Mtanzania Anarudishwa Bongo Kutoka Marekani. Ana USD 10,000 (23M Tshs) Tu. Mnampa Ushauri Aitumieje?

Aende nchi za Europe. Baadhi elimu ni bure, kazi kupata ni rahisi sio kama USA.
Ukitolewa USA kwa deportation. Na nchi za European Union, Canada et al hauwezi pata viza. Unakuwa kwenye system yao. Hapa ni bongo tu au nchi nyingine za Africa
 
Ningekua mimi ndiye yeye. Kwanza ningejifunza vitu hivi..(na assume kama mtu katoka nje basi ana exposure na ni mtu asiye na ugomvi wa vitabu)


1. Ngetumia mwaka mzima kujifunza forex

2. Ningejifunza jinsi ya kuwekeza kwenye crypto currencies..

3. Ndani ya mwaka huo mmoja ningejifunza digital marketing na SEO!

4. Ningejiuliza nini napenda then ningefungua youtube channel ili nitengeneze videos za nnacho penda.. Na kwa sababu nimesha jifunza SEO hapo kwenye namba 3 basi hapa nisinge teseka! Maana knowledge ya SEO ndio ningeitumia ku rank video zangu youtube!!

hii ni nzuri maana in the long run ina faida!

Baada ya hapo ningefanya hivi...

1. Ningetoa 1000usd ni nunue laptop mpya (kama hana kabisa ila kama anayo anaweza acha).. hii ni muhimu maana hii ndio kama jembe shambani, lazima uwe nalo ili ulime!

2. Ningetenga 3000usd na kufund account ya forex (ningefanya hivi baada ya kuhakikisha nime practise vya kutosha na nna strategy inayo eleweka otherwise ningeacha kwanza).

3. Ningetumia 2000usd na kuwekeza kwenye coin kama ENJIN, eCASH, ZIL etc pia ningeangalia hizi meme coins hasa hizi mpya mpya na kuziwekea walau dola 500...

Hapo ningekua nimebakiwa na 4000usd.. then hii 4000 usd ningefanya hivi..

A. Ningetoa 1000usd nifungue kampuni ya digital marketing.. na hapa ningekomaa sana na kazi za freelancing za nje!

B. Kwa sababu nna laptop (rejea namba 1 hapo juu) basi ningefungua youtube channel na ninge hakikisha natenga 500usd kwa ajili ya kununua mic nzuri!

Mpaka hapo nimebakiwa na kama 2500usd hivi! Hii ningeiweka reserve incase of anything pamoja na matumizi ya hapa na pale!
Mambo ya Youtube channel, forex etc watu wengi wanajaribu na hawatoboi ng'ooo. Atapoteza muda hapo na pesa itaisha na hamba kitu
 
Amtafute mwanamke wa kimachame aliyetulia, amuonyeshe namna ya kuwekeza hiyo pesa.
Ushauri wangu ni AKAE mbali kabisa na mademu wa Tz. Hio 24m itakuwa sifuri. Asitegemee mwanamke au mtu amsaidie kutoka. Ni yeye tu apambane ndio maybe ataweza
 
Nimefanya ufugaji kuku toka mwaka 2008 mpk leo, sio rahisi na inahitaji mtaji mkubwa ili utoboe. Unatakiwa uwe na ardhi, mabanda, running capital, wateja wa uhakika na utaalam kwenye ufugaji otherwise utalia
Biashara yeyote sio rahisi siku hizi.. changamoto nyingi sana. Enzi za wakina Mengi marehemu walivyoanza .. competition haikuwa kubwa sana kama siku hizi.
 
Kitendo cha kusoma mchezo 10m inakuwa imeshakatika. 24m ni mtaji mdogo sana wamachinga wengi wanao huo mtaji kwa sasa. Mambo yamebadilika sana Tanzania, watu wana pesa sana. Ukitoka nje na 24m ni kuja kuteseka tu ni ngumu kutoboa maana watu siku hizi wanajua kuchungulia fursa siyo kama zamani.
Watu sidhani wana pesa sana kama wakati wa Kikwete. Watu hawana pesa sasa ivi. Lakini watu ni wapambanaji sana wa fursa. Kwa hio japo sio watu wengi wenye 24m.. ila wenye hio hela wachache wanajua sana kuiwekeza vizuri sana na Teari wanajua biashara za Bongo vizuri. Sasa jamaa hapo ndio akienda kichwa kichwa 24 m inaisha fasta
 
Nipo hapa mkuu,
ww mpenzi ulinisikitisha sana siku moja. Ila mie bado nakupenda. Nikupe info tu za ile biashara yangu ya tours kwa sasa nimepaki tu magari na lodges hazifanyi kazi sana. Nimerudi ughaibuni huku kuna fursa nzuri za pe$$a. Bongo bado assets zangu zipo, na nitazifanyia kazi ila biashara huko covid nk zilivuruga. Ila nilihuzunika ile post fulani ukasema maneno badala ya kuniuliza.
 
Kama ni dereva anunue bajaji apige kazi boss yeye mwenyewe.atunze chombo vizuri.
Bajaji ni mkoa wowote inalipa na atajiamlia mwenyewe muda gani apumzike?
Never be ashamed of your hustle 👏👏👏
 
Anunue gari used ya 5m iliokaza ilio kama Van! Anunue mahotpot na kutafta wapishi wazuri wa mama ntilie kisha wapike na kuenda kuuza msosi kariakoo hatojuta
Extrovert uko vizuri. Problem hapo atahitaji nyumba Dar, gari aitengeneze ifae kuwa ya kutembeza chakula. Apate wafanyakazi wazuri. Hio inahitaji $$ zaidi na muda. Ila ni idea nzuri brother 👏👏👏👏
 
Anunue zile gari ndogo afanye Uber huku akijipanga vizuri kusoma mazingira ya huku bongoland, Mimi mtu akiniambia niende nje ya tanzania siendi ng'o maana ukirudi wenzako wamepiga hatua kubwa

Inategemea unaenda kufanya nini na unakifanyaje,

Kuna wale wapo wanafanya kazi sio za ujuzi na malipo ni ya kutosheleza kuishi huko tuu.

Kuna wale wanaosoma na wakimaliza wana struggle kidogo then wanarudi bila mtaji.

Kuna wale ambao wanafanya kazi za ujuzi na wana experience na pesa ni ndefu wanalipwa.

Hawa wote kinachobaki ni wanahusisha vipi akili zao na uwekezaji nyumbani.
Unatumiaje likizo zako kujifunza nini cha kufanya nyumbani, una watu wa aina gani supportive.

Maisha ya Udayaspora hayana formular
 
Anunue zile gari ndogo afanye Uber huku akijipanga vizuri kusoma mazingira ya huku bongoland, Mimi mtu akiniambia niende nje ya tanzania siendi ng'o maana ukirudi wenzako wamepiga hatua kubwa
Inategemea. Mimi binafsi USA ndio imenitoa. Ila mimi niko tofauti na waTz wengi. Nilikuja kutafta maisha. Naishi kwa kujinyima nk. Wabongo wengi wakija huku ni starehe tu na wanasahau nyumbani. Mwisho wa siku ndio inakuwa hivi. Ni kuwa na malengo. Kazi USA zipo nyingi. Ila Tz kazi za mshahara mzuri ni changamoto kwa wengi. Inategemea tu.
 
Inategemea unaenda kufanya nini na unakifanyaje,

Kuna wale wapo wanafanya kazi sio za ujuzi na malipo ni ya kutosheleza kuishi huko tuu.

Kuna wale wanaosoma na wakimaliza wana struggle kidogo then wanarudi bila mtaji.

Kuna wale ambao wanafanya kazi za ujuzi na wana experience na pesa ni ndefu wanalipwa.

Hawa wote kinachobaki ni wanahusisha vipi akili zao na uwekezaji nyumbani.
Unatumiaje likizo zako kujifunza nini cha kufanya nyumbani, una watu wa aina gani supportive.

Maisha ya Udayaspora hayana formular
Ni kweli maisha ya diaspora hayana formula ila majority waishi Kwa shida heri tu kurudi nyumbani na huyu mleta mada alienda kwa shule lakini kufika kule akashindwa shule Sasa anaona arudi home wakati angekuwa bongoland angekuwa mbali sana, home is home tu mzee
 
Inategemea unaenda kufanya nini na unakifanyaje,

Kuna wale wapo wanafanya kazi sio za ujuzi na malipo ni ya kutosheleza kuishi huko tuu.

Kuna wale wanaosoma na wakimaliza wana struggle kidogo then wanarudi bila mtaji.

Kuna wale ambao wanafanya kazi za ujuzi na wana experience na pesa ni ndefu wanalipwa.

Hawa wote kinachobaki ni wanahusisha vipi akili zao na uwekezaji nyumbani.
Unatumiaje likizo zako kujifunza nini cha kufanya nyumbani, una watu wa aina gani supportive.

Maisha ya Udayaspora hayana formular
Ww itakuwe umeishi nje ya Tz. Well said brother. Umechanganua vizuri sana. Need say no more.
 
Extrovert uko vizuri. Problem hapo atahitaji nyumba Dar, gari aitengeneze ifae kuwa ya kutembeza chakula. Apate wafanyakazi wazuri. Hio inahitaji $$ zaidi na muda. Ila ni idea nzuri brother 👏👏👏👏
Kwa hio pesa akija nayo kwangu mradi unasimama freshi tu! Mie tayari nina watu na gari ila mtaji wa kununua hayo ma vitu ndio sijapata bado ila haitahitaji zaidi ya 1M kuanza!

Asije akavamia biashara za kutumia mtaji mkubwa wakat hana uzoefu bora hela ibaki nyingi ya reserve hatosota sana kabla ya kuanza kuingiza faida. Anaweza fungua business ingine!
 
Ni kweli maisha ya diaspora hayana formula ila majority waishi Kwa shida heri tu kurudi nyumbani na huyu mleta mada alienda kwa shule lakini kufika kule akashindwa shule Sasa anaona arudi home wakati angekuwa bongoland angekuwa mbali sana, home is home tu mzee
Hapana my dear. Mimi niko vizuri. Ili uhakikishe youtube channel yangu ni

Ndio mimi kwa hio channel. Na tz nimejiwekezea vizuri sana tu. Na nina makaratasi nasafiri vizuri sana tu. Hii mada hainihusu mimi.
 
Kwa hio pesa akija nayo kwangu mradi unasimama freshi tu! Mie tayari nina watu na gari ila mtaji wa kununua hayo ma vitu ndio sijapata bado ila haitahitaji zaidi ya 1M kuanza!

Asije akavamia biashara za kutumia mtaji mkubwa wakat hana uzoefu bora hela ibaki nyingi ya reserve hatosota sana kabla ya kuanza kuingiza faida. Anaweza fungua business ingine
Poa bro. Nitumie namba yako basi inbox.. nitawaunganisha
 
Back
Top Bottom