Mtazamo: Hatari kuu za kiusalama katika Taifa la Tanzania

Poa 2

JF-Expert Member
Jul 7, 2019
1,294
1,288
Nawasalimu wote.

Moja kwa moja kwenye mada, Kama kichwa Cha uzi Hapo juu kinavyojieleza kwamba huu Ni mtazamo wangu TU na Kama nimepotoka nitakubali kushauriwa na kukosolewa kwa staha na matusi yote poa.

Kuna Mambo mawili ambayo huwa nayafikiria Sana lakini sipati majibu, na Mambo hayo ni:

(1) Mamlaka makubwa Sana ya RAIS kikatiba.

(2) Mamlaka makubwa ya tume ya uchaguzi ya Taifa

Mambo/ Mamlaka haya ipo siku na mda tutajutia na kujidharau sana watanzania, kwa kuruhusu kuishi juu ya makaburi haya.

Hivi watanzania na watawala wa Sasa mnawaza Nini? Binadamu wa Sasa na ulimwengu wa leo kweli tunaishi kwenye nchi ambayo Kuna watu wanaweza kufanya Jambo lolote bila kuthibitiwa, kuhojiwa Wala kushtakiwa.

RAIS na wale wenye Kinga ya kutoshitakiwa kwa makosa yoyote wafanyayo. Binadamu yeyote wa kizazi si wa kuaminiwa kwa kiwango hicho hata kidogo.

Magufuli alikuwa mfano mzuri Sana kwenye hili, na ccm mnaona hili Ni Jambo jema lakini hili Ni bomu lilikochumbani kwenu wenyewe na litawalipukia siku si nyingi.

Lakini pia tume ya Taifa ya uchaguzi kwamba ikishatangaza matokeo hairuhusiwa kupingwa wa kuhojiwa na yeyote ccm na watawala mnafurahia hili na kuona ndio kete ya ushindi lakini kumbukeni binadamu wa Leo si wa kuaminiwa kwa kiwango hicho hata kidogo,

Hilo Ni kaburi mnalofikiri mmewachimbia wengine lakini mtazikwa wenyewe kwenye kaburi hili siku si nyingi. Ninaomba kumalizia kwa kuweka maswali kadhaa ambayo Mara nyingi huwa najiuliza.

(1) Hivi itakuwaje siku pandikizi au adui yeyote wa Taifa letu akishika madaraka ya uraisi

(2) Hivi itakuwaje siku madaraka haya akipata kichaa,mwendawazimu, adui wa ccm akatumia Mamlaka haya kukifuta chama chenu?

(3) Hivi itakuwaje siku RAIS akaamua kuuza nchi au rasilimali za nchi atakavyo?

(4) Hivi itakuwaje siku mwenyekiti wa NEC kwa bahati mbaya, makusudi ama kwa kuhongwa au vyovyote vile akajitangazia mtu/ chama chochote kisichokuwa CCM kwamba kimeshinda uchaguzi?

Najua wachache watajigamba na kupinga kwamba haya hayataweza kutokea kwa vijisababu Kama tuna polisi majeshi na usalama wa Taifa lakini hoja hii imepungua nguvu Sana siku za karibuni hasa ukizingatia mifumo, miundo na sheria za uundwaji wa taasisi hizi.

Ninawaomba Sana CCM na watawala hayo Mamlaka haya si salama kwa nchi, CCM, watawala na watanzania na tuchukue hadhari kabla ya hatari hakuna aliye salama, kumbukeni maadui zetu wanatafuta mianya na wanaweza kuhonga yeyote tusiruhusu kwa nyakati flani kukabidhi uhai wa watanzania kwa mtu mmoja ambaye naye hajakamilika.

Haya Ni mawazo na mitazamo yangu TU jamani naomba kuelimishwa.

😁😁😁😁Ni mtazamo kutoka jamaa wa ighanuda😁😁😁
 
Mungu siku akiamua haya yote si kitu. Gwaji me wanaopinga chanjo 'hawatashindwa' Gwaji ke ni megundua leo 'kumbe ukiwapa hel'

Na akae akijua sisi wengine si wahuni, hatulipwi.

Tafuta hii kideo clip 'Kaka wa Gwajima.... U - tube
 
Akili kubwa imeandika kwa ufupi na imeeleweka. Nakazia;

1.Kwanini tume ya uchaguzi ikitangaza matokeo ya urais hayatakiwi kupingwa mahakamani?

Hoja hii inapewa nguvu na namna tatu ninazoziona Mimi ,,,.;
1.Namna mwenyekiti wa tume anavyopatikana. (Anachaguliwa na Rais)
2.Namna wakurugenzi wa halmashauri wanavyobadilika kimazingara kuwa wasimamizi wa tume ngazi ya wilaya.( Kumbuka wakurugenzi ni makada wa chama Cha mapinduzi)
3. Namna wasimamizi wa vituo na wasimamizi wasaidizi wanavyopatikana.(Mara nyingi hapa hutumika walimu manesi nk) Hawa hutishwa Sana kwamba mmeajiriwa na serikali ya ccm hivyo nilazima ishinde kwenye kituo chako) mbaya zaidi uchaguzi wa 2020 walimu Hawa walipewa matokeo kwenye vikaratasi ya Kila kituo yaliyoonyesha ccm imeshinda hivyo walichotakiwa wao ni kuhjakikisha wanabandika matokeo waliyopewa halmashauri na sio matakwa ya kura za wananchi.

Swali kwa mfumo huu kwanini matokeo ya urais yasihojiwe mahakamani?
 
Nawasalimu wote.

Moja kwa moja kwenye mada, Kama kichwa Cha uzi Hapo juu kinavyojieleza kwamba huu Ni mtazamo wangu TU na Kama nimepotoka nitakubali kushauriwa na kukosolewa kwa staha na matusi yote poa...
Wanalumba mada Kama hizi huwa mnapizipita Kama hamjui kusoma vile😁😁😁😁😁
 
unawasi wasi gani mbona nchi hii ilishaongozwa na vichaa wengi tu tena juzijuzi na hata sasa wapo
Wasiwasi ndio akili kichaa aliyepita juzi Kati alikuwa hatari kuliko hatari yenyewe na alifika kiwango Cha juu kabisa Cha kujitawaza rais wa milele na wote sio ccm Wala Nani tuliamua kukunja mbawa na kumwachia Mungu, somo Hilo lilipaswa lituingie na tuone hatari mbele lkn wapi
 
Nawasalimu wote.

Moja kwa moja kwenye mada, Kama kichwa Cha uzi Hapo juu kinavyojieleza kwamba huu Ni mtazamo wangu TU na Kama nimepotoka nitakubali kushauriwa na kukosolewa kwa staha na matusi yote poa....
Wewe ni mwelewa. Huhitaji kuelimishwa. Umesema yaliyopo na yajayo. Salama ya watawala wa leo ni hatari yao mbele ya safari. CCM imewagawa raia katika makundi mawili: Wanaocheka na kufurahia; na wanaonuna kwa hasira pamoja na kuteseka.

Matokeo ya haya ni mlipuko (social explosion) na mangamizi kwa wale wanaofurahi na kucheka. "it is only through a proper constitutional reform that will mitigate the effects arising from this eminent and deepening class struggle". Aksante kwa uzi wako mwanana.
 
Wewe ni mwelewa. Huhitaji kuelimishwa. Umesema yaliyopo na yajayo. Salama ya watawala wa leo ni hatari yao mbele ya safari. CCM imewagawa raia katika makundi mawili: Wanaocheka na kufurahia; na wanaonuna kwa hasira pamoja na kuteseka. Matokeo ya haya ni mlipuko (social explosion) na mangamizi kwa wale wanaofurahi na kucheka. "it is only through a proper constitutional reform that will mitigate the effects arising from this eminent and deepening class struggle". Aksante kwa uzi wako mwanana.
Nashukuru kwa mchango wako mzuri ndugu usisite kushauri, kupendekeza ama kuboresha chochote kwa ajili ya wengine
 
Wewe ni mwelewa. Huhitaji kuelimishwa. Umesema yaliyopo na yajayo. Salama ya watawala wa leo ni hatari yao mbele ya safari. CCM imewagawa raia katika makundi mawili: Wanaocheka na kufurahia; na wanaonuna kwa hasira pamoja na kuteseka. Matokeo ya haya ni mlipuko (social explosion) na mangamizi kwa wale wanaofurahi na kucheka. "it is only through a proper constitutional reform that will mitigate the effects arising from this eminent and deepening class struggle". Aksante kwa uzi wako mwanana.
"it is only through a proper constitutional reform that will mitigate the effects arising from this eminent and deepening class struggle"

Word word word word

Hili andiko na mwenye akili alisome, linafikirisha mnoo
 
"it is only through a proper constitutional reform that will mitigate the effects arising from this eminent and deepening class struggle"

Word word word word

Hili andiko na mwenye akili alisome,linafikirisha mnoo
Wenye mawazo hafifu wanapita kimya kimya bila hata kuacha alama😁😁😁😁
 
Mleta mada una akili kuliko watu wanaovaa Suti na kutundika tai zenye rangi za bendera ya taifa na wanaotembelea Ma-VX
 
Mleta mada una akili kuliko watu wanaovaa Suti na kutundika tai zenye rangi za bendera ya taifa na wanaotembelea Ma-VX
Duu! Ahsante Sana sijawahi kuvaa suti hasa za kibongo naogopa kuidhalilisha akili yangu
 
Magufuli aliletwa na Mungu makusudi ili Tanzania tufanye mabadiliko makubwa baada ya yeye kuondoka alijaribu Kila kitu sio kwamba akipenda la hasha Mungu alimtumia Kama somo kwetu ili tuangalie nyufa tuzizibe Ila kwakuwa system yetu na deep state ziko slow kufanya mageuzi wanasubiri mpaka damu imwagike. Kwa wenye akili magufuli alikuwa somo kamili kwa system na alert pia. Nitafafanua kwa mifano hai.

Mfano wa kwanza.

Kauli Tata kwamba nikulipe mshahara nikupe nyumba gari walinzi halafu umtangaze mpinzani. Je hapa kweli mtatuambia hakuna umuhimu wa katiba mpya?

Mfano wa pili.

Namna alivyotawala kibabe bila kujali taratibu Mila na desturi za taifa angeendelea kutawala miaka hata miwili angeipoteza sehemu hata ya system yenyewe.
 
Back
Top Bottom