Mteja ni Mfalme.

Jaguar

JF-Expert Member
Mar 6, 2011
3,438
1,025
Jamaa mmoja alikuwa na duka la kuuza dawa za binadamu(pharmacy).Siku moja,njemba moja ilifika ikaomba ipewe Dume pakti tatu.Baada ya kupewa zile pakti tatu,ile njemba ikalipa na kuondoka kwa furaha huku ikicheka sana.Muuza pharmacy akashangaa sana ila akapotezea.Ile njemba ikajenga mazoea,kila siku lazima ije kununua kondomu pakti tatu na inapotoka dukani inacheka saana.Siku moja baada ya mwenye pharmacy kumuuzia zile pakti tatu za dume,alimtuma msaidizi wake wa kazi amfuatilie yule jamaa anakoelekea,isije ikawa ni chizi anachezea kondomu kama mapulizo.Baada ya msaidizi wake kumfuatilia mpaka mwisho,alirudisha ripoti kwa bosi wake kama ifuatavyo;"ndio bosi,nimemfuatilia mpaka alipofika nyumbani kwako akapiga hodi,akafunguliwa mlango na mkeo!".
 
ehee baada ya hapo alipofunguliwa na mkeo kaomba aende msalani kujisaidia kisha mkeo kamfuata huko huko sasa mimi niliishia mlangoni.. au bosi nikaendelee kuwa angalia nini wanaenda kufanya?
 
Jamaa mmoja alikuwa na duka la kuuza dawa za binadamu(pharmacy).Siku moja,njemba moja ilifika ikaomba ipewe Dume pakti tatu.Baada ya kupewa zile pakti tatu,ile njemba ikalipa na kuondoka kwa furaha huku ikicheka sana.Muuza pharmacy akashangaa sana ila akapotezea.Ile njemba ikajenga mazoea,kila siku lazima ije kununua kondomu pakti tatu na inapotoka dukani inacheka saana.Siku moja baada ya mwenye pharmacy kumuuzia zile pakti tatu za dume,alimtuma msaidizi wake wa kazi amfuatilie yule jamaa anakoelekea,isije ikawa ni chizi anachezea kondomu kama mapulizo.Baada ya msaidizi wake kumfuatilia mpaka mwisho,alirudisha ripoti kwa bosi wake kama ifuatavyo;"ndio bosi,nimemfuatilia mpaka alipofika nyumbani kwako akapiga hodi,akafunguliwa mlango na mkeo!".
<br />
<br />
hahaha hiyo kali
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom