Mtawala azibaye midomo ya watu ni mbaya kama shetani

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,883
MTAWALA AZIBAYE MIDOMO WATU NI MBAYA KAMA SHETANI

Kwa Mkono wa Robert Heriel.

Mtu yeyote anayependa kuziba watu midomo wasimseme jua huyo ni kama shetani, hivyo ndivyo andiko hili ninavyoanza nalo.
Shetani ndio anapenda mambo ya sirini, kuficha ficha, kuziba watu midomo wasiseme mabaya yake. Kuzuia uhuru wa watu kwani katika uhuru shetani anajua ubaya wake utadhihirika.

Kwenye uhuru kuna ukweli, penye ukweli kuna uwazi, penye uwazi kuna haki, kwenye haki kuna amani, kwenye amani kuna furaha.

Mtawala yeyote hata afanye mema gani lakini kama ataminya Uhuru basi ameminya haki ya msingi ya mwanadamu, uhuru ndio maendeleo, ndio maana kila taifa kuna siku ya kusherekea uhuru wao kila mwaka. Uhuru ndio maendeleo. Sasa mtu anapoziba watu midomo ni kwamba hataki watu waongee pale anapokosea, ni kama shetani tu.

Watu wa namna hii hutumia nguvu kubwa kwenye propaganda za kujisifia na kuponda wale wote wanamkosoa ikiwezekana kutaka kibali cha kuweza kuwaua hata kama sheria haziruhusu.

Kwa vile jamii yetu wengi wa watu ni wajinga wasio na akili ya kuchambua mambo ni rahisi kwa kiongozi wa namna hii kuchota akili zao.

Huwaga nasemaga Ujinga ni upofu, hivyo watawala wa namna hii hutumia ujinga wa watu wengi kuwalaghai kwa propaganda za hovyo ili aonekane mwema.

Hatukatai mtu kuwa mjinga hilo hatuwezi kukataa, hiyo ni haki ya mtu kuchagua ujinga au werevu, tunachokataa ni kuvunja sheria na haki za binadamu kwa kisingizio cha ujinga au werevu. Tunachopishana na watawala madikteta ni kuvunja haki za watu kwa kukandamiza uhuru wa watu hasa wale werevu watakaompinga kutokana na matendo yake maovu

Madikteta huwatumia zaidi watu wajinga na masikini katika kujizatiti kushika dola. Madikteta hawawezi kushikamana na watu werevu na matajiri kwani utawala wao utakuwa mashakani. Werevu na matajiri wanajua umuhimu wa uhuru katika maisha yao. Lakini masikini na wajinga wao hawana tofauti na wanyama, wao lolote kwao ni sawa ilimradi maisha. Ni kama kuku au mbwa wa kufuga, hata uwafunge bandani wao hawaoni shida ilimradi wajipatie chakula hata kama sio mlo kamili. Lakini Watu werevu na matajiri wanajua maisha ni zaidi ya chakula, maisha ni uhuru wa kuishi bila kuathiri wengine.

Ndio maana madikteta wote wawapo kwenye majukwaa hujifanya kuponda matajiri kwa kusema ni wezi na wanawadhulumu masikini, lengo lao ni kupata wafuasi kutoka watu masikini, na kwa vile masikini wengi wao ni wajinga hujikuta wakimpenda Dikteta zaidi kwani wanaona yupo upande wao ilhali uchumi wao bado unakuwa dhoofu.

Madikteta pia, huwaponda werevu na wasomi kama vile maprofesa, na watu wote wenye vipaji vya muhimu wenye kutetea haki. Dikteta asimamapo jukwaani ni kawaida kumdhalilisha Mwerevu ili yeye(dikteta) apate sifa kwa watu wajinga wasioweza kuchambua mambo. Hivyo sio ajabu ukashangaa wajinga wakishangilia pale mwerevu adhalilishwapo na dikteta.

Mjinga na masikini wanafanana sifa kwa sehemu kubwa na wote hufurahi waonapo mwerevu na tajiri apatwapo na madhila.

Mtawala anayeziba watu mdomo kamwe usimuamini hata kama utamkuta mbinguni, ni shetani mbaya anayejaribu kuficha maovu yake.

Hata hivyo jambo moja ni dhahiri nalo ni; ukiziba watu mdomo ukiwa uhai, basi watu watakusema ukiwa Mfu. Hivyo akili kumkichwa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa, Mwanjelwa, Mbeya mjini
 
Sjui Kwa nini Mungu hakumziba midomo shetani, japo kutofanya hvyo kumemtesa yeye mwenyewe , nafkr ndo ilikuwa best solution , wakabiliane Kwa hoja whatever the cost , kuliko cheap solution ya kumziba midomo badae the whole universes kungeibuka riots .....!!

Jiwe alifanya mistake kuwaziba midomo watu , sa hv yanayotokea yawe ya kweli ama sio , lawama zinamuangukia yeye....!!! Na Hana nafasi ya kujibu tuhuma , pengine angeriluhusu haya akiwa hai angekuwa amejibu....
 
Sjui Kwa nini Mungu Hakumziba midomo shetani , japo kutofanya hvyo kumemtesa yeye mwenyewe, nafkr ndo ilikuwa best solution , wakabiliane Kwa hoja whatever the cost , kuliko cheap solution ya kumziba midomo badae the whole universes kungeibuka riots! Jiwe alifanya mistake kuwaziba midomo watu , sa hv yanayotokea yawe ya kweli ama sio , lawama zinamuangukia yeye!

Huyo jiwe anaziba watu midomo utadhani alituzaa au alituumba, au utadhani hii nchi aliitengeza yeye.

Ikiwa Aliyetupa kila kitu, MUNGU, ametoa uhuru kwa viumbe wake sembuse sisi wakoroma usiku?

Muhimu watu wasivunje sheria, na wakivunja sheria na hukumu zipo mahakamani huko, sio bangi za mtu ziamulie watu.
 
Nilisifia pakusifia, nilikosoa pakukosoa,
Hata shetani hakosi mazuri Mkuu

Mimi sio mnafiki nione kwa jicho moja, nina macho mawili naona wema na ubaya
Tetetete tulikuonya kwamba marehemu ni mpigaji sn ukatuona wapinzani sijui CHADEMA tuna tumwa na mabeberu, jiulize kwanini Ndugai na genge lake wamejiwekea kinga ya kutoshitakiwa? hawa watu ni waovu sn tena sana wanajua madudu yao.
 
Tetetete tulikuonya kwamba marehemu ni mpigaji sn ukatuona wapinzani sijui CHADEMA tuna tumwa na mabeberu, jiulize kwanini Ndugai na genge lake wamejiwekea kinga ya kutoshitakiwa? hawa watu ni waovu sn tena sana wanajua madudu yao.

:D :D :D :D

Mimi siwezi kuwa na chama kwani ukiwa na chama lazima uwe mnafiki. Kwani huko CHADEMA hakuna wahuni na wapigaji?

Mimi nilimkosoa sana Marehemu katika kipengele kimoja tuu hasa cha Haki na uhuru, huko kwingine niliona ni mambo ya kawaida.

Labda umeanza kusoma nyuzi zangu hivi karibuni, rejea miaka 2015 huko ndio utanijua vyema.
 
.
20210408_121604.jpg
 
:D :D :D :D

Mimi siwezi kuwa na chama kwani ukiwa na chama lazima uwe mnafiki. Kwani huko CHADEMA hakuna wahuni na wapigaji?

Mimi nilimkosoa sana Marehemu katika kipengele kimoja tuu hasa cha Haki na uhuru, huko kwingine niliona ni mambo ya kawaida

Labda umeanza kusoma nyuzi zangu hivi karibuni, rejea miaka 2015 huko ndio utanijua vyema
Mkuu ukiona watu wanasema ujue kuna tatizo, chukua mfano wa Ole Sabaya, why Ole Sabaya? hata CHADEMA wapigaji wapo sn tu lakini wakibainika wanafukuzwa.
 
Mkuu ukiona watu wanasema ujue kuna tatizo, chukua mfano wa Ole Sabaya, why Ole Sabaya? hata CHADEMA wapigaji wapo sn tu lakini wakibainika wanafukuzwa.

Huyo Ole asipojitathmini atajifunza kwa njia ngumu, Mark my word, na kama yupo humo asikie, asidhani hako kacheo kake ndio anaweza kufanya atakavyo
 
MTAWALA AZIBAYE MIDOMO WATU NI MBAYA KAMA SHETANI

Kwa Mkono wa Robert Heriel.

Mtu yeyote anayependa kuziba watu midomo wasimseme jua huyo ni kama shetani, hivyo ndivyo andiko hili ninavyoanza nalo.
Shetani ndio anapenda mambo ya sirini, kuficha ficha, kuziba watu midomo wasiseme mabaya yake. Kuzuia uhuru wa watu kwani katika uhuru shetani anajua ubaya wake utadhihirika.
Kwenye uhuru kuna ukweli, penye ukweli kuna uwazi, penye uwazi kuna haki, kwenye haki kuna amani, kwenye amani kuna furaha.

Mtawala yeyote hata afanye mema gani lakini kama ataminya Uhuru basi ameminya haki ya msingi ya mwanadamu, uhuru ndio maendeleo, ndio maana kila taifa kuna siku ya kusherekea uhuru wao kila mwaka. Uhuru ndio maendeleo. Sasa mtu anapoziba watu midomo ni kwamba hataki watu waongee pale anapokosea, ni kama shetani tuu.

Watu wa namna hii hutumia nguvu kubwa kwenye propaganda za kujisifia na kuponda wale wote wanamkosoa ikiwezekana kutaka kibali cha kuweza kuwaua hata kama sheria haziruhusu.
Kwa vile jamii yetu wengi wa watu ni wajinga wasio na akili ya kuchambua mambo ni rahisi kwa kiongozi wa namna hii kuchota akili zao.

Huwaga nasemaga Ujinga ni upofu, hivyo watawala wa namna hii hutumia ujinga wa watu wengi kuwalaghai kwa propaganda za hovyo ili aonekane mwema.

Hatukatai mtu kuwa mjinga hilo hatuwezi kukataa, hiyo ni haki ya mtu kuchagua ujinga au werevu, tunachokataa ni kuvunja sheria na haki za binadamu kwa kisingizio cha ujinga au werevu. Tunachopishana na watawala madikteta ni kuvunja haki za watu kwa kukandamiza uhuru wa watu hasa wale werevu watakaompinga kutokana na matendo yake maovu

Madikteta huwatumia zaidi watu wajinga na masikini katika kujizatiti kushika dola. Madikteta hawawezi kushikamana na watu werevu na matajiri kwani utawala wao utakuwa mashakani. Werevu na matajiri wanajua umuhimu wa uhuru katika maisha yao. Lakini masikini na wajinga wao hawana tofauti na wanyama, wao lolote kwao ni sawa ilimradi maisha. Ni kama kuku au mbwa wa kufuga, hata uwafunge bandani wao hawaoni shida ilimradi wajipatie chakula hata kama sio mlo kamili. Lakini Watu werevu na matajiri wanajua maisha ni zaidi ya chakula, maisha ni uhuru wa kuishi bila kuathiri wengine.

Ndio maana madikteta wote wawapo kwenye majukwaa hujifanya kuponda matajiri kwa kusema ni wezi na wanawadhulumu masikini, lengo lao ni kupata wafuasi kutoka watu masikini, na kwa vile masikini wengi wao ni wajinga hujikuta wakimpenda Dikteta zaidi kwani wanaona yupo upande wao ilhali uchumi wao bado unakuwa dhoofu.
Madikteta pia, huwaponda werevu na wasomi kama vile maprofesa, na watu wote wenye vipaji vya muhimu wenye kutetea haki. Dikteta asimamapo jukwaani ni kawaida kumdhalilisha Mwerevu ili yeye(dikteta) apate sifa kwa watu wajinga wasioweza kuchambua mambo. Hivyo sio ajabu ukashangaa wajinga wakishangilia pale mwerevu adhalilishwapo na dikteta.

Mjinga na masikini wanafanana sifa kwa sehemu kubwa na wote hufurahi waonapo mwerevu na tajiri apatwapo na madhila.

Mtawala anayeziba watu mdomo kamwe usimuamini hata kama utamkuta mbinguni, ni shetani mbaya anayejaribu kuficha maovu yake.

Hata hivyo jambo moja ni dhahiri nalo ni; ukiziba watu mdomo ukiwa uhai, basi watu watakusema ukiwa Mfu. Hivyo akili kumkichwa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa, Mwanjelwa, Mbeya mjini
tunashukuru kwa ujumbe mzuri, uovu siku zote ufunikwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom