Mtangazaji Maulid Kitenge mwenye Mahaba yasiyojificha na yaliyopitiliza kwa Yanga SC badilika kwani tumekuvumilia vya Kutosha

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,427
108,532
Haiwezekani Wewe 24/7 tu Utangazaji wako uwapo hapo Wasafi FM kwa Kushirikiana na Mpuuzi mwenzio Yusuph Mkule nyie Kazi yenu Kuu ni kutafuta tu negative angle ya Kuihusu Simba SC na Kuichafua. Mimi huwa ni mgumu sana Kumsema (Kumnanga) Mtu ila ukiona hadi hivi leo nimekuanzishia hapa JamiiForums huu Uzi jua umenikera.

Uweledi wako katika Utangazaji kila siku unazidi tu Kushuka (Kupungua) na najua wapo Wapumbavu wanaokudanganya kuwa Utangazaji wako huo wa Kinazi wa Kuipendelea sana Yanga SC kwa Gharama ya Kuikandia (Kuisiliba) Simba SC kunakupaisha na unapatia. Kitaaluma kabisa unachokifanya Kimekuharibia na Kukutengenezea Maadui kuliko Wadau muhimu.

GENTAMYCINE sisemi kuwa Wewe (ambaye ndiyo Mkuu wa Kitengo cha Michezo) hapo Wasafi FM msiwe mnaisema Simba SC pale ikitokea imeharibu. Tena nawaomba muwe mnatusema (mnaisema) Simba SC ila iwe ni katika namna ya Uwasilishaji wa Haki na Usawa lakini siyo aina yako Wewe na Kijana Mpuuzi Yusuph Mkule ambayo ni ya Kuichafua zaidi Simba SC kwa Wasikilizaji.

Kwa mfano unaweza kukuta Maulid Kitenge unatumia dakika 120 Kuijadili Simba SC na Kosa walilolifanya ( lililofanyika ) lakini aina ya Kosa hilo hilo likitokea kwa Yanga SC ama utalikwepesha lisijadiliwe (lisiongelewe) au ukiliruhusu lizungumzwe basi utalipa dakika 15 tu na Kujifanya unaharakisha kwenda katika Taarifa zingine. Huu ni Unafiki na very Unprofessional pia.

Najua uelewa wako katika Mambo ya Marketing, PR na hata Media Studies bado ni mdogo (na katika hili usinibishie kwani nakujua kuliko unavyojijua) hivyo basi umeshindwa kujua kuwa kwa Kuwakera Kwako Wasikilizaji wengi wa Simba SC tayari umeshaipunguzia Potential Audience Wasafi FM yako na nina uhakika Watu wenu wa Marketing watakubaliana nami hapa.

Ni kwanini umeshindwa tu hata Kuwaiga Wakongwe (Seniors) Kwako na Watu waliokutoa na Kukutengeneza akina Charles Nkwanga Hillary na Idrisa Abdallah Majura ambao walipokuwa Wakitangaza Vipindi vyao vya Michezo ulikuwa huwezi kujua kuwa Hillary ni Simba SC na Majura ni Yanga SC? Mbona Ibrahim Masoud wa EFM hawezi Unazi wake Simba SC akiwa Redioni?

Sina shida kabisa na aina ya Utangazaji wako kwani hata Mimi japo ni mwana Simba SC naupenda na labda nikuambie tu Wewe umekuwa ni Mtangazaji Mahiri mno wa Michezo katika Watangazaji wa Kizazi hiki cha Kati na umeweza Kuwashawishi Watu wengi (Watangazaji) wengi wa Michezo Kukuiga kwa Mikogo yako ya Kiutangazaji au Unavyohoji ila nakuomba badilika upesi.

Kama unaipenda sana Yanga SC na najua Wewe na Mpuuzi Yusuph Mkule mpo katika Payroll ya Yanga SC ambapo kila mnapokuwa mnaisema (mnaikandia) huku mkiichokonoa Simba SC basi mwisho wa Mwezi mnaingiziwa Pesa zenu. Basi waambie Yanga SC waanzishe kabisa Redio yao ili Wewe na Mpuuzi Yusuph Mkule muhamie huko na msiiharibie Wasafi FM.

Usipobadilika unaweza ukasababisha wale tuliokuwa tukikuvumilia basi kuanzia sasa nasi uvumilivu utushinde na ili nasi pia tuweze Kukunyoosha (hasa Sisi tunaokujua) tokea ukiwa pale kwa Chichi Uwanja wa Taifa na Matendo yako ya sasa hadi hizo Safari zako za Marekani ni za nini tunaweza Kuanika au Kukuanika na ukajiona hufai tena na waliokuheshimu wakakudharau.

Namalizia tu kwa Kusisitiza sisemi muogope / muache Kutusema (Kuisema) Simba SC pale ikikosea ila jaribuni Kutenda haki na msitumike vibaya.
 
mdukuzi
Naomba kwa sasa tusifike huko (huku) Mkuu japo kwa ulichokiandika kama tumetoka Dar kwenda Moro sasa hivi tupo zetu Ubena Zomoni Mkuu.
 
Haiwezekani Wewe 24/7 tu Utangazaji wako uwapo hapo Wasafi FM kwa Kushirikiana na Mpuuzi mwenzio Yusuph Mkule nyie Kazi yenu Kuu ni kutafuta tu negative angle ya Kuihusu Simba SC na Kuichafua. Mimi huwa ni mgumu sana Kumsema ( Kumnanga ) Mtu ila ukiona hadi hivi leo nimekuanzishia hapa JamiiForums huu Uzi jua umenikera...
Mkuu sawa ila maeelezo mengi hujasema alichokisema Mpaka Mkakwazika ili na 0sisi tuweze kujibu kwa hoja
 
Kwa mfano unaweza kukuta Maulid Kitenge unatumia dakika 120 Kuijadili Simba SC na Kosa walilolifanya ( lililofanyika ) lakini aina ya Kosa hilo hilo likitokea kwa Yanga SC ama utalikwepesha lisijadiliwe ( lisiongelewe ) au ukiliruhusu lizungumzwe basi utalipa dakika 15 tu na Kujifanya unaharakisha kwenda katika Taarifa zingine. Huu ni Unafiki na very Unprofessional pia.
Hapo umenena ukweli mtupu kabisa, nimekuwa nikimfuatilia sana na nimeona ana udhaifu huo (sijui labda ukiacha mapenzi kwa Yanga, huenda kuna kitu anakipigia mahesabu). Mfano amekuwa akipromote sana habari za kutowekwa kwa 20B ya Mo licha ya kupata ufafanuzi wa mara kwa mara kutoka kwa Crensesius Magori na Mo mwenyewe. Amefika hatua ya kuwaburuza wachambuzi wa kipindi kwa kulazimisha kuweka mahojiano aliyoyaandaa na anaowaita wanauchumi, ambao walikuja kuumbuka maana walisema mchakato umekwamishwa na Simba kwa sababu eti Simba haijalipa ada ya sh. milioni 80.

Anawaburuza wachambuzi kweli, leo walikuwa wakizungumzia kiwango kibovu cha beki za Yanga (Lamine, Mwamnyeto na Mukoko) katika mechi yao dhidi ya Namungo, ghafla akawakatiza eti tuwasikie wadhamini, na hata baada ya wadhamini hakuwezesha waendelee walipoishia
 
Mkuu sawa ila maeelezo mengi hujasema alichokisema Mpaka Mkakwazika ili na 0sisi tuweze kujibu kwa hoja
Una uhakika katika hizo Aya ( Paragraphs ) zangu Kenda ( 9 ) hapo juu sijasema tatizo ( kosa ) lake? Kuna Watu huwa mnanilazimisha niwadharau.
 
Hapo umenena ukweli mtupu kabisa, nimekuwa nikimfuatilia sana na nimeona ana udhaifu huo (sijui labda ukiacha mapenzi kwa Yanga, huenda kuna kitu anakipigia mahesabu). Mfano amekuwa akipromote sana habari za kutowekwa kwa 20B ya Mo licha ya kupata ufafanuzi wa mara kwa mara kutoka kwa Crensesius Magori na Mo mwenyewe....
Na hilo ndilo limekuwa tatizo lake Siku zote ambalo pia limechangiwa na Elimu ndogo ya Masuala ya Habari na Maadili aliyonayo japo anacho Kipaji.
 
Uzuri ni kwamba Kitenge sio mnafiki na unazi wake kwa Yanga upo wazi siku lakini he is a true professional. Mara ngapi anaisema vibaya Yanga na kuisema vizuri Simba?

Kuna wale wanafiki wanaoisema Yanga vibaya all the time lakini kwa wana Yanga we take them as they are. Wanajitahidi wasijulikane wao ni Simba lialia lakini mtaani wanajulikana wako upande upi.
 
Haiwezekani Wewe 24/7 tu Utangazaji wako uwapo hapo Wasafi FM kwa Kushirikiana na Mpuuzi mwenzio Yusuph Mkule nyie Kazi yenu Kuu ni kutafuta tu negative angle ya Kuihusu Simba SC na Kuichafua. Mimi huwa ni mgumu sana Kumsema (Kumnanga) Mtu ila ukiona hadi hivi leo nimekuanzishia hapa JamiiForums huu Uzi jua umenikera...
una hoja nzuri..ila haya maneno
"mpuuz"
"mpumbavu"
"mjinga" yanatawala sana ktk threads zako nyingi badilika bro..na ikiwezekana jifunza kuvumilia

hata mimi niliwahi kumchukia sana shaffih dauda kwa kutoiongelea vizuri arsenali

arsenal ilipokuwa ikishinda big match..huwezi kumsikia shaff, sasa ngoja ifungwe...
 
Yanga baba lao.. Unbeaten all over the world.

Piga kelele kwa Yanga akeeeeeeeeeeeeeeh...!!!!
 
Haiwezekani Wewe 24/7 tu Utangazaji wako uwapo hapo Wasafi FM kwa Kushirikiana na Mpuuzi mwenzio Yusuph Mkule nyie Kazi yenu Kuu ni kutafuta tu negative angle ya Kuihusu Simba SC na Kuichafua. Mimi huwa ni mgumu sana Kumsema (Kumnanga) Mtu ila ukiona hadi hivi leo nimekuanzishia hapa JamiiForums huu Uzi jua umenikera...
ONYO hili akirudia tutaaza kumuanika kila kitu,kitenge anashobo Sana na Simba sc
 
Back
Top Bottom