Mtanzania akamatwa na unga China ananyongwa J'nne

Miaka miwili nyuma kuna muingereza zuzu alibebeshwa cocaine kuingiza China na alikamatwa Airport naye alinyongwa bila kujali kama ana mtindio wa ubongo. Usichezee Peking
Kama nchi zetu za kiafrika zingekuwa na sheria kama za china, naamini Afrika pangekuwa mahali pazuri zaidi kiuchumi na kisiasa!
 
Taarifa za kuaminika nikuwa,
Mtanzania
akamatwa na unga China ananyongwa J'nne anaitwa Zuberi Mussa, Ni mkaazi wa Zanzibar aliwahi kuishi Canada! Sijui atasaidiwa vipi maana yeye ni container tu Ma don wapo Bongo
Vijana wanatakiwa kuwa makini waache tamaa, wewe unakufa matajiri wao wamepunzika tuu!!!! Matokeo ya tamaa ni hayo sasa huko China hakuna misamaa namuhurumia saana!!! Labda serikali ya Tanzania imsaidie kama waziri mhusika Mhe Bernald Membe atamkumbuka!! Tena mbona nasikia huko Canada kuna kazi nyingi tuu za casual labor na community workers, labda alitaka kutoka haraka kwenye ufukara wa bongo!!!!

 
hii sheria ingekuwa kwetu ingesaidia sana hasa nguvu kazi inayoteketea kila siku,binafsi sijawahi kusikia hukumu zake.
 
Tanzania mbona hatuwanyongi au ni kwa vile ni biashara za wakubwa? Watoto wetu wameharibika mno. Imagine boarding schools mnapeleka watoto kuanzia primary ni balaa kule, madawa, kulawitiana ni order of the day. Lakini pia huwa najiuliza ni kwa nini mzazi umpelekee mwanao shule tangu chkechea boarding? Wanangu wote walisoma day school hadi primary na secondary ndiyo boarding at ther 13th. Sasa wewe mwanao 3 yrs unamtoa nyumbani hajui hata pendo la mama. Ukiwatelekeza watoto bila sababu ya msingi jua wanakosa malezi na upendo (parental care and love) mwishowe watatafuta upendo na care nyingine toka kwa makundi na mwishowe wataishia kuwa mabahasha na containers wa dawa za kulenvya.
Kwani mkuu hiyo ndio sababu ya mambo hayo ya unga????? Mimi sidhani naona kuna sababu nyingine tuu, hata hivyo pole yake na familia yake!!!!

 
Sasa, na sisi tumnyonge yele dada wa Ghana aliyeshikwa na kilo6 za heroin jana. Yule haitaji hata kesi
 
Tanzania mbona hatuwanyongi au ni kwa vile ni biashara za wakubwa? Watoto wetu wameharibika mno. Imagine boarding schools mnapeleka watoto kuanzia primary ni balaa kule, madawa, kulawitiana ni order of the day. Lakini pia huwa najiuliza ni kwa nini mzazi umpelekee mwanao shule tangu chkechea boarding? Wanangu wote walisoma day school hadi primary na secondary ndiyo boarding at ther 13th. Sasa wewe mwanao 3 yrs unamtoa nyumbani hajui hata pendo la mama. Ukiwatelekeza watoto bila sababu ya msingi jua wanakosa malezi na upendo (parental care and love) mwishowe watatafuta upendo na care nyingine toka kwa makundi na mwishowe wataishia kuwa mabahasha na containers wa dawa za kulenvya.


Sio kuwa watu wanapenda kupeleka watoto wao wadogo bording ni kutokana na mazingira ya kukosa madada wa nyumbani ( housegirls)
 
Kama ni kweli basi aanze kutafuta amani na muumba wake. Wale jamaa hawana mchezo. Wanaua hata generals in their army kwa ajiri ya rushwa na mambo kama hayo sembuse huyu ambaye hakuna anayemjua!
 
Sasa, na sisi tumnyonge yele dada wa Ghana aliyeshikwa na kilo6 za heroin jana. Yule haitaji hata kesi
Aisee kunamtu kakamatwa jana maeneo gani tena? Daah nadhani tushinikize sheria hii iwepo tz na ianze utekelezwaji haraka!
 
Taarifa za kuaminika nikuwa,
Mtanzania
akamatwa na unga China ananyongwa J'nne anaitwa Zuberi Mussa, Ni mkaazi wa Zanzibar aliwahi kuishi Canada! Sijui atasaidiwa vipi maana yeye ni container tu Ma don wapo Bongo


Astakafillulah!!! Wazanzibari siye ni wacha Mungu sana yakhe!!! Hatuwezi kufanya biashara hii ati!!! Huyo lazima atakuwa mbara tu!!! Mnatuchafua tu nyie!!! ndiyo maana tunataka muungano uvunjwe!!!
 
China hawana mchezo na ufisadi. Wale jamaa zetu wanaojirahisi kutumiwa kubeba miunga waogope uchina na uarabuni. kule hakuna upuuzi kama Bongo ambapo wanapita Airport na kutoa chochote kitu na kupeta. RIP Zuberi.

Mkuu mpayukaji, he's not dead yet.. khaaa!
 
Last edited by a moderator:
Mwaka juzi alinyongwa jaji mkuu wa China kwa kosa la rushwa ktk kesi ya kibiasha iliyohusisha makapuni mawili ya kikandarasi, jamaa hawana dogo kabisa!
Kama mtakumbuka mwaka juzi pia kuliibuka kashfa ya utengenezaji wa maziwa yenye sumu pale china, nikuwa mmiliki wa kiwanda kile, pamoja waziri mwenye dhamana ya vyakula walinyongwa ndani ya masaa 12 baada ya kutiwa hatiani!
 
kama kakamatwa huko china basi hilo halina kuuliza hatamaliza hata mwezi mmoja ..alazwe pema peponi
 
Sasa, na sisi tumnyonge yele dada wa Ghana aliyeshikwa na kilo6 za heroin jana. Yule haitaji hata kesi


yule dada hutasikia kesi yake hata siku moja na mwisho wa siku mzigo utapungua kilo ukiwa polisi na dada kurudi kwao kujaribu tena safari ya pili kuleta madawa tanzania
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom