Mtatiro: Hatua za Bunge, Lipumba na msimamo wangu! Na maajabu ya Bunge na serikali ya CCM

"Pambana na hali yako"

Ningependa kujua ni nani aliyesema hii kauli tata...

Yote kwa yote, hakuna cha kumshangaza mtu kwa kile kinachotokea cuf. Nadhani uko mbeleni kinaweza tokea hata kwa chadema. Watu wana "majina" makubwa na sauti kubwa kuliko chama....
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Nyakati za sasa inatakiwa kuwa very smart kwa wapinzani kuendelea kuoperate
Hapana mkuu ...upinzani una miaka 25 ya uhai lakini wanafanya makosa yale yale ....wengine tulijiaminisha Chadema ni tofauti lakini nao wanapita kule kule ....hii CUF inakufa sababu ya Chadema na CCM ....Maalim na kundi lake wanaungwa mkono na Chadema while Lipumba yupo na CCM ....ushawishi wa hawa wana CUF nje ya CUF hautakuwa na nguvu ile ile ....hesabu za hovyo hovyo tu ....subiri uone hii vita inapoenda ...
 
Kwa nini serikali ya ccm inaonyesha dhahiri kabisa kuwa inayatafuta machafuko nchi hii? Maamuzi ya Ndugai yanaonyesha yana baraka za juu na vyombo vyote vinavyosimamia usalama. Maana kama vingekuwa huru vingeshauri kuwa ujinga huu utatupeleka pabaya.
Huko MKIRU mumeona kaeneo kadogo kalivyo tusumbua, jee haya ya CUF wale wanachama kindakindaki wakichoka hii tabia ya kuwaonea pande zote za nchi tutaweza kweli kuwadhibiti wakianza kama MKIRU? Tujichunge, na hili hata wale wana ccm wapenda haki walipigie kelele kwani likilipuka halitajua wewe ni nani au yule ni nani
 
Kwani jamani, mmi sielewi, Taasisi ya Usalama wa Taifa kazi yake imejikita zaidi kudil nakuvidhoofisha vyama vya siasa ambavyo vinastawi na kukuza demokrasia Nchini au kazi ya Taasisi hii nikudil na usalama wa Rais kwa mlengo chanya!?
Mara nyingi Taasisi hii hulaumiwa mno, kwa mjibu wa katiba ya Nchin, inajitadhimini vipi ktk viwango vya ubora!?
 
Ni mpumbavu pekee anayeweza kushangilia ujinga huu!
Na ni Kiongozi asie makini pekee ndiye anayeweza kubariki unajisi huu wa haki!
Duniani kote na sehemu zote zilizopoteza Amani, watu wake hasa viongozi walitenda matendo haya.
Natabiri Amani ya Nchi hii itavurugika si muda mrefu. Ni vigumu kupora haki za watu kila kukicha kisha mtarajie utulivu.
Na kwa kuwa tumejawa unafiki, sitashangaa wapinzani wakipewa lawama baada ya Amani kutoweka!
Ifikie wakati wenye magonjwa mazito wazuie kuendelea na nyadhifa nyeti kwa usalama wa Nchi hii!
Uwezo wao wa kufanya maamuzi sahihi umeyumba!
 
Wakuu mnakumbuka mahakama ilichukua juma moja kuondoa utata wa amri ya TRUMP Kwamba ni halali au sio halali. Jibu likawa ni HALALI na watu wakaendelea kuingia USA.

Sasa huku TZ, kuna utata, na kesi ipo mahakamani: LIPUMBA ni mwanachama/mwenyekiti halali au sio halali?

Sasa umekatika mwaka na nionavyo mimi uamuzi utatolewa 2021. Sababu ni nini?
je, athari za kuchelewesha kuondolewa utata ni zipi? je, mahakama zetu zipo huru kweli?
Amri kutoka juu marekani amri inatoka chini kwenda juu na ndio democracy
 
HATUA ZA BUNGE, LIPUMBA NA MSIMAMO WANGU!

[HASHTAG]#Mtatiro[/HASHTAG] J,
[HASHTAG]#NewYork[/HASHTAG].

1. Juzi Jumatatu Lipumba na Sakaya walimuandikia Spika wa Bunge kumjulisha kuwa "Baraza Kuu la CUF" (feki) limewafukuza uanachama Wabunge 8 wa Viti Maalum wa CUF. (Spika alishaandikiwa na Katibu Mkuu kumjulisha kuwa Baraza Kuu halali la CUF ni lile lililochaguliwa mwaka 2014 na muda wake utaisha mwaka 2019 na Baraza hilo halali ndilo lililomfukuza Lipumba).

2. Jana, Jumanne, Ofisi ya Bunge ilitoa taarifa kwa umma kuujulisha kuwa imepokea maelekezo kutoka kwa Sakaya na Lipumba kuwa wabunge hao 8 si wanachama na Ofisi hiyo ikaeleza kuwa bado inatafakari hatua za mwisho za kuchukua.

3. Leo Jumatano, Ofisi ya Bunge imetangaza uamuzi wake, kwamba inakubaliana na maelekezo ya Lipumba na Sakaya na kuwa imewavua wabunge hao 8 ubunge wao wa Viti Maalum, na kuwa imeiandikia Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuijulisha kujaza nafasi hizo zilizo wazi.

_________________________________________
Nataka kuwaeleza wanachama na watanzania wote, kwamba viongozi wa chama wanakutana kuendelea kuchukua hatua.

Tunajua kuwa Vyombo vya Serikali hivi sasa vinafanya kazi kubwa kuhakikisha kuwa aidha CUF inamkubali "MSALITI" Lipumba kuwa Mwenyekiti wake, au CUF isambaratike. Na suluhisho la hali hii haliwezi kuwa kukaa chini na MSALITI.

Mnapopambana na WASALITI WALIOKUBUHU na wako ndani ya nyumba yenu, vita yake siyo ndogo. Lakini mimi binafsi ni muumini mkubwa wa HAKI na UKWELI. Naamini kuwa CUF itavuka misukosuko hii.

Kwa jicho moja wapo watu wanachekelea na kudhani kadhia hii ni ya CUF tu, mimi natizama hali hii kama Mapambano ya Dola ya kuhakikisha vyama mbadala vinaongozwa na wasaliti ili Dola iendelee kuwatumia kuzamisha demokrasia na ushindani wa kisiasa nchini.

Dola ikifanikiwa kuisambaratisha CUF, vyama vingine vya upinzani havitakuwa salama, taasisi zingine za kiraia hazitakuwa salama pia. Anayeyatizama mapambano haya kama vita ya ndani ya CUF hajaisoma dunia - haya ni mapambano makubwa, dhidi ya demokrasia ya Tanzania.

Mimi ni mwanademokrasia imara na sitayumbishwa na WASALITI. Kumkubali Lipumba na genge lake itakuwa na maana ya kuiua CUF moja kwa moja Tanzania Bara, maana alipojaribu kukimbia mwaka 2015, ndipo CUF iliibuka na kuwa chama imara mara 10 Tanzania bara. Na kurudishwa kwake kwa nguvu kunakofanywa na dola ni mkakati wa kuimaliza CUF na suluhisho lake haliwezi kuwa CUF kumtambua Lipumba.

Hata DOLA ikifanya nini, LIPUMBA ameshadharaulika na hawezi kuisaidia tena dola hii yenye upofu. Katibu Mkuu wa Chama, Mhe. Seif Sharif Hamad na viongozi wa chama wanaendelea na hatua mbalimbali muhimu na mtajulishwa

Vita imeshapanuka, sasa ni LIPUMBA, OFISI YA MSAJILI WA VYAMA, RITA, BUNGE, NEC, IKULU, USALAMA WA TAIFA na CCM. Kundi lote hilo linaamini kuwa bila kumrudisha Lipumba halitaweza kuidhibiti CUF. Sisi viongozi tuko imara sana na tunaamini kuwa HAKI huweza kucheleweshwa tu!

We shall OVERCOME this! More Stable! And more Vibrant!

[HASHTAG]#JSM[/HASHTAG], 26 Julai 2017.
Hakika huku kutumika kwa lipumba na ccm na serikali yake iko siku italigharimu Taifa hili na mwisho wake unakuja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maoni yangu hayahusu Zitto Kabwe, yanahusu consistency. Zitto Kabwe alifukuzwa uanachama wa CHADEMA lakini hakuondolewa bungeni na spika. Hii inaleta picha gani?? Nilidhani Msajii wa vyama ndie mjuzi wa Katiba za vyama na ndiye angemtaarifu Spika kuhusu kuvuliwa uanachama wa wabunge husika. Na hapo hapo kumpelekea majina ya wabunge watakaochukua nafasi za hawa wanaoondolewa.

Huenda sijaelewa vizuri na ninadhani nitaeleweshwa hapa.
 
Mwisho wa haya ni timu ya Maalim na Mtatiro kwenda Chadema ....huu mgogoro unakuzwa kupitia CCM na Chadema ....CUF inasambaratika ....Mtatiro anajipa moyo lakini hii ngoma wameshapigwa ....
Hakika. Cuf wanaelekea shimoni. Kwani mwisho wa kadhia hii ni Lipumba kubaki na cuf isiyo na nguvu kwani Zanzibar hawamtaki. Na maalim baada ya kuaibishwa na Lipumba huku akishikwa mkono na cdm kuelekea shimoni atawapigia debe cdm Zanzibar na yeye kubaki kuwa kibaraka wa cdm na huo ndio utakuwa mwisho wa cuf

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni mpumbavu pekee anayeweza kushangilia ujinga huu!
Na ni Kiongozi asie makini pekee ndiye anayeweza kubariki unajisi huu wa haki!
Duniani kote na sehemu zote zilizopoteza Amani, watu wake hasa viongozi walitenda matendo haya.
Natabiri Amani ya Nchi hii itavurugika si muda mrefu. Ni vigumu kupora haki za watu kila kukicha kisha mtarajie utulivu.
Na kwa kuwa tumejawa unafiki, sitashangaa wapinzani wakipewa lawama baada ya Amani kutoweka!
Ifikie wakati wenye magonjwa mazito wazuie kuendelea na nyadhifa nyeti kwa usalama wa Nchi hii!
Uwezo wao wa kufanya maamuzi sahihi umeyumba!

Tunakoelekea ni kubaya sana ninashindwa kuelewa kwa nini watanzania hawawezi kusoma nyakati, sasa hivi chuki imekithiri watu wamejaa ushabiki wa vyama huku hawana mbele wala nyuma tunawaona huku mitaani wanatembea na viraka huku kutwa ushabiki wa vyama yetu macho
 
Back
Top Bottom