jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,987
- 22,515
- Thread starter
- #41
JK kukubali Balali akamatwe mean yuko tayari kuachia Urais maana hataweza kusaliika na na pesa za EPA hadi kwenye Uchaguzi ambazo ndiyo zikimpa ushindi .JK hawezi kukata tawi la mti huku kalikalia .
Lunyungu...Sasa kama ulikuwa unajua Kikwete hawezi kulikata tawi la mti alilokalia then kwanini aendelee kupewa sapoti na hata kuitingisha JF na kusababisha wengine tufungiwe ili tuendelee kumwita majina mazuri?
Ni bora iwekwe wazi kuwa EPA ISAHAULIWE,RICHMOND NK..Na kwamba Kikwete ni safi na CCM idumu milele!
NB:Ukiitembelea hii thread utaona ni kwa jinsi gani nilipambana toka Ballali akiwa hai...Hadi akisubiriwa afe kama mtuhumiwa huru!
Na huku sasa tukiongozwa na mama Killango kuwa warudishe pesa ambazo tayari wameshaanza kuzirudisha badala ya kuwakamata!
HAKUNA NJIA NYINGINE WABUNGE...KAMATENI HAWA WATU...Huu mjadala ulianza Ballali akiwa hai...Na sasa kuna habari kuwa kafa.Na inawezekana alikuwa akiusoma...Ni wengi wanakuja hapa kusoma haya mambo..Wenye nia nzuri na mbaya.Mungu aendelee kutuepusha na wale wenye nia mbaya.
Mgawanyiko huu...Niliutabiri na bado upo...Ila Mungu atuepushie mbali kwasababu mara zote binadamu hutofautiana kimawazo na pia hueshimiana.
Kwa hili...Ni wazi kuna mengi tusiyoyajua...Ila tuna maswali mengi muhimu ambayo kama hayatapuuziwa...Basi ukweli utawekwa bayana.