Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,888
- 143,985
Iwapo Lowassa ataonyesha mwnenondo wa kutia mashaka ikiwamo kutohudhuria kikao cha kamati kuu cha leo bila kuwa na sababu za msingi au za kueleweka au mienendo mingine yoyote ile ya kutilia shaka katika siku zijazo, wanachoweza kufanya CHADEMA Kwa sasa,kulingana na mtazamo wangu,sana sana itakuwa ni kumvua ujumbe wa kamati kuu na si kumfukuza uanachama moja kwa moja.
Huu ni mtazamo wangu lakini pia unaweza ukawa ni ushauri wangu hasa endapo mzee huyu ataonenyesha mwenendo wa mashaka kwa siku zijazo ila natural justice ni muhimu sana hapa kabla ya kuchukua uamuzi wowote ule.
Binafsi siwashauri CHADEMA kumfukuza huyu mzee iwapo tu atakuwa amekwenda Ikulu kwa mambo yake binafsi unless mmebaini ana agenda ya siri lakini msikilizeni na mjipe muda wa kutafakari kabla ya kuchukua maamuzi yoyote yale.
Hili la kusifia tulivumilie tu maana binadamu tunatofautiana uvumilivu na mitazamo ingawa kwakweli kusifu katika mazingira kama haya tuliyonayo sasa kunataka uwe na moyo wa chuma kutokana na huu unyanyasaji na ukandamizaji wa wapinzani unaoendelea.
Tusifanye dhambi ya kufukuza mtu waacheni waondoke wenyewe unless mnabaini kuna hujuma wanataka kutufanyia ingawa hata hii hamahama ni aina fulani ya hujuma ila tuipuze kwasababu katiba inawapa haki hiyo.
Tuonyeshe mfano wa uvumilivu tofauti na wengine ili mradi tu tuna hakika hatuhujumiwi.
Tukumbuke huyu mzee amekwenda Nairobi kumuona Lissu karibu mara mbili kama sikosei hivyo kama ni kupongeza tu basi tunaweza kumvumilia unlesa mnagundua jambo la tofauti.
Tukimfukuza kwasababu ya matamshi yake tu dunia haitatuelewa na tujiandae kwa propaganda nziti sana kutoka upande wa pili kuwa sisi ni madikteta,hatuheshimu uhuru wa mawazo kama tunavyolalamika sisi wenyewe,n.k.
Na kama sababu za kumfukuza zipo basi ziwekwe wazi na hakikisheni anapata nafasi ya kujitetea tofauti na hapo tutachafuliwa sana na tutaambiwa hatuna haki ya kulilia uhuru wa kutoa mawazo na kukosoa na huu ndio mtego unaotukabili katika kushughulikia hii issue
Tusisahau maadui zetu wanapenda kuona tunafarakana na watafanya kila juhudi na kutumia kila mwanya kufanikisha azima yao hiyo.
Vile vile,tofauti na mtazamo wa watu wengi,kikao hiki cha dharura huenda kimeitishwa mahususi kwa yeye kutoa taarifa ya nini hasa aliongea akiwa Ikulu na nini walikubaliana iwapo hakwenda kwa agenda binafsi ingawa alienda kimya kimya bila kutoa taarifa kwa wenzake na atapaswa kueleza sababu ya kushindwa kuarifu chama.
Pia, kikao hiki cha dharura kinaweza kuwa na agenda ya kumaliza au kuzika dalili ya mivutano iliyotaka kuanza kujitokeza baina ya wanachama na wajumbe wa kamati kuu baada ya Lowassa kutoa matamshi yale na pengine kuweka mikakati ya kuepuka hali kujirudia tena katika siku zijazo.
Tusubiri.
Huu ni mtazamo wangu lakini pia unaweza ukawa ni ushauri wangu hasa endapo mzee huyu ataonenyesha mwenendo wa mashaka kwa siku zijazo ila natural justice ni muhimu sana hapa kabla ya kuchukua uamuzi wowote ule.
Binafsi siwashauri CHADEMA kumfukuza huyu mzee iwapo tu atakuwa amekwenda Ikulu kwa mambo yake binafsi unless mmebaini ana agenda ya siri lakini msikilizeni na mjipe muda wa kutafakari kabla ya kuchukua maamuzi yoyote yale.
Hili la kusifia tulivumilie tu maana binadamu tunatofautiana uvumilivu na mitazamo ingawa kwakweli kusifu katika mazingira kama haya tuliyonayo sasa kunataka uwe na moyo wa chuma kutokana na huu unyanyasaji na ukandamizaji wa wapinzani unaoendelea.
Tusifanye dhambi ya kufukuza mtu waacheni waondoke wenyewe unless mnabaini kuna hujuma wanataka kutufanyia ingawa hata hii hamahama ni aina fulani ya hujuma ila tuipuze kwasababu katiba inawapa haki hiyo.
Tuonyeshe mfano wa uvumilivu tofauti na wengine ili mradi tu tuna hakika hatuhujumiwi.
Tukumbuke huyu mzee amekwenda Nairobi kumuona Lissu karibu mara mbili kama sikosei hivyo kama ni kupongeza tu basi tunaweza kumvumilia unlesa mnagundua jambo la tofauti.
Tukimfukuza kwasababu ya matamshi yake tu dunia haitatuelewa na tujiandae kwa propaganda nziti sana kutoka upande wa pili kuwa sisi ni madikteta,hatuheshimu uhuru wa mawazo kama tunavyolalamika sisi wenyewe,n.k.
Na kama sababu za kumfukuza zipo basi ziwekwe wazi na hakikisheni anapata nafasi ya kujitetea tofauti na hapo tutachafuliwa sana na tutaambiwa hatuna haki ya kulilia uhuru wa kutoa mawazo na kukosoa na huu ndio mtego unaotukabili katika kushughulikia hii issue
Tusisahau maadui zetu wanapenda kuona tunafarakana na watafanya kila juhudi na kutumia kila mwanya kufanikisha azima yao hiyo.
Vile vile,tofauti na mtazamo wa watu wengi,kikao hiki cha dharura huenda kimeitishwa mahususi kwa yeye kutoa taarifa ya nini hasa aliongea akiwa Ikulu na nini walikubaliana iwapo hakwenda kwa agenda binafsi ingawa alienda kimya kimya bila kutoa taarifa kwa wenzake na atapaswa kueleza sababu ya kushindwa kuarifu chama.
Pia, kikao hiki cha dharura kinaweza kuwa na agenda ya kumaliza au kuzika dalili ya mivutano iliyotaka kuanza kujitokeza baina ya wanachama na wajumbe wa kamati kuu baada ya Lowassa kutoa matamshi yale na pengine kuweka mikakati ya kuepuka hali kujirudia tena katika siku zijazo.
Tusubiri.