Mtazamo wa watu kuhusu vitisho vilivyotolewa na serikali kwa chadema

mmzalendo

Senior Member
Nov 1, 2010
165
1
MAONI KUHUSU KAURI ZA VIONGOZI WA SERIKALI ZIDI YA MAANDAMANO YA CHADEMA

baada ya serikali kutoa kauri kupitia viongozi wake mbalimba kuhusu maandamano ya chadema
lifeofmshaba imekua ikifanya uchunguzi kuona wananchi wananchi wazipokeaje hizo kauri za viongozi wetu wa juu kabisa wa serikali
tukianza na mtandao wa facebook
wengine wameonyesha kukerwa na wanazitafusiri kauri hizo kama vitisho na zisizo na umuhimu
wote kutolea kwa kuwa matatizo yote wanayodai waandamani ni ya kweli yapo na yanaisumbua jamii ya kitanzania kutoka hilo wengi wametoa maoni kwa mtazamo kwamba badala serikali kujaribu kupuza madai hayo no bora kuangalia uwezekano wa kuondoa hayo matatizo na wengi wameonekana kutoridhika na matumizi ya viongozi wa serikali ukilinganisha na maisha wanayoishi watanzania
sehemu ya maoni
WAKATI CCM ikitaka dola ikidhibiti Chadema, Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya tatu, Fredrick Sumaye, amekitaka chama hicho tawala kukabiliana na hoja za Chadema kisiasa badala ya kuiachia Serikali
Eti Rais atachoka kuvumilia!!?!? Den afanye nini? C achoke kuvumilia issue za dowans,mgao wa umme,ufisadi,na mfumko.?? Chadema wana point na tupo nyuma yao daima wasife moyo!
Hapo sasa,hoja za Chadema na CCM katika mpambano,sio serikali na chadema naona sasa wananchi wanaelewa somo na wahamishie ktk halmashauri wanazoongoza wao chadema watupe mfano wa kiutendaji haswa 2nawasubiri.


Mjini Daslam kiza ni totoro!wenyeji wakomkimya mioyoyao ikisononeka.kila kona ya nchi sasa ina majonzi,hakuna matumaini..haijulikani mwokozi atazaliwa lini,shujaa wa kuwainua wanyonge wa TZ.mko wapi wenye hekima?wamekwenda wapi wenye uwezo na ujuzi?je miongoni mwenu hamna waliohodarii?elim zenu zimewasaidiaje vikongwe,walio utunza urithi wenu? TZ inajifunza nini kutoka Libya!nchi tajiri miongoni mwa Africa,huko huduma zote ni bure..lakini wanasema Ghadafi must go!
katika mtandoo wa jamii forum hali bado ilikuwa inalemea kwa serikali japo kuna watu wachache wanaona kama amani inapotelwa na haya maandamano ya chadema kimsingi bado kuna kundi kubwa linawatetea chadema na kuponda kauri za serikali
na sisi tulipojaribu kupitia maoni mbalimbali yaliyo hachwa kwenye blog yetu na wasomaji wetu bado hali n hiyo hiyo

sijui hii inatoa ujumbe gani kwa serikali yetu lakini sisi tunaona kuna kila sababu sasa ya kuwa wakweli kwa wananchi na wakati ni sasa

UCHUNGUZI HUU UMEFANYWA NA www.lifeofmshaba.com

SAUTI YA UMMA
 
Back
Top Bottom