babalao
Forum Spammer
- Mar 11, 2006
- 427
- 58
Kuna rafiki yangu mmoja wa kiume alinisimulia kisa kimoja kilichomkuta aliposafiri kikazi na dada mmoja ambaye wanafanya naye kazi pamoja na wanaheshimiana sana kama ifuatavyo. Walikodi vyumba viwili na Guest house zote zilikuwa zimejaa.
Ilipofika saa 4 usiku yule dada alipiga hodi kwenye chumba cha yule kaka akidai kuwa chumbani kwake kuna mdudu nge na anaogopa kulala kwenye chumba hicho. Yule kaka alijitahidi kumulika kwa tochi uvunguni mwa kitanda na kila mahali ili amuue yule nge lakini hakuonekana.
Baada ya hapo yule kaka alimshauri yule dada ahamie chumbani kwake kwa kuwa kitanda kilikuwa kimoja walikubaliana kulala mzungu wa nne yaani kila mmoja akilala kichwa kimoja kwenye mchago na kingine kwenya tendegu ili kukwepa kupata kishawishi.
Yule kaka alipata shida sana lakini alimudu mtihani kwa kujizuia na tamaa ya mwili, alifikiri mambo mengi kwamba yawezekana ni mtego wa yule dada kutaka kumpima au pengine huenda alikuwa na nia mbaya kama angeshindwa kuvumilia amwingize kwenye kesi ya kubaka.
Wana JF naomba mchango wenu Jee yule dada alikuwa na lengo gani kwa huyo kaka, kwani kama alikuwa anampenda au anamtaka si angemueleza kuliko kumtia majaribuni?
Karibuni mwenye hoja atoe hoja yake kwani suala hili bado lina mtesa yule rafiki yangu.
Ilipofika saa 4 usiku yule dada alipiga hodi kwenye chumba cha yule kaka akidai kuwa chumbani kwake kuna mdudu nge na anaogopa kulala kwenye chumba hicho. Yule kaka alijitahidi kumulika kwa tochi uvunguni mwa kitanda na kila mahali ili amuue yule nge lakini hakuonekana.
Baada ya hapo yule kaka alimshauri yule dada ahamie chumbani kwake kwa kuwa kitanda kilikuwa kimoja walikubaliana kulala mzungu wa nne yaani kila mmoja akilala kichwa kimoja kwenye mchago na kingine kwenya tendegu ili kukwepa kupata kishawishi.
Yule kaka alipata shida sana lakini alimudu mtihani kwa kujizuia na tamaa ya mwili, alifikiri mambo mengi kwamba yawezekana ni mtego wa yule dada kutaka kumpima au pengine huenda alikuwa na nia mbaya kama angeshindwa kuvumilia amwingize kwenye kesi ya kubaka.
Wana JF naomba mchango wenu Jee yule dada alikuwa na lengo gani kwa huyo kaka, kwani kama alikuwa anampenda au anamtaka si angemueleza kuliko kumtia majaribuni?
Karibuni mwenye hoja atoe hoja yake kwani suala hili bado lina mtesa yule rafiki yangu.