Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 872
Mtei muda wake umeshapita...
Kwa hiyo hana haki ya kujadili juu ya mustakabali wa nchi yake?
Mtei muda wake umeshapita...
Aende zake huko, kwanza maoni ya watu watu kama yeye hayana tija kwa taifa, au humjui kuwa alikuwa mnafiki kwa baba yetu wa Taifa?
Hayo maoni yake amelenga kuiokoa CHADEMA, kwani baada ya upuuzi wa majimbo kutoingizwa kwenye rasimu, hajaridhika na mgombea binafsi ili aendelee kumkandamiza Zitto, yeye na genge lake.
Wrong!! rais anachaguliwa na wananchi na anawajibika kwao tu, na siyo kwa vyama vya siasa. Haya mambo ya kamati kuu za vyama hayana maana.
Wakati ule Mtikila ameshinda kesi yake ya kutaka Mgombea binafsi NA serikali kumbania, wewe Ritz NA ndugu zako akina Malaria sugu mlikuwa mstari WA mbele sana kumpinga mgombea binafsi. Leo hii, wamemkubali mmeamua kuwa Bender
a! Duh!
True That... Tutakuwa ni NCHI PEKEE DUNIANI yenye MGOMBEA BINAFSI na hii ni kwasababu ya VIONGOZI waliobaki NCHINI hawakuwa VIONGOZi walipewa nafasi kuzijaza tuuu kwasababu ya UNYENYEKEVU na SIO UELEWA wa SIASA...
Sasa we ARE GOING TO PAY DEARLY...
Nilitoa maoni yangu kwamba Rais awe ni kiongozi wa chama cha siasa kilicho na sera zinazokubalika na pia wasaidizi wanaojulikana na kukubalika kwa wapiga kura. Wapiga kura wachague chama chenye sera na viongozi waadilifu, wazalendo na wenye kutaka kutuondoa katika lindi la umaskini.
Fisadi lililokwapua maliasili na rasilimali za umma na kuzificha katika akaunti za siri nje ya Tanzania, linaweza kuzirudisha na kuzitumia kununua kura na kuchakachua matokeo ya Uchaguzi Mkuu, ili lituongoze kama Rais wa kujitegemea. Likifaulu kuchaguliwa ndio tumekwisha!
Naamini pia tatizo la gesi Mtwara, ambalo naliona kama Janga la Kitaifa, lingeweza kuepukwa kama serikali za majimbo au wilaya zingepewa uwezo wa kutumia raslimali zao kwa maelewano na Serikali Kuu.
Nawasamehe wanaotumia lugha isiyokuwa na heshima kwa wazee kama mimi. Wamelelewa vibaya. Poleni sana.
Mkuu Kiranga unaweza kutupa mifano ya nchi ambazo zinaongozwa na wagombea binafsi?
Watu wengine tuna wasi wasi kama Mzee Mtei, lakini tukipata mifano hai iatatusaidia.
Wakati ule Mtikila ameshinda kesi yake ya kutaka Mgombea binafsi NA serikali kumbania, wewe Ritz NA ndugu zako akina Malaria sugu mlikuwa mstari WA mbele sana kumpinga mgombea binafsi. Leo hii, wamemkubali mmeamua kuwa Bender
a! Duh!
Mawazo ya Mzee Mtei tunayaheshimu. Hata hivyo, afahamu kuwa asilimia kubwa ya wapiga kura siyo wanachama wa Chama chochote cha siasa. Kwa mantiki hiyo, hawahitaji sera za chama cha siasa. Wananchi wanachotaka ni maendeleo yao na nchi kwa ujumla![/QUOT
PAMOJA NA LIKE YANGU NILIOKUPA MKUU MAWAZO YAKO MAZURI MNO.
Toka lini? Sasa kama Haujui ITIKADI ya CHAMA Huyo MTU akkisema yeye ni Fascist au Segregationist alisahau kuwaambia Majuwaani sababu hana chama itikadi zake zinatoka kichwani mwake wewe bado utakaa akuchinje akubague sababu tu alikupa huo UONGO wake JUKWAANI?
Marekani...
si ndo ushangae sasa,kwani ukigombea kupitia chama ndo huwezi kuwa fisadi?Kwani fisadi huyo anashindwa vipi kuanzisha chama cha siasa akanunua kura? Kwani kununua kura mpaka awe mgombea binafsi?
Kama wewe uliweza kuanzisha CHADEMA, fisadi huyo unayemuogopa atashindwa vipi kuanzisha CCJ?