Mtanzania apata ajali Michigan, Mahututi..

Status
Not open for further replies.

Ab-Titchaz

JF-Expert Member
Jan 30, 2008
14,631
4,225
Kwa mujibu wa Chinga Networks hapa Detroit tumepata ujumbe huu:


"Wanajumuiya,
Mmoja wetu amepata ajali mbaya ya gari na yuko kwenye coma
University Of Michigan Hospital.Habari zaidi tutaleta kadri tunapopata.
Sala zitasaidia m'da huu"


Kijana wa Kitanzania Bw. Ndalima Nzaro yuko mahututi kwenye hospitali ya Chuo Kikuu cha Michigan Ann Arbor, nje kidogo ya Jiji la Detroit nchini Marekani baada ya ajali iliyosababisha na kijana wa miaka 15 aliyeiba gari kugonga gari la Ndalima lililokuwa limesimama kwenye taa za kuongozea magari likisubiri rangi ya kijani.



ndalima.jpg


Kijana huyo aliyegonga gari alikuwa anafukuzwa na Polisi.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa mji mdogo wa Westland kijana huyo aliyeiba gari na ambaye hakuna leseni ya kuendesha gari alikuwa anaendesha gari kwa kasi zaidi ya maili 100 kwa saa na aliyagonga magari ubavuni yaliyokuwa yamesimama hapo kwenye taa za kuongezea magari kwenye barabara ya Merriman.

"Wale madereva waliokuwa wanasubiri rangi ya kijani kuwaruhusu hawakuwa na jinsi yeyote ya kukwepa ajali hiyo" alisema Chifu Jim Ridener. Bw. Ndalima aliyekuwa anaendesha gari ndogo aina ya Honda Accord alitibiwa kwa dharura kwenye hospitali ya Garden City lakini kutokana na majeraha yake aliitiwa Helikopta ya Hospitali ambayo ilimchukua na kumkimbiza kwenye hospitali ya Chuo Kikuu cha Michigan mjini Ann Arbor.

Hospitali hiyo ni mojawapo ya hospitali zenye uzoefu mkubwa katika kuhudumia dharura za ajali katika eneo hili la Michigan.

Mtoto huyo wa miaka 15 alikuwa anaendesha gari aina ya Mercedes Benz S55MG ambalo ni la rafiki ya kiume wa mama yake. Kutokana na kijana huyo kuwa chini ya umri jina lake halitajwi kwenye vyombo vya habari.

Hata hivyo kijana huyo yuko mikononi mwa Polisi wakati uchunguzi ukiendelea na mashtaka dhidi yake yatategemea hali ya Ndalima inaendeleaje.

Habari ambazo tunazipata sasa hivi, hali ya mgonjwa siyo nzuri.

Tutawaletea habari zaidi kwa kadiri tunavyozipata.
 
Kwa mujibu wa Chinga Networks hapa Detroit tumepata ujumbe huu:


"Wanajumuiya,
Mmoja wetu amepata ajali mbaya ya gari na yuko kwenye coma
University Of Michigan Hospital.Habari zaidi tutaleta kadri tunapopata.
Sala zitasaidia m'da huu"

Tupe jina basi walau, ama hata hilo mnaficha identity yake, Mungu amsaidie mwenzetu apate nafuu...
 
Last edited:
Tupe jina bas walau ama hata hilo manaficha identity yake, Mungu amsaidie mwenzetu apete nafuu...


Ushirombo,

Mimi ndo napata hii nyuzi na bado nacheza na simu.Subiri kidogo
ni-confirm afu nitawajulisheni.Ni kitu serious as we speak so be patient.
 
Kwa mujibu wa Chinga Networks hapa Detroit tumepata ujumbe huu:


"Wanajumuiya,
Mmoja wetu amepata ajali mbaya ya gari na yuko kwenye coma
University Of Michigan Hospital.Habari zaidi tutaleta kadri tunapopata.
Sala zitasaidia m'da huu"

Mungu, Muumbaji wetu amponye.
 
Ushirombo,

Mimi ndo napata hii nyuzi na bado nacheza na simu.Subiri kidogo
ni-confirm afu nitawajulisheni.Ni kitu serious as we speak so be patient.

Mungu ampe nafuu,

ila wewe ndio ulitakiwa kuwa patient kabla ya kutujulisha ulitakiwa u confirm kwanza ili ulete habari kamili.

Tunamuombea mwenzetu mungu ampe nafuu.
 
Mungu ampe nafuu,

ila wewe ndio ulitakiwa kuwa patient kabla ya kutujulisha ulitakiwa u confirm kwanza ili ulete habari kamili.

Tunamuombea mwenzetu mungu ampe nafuu.

Mkuu hotsfede,

I hate to be the bearer of bad messages lakini nd'o hivyo tena.

The reason nilisita ni kwa sababu mshkaji alikua anatembelea pabaya and even as we speak amepelekwa OR kujaribu kuzuiya bleeding tumboni.

OK here we go.....Kwa jina ni Ndalima Nzaro na ajali imetokea usiku wa jana na kama sijakosea ili-involve gari la mamwera waliokua wanafukuza gari lengine.

After ashagongwa ilibidi wale mwera waite helicopter iliofanya evac mpaka University of Michigan ambapo iligunduliwa kua ile traumatic brain injury ili-result in inter-cranial bleeding.Kwa hivyo kuna
kazi ya kujaribu kuzuia bleeding in the brain na ile ya GI tract.

Meanwhile the brother is on a vent na tunaomba sala za kila namna so that we can be together again in fullness of health.

Naelekea hospitali kupata updates za karibu na details from the medical staff if possible.

Asanteni.
 
Tunamuombea uponaji wa haraka. Kutokana na seriousness ya alivyoumia na delicatness ya hali yake, nawaomba wana JF wenzangu at the moment tuchangie kuhusu sala na prayers za survival yake tusiingize mambo mengine yoyote ya binafsi kumhusu Ndalima bali tuendeleze maombi huku tukipokea feedback. Natanguliza shukrani.
 
Pole kwa Bw. Ndalima na vile vile pole kwa familia nzima ya Nzaro. Sala zetu ziko na nyinyi katika hichi kipindi kigumu cha kuuguliwa.
 
Namuomba Mungu asikilize sala zetu ili mwenzetu apate nafuu haraka na kurudia uzima wake. Familia ya Ndalima Nzaro poleni sana kwa haya matatizo yaliyowakuta.
 
Pole sana Ndalima Nzaro na familia yako... Mwenyezi Mungu akuponyeshe na urejee katika afya yako mapema.

Invisible
 
Sala nyingi ingawa nzuri lakini wengine tunaamini "God Help those who help themselves"

Kuna mipango gani ya kumsaidia yeye na wa karibu yake? Kuna uwepo wa jumuiya huko? Emergencies kama hizi zinapewa umuhimu wa kumtibu mtu regardless halafu maswali mengine baadaye, kuna watu wako one step ahead of the game wanaojiuliza maswali haya? Mambo ya insurance yakoje? Gharama za kumhudumia ndogo ndogo kama zipo zinachukuliwa na nani na kivipi? Wale watu wa kuwafuatilia madaktari kwa karibu wapo? Isije kuonekana huyu muhamiaji hana nyimbo na care yake ikawa ya kiserikali serikali tu.

Mimi hiyo ndiyo sala yangu.
 
Sala nyingi ingawa nzuri lakini wengine tunaamini "God Help those who help themselves"

Kuna mipango gani ya kumsaidia yeye na wa karibu yake? Kuna uwepo wa jumuiya huko? Emergencies kama hizi zinapewa umuhimu wa kumtibu mtu regardless halafu maswali mengine baadaye, kuna watu wako one step ahead of the game wanaojiuliza maswali haya? Mambo ya insurance yakoje? Gharama za kumhudumia ndogo ndogo kama zipo zinachukuliwa na nani na kivipi? Wale watu wa kuwafuatilia madaktari kwa karibu wapo? Isije kuonekana huyu muhamiaji hana nyimbo na care yake ikawa ya kiserikali serikali tu.

Mimi hiyo ndiyo sala yangu.


Kazi kweli kweli! Kulikuwa na ulazima wa yote haya especially katika wakati huu?? Haya...!!
 
Nimeomba aliyepata ajali apewe heshima kwa kuwa addressed properly, kwa lugha rasmi. Kwa nini moderator unasema hii ni off point?

Nimeandika hivi:

Habari za kutisha. Kila la heri.

Ab-Tichaz ahsante kwa kutupasha hizi habari.

Hata hivyo nakuomba uipe uzito na heshima hii taarifa ya kusikitisha kwa kutumia lugha rasmi kum address muathirika na yaliyomfika, sio "Ajali Mbaya ya Mbongo Michigan!"

Ndio haya haya ya "Denti azolewa na Kipanya!"
 
Kwa mujibu wa Chinga Networks hapa Detroit tumepata ujumbe huu:


"Wanajumuiya,
Mmoja wetu amepata ajali mbaya ya gari na yuko kwenye coma
University Of Michigan Hospital.Habari zaidi tutaleta kadri tunapopata.
Sala zitasaidia m'da huu"

Mungu atampa Afuweni
 
Kigoma, Pundit alichosema ndio ukweli wenyewe. At times like these someone needs to be practical, especially in a foreign land
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom