ya 10000"

Si kwa nia ya kuweka mashindano baina ya mashujaa wetu wa TZ sababu wote kwa nafasi na wakati wao walitetea na kupigania watu wao,

Kuna mwalimu wangu wa form two alikua na degree ya Historia kabisa( tuliambiwa hivyo) alikua anapenda kutuita walugaluga (vijana wa kiume) , baada ya kumuuliza kwanini anapenda kutuita hivyo ndio akatumbia kuwa walugaluga lilikua jina la wanajeshi wa mtemi Mirambo na kutuhadhithia story ya Mtemi Mirambo katika upande ambao sikuwahi kuskia kabla, jamaa alikua mwamba, hodari na shupavu kiongozi kiukweli nilitamani hata mtu angeitengeneza Muvi.

NB: sidhani kama kuna ushahidi wa kutosha kumsupport chief Mirambo coz niliwahi kwenda Kwihara kwenye eneo la kumbukumbu za kihistoria pale TBR bt sikukutana na recods zakutosha sana kumuhusu, pia wakati napita kurudi town kwa mbaali nikaonyeshwa yaliyokuwa makazi yake pia ilikua kawaida sana.
 
Kama hajui tu, waunguja wengi wa leo hapa Zanzibar, babu na bibi zao walikuwa wanyamwezi, waliuzwa na mtemi Mirambo. Asili ya sisi wazanzibar wengi ni unyamwezini (waunguja) na Uarabuni (wapemba).

Kiufupi tu, mtemi Mirambo na Sultan wa Zanzibar walikuwa wanafanya biashara moja, biashara ya utumwa. Muuzaji alikuwa Mtemi Mirambo na Mnunuzi alikuwa Sultan.
Mkuu usipotoshe historia. Mtemi Mkasiwa ndiye alikuwa anauza watu wake na ndiye aliye wakaribisha waarabu Tabora. Kuhusu Napoleon wa Afrika ni bahari kubwa usisikilize propaganda mkuu.

Mtemi Mirambo akisikia unauza watu kama watumwa anakuja kukupiga nakuchukua himaya yako inakuwa yake. Ndicho kilichomfanya Mtemi Mkasiwa kuwaalika waarabu aishi nao akimuhofia Mtemi Mirambo.

Hiki nacho kieleza sio propaganda za Magumashi. Ndio ukweli 100%.

MAGUFULI4LIFE.
 
"Wakati Mkwawa anasilaha za jadi kabla hajaletewa bunduki moja na Mwarabu, Mirambo alikuwa anatengeneza bunduki yeye mwenyewe na alimiliki jeshi lilikowa na active personnel zaidi ya 10000"

Si kwa nia ya kuweka mashindano baina ya mashujaa wetu wa TZ sababu wote kwa nafasi na wakati wao walitetea na kupigania watu wao,

Kuna mwalimu wangu wa form two alikua na degree ya Historia kabisa( tuliambiwa hivyo) alikua anapenda kutuita walugaluga (vijana wa kiume) , baada ya kumuuliza kwanini anapenda kutuita hivyo ndio akatumbia kuwa walugaluga lilikua jina la wanajeshi wa mtemi Mirambo na kutuhadhithia story ya Mtemi Mirambo katika upande ambao sikuwahi kuskia kabla, jamaa alikua mwamba, hodari na shupavu kiongozi kiukweli nilitamani hata mtu angeitengeneza Muvi

NB: sidhani kama kuna ushahidi wa kutosha kumsupport chief Mirambo coz niliwahi kwenda Kwihara kwenye eneo la kumbukumbu za kihistoria pale TBR bt sikukutana na recods zakutosha sana kumuhusu, pia wakati napita kurudi town kwa mbaali nikaonyeshwa yaliyokuwa makazi yake pia ilikua kawaida sana.
Historia ya Mtemi Mirambo ipo nyumbani kwake Urambo pale Kwihara kilikuwa kituo cha kupumzika misafara ya wazungu na biashara zao na ndipo kodi ilikusanyiwa pale na jeshi la Mirambo. Mji wa Tabora ulipo sasa hivi ulifata reli tu. Ila nashukuru kwakuwa ulikuwa nacho hata hicho kidogo.


MAGUFULI4LIFE.
 
Mkuu usipotoshe historia. Mtemi Mkasiwa ndiye alikuwa anauza watu wake na ndiye aliye wakaribisha waarabu Tabora. Kuhusu Napoleon wa Afrika ni bahari kubwa usisikilize propaganda mkuu. Mtemi Mirambo akisikia unauza watu kama watumwa anakuja kukupiga nakuchukua himaya yako inakuwa yake. Ndicho kilichomfanya Mtemi Mkasiwa kuwaalika waarabu aishi nao akimuhofia Mtemi Mirambo.
Hiki nacho kieleza sio propaganda za Magumashi. Ndio ukweli 100%.


MAGUFULI4LIFE.
Toa source ya habari zako.
Cheif mkwawa ni habari nyingine na vitabu vingi vinatuambia himaya yake ilikuwa haifikiki kirahisi ila tabora ilikuwa njia na chimbo la watumwa.

Wewe umeskia wapi hicho unachotuambia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom