Mtangazaji wa Clouds tv 360 awataka Wasomi wadaiwa HESLB wakauze Ice Cream walipe deni

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,369
108,411
Katika hali ya kuonyesha kuwa ni mwenye dharau na asiye na huruma na Watanzania wasomi ambao kila uchao wanahangaika kutafuta Ajira kutokana na mfumo mbovu na mazingira yaliyopo na bado mpaka leo hawajafanikiwa Mtangazaji wa Clouds tv 360 Hassan Ngoma akizungumza tena bila aibu na akiwa mkavu kabisa na akili timamu amewataka wale Wasomi wote wanaodaiwa na Bodi ya Mikopo nchini Tanzania ( HESLB ) kuanza kutembea popote katika miji yao walipo wauze Ice Cream katika Ofisi mbalimbali ili waweze kupata Pesa ya kulipia madeni yao wanayodaiwa.

Niwe wa kwanza kutaka kumwomba huyu Mtangazaji Hassan Ngoma awaombe radhi haraka sana Wadaiwa wa HESLB kwani nina uhakika kuwa hata alivyokuwa anayasema haya maneno hakuwa akitania bali alikuwa anamaanisha kitendo ambacho hadi Watangazaji wenzake Babie Kabae na Sam Sasali wakawa wanamshangaa.

Kuna wale vimbelembele ambao hudhani kuwa huwa nakurupuka tu kuwasema Watu humu hivyo kwa mnaotaka kujionea alichokisema bahati nzuri Clouds tv 360 Vipindi vyao huwa vipo Youtube hivyo kitafuteni Kipindi cha leo ili mjionee hizo dharau za wazi wazi alizozifanya Mtangazaji Hassan Ngoma kwa Wadaiwa sugu wa HESLB.

Kuwaambia Watu tena Wasomi ambao wanahangaika kutwa kutafuta ajira kuwa Watembeze Ice Cream ili waweze kulipia Madeni yao HESLB ni dharau kubwa, kali na isiyovumilika na ambayo imetolewa na Mtu ambaye tulidhani ndiyo angekuwa mfano mwema katika Jamii yetu kumbe ndiyo Kiongozi wa kuwadhihaki Wasomi Wadaiwa wa Bodi ya Mikopo.
 
Yeye na huyo mkurugenzi wa bodi wana matatizo ya akili, huyu mkurugenzi anajaribu kujitafutia sifa za kijinga katika kipindi ambacho hiyo hela haipo na haipatikani.
Miaka miwili aliyoweka alikubaliana na nani kwenye mkataba wa kuomba mkopo? Ngoja awape kazi mahakama zetu na atakapoanza kulipa fidia hapo ndio atamjua aliyemteua ni mtu wa aina gani
 
Anapalilia kibarua asitumbuliwe kule kwenye ghala la chenji ninasikia ni kweupe sana.
Hawa watangazaji wengi ni weupe sana kichwani

Elimu yao ya kuunga unga ndio wanataka kuitumua kutafuta sifa

Niliapa sitalipa deni la chuo labda wanifate nje kwa jinsi nilivyo angaika pale Udsm kuandamana kutafuta huo mkopa

Wakati wanaodai pesa kwa nguvu wanapunguza watu wa kuwakopesha kila siku,bora hata idadi ya wakopeshwaji ingeongezeka kuliko kupungua ningelipa.
 
Hawa watangazaji wengi ni weupe sana kichwani

Elimu yao ya kuunga unga ndio wanataka kuitumua jutafuta sifa

Niliapa sitalipa deni la chuo labda wanifate nje kwa jinsi nilivyo angaika pale Udsm kuandamana kutafuta huo mkopa

Wakati wanaodai pesa kwa nguvu wanapunguza watu wa kuwakopesha kila siku,bora hata idadi ya wakopeshwaji ingeongezeka kuliko kupungua ningelipa.
Wataanzisha utaratibu wa kudaka watu wanaokwenda holiday Tanzania, labda kama umebadili jina.
 
Wataanzisha utaratibu wa kudaka watu wanaokwenda holiday Tanzania, labda kama umebadili jina.
Wanajisumbua tu hawawezi kamata kila mtu.

Kwanza data base yao ni mbovu kuna watu walisoma miaka ya 80 alafu eti ni wadaiwa kichekesho.

Kuna brother wangu alimaliza mwaka 1989 eti na yeye alitajwa kuwa anadaiwa.
 
Lakini si ni mawazo yake tu? Kwani ni lazima ushauri wake kufuatwa?

Mawazo ya kuwadhihaki Watu huwa siyo mawazo ya Tija na acha kutetea Upumbavu. Huwezi kutumia platform kubwa kama ya kuwa katika Kipindi kinachoheshimiwa cha 360 Clouds tv halafu ukatokwa na comment ya Kifedhuli kabisa kama aliyoisema huyo Mtangazaji Hassan Ngoma. Na kibaya zaidi basi bora angekuwa kasema hayo maneno Kiutani tungemwelewa ila kayasema akimaanisha kabisa na kuonyesha kuwa alidhamiria kutuonyesha dharau na nyodo zake aliyarudia tena mara mbili tatu na kusisitiza kuwa Wasomi Wadaiwa sugu wote wa HESLB wafanye hima watembeze madeli ya Ice Cream wauze ili wapate Mamilioni ya Bodi ya Mikopo.

Hii ni dharau isiyovumilika na tunamtaka huyu Mtangazaji Hassan Ngoma wa Clouds tv upesi na haraka sana awaombe radhi hao wote aliowadhihaki. Kuna Watu hadi sasa wana maumivu makubwa ya kukosa Ajira huku wengine wakiwa wameshaathirika Kisaikolojia baada ya kujua wanadaiwa na HESLB na kimsingi tulidhani Mtu kama yeye mwenye Heshima yake Kijamii angekuwa na kauli nzuri na za kuwatia matumaini Wadaiwa na badala yake sasa anawadhihaki na kuwadharau.

Amenisikitisha mno.
 
-->>hata hivyo kulipa fedha hizi kwa heslb ni suala lisilokwepeka kwa binafsi naona ni lazima zilipwe /ILI WENGINE NAO PIA WAWEZE KUSOMA.
•NI LAZIME KUWE NA BALANCES YA UTOAJI WA FEDHA HIZI NA MAREJESHO YA FEDHA HIZI.
•PIA NADHANI MFUMO WA UKOPESHWAJI UREKEBISHWE KWA MAANA YA KWAMBA "MKOPESHWAJI ATALIPA FEDHA HIZI BILA YA KIGEZO CHA KUWA AMEPATA AJIRA AU LA"
•HILI LITAMJENGA MWANAFUNZI NA FAMILIA YAKE KISAIKOLOJIA MAPEMA....(kwamba kuna deni)
 
Wanajisumbua tu hawawezi kamata kila mtu.

Kwanza data base yao ni mbovu kuna watu walisoma miaka ya 80 alafu eti ni wadaiwa kichekesho.

Kuna brother wangu alimaliza mwaka 1989 eti na yeye alitajwa kuwa anadaiwa.
Kwani mabadiliko ya bursary kuwa mkopo yalianza mwaka gani?
 
Mawazo ya kuwadhihaki Watu huwa siyo mawazo ya Tija na acha kutetea Upumbavu. Huwezi kutumia platform kubwa kama ya kuwa katika Kipindi kinachoheshimiwa cha 360 Clouds tv halafu ukatokwa na comment ya Kifedhuli kabisa kama aliyoisema huyo Mtangazaji Hassan Ngoma. Na kibaya zaidi basi bora angekuwa kasema hayo maneno Kiutani tungemwelewa ila kayasema akimaanisha kabisa na kuonyesha kuwa alidhamiria kutuonyesha dharau na nyodo zake aliyarudia tena mara mbili tatu na kusisitiza kuwa Wasomi Wadaiwa sugu wote wa HESLB wafanye hima watembeze madeli ya Ice Cream wauze ili wapate Mamilioni ya Bodi ya Mikopo.

Hii ni dharau isiyovumilika na tunamtaka huyu Mtangazaji Hassan Ngoma wa Clouds tv upesi na haraka sana awaombe radhi hao wote aliowadhihaki. Kuna Watu hadi sasa wana maumivu makubwa ya kukosa Ajira huku wengine wakiwa wameshaathirika Kisaikolojia baada ya kujua wanadaiwa na HESLB na kimsingi tulidhani Mtu kama yeye mwenye Heshima yake Kijamii angekuwa na kauli nzuri na za kuwatia matumaini Wadaiwa na badala yake sasa anawadhihaki na kuwadharau.

Amenisikitisha mno.
Hassan Ngoma anapigia pande ukurugenzi wa wilaya.
 
Back
Top Bottom