SoC01 Mtanzania yeyote, hata asiye na Elimu ni muhimu ajifunze lugha ya Kiingereza

Stories of Change - 2021 Competition

hustler Tz

Member
Mar 16, 2018
8
21
Habari zenu wanajukwaa la Story of change.
Katika uzi huu nataka kuelezea ulazima wa kujifunza lugha ya kiingereza kwa mtanzania hata asie na elimu kubwa. Hili suala huwa haliongelewi kabisa na kumekuwa na upotoshaji mkubwa sana kuhusu lugha ya kiingereza.

JE, HUO UPOTOSHAJI UPOJE?

Hapa nchini Tanzania, hasa miaka ya hivi karibuni kumekuwa na upotoshaji mkubwa kuhusu lugha ya kiingereza. Hasa viongozi wakubwa serikalini ndio wamekuwa wahusika wa hili. Watanzania wameaminishwa kuwa lugha ya kiingereza ni ukoloni na kujifunza lugha hiyo si uzalendo na hata kuna kiongozi mmoja aliwahi kusema kuwa "hata mwanafunzi akimaliza form four na hajui kiingereza ni sawa kabisa kwani hatukwenda kumfundisha kiingereza bali tumeenda kumpa elimu" . Sasa swali ni kwamba, elimu gani hiyo aliopata wakati lugha ya kufundishia haijui??

Lugha ya kiinereza kwa sasa haihusiani tena na ukoloni bali ni njia kuu ya kuwaunganisha watu duniani kote. Lugha ya kiingereza inatumika katika biashara na kijamii pia. Mitandao karibia yote ya kijamii inatumia lugha ya kiingereza.

KWANINI KIINGEREZA SI UKOLONI KWASASA?

Kwa karne ya sasa ukisema kuwa kujifunza kiingereza ni ukoloni basi wewe utakuwa hujui hata dunia inaendaje kwasasa. Lugha ya kiingereza ndio Lugha kubwa na iliosambaa zaidi duniani.

Nchi kubwa na zenye ushawishi duniani kama Marekani, Uingereza, Canada, Australia na Afrika kusini zinatumia lugha ya kiingereza. Pia nchi nyingi za Afrika zinatumia lugha ya kiingereza.

Lugha ya kiingereza si ukoloni bali ni nafasi ya kuiunganisha dunia kwa lugha moja.

JE, TOFAUTI YA MTANZANIA ANAEJUA KIINGEREZA NA ASIEJUA KIINGEREZA NI IPI?

Mtanzania anaejua kiingereza anakuwa na upeo mkubwa wa kujua mambo mengi duniani ukilinganisha na yule asiejua. Hapa haijalishi elimu yao.

Mtanzania anaejua kiingereza anakuwa na akili iliyopevuka katika kuchambua mambo mengi zaidi. Mtu asiejua kiingereza hataweza kamwe kuendana na kasi ya dunia kwa sasa (Teknolojia).

USHAURI KWA SERIKALI

Serikali inatakiwa kuanzisha program mbalimbali za kuhamasisha watu kujifunza kiingereza ili kuwasaidia kuendana na kasi ya dunia ya kimaendeleo na teknolojia.

Kuna mambo mengi sana ya muhimu ya kujifunza kwenye mitandao lakini kwakua mengi yameandikwa kwa kiingereza na watu wengi hawajui kiingereza basi watu wengi huishia kufanya mambo yasiyo na manufaa yoyote.

Chaguo ni kujifunza kiingereza au kukubali kuishi katika zama za mawe ndani ya karne ya 21.

Nawasilisha.

images (16).jpeg
 
Exception lazima izingatiwe,huwezi jua huyu exception mmoja atakuja kufanya mapinduzi gani kwenye tasnia husika.

Kuweka mfumo ambao utawasapoti exception ni muhimu,muhimu kuweko na mazingira ambayo huo uchache wao hautaleta hasara katika mfumo huo.

Yaani mtu akiamua kurudia mtihani basi alipie kama ilivyo sasa na kama hajaamua iwe kataka yeye kutokurudia.

Na yapo mambo ambayo wafanyaji ni wachache lakini bado yametizamwa kwa upana wake.

Mfano ipo mifumo maalumu ya kuwafundisha viziwi japokuwa ni wachache lakini wamejaliwa.

Ipo mifumo ya kuwafundisha kusoma na kuandika watu ambao ni vipofu japokuwa ni wachache ukilinganisha na watu wazima wa viungo hivyo.

Kwa mantiki hiyo waendelee kuweka mazingira rafiki ya kuwaruhusu waliofeli kurudia mtihani kama vile ilivyokuwa sup ya chuo tu.

Maamuzi ya namna hii ndiyo yaliyotufikisha hapa,tulipo leo kama nchi,vilaza every where.Hatuwezi ku-sacrife well being ya a whole narion kwa sababu ya a few individuals.Naamini decision ya kuruhusu watu wa kufeli feli kurudia mitihani na hatimaye kuingia kwenye system yetu ya utumishi wa umma ulichukuliwa kwa nia ovu.
 
Maamuzi ya namna hii ndiyo yaliyotufikisha hapa,tulipo leo kama nchi,vilaza every where.Hatuwezi ku-sacrife well being ya a whole narion kwa sababu ya a few individuals.Naamini decision ya kuruhusu watu wa kufeli feli kurudia mitihani na hatimaye kuingia kwenye system yetu ya utumishi wa umma ulichukuliwa kwa nia ovu.
Mfumo wa kupata sup na ukarudia mtihani chuo haupo katika nchi ambazo zimeendelea kielimu ?
 
Habari zenu wanajukwaa la Story of change.
Katika uzi huu nataka kuelezea ulazima wa kujifunza lugha ya kiingereza kwa mtanzania hata asie na elimu kubwa. Hili suala huwa haliongelewi kabisa na kumekuwa na upotoshaji mkubwa sana kuhusu lugha ya kiingereza.

JE, HUO UPOTOSHAJI UPOJE?

Hapa nchini Tanzania, hasa miaka ya hivi karibuni kumekuwa na upotoshaji mkubwa kuhusu lugha ya kiingereza. Hasa viongozi wakubwa serikalini ndio wamekuwa wahusika wa hili. Watanzania wameaminishwa kuwa lugha ya kiingereza ni ukoloni na kujifunza lugha hiyo si uzalendo na hata kuna kiongozi mmoja aliwahi kusema kuwa "hata mwanafunzi akimaliza form four na hajui kiingereza ni sawa kabisa kwani hatukwenda kumfundisha kiingereza bali tumeenda kumpa elimu" . Sasa swali ni kwamba, elimu gani hiyo aliopata wakati lugha ya kufundishia haijui??

Lugha ya kiinereza kwa sasa haihusiani tena na ukoloni bali ni njia kuu ya kuwaunganisha watu duniani kote. Lugha ya kiingereza inatumika katika biashara na kijamii pia. Mitandao karibia yote ya kijamii inatumia lugha ya kiingereza.

KWANINI KIINGEREZA SI UKOLONI KWASASA?

Kwa karne ya sasa ukisema kuwa kujifunza kiingereza ni ukoloni basi wewe utakuwa hujui hata dunia inaendaje kwasasa. Lugha ya kiingereza ndio Lugha kubwa na iliosambaa zaidi duniani.

Nchi kubwa na zenye ushawishi duniani kama Marekani, Uingereza, Canada, Australia na Afrika kusini zinatumia lugha ya kiingereza. Pia nchi nyingi za Afrika zinatumia lugha ya kiingereza.

Lugha ya kiingereza si ukoloni bali ni nafasi ya kuiunganisha dunia kwa lugha moja.

JE, TOFAUTI YA MTANZANIA ANAEJUA KIINGEREZA NA ASIEJUA KIINGEREZA NI IPI?

Mtanzania anaejua kiingereza anakuwa na upeo mkubwa wa kujua mambo mengi duniani ukilinganisha na yule asiejua. Hapa haijalishi elimu yao.

Mtanzania anaejua kiingereza anakuwa na akili iliyopevuka katika kuchambua mambo mengi zaidi. Mtu asiejua kiingereza hataweza kamwe kuendana na kasi ya dunia kwa sasa (Teknolojia).

USHAURI KWA SERIKALI

Serikali inatakiwa kuanzisha program mbalimbali za kuhamasisha watu kujifunza kiingereza ili kuwasaidia kuendana na kasi ya dunia ya kimaendeleo na teknolojia.

Kuna mambo mengi sana ya muhimu ya kujifunza kwenye mitandao lakini kwakua mengi yameandikwa kwa kiingereza na watu wengi hawajui kiingereza basi watu wengi huishia kufanya mambo yasiyo na manufaa yoyote.

Chaguo ni kujifunza kiingereza au kukubali kuishi katika zama za mawe ndani ya karne ya 21.

Nawasilisha.

View attachment 1856433
Hata hivyo Kingereza ndio lugha rasmi ya kwanza katka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo kuna kila namna na haja ya kuijua.😎
 
Sisi ni wajinga mpaka inatia kichefuchefu. Basi tu-assume watanzania wote tunajua kiingereza au lugha za kigeni kwa ufasaha sawia Waingereza/ wageni , So what? Wote tukafanye kazi za kimataifa? Akili za kitumwa hizi.

Tuwezeke katika elimu ili kupata maarifa ya kutosha katika lugha tunayoimudu kwa ufasaha. Tukishakuwa na maarifa, washika dau watakuja na mitaji yao ili tufanye biashara. Hakuna mshika dau atakayekuja kwako et kisa lugha yako bali atakuja kwa sababu ya maarifa uliyonayo.

Kuna msemo unasema "knowledge is power" ukimaanisha kuwa ukiwa na maarifa unakuwa na nguvu na sio kwamba ukijua kiingereza au lugha flani ya kigeni ndio unakuwa na nguvu.
 
Sisi ni wajinga mpaka inatia kichefuchefu. Basi tu-assume watanzania wote tunajua kiingereza au lugha za kigeni kwa ufasaha sawia Waingereza/ wageni , So what? Wote tukafanye kazi za kimataifa? Akili za kitumwa hizi.

Tuwezeke katika elimu ili kupata maarifa ya kutosha katika lugha tunayoimudu kwa ufasaha. Tukishakuwa na maarifa, washika dau watakuja na mitaji yao ili tufanye biashara. Hakuna mshika dau atakayekuja kwako et kisa lugha yako bali atakuja kwa sababu ya maarifa uliyonayo.

Kuna msemo unasema "knowledge is power" ukimaanisha kuwa ukiwa na maarifa unakuwa na nguvu na sio kwamba ukijua kiingereza au lugha flani ya kigeni ndio unakuwa na nguvu.
Rejea chapisho langu, linaloitwa 'haja ya kutumia lugha ya kiswahili katika kujifunzia na kufundishia" nadhani majibu sahihi utayapata ambayo yameenda sambamba na tafiti zilizofanywa na wataalamu. Lkn ngoja nimuulize muandishi,je china, urusi,Korea,ujerumani,japani na nchi nyingi zilzoendelea wanatumia kingereza kufundishia wanafunzi wao?? Kama jibu ni ndiyo basi kuna haja ya kutumia kiingereza
 
Rejea chapisho langu, linaloitwa 'haja ya kutumia lugha ya kiswahili katika kujifunzia na kufundishia" nadhani majibu sahihi utayapata ambayo yameenda sambamba na tafiti zilizofanywa na wataalamu. Lkn ngoja nimuulize muandishi,je china, urusi,Korea,ujerumani,japani na nchi nyingi zilzoendelea wanatumia kingereza kufundishia wanafunzi wao?? Kama jibu ni ndiyo basi kuna haja ya kutumia kiingereza

Me mwenyew mwenyew nataka nijui kiingereza
 
Niki kosa kasichana kakizungu kisa hiyo ngeri ya genge, mtoto alizimika na mimi tatizo ikawa ni lugha gongana
 
Back
Top Bottom