Mtanzania anaweza Kutajirika

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,695
1,696
Tanzania ni moja kati ya nchi masikini duniani ambayo zaidi ya asilimia 50 ya watu wake wanaishi katika umasikini ambao unachangiwa na ukosefu wa Ajira, Uzalishaji Kidogo, Ujinga, uchanga wa Sayansi na Technolojia na ukosefu wa Uwiano wa Biashara unaosababishwa na Madeni Makubwa ya Nje, na Usawa wa Biashara katika Masoko ya Nje na Sera sizizo nzuri.

. . . . Kwa kuzingatia hali halisi ya nchi yetu na jinsi inavyokosa uongozi thabiti wenye kutetea maslahi ya taifa kwa nguvu zote na uzalendo wa hali ya juu katika ubunifu wa sera nzuri . . .

. . . . Pia kwa kuzingatia kuwa katika Jambo Forum wengi wameonyesha uzalendo wa juu katika kutetea maslai ya taifa na kuwa wana uwezo wa hali ya juu katika kuyachambua mambo kwa kuzingatia hali halisi . . .

. . . . Na pia kwa kuzingatia kuwa kuna baadhi ya watanzania mijini na vijijini wamweza kujikwamua katika lindi la umasikini katika mazingira ya sasa tuliyomo kwa njia halali na zinazokubalika . . .

Napenda kutoa hoja ya kudumu sasa kuwa JF ijadili kwa kina na umakini wa hali ya juu ni namna gani Mtanzania Masikini na Kawaida katika Mazingira ya sasa hivi anaweza akabadili hali yake ya kawaida na kuondoka katika lindi la umasikini na hatimaye kujitengenezea utajiri kwa njia halali bila kutumainia siasa.

Maoni na mapendekezo yote yanaweza kuratibiwa baadaye na JF na machapisho kufanywa kwa ajili ya kuweza kuwasaidia watanzania wote kuondokana na umasikini. Ni matumaini yangu kuwa huu utakuwa ni mchango wetu bora hasa kwa watanzania wasio na namna ya kutembelea Jukwaa hili.

Naomba sasa kutoa hoja.
 
hizi ndio hoja sio kulalamika tu ooh waziri waziri ila naona watu wanachelewa kuchangia hoja hii kwa sababu aliyeanzisha sio member mwenye jina wanasubiri mwanakijiji aandike hata upuuzi wajibu.Big hizi ndio hoja na ntakuja na tathmini yangu jinsi gani mtanzania wa kwaida anvyoweza kujiondoa kwenye lindi hili la umasikini
 
hizi ndio hoja sio kulalamika tu ooh waziri waziri ila naona watu wanachelewa kuchangia hoja hii kwa sababu aliyeanzisha sio member mwenye jina wanasubiri mwanakijiji aandike hata upuuzi wajibu.Big hizi ndio hoja na ntakuja na tathmini yangu jinsi gani mtanzania wa kwaida anvyoweza kujiondoa kwenye lindi hili la umasikini

077, I doubt unawasoma watu vibaya. Hoja nyingine zinakosa response kutokana na presentation yake. Mwanzishaji mada huwa anatakiwa kuangalia namna ya kuwasilisha mawazo yake na forum gani hoja hiyo iwekwe. Aidha, majibu ya haraka yenye kuonyesha mlengo flani huwafanya wachangiaji kuhisi shari na hivyo kuiacha hoja ijimalize yenyewe. Hapa ndipo utaona kuwa uchangiaji wako wa haraka kuwalaumu wanachama kunaweza kuinyamazisha hoja hii.

Binafsi nadhani hoja hii ilitakiwa kuwekwa "Jukwaa la Uchumi" na si "Hoja nzito" kama alivyofanya mwanzishaji. Hata hivyo, inferiority ya watu kutoichangia hoja flani kisa mwanzishaji ni mwanachama mpya naomba ifutike akilini mwa wengi kwakuwa kila mwanachama alianza na post 1 (including me). Ni kwa sababu hiyo basi, naihamisha hoja hii kwenda Jukwaa la Uchumi kwakuwa naona inafaa sana kuwa kule.

Ahsante kwa mwanzishaji wa hoja hii na karibu sana na nikuhakikishie kuwa hoja yako ni nzuri sana na ya manufaa kwa watanzania. Tunahitaji vichwa zaidi kama chako.

Karibu
 
Ni kwa sababu hiyo basi, naihamisha hoja hii kwenda Jukwaa la Uchumi kwakuwa naona inafaa sana kuwa kule.
Nimeonelea niiache kwakuwa nshatoa maelezo, nitaihamisha endapo kutakuwa na ulazima wa kufanya vile. Nawakaribisha wachangiaji kuweza kudadavua hoja iliyowasilishwa.

Invisible
 
Kwa maoni yangu,

Tufanye kazi zinazopatikana, tuachene na mambo ya kuchagua kazi. Fanya iliyopo wakati ukitafuta ile unayoitaka wewe/uliyoisomea.

Wanawake wafanye kazi pia, tuachane na tamaduni za kijinga za kukaa nyumbani kisa Mume ana kazi/pesa. Kila mwenye uwezo wa kufanya kazi na afanye kazi.

Watu na wafanye biashara kulingana na mitaji waliyonayo, sio lazima biashara kubwa kubwa, mwanzo wa hesabu moja.

Serikali ama watu husika wawasaidie wakulima katika bei hasa masoko ya kimataifa. Ama kwa sisi wakulima wa ndani, basi wanunuzi wa ndani msituminye bei sana kwani wenzetu mnaenda uza kimataifa mnapata faida kubwa mkituacha hoi. At the same time, kwa wakulima wasiuze mazao yote na kusahau kujiwekea akiba, hasa kwa vyakula.
 
1. Tunahitaji tupatiwe huduma muhimu kama barabara ziweze kuwekwa kwa kiwango cha lami vijijini kote,kwani mazao yetu na mifugo yetu tuisafirishe bila matatizo

Hapa ieleweke kwamba lami ni muhimu kwani hudumu muda mrefu hivyo kutupunguzia stress za matengenezo ya mara kwa mara.

2. Maji ni muhimu kwa kila mtu (nyumba) mijini na vijijini kwani humpunguzia mama na watoto kupoteza muda wa kujielimisha na kufanya mambo mengine ya maendeleo wanapohangaika kutafuta maji.

Kama tunavyojua asilimia 75% ya mwili wa mwanadamu ni maji(nisahihisheni kama hapa nimekosea)hivyo tunahitaji huduma ya maji safi kwa afya.

Pia tunapotumia maji haya safi tunazalisha maji machafu(taka) pia kwa hiyo ni lazima tuwe na mifereji ya kusafirisha maji taka kutoka katika nyumba zetu bila kuathiri afya zetu.Kwa hiyo ujenzi wa barabara zetu uambatane na ujenzi wa mifereji ya kudumu itakayosafirisha maji taka ambayo hayaingiliani na mfumo wa maji safi.

3.UmemeTunahitaji huduma ya umeme kwa matumizi ya kila siku nyumbani kama kupika ,kufua,kunyoosha nguo,kuhifadhi vyakula (friji).Hapa ieleweke kuwa umeme sio starehe ni huduma ya muhimu ya kila mtu ambayo anastahili aipate.

Kwa kadri teknolojia inavyozidi kupanuka tunahitaji umeme kwa mawasiliano ya simu,mtandao(internet),tv,redio n.k

4. Ardhi (Nyumba au makazi) Ardhi iliyopimwa kwa ujenzi wa nyumba ni njia mojawapo ya kurahisisha maendeleo kwa haraka kwani huduma zote nilizozitzja hapo juu zitafanikiwa bila bomoa bomoa ambayo huingiza taifa hasara ya mamilioni ya fedha.

5. Elimu ni msingi mkubwa wa maendeleo,tunahitaji shule ambazo zina waalimu wa kutosha na wenye sifa zinazostaili,vifaa vya mazoezi ya vitendo na nadharia.

6 Hospitali Tunapouguwa,ajali,kuzaliwa kwa watoto tunahitaji huduma hii kwa haraka zaidi bila kusita.Hospitali ni majengo,vifaa kamli vya maabara na watumishi(doctors.nurses,midwifes,ets)wenye ujuzi kamili na sio kubabaisha.at least kila kijiji kingekuwa na hospitali.

Sasa tujadili tutapataje hizo nguzo sita za maendeleo kwa mtanzania???

Ndio maana tunarudi tena kwa ufisadi uliojaa katika nchi yetu tuuondoe kwanza,tukusanye fedha zetu ili tuanze kujenga nguzo moja baada ya nyingine.Kuijenga nchi sio kazi ya siku moja au rahisi kama wengi tunavyofikiria ingawaje inawezekana mtanzania akawa tajiri.

Maendeleo ya watanzania yataletwa na sisi wenyewe kwani mjenga nchi ni mwananchi na mbomoa nchi n mwananchi pia.

Kwa mawazo yangu

(a) naona tuungane na WanaJF kuutokomeza ufisadi(viongozi wabovu wote),

(b) Kuchunga rasilimali zetu na ikiwezekana kila mwananchi ajue nini kinaendelea katika nchi hii kila siku ya mungu kwani maskini kuna sehemu zingine za vijijini ambako mpaka leo hii hawajui hata kuvunjwa kwa baraza la mawaziri(mfano)kwa sababu ya kukosa vyombo vya habari.

(c)Tunataka kuona serikali yetu ikirudisha fedha zote za wizi mikononi mwa wananchi ,kwa kufanya hivi kuambatane na kufunguliwa mashtaka kwa wote walohusika kwa ufujaji wa fedha hizo.Hapa namaanisha kuna majengo mengi tu ambayo yamejengwa kwa fedha hizo yataifishwe kutoka kwao,na yafanywe vitega uchumi vya taifa na si mali ya mtu binafsi.

Viongozi wanaohusika wasione haya kushughulia hili kwani ndio tunasubiri kwa hamu kubwa ili safari yetu ya maendeleo ianze. Hatuwezi kwenda mbele kama fedha yetu inaliwa na watu binafsi kwa manufaa yao.

(d) Hatua hii ingeanza mara moja ili kumpa tumaini mtanzania (mlala hoi) kuwa siku moja itafika ambapo mtanzania atakuwa nautajiri
 
Superman umesikika.

Nimesoma kwa makini ulichokiandika na nafikiri sasa ni wakati mzuri wa kujulishana mbinu mbalimbali za kutufanya tuondokana na huu umasikini bila kutumia mbinu za akina Jeetu Patel maana 077 katukataza kwa mafumbo tusilalamike kuwa Ooo Waziri Ooo Waziri ingawa hatulalamiki kwa nia mbaya lakini hili linatufanya tuwe na pakuanzia kujitetea katika umasikini tulionao huu ni utangulizi.

Nije katika kujaribu kujibu baadhi ya mbinu ambazo naziona zinaweza kutusaidia kuondoka kwenye umasikini, jambo la kwanza ni MAWAZO yaani hapa nina maana inakupasa kuwaza utajiri hivyo utafikiri kufanikiwa hutakuwa na mawazo ya kushindwa hata kidogo.

Kitu cha pili ni MANENO, maneno unayosema yanaweza kujenga au kubomoa maisha yako vilevile yanaweza kukufanya uwe tajiri au masikini inakupasa uwe makini sana katika kutamka. Jibidishe sana kutamka maneno yenye mtazamo CHANYA kwa kifupi maneno yote ambayo mtazamo wake ni hasi usiyatamke kabisa kwa lugha nyepesi usikiri kushindwa ni hatari.

Jambo lingine linaloweza kututoa UMASIKININI ni kufanya kazi kwa bidii hata kama haina kipato hii itatujenga kutokuwa wavivu tutafanya kazi kama wajapani ambao wanalazimishwa kupumzika na sisi inatupasa kufanya hivyo kumbuka kuwa tanzania sasa hivi kila baada ya nyumba mbili kuna bar sasa unafikiri lini tutafanya kazi wakati kila utakapotembea unakutana na bar na kila ukigeuka unaona G/HSE wageni hao wa kulala kila kukicha wanatoka wapi? kama sio watu wanaoenda kupumzika mala baada ya kutoka Bar?

Fanya utafiti ukienda kwenye hizo G/hse utaambiwa zimejaa ingawa hazina watu hata uende usiku wa manane utaambiwa zimejaa lakini watu waliolala humo hawamo.Jambo lingine KUSOMA sisemi elimu kuuuubwa sana hapana tujue tu kurudisha chenji na kusoma Expire Date hapo ndipo mali itakuwa na Daftali vinginevyo mali hiyo itapotea bila habari.

Tukifanya vitu hivi vyote maisha yetu yataenda katika mtiririko bora na sisi tutafanya mambo kama jinsi wasomi waliokubuhu wanavyosema.Achana na maneno ya siasa ya ujamaa wasomi wanasema kwamba ili nchi iendelee inahitaji WATU, KILIMO CHA CHAKULA, KILIMO CHA BIASHARA, MIUNDO MBINU, VIWANDA.

Hapa ufafanuzi wake uko hivi watu watafanya kazi zote hizo watalima mazao ya chakula, watalima mazao ya biashara wakitosheka kwenye chakula watabadilisha mazao ya chakula kuwa ya biashara mfano mzuri ni Mapeasi tunayoyapata toka South Africa yale ni mazao ya chakula wenzetu wameyafanya ya biashara, sijui kama naeleweka.

Kwa kifupi mimi nafikiri tutatajirika kwa njia hii.
 
Superman,
Hii hoja imejadiliwa sana kwa kina na mapana tayari! soini haja kuanzisha thread mpya!

1. Sasa huo moyo wa kujitolea uko wapi wakati ufisadi umejaa na watu wanapora na kuiba? Mfuko umetoboka tayari.. na maadili ya kulinda national cake hakuna! Sasa angalia majumba ya kifahari, magari ya kifahari ya wafanyakazi wa serikali wenye mshahara tu wa 300,000 kwa mwezi.. hizi pesa wanapata wapi? Angalia ni only 30% ya kodi hukusanywa.. na matajiri hupewa excemptions!

2. Tuimarishe sana kwanza legal framework institutions kuwa na sheria kali na kuzizingatia kama Singapore..kwanza watu wafanye kazi kwa bidii na waogope na kuheshimu serikali awe waziri au mtu wa kawaida!

We need total overhaul to restore sanity in our institutions, then ndo mikakati ya kuondoa umaskkini ifuate!

3. Pia tuwe na time frame ya 5-10 years tuondokane na misaada!
 
Thanks For the Post.

Pili ningetoa pole na hongera kwa wana Jf kwa yaliyotokea nilikua Gizani mpaka nilipomsikia mwanakijiji ktk BBC.

Nini kifanyike.
1; Tunatakiwa kubadili mfumo wetu wa elimu from current system ambayo imeshindwa kumsaidia mtanzania wa kawaida.
2;Elimu iwe bure kuanzaia Primary to Higher learning institution.
3;Serekali ibadili mfumo wa uongozi i mean to streamline gvt opertions eg kuondoa nafasi ambazo zina dublication so that to cut down cost mfano haina maana kua na DC na MP ktk wilaya moja na hapo hapo tuna madiwani na wenyeviti wa halmashauri na wakurugenzi there is need ya kuevaluete mfumo huu na kufanaya COST BENEFIT ANNALYSIS.
4;Kumpa subsidy Mkulima wa kawaida na serekali kuanzisha mfumo wa kununua mazao ya wakulima yanapokua hayana soko bila kumsababishai hasara.
5;Kutaifisha migodi yote au investors kukubali 50;50 sharing ya migodi.
6;Sera ya kilimo iwe rivesed na kuifanya serekali itambue kua kilimo ni Priority na si kitu kingine.
7;Kuainisha Main source of Revenua na serekali kuidentify priority za nchi ktk specific period of time eg;INfustructure i.e barabara kupewa uzito sawa na sector ya kilimo investment kubwa nchi iwe ktk barabara,elimu,Afya,na kilimo uwekezaji wa nje haouna manufaa sana sasa hivi why na sema hivi INCOME OUT FLOW NI KUBWA SANA KULIKO INCOME INFLOW mpaka uchumi wetu utakapo kuwa mkubwa we dont need ku attaract more investor from out side since we have less inthere country.
 
Thank you 077 (Licence to Kill? LOL) for Breaking the ice. Well I am a bit new in JF but I promise to be active and get to Invisible Level (Robot). As I am a Superman I do not see any problem with my ambition. I also believe although I am a Junior Member, but the Senior Members will always conribute when the Topic is interesting and challenging. What do u think 077?

Invisible (Robot), thank you for your guidance, may be I was a bit fast in my posting as I was excited when JF come back after we missed it for some time. I also must admit that I was not very familiar with the Forums and Threads postings. However I have gone through the structure of JF and in future will be OK. Please keep on guiding us whenever we make other mistakes unwillingly. Big up for a hard work to bring up JF and also to bring it back Online. Thanks.

Lizy . . . . "Never say Never". Thanks for a very positive contribution. It makes a lot of sense if your conribution can be followed by Stakeholders. I know you have been thinking more in some other areas and I am waiting to hear from you more. We need JF to publish the findings . . . That is what I volunteer. So, send more comments.

Omba and Kizito, I think your contributions are excellent. I am digesting them and wonder how far we would have gone as a country if we were all serious on implementing the ideas.

Mzalendohalisi . . . My sincere apology if this thread was discussed before. It was not my intention. As I said, I am a bit new in the forum and may be I do not know much about the previous threads. Please advise me of the Thread which has been discussed so that I can make a reference and if possible compile together with this thread on the conclusion. Otherwise thank you for your input. You was brief and to the point confirming your maturity and understanding as JF Senior Expert Member.

BabaH, thank you for your support to Mzalendo Halisi point and insisting about the Rule of Law na kufuata sheria.

Mtoto wa Mkulima . . . . You also made brief point with a big impact.

Thank you all.

I would like to call upon all Senior Members (To challenge 077) that Senior Members can contribute to any topic posted by a Junior Member. I think this Forum do not base on Seniority but on Issues. Please prove this to Junior Members by conributing to this Thread.


Hoja yenyewe ni hii . . .

Napenda kutoa hoja ya kudumu sasa kuwa JF ijadili kwa kina na umakini wa hali ya juu ni namna gani Mtanzania Masikini na Kawaida katika Mazingira ya sasa hivi anaweza akabadili hali yake ya kawaida na kuondoka katika lindi la umasikini na hatimaye kujitengenezea utajiri kwa njia halali bila kutumainia siasa.
 
Kuna Mdau kanitumia hii na mimi naiwakilisha kama ilivyo.

Kwa upande wangu ili nchi iendelee au kujiondoa umasikini anza na baby steps

1. Know your people...yale mambo ya nyumba kumi kumi yangerudi kusaidia kupata idadi ya watu wote Tanzania bila kutumia mamilioni ya hela. Huwezi uakendelea kama hujui una watoto wangapi wa kuwalisha.... Kila mtu awe na mjumbe wa nyumba kumi na hapo ndipo patawezasha kupatikana kwa vitambuslisho n.k.

2. Ukijua nani ni nani na anafanya nini na anaingiza hela ngapi kwa mwaka basi utaelewa jinsi ya kuallocate resources zilizopo nchini...

3. Kodi ya the more you earn the more you pay ni muhimu. Hii hata kwa wafanya biashara sio kwa watu wamaofisini tu kila mtu alipe kodi. Na hizi hela sio ziende kwenye kuanzisha maidara tu na maofisi yasiyo na maana ni kuwasaidia wasiokua na kazi...matajiri na mashirika wakiona hela yao inaenda kwa wacheza bao mchana basi wata create jobs ili wacheza bao warudi kufanya kazi nao wachangie kodi.

4.Give back to your community- Maendeleo yanaletwa na watu - Tuanze tabia ya kuchangia maendeleo ya nchi bila kutegemea kulipwa...Community service ni muhimu kwa nchi kupunguza gharama za ajabu ajabu.

Sio lazima serikali itegemewe kupeleka maji vijijini...kama mtu unaishi huko una hela peleka maji kwa kijiji, kama mtu una hela fungua library watu wajue kusoma, kama unahela do something for your country...Huku watu wakifa tunaona wills zao kila siku zinasema hela hii iende kusaidia shule hii, hospital hii, kanisa hili etc lakini wabongo kwa uchoyo wills zetu ni watoto wetu tu basi hata kama mtoto wako amebarikiwa tayari na ana uwezo wakuishi mpaka afe bila kutegemea hela yako basi utamwengezea nyingine tu...Wape watu wasio na uwezo na utabarikiwa sana tu ipe kijiji chako kitafanya la maana na hiyo hela....

5. Tupunguze idara sizizo na mbele wala nyuma na title zisizo na mbele wala nyuma...Income ikiwa ndogo kuliko matumizi ni deficiency. Je bajet za bunge vitabu vyake vuna balance kila mwaka au zikisha somwa hadharani the rest ni Mungu ndio anayejua? Kila siku tuna spend more than we earn and then tuna carry on madeni tu.

6. Globolization ni nzuri lakini tuajiri watu wa nyumbani kwanza kabla ya kuwapa nafasi watu wa nje...Na hii iwe law anyeivunja ashitakiwe...kama kuna position fulani ya kazi kwenye shirika au office yeyote ni lazima zitangazwe kwa muda wa kipindi fulani wakikosa mtu anaye qualify kutoka nchini basi ndio watafute expart kutoka nje. Sasa hivi wamarekani wengi wamekimbilia nje ya nchi kwa vile kazi zilipungua na kazi zikirudi watarudi na wataajiriwa na nchi yao kama kawaida kabla ya wageni...Sasa sisi tumesahau watu wetu na kuwapokea watu wa nje wengi tu na kuacha vijana wasomi wakiwa hawana kazi. Ni shule ngapi za kitaifa zilizofunguliwa zina walimu wanaotoka congo, kenya, Africa kusini etc...? Unataka kuniambia mtu aliyemaliza chuo kikuu hawezi kufundisha darasa la kwanza mpaka form 4 ya medium english school hata kama major yake haikuwa education? Wake up guys....Kulivyo na shortage ya walimu US kamauna degree unaenda unafundisha high school vizuri sana tu.....

7. Rushwa rushwa sushwa ni adui wa nchi....bila kuzuia hii hata iweje hamna kitakachoendelea..Kungekua na sheria kali ya rushwa basi kila kitu kingeenda kwa law na vizuri sana na wasio na hela wangeishi vizuri sana.Sasa hivi huendi mahali au hupati kitu bila kutoa kitu kidogo....Je tutaendelea hivi...Najua hatuwezi kuondoa kabisa rushw alakini hata tukigusa 50% tutafika mbali sana...

uongozi ungeanzia chini kwenda juu sio juu kwanda chini....Yaani nina maana raia-mjumbe wa nyumba kumi- then mtaa-then town - then kata-then- sijui tarafa na kuendele...sio uongozi uliopo wa sasa rais- waziri- mkuu wa mkoa- wilaya etc....

Good management na kujua wakureport kwake sasa hivi nadhani raisi akituma jambo lifanyike nahisi linaishia katikati kwa vile hamna mtu wa kumfikishi raia legally...kuna link in miss some where.... in reality there is no connection btn Our president and a regular citizen.......

Nchi zilizoendelea atleast unajua kuna rank na wapi panaenda wapi...sisi hapo juuu TZ tuna vyeo vingi na watu wengi lakini ukienda kwenye ngazi za kata na vijiji kote kumesahauliwa na raia wako wenyewe wenyewe tu yaani it is chaos like a circus.
 
Napenda kuongezea katika yote mliyosema watanzania waongeze morali ya kusoma vitabu maana wabongo kwa uvivu wa kusoma vitabu nenda hata chuo uone vitabu vinavyoozea library kuna msemo kkuwa ukitaka kuficha pesa mtanzania asione ficha kwenye kitabu itakaa kwa usalama hata miaka 100 ial tunachotakiwa kujua hakuna maendeleo pasipo kusoma vitabu ambapo udadisi uibuka na kuleta ari ya kimaendeleo ila ni kweli pamoja na yote tunayoyazungumzia nchi pasipo siasa safi hakuna lolote haya si maneno yangu baba yetu Nyerere(RIP)alikwisha tamka.Kwa hiyo wananchi wachague viongozi safi pia
 
Nimeanzisha shamba, muda wa kupanda umefika nina mazao mawili ya kupanda karanga na mahindi. Limitation yangu ni eneo, sijui mavuno ya karanga kwa eka najua miche ya mahindi kwa eka ni 45,000. Lengo langu ni maximize return ya eneo langu. Nimetafuta uzalishaji wa karanga kwa eka sijafanikiwa bado. Sijasoma kilimo, naomba aliyesoma kilimo anisaidie au yeyeto anayejua mavuno ya karanga kwa eka. Jumamosi ndio siku ya kupanda, nitafurahi nikipata jibu mapema.

Nimeamua kutokuwa masikini tena nisaidieni wanaJF ninachotaka ni mawazo yetu tu yananitosha.
 
Tanzania ni moja kati ya nchi masikini duniani ambayo zaidi ya asilimia 50 ya watu wake wanaishi katika umasikini ambao unachangiwa na ukosefu wa Ajira, Uzalishaji Kidogo, Ujinga, uchanga wa Sayansi na Technolojia na ukosefu wa Uwiano wa Biashara unaosababishwa na Madeni Makubwa ya Nje, na Usawa wa Biashara katika Masoko ya Nje na Sera sizizo nzuri.

. . . . Kwa kuzingatia hali halisi ya nchi yetu na jinsi inavyokosa uongozi thabiti wenye kutetea maslahi ya taifa kwa nguvu zote na uzalendo wa hali ya juu katika ubunifu wa sera nzuri . . .

. . . . Pia kwa kuzingatia kuwa katika Jambo Forum wengi wameonyesha uzalendo wa juu katika kutetea maslai ya taifa na kuwa wana uwezo wa hali ya juu katika kuyachambua mambo kwa kuzingatia hali halisi . . .

. . . . Na pia kwa kuzingatia kuwa kuna baadhi ya watanzania mijini na vijijini wamweza kujikwamua katika lindi la umasikini katika mazingira ya sasa tuliyomo kwa njia halali na zinazokubalika . . .

Napenda kutoa hoja ya kudumu sasa kuwa JF ijadili kwa kina na umakini wa hali ya juu ni namna gani Mtanzania Masikini na Kawaida katika Mazingira ya sasa hivi anaweza akabadili hali yake ya kawaida na kuondoka katika lindi la umasikini na hatimaye kujitengenezea utajiri kwa njia halali bila kutumainia siasa.

Maoni na mapendekezo yote yanaweza kuratibiwa baadaye na JF na machapisho kufanywa kwa ajili ya kuweza kuwasaidia watanzania wote kuondokana na umasikini. Ni matumaini yangu kuwa huu utakuwa ni mchango wetu bora hasa kwa watanzania wasio na namna ya kutembelea Jukwaa hili.

Naomba sasa kutoa hoja.

SuperMan:

Umasikini unaweza kutokana na watu kukufanya wewe kuwa masikini. Na umasikini mwingine unatokana na mazingira uliyopo. Na sehemu kubwa ya umasikini wetu unatokana na mazingira yetu.
 

4.Give back to your community- Maendeleo yanaletwa na watu - Tuanze tabia ya kuchangia maendeleo ya nchi bila kutegemea kulipwa...Community service ni muhimu kwa nchi kupunguza gharama za ajabu ajabu.

Sio lazima serikali itegemewe kupeleka maji vijijini...kama mtu unaishi huko una hela peleka maji kwa kijiji, kama mtu una hela fungua library watu wajue kusoma, kama unahela do something for your country...Huku watu wakifa tunaona wills zao kila siku zinasema hela hii iende kusaidia shule hii, hospital hii, kanisa hili etc lakini wabongo kwa uchoyo wills zetu ni watoto wetu tu basi hata kama mtoto wako amebarikiwa tayari na ana uwezo wakuishi mpaka afe bila kutegemea hela yako basi utamwengezea nyingine tu...Wape watu wasio na uwezo na utabarikiwa sana tu ipe kijiji chako kitafanya la maana na hiyo hela....

Superman,
Nimekipenda sana kipengele hiki.

Hivi tujiulize ni Watanzania wangapi wenye uwezo wa kielimu, kifedha, na kimaarifa/kiujuzi wanajitumikisha kwenye community service? Generally, wengi wetu hatuna moyo wa ku-give back to the community. Unajua, hakuna msaada wenye akili wa kumpatia mtanzania mwenzako kama wa kumu-empower with knowledge and skills.

Kama ni kweli watu wanavyosema kuhusu kwamba kuna wataalamu wengi wa kitanzania nchi za nje, then kwa nini hawatumii knowledge na exposure yao kujitolea kuchangia kwenye community zao za nyumbani? Cummunity service ni msaada mmoja makini mtu unaweza kuutoa kwa faida ya taifa.

Mfano, nchi yetu haina entrepreneurs wa kutosha. Na hao wachache waliopo ni wavivu wa explore aina/mbinu mpya za kibiashara. Na matokeo yake wanakesha kuigana kila kitu kwenye biashara. Leo hii ukianzisha biashara yako ya ashikirimu za ukwaju, ukiamka kesho asubuhi utakuta mtaa mzima wanauza ashikirimu za ukwaju. Yani hakuna hata jirani mmoja hatakayefikiria angalau kuuza ashikirimu za maziwa. Sasa basi, ni kwa nini watanzania wenye elimu na/au ujuzi wakibiashara wasijitokeze kwa wingi kuanzisha kongamano za kibishara?

Hivi kuna Watz wowote ambao wanafikiria kuanzisha program ya kutembelea vyuo mbalimbali bongo na kuwa guest speakers madarasani bila ya kutegemea kulipwa posho? I can only imagine, kama mfanyabiashara akitembelea darasa la biashara UDSM na ku-discuss his/her personal business experience, ni wanafunzi wangapi watatoka na real business knowledge at the end of the lecture?

I mean, biashara ni mfano mmoja tu. Lakini kuna sayansi, tech, kilimo, law, mazingira.....the list goes on
 
Superman,
Nimekipenda sana kipengele hiki.

Hivi tujiulize ni Watanzania wangapi wenye uwezo wa kielimu, kifedha, na kimaarifa/kiujuzi wanajitumikisha kwenye community service? Generally, wengi wetu hatuna moyo wa ku-give back to the community. Unajua, hakuna msaada wenye akili wa kumpatia mtanzania mwenzako kama wa kumu-empower with knowledge and skills.

Kama ni kweli watu wanavyosema kuhusu kwamba kuna wataalamu wengi wa kitanzania nchi za nje, then kwa nini hawatumii knowledge na exposure yao kujitolea kuchangia kwenye community zao za nyumbani? Cummunity service ni msaada mmoja makini mtu unaweza kuutoa kwa faida ya taifa.

Mfano, nchi yetu haina entrepreneurs wa kutosha. Na hao wachache waliopo ni wavivu wa explore aina/mbinu mpya za kibiashara. Na matokeo yake wanakesha kuigana kila kitu kwenye biashara. Leo hii ukianzisha biashara yako ya ashikirimu za ukwaju, ukiamka kesho asubuhi utakuta mtaa mzima wanauza ashikirimu za ukwaju. Yani hakuna hata jirani mmoja hatakayefikiria angalau kuuza ashikirimu za maziwa. Sasa basi, ni kwa nini watanzania wenye elimu na/au ujuzi wakibiashara wasijitokeze kwa wingi kuanzisha kongamano za kibishara?

Hivi kuna Watz wowote ambao wanafikiria kuanzisha program ya kutembelea vyuo mbalimbali bongo na kuwa guest speakers madarasani bila ya kutegemea kulipwa posho? I can only imagine, kama mfanyabiashara akitembelea darasa la biashara UDSM na ku-discuss his/her personal business experience, ni wanafunzi wangapi watatoka na real business knowledge at the end of the lecture?

I mean, biashara ni mfano mmoja tu. Lakini kuna sayansi, tech, kilimo, law, mazingira.....the list goes on

Una-give back kwenye community pale unapokuwa na surplus.
 
Una-give back kwenye community pale unapokuwa na surplus.

Bin Maryam,
Nakubaliana na wewe kama tunazungumzia tangible assets. Lakini ni surplus gani mtu anahitaji kuwa nayo kabla hajahamua ku-give back to the community kwenye masuala ya intangible assets kama elimu na maarifa/ujuzi?
 
Bin Maryam,
Nakubaliana na wewe kama tunazungumzia tangible assets. Lakini ni surplus gani mtu anahitaji kuwa nayo kabla hajahamua ku-give back to the community kwenye masuala ya intangible assets kama elimu na maarifa/ujuzi?

Nadhani kwenye mambo ya maarifa na ujuzi kuna matatizo fulani. Wengi waliopata ujuzi na maarifa waliacha jamii zao wakiwa na miaka 15 kwenda kusoma. Na wanapomaliza masomo wanapangiwa mbali na mikoa yao, hivyo uhusiano wa kurudisha unakuwa umepungua.

Hivyo unapohamua kupiga ukabila au udini kwa kuwapeleka watu mikoa tofauti unaondoa-bond ya watu na sehemu zao na hiyo ni hasara ya kuimeza.
 
Nadhani kwenye mambo ya maarifa na ujuzi kuna matatizo fulani. Wengi waliopata ujuzi na maarifa waliacha jamii zao wakiwa na miaka 15 kwenda kusoma. Na wanapomaliza masomo wanapangiwa mbali na mikoa yao, hivyo uhusiano wa kurudisha unakuwa umepungua.

Hivyo unapohamua kupiga ukabila au udini kwa kuwapeleka watu mikoa tofauti unaondoa-bond ya watu na sehemu zao na hiyo ni hasara ya kuimeza.

Well sometimes home is where you live....ukiondoa ughaibuni for some of us:) Kwa hiyo hao wanajamii waliohamishwa kwenye makazi mapya enzi hizo, itabidi watambue kuwa wanapoishi ndipo cummunity yao ilipo, na wanapaswa kuitumikia kwa nguvu na mali zote. Mimi siku zote naona haijakaa sawa, kwa mchaga aliyezaliwa na kulowea Mtwara (anaongea mpaka kimakonde, let alone kula panya) anapohamua kwenda kuchangia ujenzi wa shule Machame wakati anapoishi kuna ukosefu wa shule za kutosha.

On the other hand, bado kuna community ya tanzania yote as awhole. Mfano nilioutoa wa kuwa guest speaker vyuoni unalenga ku-give back to the Tz community bila ya kujali kabila, dini, na tabaka.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom