assadsyria3
JF-Expert Member
- Apr 9, 2013
- 6,904
- 4,050
Naibu Katibu Mkuu wa CUF Tanzania Bara, Julius Mtatiro ameonya harakati za vyama vya upinzani kuelekea uchaguzi ujao.
Waraka wa Mtatiro ulionaswa na Habarimpya.com unalenga kuvionya vyama ya upinzani hususan CUF na CHADEMA kutokana na mkakati aliouita kuwa ni feki na ambao Chama Cha Mapinduzi CCM wanauchekelea.
Katika waraka huo ambao Mtatiro alielezea kuwa unalengo la kuidhoofisha CUF kutokana na jitihada za CHADEMA kukishambulia Chama hicho kila wakati, badala ya kuunganisha nguvu za upinzani kwa lengo la kuing'oa CCM madarakani.
"CHADEMA wanapoteza muda kuitukana CUF ambayo haihusiki hata kidogo na umasikini ulioasisiwa na CCM kwa nusu karne,kitendo cha Wenje kuihusisha CUF na siasa za ushoga ni cha kipuuzi na cha kitoto mno. Ezekiel Wenje na CHADEMA , wala hamtaishia hapo, mtaanza kutukanana ninyi kwa nyinyi"alisema Mtatiro katika waraka wake.
"Hatuwezi kuendelea kuwa na Bunge na Wabunge wanaotumia vibaya nafasi tulizowapa, na maposho yanayotokana na jasho letu kwa kuanza kufanya mambo yasiyo na maana, mtu unapewa fulsa ya kusoma maoni ya kambi rasmi ya upinzani, badala yake unaanza kurusha vijembe na matusi, Watanzania wanataka kuona kambi rasmi inayojitambua na yenye hadhi ya kutoa hoja zenye mashiko kuliko hizi siasa za upinzani kutukana mpinzani mwenzie tena mahali rasmi kama Bungeni,tunahitaji Kambi rasmi inayojiheshimu na isiyofanya siasa za kihuni
Waraka wa Mtatiro ulionaswa na Habarimpya.com unalenga kuvionya vyama ya upinzani hususan CUF na CHADEMA kutokana na mkakati aliouita kuwa ni feki na ambao Chama Cha Mapinduzi CCM wanauchekelea.
Katika waraka huo ambao Mtatiro alielezea kuwa unalengo la kuidhoofisha CUF kutokana na jitihada za CHADEMA kukishambulia Chama hicho kila wakati, badala ya kuunganisha nguvu za upinzani kwa lengo la kuing'oa CCM madarakani.
"CHADEMA wanapoteza muda kuitukana CUF ambayo haihusiki hata kidogo na umasikini ulioasisiwa na CCM kwa nusu karne,kitendo cha Wenje kuihusisha CUF na siasa za ushoga ni cha kipuuzi na cha kitoto mno. Ezekiel Wenje na CHADEMA , wala hamtaishia hapo, mtaanza kutukanana ninyi kwa nyinyi"alisema Mtatiro katika waraka wake.
"Hatuwezi kuendelea kuwa na Bunge na Wabunge wanaotumia vibaya nafasi tulizowapa, na maposho yanayotokana na jasho letu kwa kuanza kufanya mambo yasiyo na maana, mtu unapewa fulsa ya kusoma maoni ya kambi rasmi ya upinzani, badala yake unaanza kurusha vijembe na matusi, Watanzania wanataka kuona kambi rasmi inayojitambua na yenye hadhi ya kutoa hoja zenye mashiko kuliko hizi siasa za upinzani kutukana mpinzani mwenzie tena mahali rasmi kama Bungeni,tunahitaji Kambi rasmi inayojiheshimu na isiyofanya siasa za kihuni