Kwa hivyo wewe unaamini sisi ndio tunaweza kuweka vifaa vizuri vya uchunguzi wa afya kuliko Marekani, Ufaransa, Italia, Spain na Uingereza?

Kwanini wale hali imekuwa vile na vifaa vyao vyote?
Subiri huo muingiliano na wenzetu utatupa majibu karibu, tena nasema umeshaanza kutupa majibu.
Si tulikuwa na wagonjwa sita mara siku mbili tatu wakafika 12, na wengi wao ndio wametokana na huo muingiliano unaotaka tuendelee nao.
Mkuu sina maana hiyo, ila hata kwa trend ya ugonjwa huu kwa upande wa Africa hauonyeshi kuwa na madhara makubwa sana ukilinganisha na mabara ya wenzetu yenye baridi kali.

Kwa kusema hivyo sinabezi kwamba ugonjwa huu sio hatari.

Tuchukue tahadhali kwa kufuata maelekezo tupewayo na mamlaka husika.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha na hii serikali haya mambo haya bhana ni Mungu tu anatusaidia tu.
Ni kweli Mungu hutusaidia, imetupasa kuwaamini pia tuliowapa nafasi kutuongoza kwani wanataarifa sahihi na hivyo naamini hufanya maamuzi sahihi kutokana na taarifa walizonazo au wanazozipata.

Na ikiwa tunamaoni au taarifa ni vema kuzifikisha kwa mlengo wa kujenga au kusaidia.

Jamii ni yetu sote na serikali ni yetu pia ni kubadili mitazamo tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali imejitahidi hadi Sasa Kufanya inachotakiwa Kufanya juu ya Janga hili la Corona.
Kwa Upande wetu sisi Wananchi naona bado tunapuuzia Kama desturi yetu Watanzania, Sisi tumekuwa watu wa Kuchukulia poa Vitu/Mambo yaliyo Serious. Huwa tunasubiri hadi Hali iwembaya ndiyo tuone Kwamba Jambo hili ni serious, tusifike uko kwani Kinga ni Bora kuliko tiba.

Serikali pia inapaswa Kisimamia kile inachoelekeza Kwa Wananchi wake ikiwezekana ku-enforce hizi taratibu za Kufanya kupambana na Corona. Kwamfano, Askari wa Usalama barabarani wanaweza Kushughulikia Suala la Daladala Kujaza abiria Kupita Kiasi, hapa naona ule utaratibu wa levositi unaweza Kurudi tumika.
Suala lingine la Msingi, Serikali ijaribu kutazama namna Bora ya Kushughulikia suala la Watu wanaoingia ndani ya nchi Kutoka Mataifa Mbalimbali. Suala la Kutegemea Kipimo ambacho majibu yake hayana uhakika Kwenye ili Janga la Corona sidhani Kama ni busara, ninafikilia hapa tungefanya hili; lakwanza Kupunguza watu wanaoingia nchini na pili wale wanaoruhusiwa kuingia basi wakae Kwenye Karantini kwa siku 14 ili Kujiridhisha Kama wapo fiti, then ndiyo muwaruhusu.

Zingatio :

Maisha ya Mwanadamu ni Muhimu zaidi ya Uchumi, ndiyo Maana ata izo nchi zenye Uchumi Mkubwa dunia Wamechukua hatua bila Kujali Uchumi wao Utadondoka Kiasi gani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pamoja mkuu
Serikali imejitahidi hadi Sasa Kufanya inachotakiwa Kufanya juu ya Janga hili la Corona.
Kwa Upande wetu sisi Wananchi naona bado tunapuuzia Kama desturi yetu Watanzania, Sisi tumekuwa watu wa Kuchukulia poa Vitu/Mambo yaliyo Serious. Huu tunasubiri hadi Hali iwembaya ndiyo tuone Kwamba Jambo ili ni serious, tusifike uko kwani Kinga ni Bora kuliko tiba.

Serikali pia inapaswa Kisimamia kile inachoelekeza Kwa Wananchi wake ikiwezeka enforce hizi taratibu za Kufanya kupambana na Corona. Kwamfano, Askari wa Usalama barabara wanaweza Kushughulikia Suala la Daladala Kujaza abiria Kupita Kiasi, hapa naona ule utaratibu wa levositi unaweza Kurudi tumika.
Suala lingine la Msingi, Serikali ijaribu kutazama namna Bora ya Kudhughulikia na Watu wanaoingia ndani ya nchi Kutoka Mataifa Mbalimbali. Suala la Kutegemea Kipimo ambacho majibu yake hayana uhakika Kwenye ili Janga la Corona sidhani Kama ni busara, ninafikilia hapa tungefanya hili; lakwanza Kupunguza watu wanaoingia nchini na pili wale wanaoruhusiwa kuingia basi wakae Kwenye Karantini kwa siku 14 ili Kujiridhisha Kama wapo fiti, then ndiyo muwaruhusu.

Zingatio :

Maisha ya Mwanadamu ni Muhimu zaidi ya Uchumi, ndiyo Maana ata izo nchi zenye Uchumi Mkubwa dunia Wamechukua hatua bila Kujali Uchumi wao Utadondoka Kiasi gani.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Najiuliza tu waungwana hawa watanzania walioko nje ya nchi kipindi hiki cha mapambano ya Corona je wabakie huko huko?

Rais wa Uganda mh Museveni amefanya maamuzi magumu ya kuwazuia waganda walio nje ya nchi kurejea nchini hadi pale ugonjwa wa Corona utakapodhibitiwa.

Je, uamuzi wa mh Yoweri unafaa kuigwa?

Maendeleo hayana vyama!
 
Unatakiwa ubaki uko uko. Uwe mzima au hapana. Alafu hta kma mimi ningekuwa nipo nje narudije kwenye nchi kma Tz ambapo Rais kaonesha kuwa careless juu maisha ya watu, yeye kaangalia tu uchumi ila ksahau uchumi unajengwa na watu wenye afya njema.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom