Kwa wale mnaofuatilia habari, jana warioba alipoulizwa kuhusu mtazamo wake juu ya chadema kutoka nje ya bunge alisema'' kutoka nje wakati MTU mmoja anaongea siotati'' na hata hivyo chadema hawajakiuka kifungu chochote cha kanuni za bunge,vile vile Jaji mkuu nae alisema kwa jinsi anavyo fahamu hakuna kifungu kilichokiukwa ispokuwa ni swala la ustaarabu.pia wakubwa hao walisema haya mambo yanaweza kujadiliwa tu kwani katiba ni kitu kinachoishi hata hivyo katiba imeisha badilishwa mara kibao tangu kutungwa kwake 1977,pia warioba alisema ni swala la kuangalia kwamba katiba ilele iendelee kuwekewa viraka au itungwe mpya na wananchi wataamua wenyewe.sasa ccm wanalalamika nini,chadema imewakosea wapi na kwa kukiuka kifungu gani ambacho wao wanakijua ambacho Jaji mkuu mstaafu pamoja na Jaji mkuu wa sasa wasichokifahamu.Jamani mambo haya hayaendeshwi kwa hisia tu,yanataratibu zake.Mtu hawezi kukurupuka na hoja zake binafsi ambazo hazijulikani, tatizo ccm wamezoea kupeleka washangiliaji bungeni kama vile wanaenda nje ya nchi kucheza mpira na hivyo kwenda na washabikiaji na washangiliaji, mtu ukimuuliza chadema wamevuja kanuni gani ,hajui lakini anashangilia tu ccm ccm ccm ccm sasa jamani wana ccm bungeni sio mpirani ambapo unaweza kushangilia tu hata timu yako ikifungwa,na ndio maana ccm walikuwa wana shangilia na kupiga mafoki wakati chadema walipokuwa wakitoka nje bunge.