JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF), limesema limepata taarifa zinazoonyesha kuwa, Jeshi la Polisi Mkoani Iringa, lina mpango maalum wa kuwashughulikia baadhi ya waandishi wa habari mkoani Iringa.
Taarifa hiyo ilitolewa jana na Katibu wa Jukwaa hilo, Neville Meena katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.
Jukwaa la Wahariri Tanzania, limepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, mkoani Iringa, Daudi Mwangosi.
Mwangosi ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari, Mkoa wa Iringa, aliuawa akiwa kazini juzi wakati polisi walipokuwa wakiwadhibiti wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
source: Mtanzania la leo
Taarifa hiyo ilitolewa jana na Katibu wa Jukwaa hilo, Neville Meena katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.
Jukwaa la Wahariri Tanzania, limepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, mkoani Iringa, Daudi Mwangosi.
Mwangosi ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari, Mkoa wa Iringa, aliuawa akiwa kazini juzi wakati polisi walipokuwa wakiwadhibiti wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
source: Mtanzania la leo