wazanaki
JF-Expert Member
- Mar 20, 2020
- 1,092
- 804
Wakuu huu mpambano wa Boxing wengi wanasema Wilder alipigwa kihalali, lakini kuna wengine wanasema Tyson Fury alidanganya. Upi ni ukweli?
Tukiangalia mpambano wa kwanza, Wilder almost alitaka kumuua Fury, alimdondosha mara mbili. Bila refa kuongeza kuzidisha sekunde kumi za kuhesabu game ilikua over.
Kiufupi, Fury anauwezo wa kubox ila hana power, mikono yake ni kama mito (kauli ya Wilder). Kwa hiyo game ya kwanza kwa mtazamo wangu wilder alishinda. Na kwa sasa trilogy itaendelea (mechi ya tatu).
Game ya pili, kuna fununu kuwa Tyson Fury alidanganya kipindi yupo chumba cha kuvaa gloves, nasikia alifunika kamera katika chumba cha kuvaa gloves ambapo ni kinyume na sheria na kuna kitu kigumu aliweka ndani ya gloves.
Kwenye mpambano, Fury aliweza kupasua mfupa wa sikio wa wilder na kutengeneza crack, kwa mujibu wa madoctor wa mifupa wanasema haiwezekani glove ya kawaida kupasua mfupa wa fuvu, kuna kitu. So wilder alifungua kesi na alishinda kesi.
Lakini kwa sababu Fury alikua ni mzungu, na kwa sababu media zote kubwa duniani ni za wazungu, ikaenezwa propaganda kuwa Wilder amepigwa kihalali na media zote kumshambulia Wilder. Hata ukija bongo hapa umuulize mtu yupi mkali kati ya Fury na Wilder atakwambia Fury kutokana na impact ya propaganda ya global media.
Kwa Watanzania haya mambo muwe mnayafatilia kiundani. Wilder ni mwenzetu ambaye anatuwakilisha. Tutoe sapport na kuonesha love.
Otherwise global media zitakua zinawapangia kila siku mtu wa kumpenda na mtu wa kumchukia.