Mteja wa Vodacom sasa anaweza kupokea pesa kutoka nchi za nje akitumiwa kwa njia ya World Remit, Money Gram na Juba express

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,908
51,904
Kilio cha wadau cha kutaka kurahishwe njia za kupokea pesa zimeanza kusikilizwa

Sasa hivi Mteja wa vodacom mwenye Mpesa Sasa waweza pokea pesa toka nchi za nje kwenye simu yako ukitumiwa kwa njia ya World Remit,Money Gram na Juba express.

Kama una mtu nje na una namba ya vodacom yenye Mpesa mwambie akutumie kwenye namba yako ya simu pesa zitaingia kwa hela za Tanzania na zitakufikia kwenye simu yako popote ulipo hata porini kijijini na utazitoa kwa wakala kwa wakati wako au ukitaka ku zi deposit kwenye akaunti yako ni wewe tu Pesa inakuwa kiganjani mwako

Tunashukuru kwa hatua hii kubwa

Tunaomba pia serikali iruhusu watu kupokea pesa kupitia Paypal kwa sababu:

Tanzania kumekuwa na tatizo kubwa la ajira. Njia moja ya kuondoa hilo tatizo ni kwa watu kutafuta kazi za kufanya online, yaani mitandaoni. Kazi zipo nyingi. Mfano, waweza pata kazi ya kutafsiri website ya kampuni au mtu kwa Kiswahili au kutafsiri kitabu. Unafanya online malipo yanakuwa kwa njia ya PayPal hata kwenye simu yako ya mkononi, hata mwajiri au mnunuzi awe Ulaya au Marekani

Pia, mtu waweza chora hata katuni, ramani za nyumba n.k ukauza online. Au, ukajitungia wimbo wako wa kienyeji binafsi nyumbani kwako bila hata kwenda studio, ukauweka kwa mfumo wa video au audio ukauuza online kwenye maduka kibao ya online.

Tatizo kwa Tanzania haijaruhusu matumizi ya kupokea pesa kwa njia ya PayPal ambapo mtu aki-click tu kununua bidhaa yako, pesa yako inaingia chapchap kwenye PayPal account yako.

Kenya walisharuhusu; vijana wengi hushinda mitandaoni wakitengeneza pesa wakiuza bidhaa zao, viwe vichekesho, michezo ya kuigiza n.k ambavyo huviuza online. Wanaweka clip zao kwenye maduka ya online mtu ananunua anamlipa online kupitia Paypal.

Kuna shughuli nyingi za ujasiliamali online. Kikwazo kwa nchi yetu ni upataji wa pesa wa kazi yako au mauzo yako online. Bado tuko enzi za mawe tukiamini minjia ya kizamani ya kupokea hela. Na hivyo kuifanya nchi yetu kuwa ni ya kulipa zaidi pesa za kigeni na si ya kupokea pesa za kigeni.

Serikali ikiruhusu upokeaji pesa kupitia PayPal itafanya vijana wengi waingie mitandaoni kutafuta pesa

Biashara za online zaweza kufungua Watanzania wengi kupata pesa toka nje, sababu ni juhudi ya mtu binafs na ubunifu wake tu auze nini. Waweza kujirekodi unarukaruka kama ngedere ukiimba hovyohovyo tu bila hata vyombo halafu ukaita wimbo Crazy Monkey Song ukauweka online na ukauza. Wapo watu wana pesa wanapenda vituko wananunua.

Taasisi za elimu nazo ziweke kwenye mitaala ujasiliamali wa online wasibakie tu kufundisha ujasiriamali wa kuzurura tu juani wa kimachinga
 
Ni jambo jema sana ila naamini kwa baadae serikali(TRA) itaingilia kati hasa kiwango/kiasi cha kupokea mtanzani kama sio kodi kwa cho chote utakachotumiwa!
 
Ni jambo jema sana ila naamini kwa baadae serikali(TRA) itaingilia kati hasa kiwango/kiasi cha kupokea mtanzani kama sio kodi kwa cho chote utakachotumiwa!
Kodi zinakatwa mbona.Kampuni ya vodacom inakatwa kodi kwa miamala na wewe mteja ukifanya muamala wa kutuma au kutoa pesa unakatwa kodi.Wakala wa Mpesa naye hukatwa kodi unapofanya miamala .Unataka TRA wakate kodi mara ngapi kwenye hiyo pesa yako?
 
Hilo swala la PayPal sidhani kama BOT watakusikia na hizo PhD zao!
Limeshasemwa mno sijui nini kinawashinda!.. tumeshawasimanga mno lkn wapi..😅
Chakushangaza unaweza kuweka hela PayPal au Skrill kwa kutumia MasterCard ya mpesa lkn huwezi kupokea wewe pesa!..

Sasa sisi tusio na ndugu wakututumia hela sijui wanatuonaje.. halafu wanahubiri vijana mjiajiri then hawaweki mazingira rafiki!.. hii inamaana wao pia ni kikwazo ktk kujiajiri kwetu!.. waziri wa fedha sijui halijui hili.. gavana wa BOT nae sijui halioni hili..!
Kenya huko napokea pesa yako toka PayPal hadi mpesa yako huku wamelala!..
Makampuni ya simu wao wanahitaji milango iwe wazi tu watekeleze..

Sintashangaa hizo huduma ulizotaja hapo zikaja sitishwa maana ndivyo walivyo!.. usishangilie sana hawaeleweki Hawa..😜
 
Ni jambo jema sana ila naamini kwa baadae serikali(TRA) itaingilia kati hasa kiwango/kiasi cha kupokea mtanzani kama sio kodi kwa cho chote utakachotumiwa!
Unachosema ni kuwa akaunti mtu ukiweka pesa kwenye akaunti yako unatakiwa kukatwa kodi!!! au mfano mtu unaingiza pesa akaunti ya shule ya mwanao ikatwe kodi!!! Au unalipia pesa akaunti ya mfanyabiashara ununue vitu sababu hataki hela taslimu hiyo hela unayoingiza kwenye akaunti yake ikatwe kodi au mtu ananunua korosho tanzania anatuma pesa kwenye bodi ya korosho hiyo hela inayoingia bodi ya korosho ikatwe kodi


Au uko nje ya nchi unajiingizia pesa kwenye Mpesa yako mwenyewe iliyoko Tanzania kwa hiyo ukatwe kodi!!!

Au unatuma pesa akaunti ya hospitali ni kuwa hiyo inayoingia hospitali ikatwe kodi!!! MPesa NI kama akaunti yeyote ile kama ilivyo ya benki .Pesa ukiingiza huwezi katwa kodi!!!

Ha ha ha
 
Hilo swala la PayPal sidhani kama BOT watakusikia na hizo PhD zao!
Limeshasemwa mno sijui nini kinawashinda!.. tumeshawasimanga mno lkn wapi..😅
Chakushangaza unaweza kuweka hela PayPal au Skrill kwa kutumia MasterCard ya mpesa lkn huwezi kupokea wewe pesa!..

Sasa sisi tusio na ndugu wakututumia hela sijui wanatuonaje.. halafu wanahubiri vijana mjiajiri then hawaweki mazingira rafiki!.. hii inamaana wao pia ni kikwazo ktk kujiajiri kwetu!.. waziri wa fedha sijui halijui hili.. gavana wa BOT nae sijui halioni hili..!
Kenya huko napokea pesa yako toka PayPal hadi mpesa yako huku wamelala!..
Makampuni ya simu wao wanahitaji milango iwe wazi tu watekeleze..

Sintashangaa hizo huduma ulizotaja hapo zikaja sitishwa maana ndivyo walivyo!.. usishangilie sana hawaeleweki Hawa..😜
Ndio tatizo la kuwa na viongozi wazee....
ni wagumu sana kubadilika.....
ulimwengu ulishachenji kitambo.....
sisi bado tupo nyuma.....
 
Back
Top Bottom