Mtazamo wa raia wa nchi za Afrika wanaoishi Ulaya na Marekani juu ya Hayati Rais Magufuli

Ndugu wana JF nimeona nishare na ninyi kile walichonieleza hawa marafiki zangu niliokutana nao South Africa kipindi nahangaikia ndoto zangu kuhusu mtazamo wao kwa aliyekuwa rais wetu JPM.

Kuna rafiki yangu raia wa Kameruni ila kwa sasa anaishi Marekani. Jamaa ni PhD wa uchumi na amefundisha baadhi ya vyuo hapo Johannesburg kabla ya kwenda Marekani kutafuta maslahi zaidi. Mwezi uliopita alikuja Tanzania baada ya kuzuiwa kuingia Australia ambako pia alikuwa anafanya consultation na makampuni flani yaliyokuwa yanahitaji huduma yake. Alipozuiliwa kuingia Australia kwa sababu ya restrictions za Covid 19 aliamua kuja Tanzania kupumzika hivyo nilipata wasaa wa kuonana na kuongea naye, maana tulikuwa hatujaonana zaidi ya miaka 10.

Huyu bwana alinishangaza sana kuhusu jinsi alivyokuwa anamwongelea JPM. Jamaa alikuwa anasema Tanzania tumempoteza rais bora. Acha ninukuu maneno yake. "Magufuli was the best president in Africa". Anasema "the guy was doing a good job"

Kiufupi jamaa anasema Magufuli alikuwa kiboko, na nchi alikuwa anaipeleka mbele. Nilijaribu kumwuliza kipi kinachomfanya aseme Magufuli alikuwa rais bora. Alisema yeye kama mwanauchumi na mfuatiliaji mzuri wa Siasa za Africa mambo aliyokuwa anayafanya Magufuli ni makubwa sana na hakuna rais yeyote wa Afrika mwenye huo uthubutu. Alitaja issue ya kusimamia madini na kuyabana makampuni ya kigeni kuchota madini ni kitu ambacho marais wengi Afrika kimewashinda.

Jamaa alikuwa anasema Magufuli alikuwa ni rais wa ajabu sana ambaye haogopi wazungu. Nilijaribu kumwambia mbona sisi humu nchini tunaona kama alikuwa anatupelekesha tu, tulikuwa hatuna uhuru hata wa kuongea, hofu imetanda, anaminya demokrasia. Jamaa akajibu hayo mambo ya kuminya demokrasia na kunyima uhuru hayaoni kama ni issue ya msingi ukilinganisha na kazi kubwa ya kuijenga nchi aliyokuwa anaifanya. Anasema huko nje (west Africa) Magufuli ni popular sana. Jamaa anasema Magufuli was the best president in Africa.

Kuna jamaa zangu wengine raia wa Zambia na DRC. Huyu wa Zambia ameoa muaustralia na anaishi Sydney na huyu wa DRC yeye yuko Durban South Africa. Wote hawa nikiwa naongea nao huwa wanasema Magufuli was the best president ever.

Pia kuna kidada flani kizungu kiraia cha Ireland (UK) kinaishi South Africa, ni kisanii yani kinaimba mziki tulikuwa tunasoma nacho chuo kimoja na pia tunasali pamoja huwa kinaniambia Magufuli alikuwa the best president. Kilikuwa very interested na siasa za Tanzania baada ya kumwona Magufuli akifanya usafi kule feri. Kuna picha kilinitumia ya Magufuli anafanya usafi kule feri amezungukwa na wauza samaki.

Binafsi sikuwa mshabiki sana wa Magufuli ila kusema ukweli nimeanza kushawishika na kuamini kuwa jamaa alikuwa rais mzuri. Nikiangalia ile miradi aliyoianzisha kwa muda mchache aliotawala, je kama angeendelea kuwepo kwa mhula mwingine ingekuwaje. Iangalie Morogoro road kutokea Kimara kuelekea Kibaha jinsi inavyopendeza utadhani nipo barabara za South Africa. Ukiweka pembeni mapungufu yake jamaa alikuwa anaipeleka nchi mbali sana.
Tumsamehe kwa mapungufu yake na tumwombee pumziko la amani huko aliko.
Magufuli alikuwa Rais mbovu humu Jamii Forums na twitter only.
 
Sikia dogo sisi kamwe hatumchukii Magufuri! msitulishe maneno ni dhambi pia kwenu km baba yenu huyo! ila tunacho chukia ni vitendo vyake vya kikatili dhidi ya Binadamu wenzake tena wabongo wa chini tu wasiokuwa na hatia, anao paswa kuwalinda,

Yeye angekuwa mbabe angeenda kusaidia nchi jirani zisipigwe na Al shaabab km Somalia na kenya, siyo kukimbizana na vijitu vidogo vidogo hivi !! Nyerere kidume kilikuwa frontline state! dhidi ya kaburu! na kweli ili tick!

afadhali hata angewafunga tu yakaisha lkn chuki za kutaka kuua kwa siri tena kwa risasi za moto bila kujali! km vipi si ange waita tu wampe mshiko! kwani unaona yule kijana muhindi alikwenda kumzika?

alikuwa anaua km anaua nzi! ili apate hela za ziada eti akaishi kwa anasa kijijini kwao tu basi! na kuwapendezesha wapiga kura wake! ni wazi Mungu hakupenda atawale, angesikia sauti ya Mungu nyikani angeishi mpaka leo! lkn kibri!!
Acha kutumia nguvu nyingi kutuaminisha upumbavu wako,mpo wachache sana majinga kama nyinyi na mafisadi wenzenu ndo mlimchukia,Kuleni nchi Basi kuishi mile,msitake kutuforce
 
Acha kutumia nguvu nyingi kutuaminisha upumbavu wako,mpo wachache sana majinga kama nyinyi na mafisadi wenzenu ndo mlimchukia,Kuleni nchi Basi kuishi mile,msitake kutuforce
Na bado!! mtaumuka sana, hamjui tu! Mungu wetu hadhihakiwi dogo nuna pasuka!!.... ndo zenu hizo tutaishi tutajaa umri!! Muhindi huyo hapo ndo kwaanza kateuliwa kuwa mshauri wa fedha wa Rais Ramaphosa!

Kabendera yuko kwa Beberu ana kula Bata!! jiwe anakandamizwa na Dongo tani saba tena yuko hai kule ujue?? kuna nini hapo? .. hakukumbuka hata kutubu?.....mjifunzege!! hamtaki! mweee!
 
Alikuwa na mabaya mengi kuliko mazuri,na alikuwa mtaalam wa propaganda kuliko hata hitler hao wanaomsifia walijazwa propaganda tu ni kama kagame tu,ana zuri moja tu ila mabaya mengi
Kwamba wanajazwa propaganda, hawana macho?
 
Back
Top Bottom