Mtaturu na NEC wajumuishwe katika Kesi ya Msingi dhidi ya maamuzi ya Ndugai

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,874
Nilikuwepo mahakamani leo wakati Jaji Sirilius Matupa akitoa uwamuzi wake juu ya shauri la kupinga kuvuliwa Ubunge Mh.Tundu Lisu.

Nilivyomuelewa Jaji, tayari alikuwa anajua fika kuwa kitendo cha Spika kumvua ubunge Tundu Lissu kilikuwa batili.

Ndio maana hata kesi ya msingi kama ingeendelea Tundu Lissu angeshinda kesi asubuhi mapema na maamuzi ya Ndugai yangebatilishwa.

Ila Jaji alisema kuwa katika shauri hili, uchaguzi wa Mtaturu (kuchaguliwa Mtaturu) haukupingwa Mahakamani ila kulipingwa kiapo cha mtaturu (Mtaturu kuapishwa).Jaji akaendelea kusema kupinga kuapishwa sio kupinga mtu kuwa Mbunge ,kesi nyingi zinazofunguliwa huwa ni za kupinga uchaguzi (Mchakato wa uchaguzi) sio kuapishwa,hivyo mahakama haiwezi kupinga kiapo cha Mtaturu cha Ubunge sababu ni kuingilia muhimili ungine. Hivyo Mtaturu ataendelea kuwa Mbunge.

Kuja kwa kutengua maamuzi ya Spika Ndugai,kama kesi ya msingi itaendelea na mahakama ikatengua uwamuzi wa Ndugai ,hali itakuwaje?

Maana yake moja kwa moja ,Mh.Tundu Lissu atakuwa Mbunge wa Jimbo lake ,vipi Mh. Mtaturu? Je, Jimbo linaweza kuwa na Wabunge wawili?

Akasoma kifungu cha katiba kikisema ,Jimbo litakuwa na Mbunge mmoja tuu .Hivyo kutengua maamuzi ya Spika itakuwa uvunjivu wa katiba sababu jimbo la Mh.Tundu Lisu tayari kuna mbunge ambaye mchakato wa uchaguzi wake haujapingwa na mtu yeyote .

Ushauri wangu

Kwa namna kesi ilivyo hakuna haja ya kukata rufaa,jambo kubwa hapa ni kurudisha kesi mpya mahakama kuu ,ila kuwe na marekebisho kesi hiyo mpya ijumuishe wote , Ndugai na NEC kupitia AG kwa kuitisha uchaguzi jimbo lenye Mbunge na huyo Mtaturu pia kama mshtakiwa namba tatu kwa kushtaki mchakato wake mzima wa kuchaguliwa kwake kuwa Mbunge.

Kuwa alichaguliwa kinyume na sheria na sio kihalali (illegally ) sababu jimbo hilo lilikuwa na Mbunge ila yeye hakukataa kugombea, alikubali huku akijua jimbo hilo linamtu ambaye ni Mbunge halali wa Jimbo hilo Mh.Tundu Lisu.

Kufanya hivi ni kuitengenezea mahakama njia ya kutoingia katika mgogoro wa kikatiba , Mtaturu akijumuishwa ndio njia pekee ya mahakama kumgusa kwa kumtengua na Mtaturu akitenguliwa kuna kuwa na uhuru wa mahakama kutengua uwamuzi wa spika Ndugai ,sababu jimbo litakuwa wazi hivyo maamuzi ya Ndugai yakitenguliwa ubunge utarudi kwa Mh.Tundulisu katika jimbo ambalo litakuwa wazi.

Tofauti na sasa Mtaturu hajaguswa yaani hajashtakiwa kupinga mchakato wake batili wa uchaguzi .Hivyo mahakama imejikuta katika mgogoro mkubwa wa kikatiba.

Nashauri kesi ifunguliwe upya vizuri , Mtaturu ajumuishwe yeye na Spika na NEC (kupitia AG) ili kuipa mahakama uhuru wa kutengua maamuzi ya Spika Ndugai,bila kuingia mgogoro na katiba.

Pia rai yangu,watu tupinguze kulalamika kuwa mahakama inatuonea ,hivi tusipokimbilia au kuiamini mahakama tutakuwa wageni wa nani tena ? ,Kama tunajua hatuwezi kuingia barabarani sasa hivi basi tuendelee kuamini mahakama kama kimbilio letu la kila jambo, tupunguze kulalamika.Mahakama ndio pumzi tuliyobaki nayo sasa ,tusilazimishe kuikata wakati hatuna mbadala ungine.

Shukrani.

Abdul Nondo

abdulnondo10@gmail.com

0659366125.
 
Pia rai yangu,watu tupinguze kulalamika kuwa mahakama inatuonea ,hivi tusipokimbilia au kuiamini mahakama tutakuwa wageni wa nani tena ? ,Kama tunajua hatuwezi kuingia barabarani sasa hivi basi tuendelee kuamini mahakama kama kimbilio letu la kila jambo, tupunguze kulalamika.Mahakama ndio pumzi tuliyobaki nayo sasa ,tusilazimishe kuikata wakati hatuna mbadala ungine.
Ukiacha viroba unakua smart sana
 
Kwa mtazamo wangu jaji katepeta, haiwezekana swala la kumpinga spika lihusishwe Na tume moja kwa moja. Mahakama ingethibitisha maamuzi ya spika sio sahihi maana yake agizo la uchaguzi nalo Ni batili.bado kesi ya lissu iko sahihi hakuna haja ya kufungua nyingine.
 
Kesi imeishahukumiwa irudishwe ianze upya, inakubalika hii kweli kisheria?
Nilikuwepo mahakamani leo wakati Jaji Sirilius Matupa akitoa uwamuzi wake juu ya shauri la kupinga kuvuliwa Ubunge Mh.Tundu Lisu.

Nilivyomuelewa Jaji, tayari alikuwa anajua fika kuwa kitendo cha Spika kumvua ubunge Tundu Lissu kilikuwa batili.

Ndio maana hata kesi ya msingi kama ingeendelea Tundu Lissu angeshinda kesi asubuhi mapema na maamuzi ya Ndugai yangebatilishwa.

Ila Jaji alisema kuwa katika shauri hili, uchaguzi wa Mtaturu (kuchaguliwa Mtaturu) haukupingwa Mahakamani ila kulipingwa kiapo cha mtaturu (Mtaturu kuapishwa).Jaji akaendelea kusema kupinga kuapishwa sio kupinga mtu kuwa Mbunge ,kesi nyingi zinazofunguliwa huwa ni za kupinga uchaguzi (Mchakato wa uchaguzi) sio kuapishwa,hivyo mahakama haiwezi kupinga kiapo cha Mtaturu cha Ubunge sababu ni kuingilia muhimili ungine. Hivyo Mtaturu ataendelea kuwa Mbunge.

Kuja kwa kutengua maamuzi ya Spika Ndugai,kama kesi ya msingi itaendelea na mahakama ikatengua uwamuzi wa Ndugai ,hali itakuwaje?

Maana yake moja kwa moja ,Mh.Tundu Lissu atakuwa Mbunge wa Jimbo lake ,vipi Mh. Mtaturu? Je, Jimbo linaweza kuwa na Wabunge wawili?

Akasoma kifungu cha katiba kikisema ,Jimbo litakuwa na Mbunge mmoja tuu .Hivyo kutengua maamuzi ya Spika itakuwa uvunjivu wa katiba sababu jimbo la Mh.Tundu Lisu tayari kuna mbunge ambaye mchakato wa uchaguzi wake haujapingwa na mtu yeyote .

Ushauri wangu

Kwa namna kesi ilivyo hakuna haja ya kukata rufaa,jambo kubwa hapa ni kurudisha kesi mpya mahakama kuu ,ila kuwe na marekebisho kesi hiyo mpya ijumuishe wote , Ndugai na NEC kupitia AG kwa kuitisha uchaguzi jimbo lenye Mbunge na huyo Mtaturu pia kama mshtakiwa namba tatu kwa kushtaki mchakato wake mzima wa kuchaguliwa kwake kuwa Mbunge.

Kuwa alichaguliwa kinyume na sheria na sio kihalali (illegally ) sababu jimbo hilo lilikuwa na Mbunge ila yeye hakukataa kugombea, alikubali huku akijua jimbo hilo linamtu ambaye ni Mbunge halali wa Jimbo hilo Mh.Tundu Lisu.

Kufanya hivi ni kuitengenezea mahakama njia ya kutoingia katika mgogoro wa kikatiba , Mtaturu akijumuishwa ndio njia pekee ya mahakama kumgusa kwa kumtengua na Mtaturu akitenguliwa kuna kuwa na uhuru wa mahakama kutengua uwamuzi wa spika Ndugai ,sababu jimbo litakuwa wazi hivyo maamuzi ya Ndugai yakitenguliwa ubunge utarudi kwa Mh.Tundulisu katika jimbo ambalo litakuwa wazi.

Tofauti na sasa Mtaturu hajaguswa yaani hajashtakiwa kupinga mchakato wake batili wa uchaguzi .Hivyo mahakama imejikuta katika mgogoro mkubwa wa kikatiba.

Nashauri kesi ifunguliwe upya vizuri , Mtaturu ajumuishwe yeye na Spika na NEC (kupitia AG) ili kuipa mahakama uhuru wa kutengua maamuzi ya Spika Ndugai,bila kuingia mgogoro na katiba.

Pia rai yangu,watu tupinguze kulalamika kuwa mahakama inatuonea ,hivi tusipokimbilia au kuiamini mahakama tutakuwa wageni wa nani tena ? ,Kama tunajua hatuwezi kuingia barabarani sasa hivi basi tuendelee kuamini mahakama kama kimbilio letu la kila jambo, tupunguze kulalamika.Mahakama ndio pumzi tuliyobaki nayo sasa ,tusilazimishe kuikata wakati hatuna mbadala ungine.

Shukrani.

Abdul Nondo

abdulnondo10@gmail.com

0659366125.
 
Hata ukifungua kesi upya,yatakuja maamuzi mengine yatakayozua mjadala zaidi badala ya kumaliza mjadala uliopo.
....nimeona sipika anajigamba bungeni kabla ya uamuzi wa mahakama maana yake hukumu ilipangwa kabla na yeye alikuwepo....Kama jaji anaogopa kutoa maamuzi ya haki akihofia mgogoro wa kikatiba maana yake alieonewa achukue sheria mkononi au?....leo nimeamini mwafrica alitokana na nyani tena uyo nyani alikua mgonjwa wa akili..lisu kaumizwa mchana kweupe kapigania uhai wake kwa maumivu makali alafu binadamu mwenzake anashangilia kumpoka madaraka aisee..naamini hakuna atakae ishi milele wote tutazikwa udongoni na kuoza mali na madaraka havitakua na msaada tena...ndg tutendeane wema tujiwekee azina mbinguni
 
Nadhani maranyingine maamuzi ya mahakama yaheshimiwe tu maana siku zingine tukishinda tunashangilia,na majibu yakija kinyume tuwe wavumilivu tu,kuendelea kuitukana mahakama wakati siku ikitoa hukumu zinazokuwa upande wetu tunaisifia nakusema imetenda haki itakuwa ni ukinyonga.
 
Kuwa alichaguliwa kinyume na sheria na sio kihalali (illegally ) sababu jimbo hilo lilikuwa na Mbunge ila yeye hakukataa kugombea, alikubali huku akijua jimbo hilo linamtu ambaye ni Mbunge halali wa Jimbo hilo Mh.Tundu Lisu.
Hapa unataka kumuonea mbunge mteule kwa sababu alipata taarifa kutoka NEC Kuwa jimbo liko wazi .tafuta hoja nyengine
 
Ndugai na NEC kupitia AG kwa kuitisha uchaguzi jimbo lenye Mbunge na huyo Mtaturu pia kama mshtakiwa namba tatu kwa kushtaki mchakato wake mzima wa kuchaguliwa kwake kuwa Mbunge.
jimbo halikuwa na mbunge kwa sababu ameshavunja au kukosa sifa za kuwa mbunge kwa kutohudhuria ikao vitatu vya bunge bila kutoa taarifa yoyote,kukiuka sheria ya maadili kama katiba inavyosema
 
.lisu kaumizwa mchana kweupe kapigania uhai wake kwa maumivu makali alafu binadamu mwenzake anashangilia kumpoka madaraka aisee.
shida haiko kushambuliwa kweupe ,wala issue siyo kuonewa in such bali ni uzembe wa mheshimiwa mwenyewe kwa kutotoa taarifa ya maendeleo ya matibabu yake na sababu ya kutohudhuria vikao vya bunge.yamkini kwa makusudi,kudharau au kutokujua
 
Nilikuwepo mahakamani leo wakati Jaji Sirilius Matupa akitoa uwamuzi wake juu ya shauri la kupinga kuvuliwa Ubunge Mh.Tundu Lisu.

Nilivyomuelewa Jaji, tayari alikuwa anajua fika kuwa kitendo cha Spika kumvua ubunge Tundu Lissu kilikuwa batili.

Ndio maana hata kesi ya msingi kama ingeendelea Tundu Lissu angeshinda kesi asubuhi mapema na maamuzi ya Ndugai yangebatilishwa.

Ila Jaji alisema kuwa katika shauri hili, uchaguzi wa Mtaturu (kuchaguliwa Mtaturu) haukupingwa Mahakamani ila kulipingwa kiapo cha mtaturu (Mtaturu kuapishwa).Jaji akaendelea kusema kupinga kuapishwa sio kupinga mtu kuwa Mbunge ,kesi nyingi zinazofunguliwa huwa ni za kupinga uchaguzi (Mchakato wa uchaguzi) sio kuapishwa,hivyo mahakama haiwezi kupinga kiapo cha Mtaturu cha Ubunge sababu ni kuingilia muhimili ungine. Hivyo Mtaturu ataendelea kuwa Mbunge.

Kuja kwa kutengua maamuzi ya Spika Ndugai,kama kesi ya msingi itaendelea na mahakama ikatengua uwamuzi wa Ndugai ,hali itakuwaje?

Maana yake moja kwa moja ,Mh.Tundu Lissu atakuwa Mbunge wa Jimbo lake ,vipi Mh. Mtaturu? Je, Jimbo linaweza kuwa na Wabunge wawili?

Akasoma kifungu cha katiba kikisema ,Jimbo litakuwa na Mbunge mmoja tuu .Hivyo kutengua maamuzi ya Spika itakuwa uvunjivu wa katiba sababu jimbo la Mh.Tundu Lisu tayari kuna mbunge ambaye mchakato wa uchaguzi wake haujapingwa na mtu yeyote .

Ushauri wangu

Kwa namna kesi ilivyo hakuna haja ya kukata rufaa,jambo kubwa hapa ni kurudisha kesi mpya mahakama kuu ,ila kuwe na marekebisho kesi hiyo mpya ijumuishe wote , Ndugai na NEC kupitia AG kwa kuitisha uchaguzi jimbo lenye Mbunge na huyo Mtaturu pia kama mshtakiwa namba tatu kwa kushtaki mchakato wake mzima wa kuchaguliwa kwake kuwa Mbunge.

Kuwa alichaguliwa kinyume na sheria na sio kihalali (illegally ) sababu jimbo hilo lilikuwa na Mbunge ila yeye hakukataa kugombea, alikubali huku akijua jimbo hilo linamtu ambaye ni Mbunge halali wa Jimbo hilo Mh.Tundu Lisu.

Kufanya hivi ni kuitengenezea mahakama njia ya kutoingia katika mgogoro wa kikatiba , Mtaturu akijumuishwa ndio njia pekee ya mahakama kumgusa kwa kumtengua na Mtaturu akitenguliwa kuna kuwa na uhuru wa mahakama kutengua uwamuzi wa spika Ndugai ,sababu jimbo litakuwa wazi hivyo maamuzi ya Ndugai yakitenguliwa ubunge utarudi kwa Mh.Tundulisu katika jimbo ambalo litakuwa wazi.

Tofauti na sasa Mtaturu hajaguswa yaani hajashtakiwa kupinga mchakato wake batili wa uchaguzi .Hivyo mahakama imejikuta katika mgogoro mkubwa wa kikatiba.

Nashauri kesi ifunguliwe upya vizuri , Mtaturu ajumuishwe yeye na Spika na NEC (kupitia AG) ili kuipa mahakama uhuru wa kutengua maamuzi ya Spika Ndugai,bila kuingia mgogoro na katiba.

Pia rai yangu,watu tupinguze kulalamika kuwa mahakama inatuonea ,hivi tusipokimbilia au kuiamini mahakama tutakuwa wageni wa nani tena ? ,Kama tunajua hatuwezi kuingia barabarani sasa hivi basi tuendelee kuamini mahakama kama kimbilio letu la kila jambo, tupunguze kulalamika.Mahakama ndio pumzi tuliyobaki nayo sasa ,tusilazimishe kuikata wakati hatuna mbadala ungine.

Shukrani.

Abdul Nondo

abdulnondo10@gmail.com

0659366125.
Toto dogo PSPA si sheria,usifanye propaganda kwa usiyoyajua
 
Back
Top Bottom